Kuna pepo likiingia kwenye familia hutafuna vizazi vingi

Kuna pepo likiingia kwenye familia hutafuna vizazi vingi

"... Malezi na makuzi bila wazazi wote wawili. Mama akiwa marehemu lakini asiyejulikana! Inauma sana!..."

HAKIKA INAUMA MNO, TENA MNO! NATAMANI KUJUA WATOTO WALIPO, NIKAWACHUKUE WAWE WANANGU WA KUWALEA.
Basi baaasi usilie ndugu acha kulia maana umepiga ukunga hadi simu yangu imevibrate.
 
Pepo la Umaskini
Pepo la mikosi
Pepo la kukosa ndoa
Pepo la kuzalia nyumbani
Pepo la ugumba
Pepo migogoro na mafarakano
Pepo la wizi, utapeli na udanganyifu
Pepo la madeni na mikopo isiyolipika nknk

Haya mapepo hutembea na vizazi mpaka cha tatu ama cha nne.. Unapoona kwenye familia yako kuna dalili za mojawapo kati ya hayo fanya hima lisisambae na kuathiri wengine.

Kuna ujumbe uliotoka Twitter unaoutaarifu uma kuhusu binti mmoja aliyefariki Morogoro na mwili wake uko mochwari. Hana ndugu ama kwa lugha nyingine ndugu zake hawajulikani ni akina nani.

Kilichonifanya niandike mada hii ni marehemu wakati wa ugonjwa wake akiwa kalazwa hospital kusema hana wazazi (haikufafanuliwa kama ni marehemu ama hajawahi kuwajua ama vinginevyo)

Cha kuumiza zaidi ni kwamba naye kafa kaacha watoto wadogo wawili.. Ni wazi hao watoto wana baba zao/yao lakini hawajulikani walipo. Inaumiza mno kwamba nao watakua katika mkondo wa mama yao.. Malezi na makuzi bila wazazi wote wawili. Mama akiwa marehemu lakini asiyejulikana! Inauma sana!

Ni maisha ya namna gani yanawasubiri hawa malaika? Mama kabla ya kifo kasema hana wazazi japo kataja alikotokea! Vipi kuhusu ndugu? Vipi kuhusu baba wa watoto?

Itakuwa faraja kubwa kama nduguze watajitokeza na kumchukua marehemu wakamzike na kuwachukua watoto wakawalee. Upendo hawatapata kama wa mama lakini at least watajulikana asili yao ili nao wasijekuja kusema huko ukubwani kwamba hawana wazazi wala ndugu[emoji25]


Kuna familia zina laana ya asili



Upungufu wa kinga za kiroho

Kwa mujibu wako ukizaliwa binadamu una pepo.
 
Wanapaswa kumlilia Mungu aisee
Sasa MUNGU awasaidie nini tena kama wameshindwa kutumia akili aliyopatia kujitengenezea maarifa ya kujijenga vema na kuwa na maisha mazuri na sio kuwa wabangaizaji. MUNGU hakuwataka wawe hapo ni matokeo ya namna wao walikuwa wanapanga ratiba zao za kila siku.
 
PEPO LA KUSOMA AF KUKOSA KUAJIRIWA

Sent from my itel L5007 using JamiiForums mobile app
Hilo sio pepo ni upumbavu wa serikali ya kijani na raia wasiokuwa na maamuzi na serikali yao. Wewe unaona ni mapepo sababu unatazama hili tatizo la kukosa ajira kwenye individual level.

Ungelitazama katika level ya taifa ungeelewa kuwa haimake sense idadi ya wahitimu wasomi kuongezeka kila mwaka huku nafasi za kazi na taasisi zikiwa zile zile na watu hawastaafu wanang'ang'ania kubakia serikalini.

This means kuna mfumo ambao unakinzana na mahitaji ya uhalisia. Sasa hapo mapepo yanafanyaje huo upepo wao.
 
Pepo ni neno linalotokana na Kiyunani daimon, ambayo inamaanisha 'fikra' au 'roho' isiyojumlishwa. Fikra au roho hii pia inaweza kueleweka kama nguvu, lakini sio kama mtu aliye na mapenzi au mhusika.

Kwa sababu ya ukweli kwamba Injili zinasimulia hadithi tofauti juu ya kutoa pepo kutendwa na Yesu, imani imeenea kuwa pepo siku zote ni nguvu hasi au za kishetani, au ni shetani mwenyewe. Walakini, haya hayapaswi kuchanganywa na mfano wa shetani.

Mapepo, Ujuzi, au Roho zinaweza kuwa nzuri au mbaya. Katika eneo la imani za kiroho, inaaminika kwamba pepo, kama nguvu isiyo ya kibinafsi, hufanya kupitia watu katika mfumo wa milki, na kwa hivyo, inaweza kukuchochea wewe na uumbaji na uharibifu, mzuri na mbaya. Sasa, katika visa vyote viwili, "pepo" lazima aachiliwe ili mtu aliye na uwezo tena atumie mapenzi na uhuru wake.
Pepo wanaozungumzwa kwenye biblia, au wale mapepo waliotolewa na yesu kwenye injili ni malaika wabaya, ni kundi la malaika walioasi na kufukuzwa mbinguni pamoja na shetani.

na wala hayo tunayoita mapepo (mashetani waasi) hawapo kwenye makundi kiivyo kwamba pepo la ngono, pepo la umasikini, pepo la maradhi, pepo la ulevi, pepo la kubeti nk. Ni wapo makundi mawili tu malaika waasi waliofukuzwa mbinguni pamoja na shetani na malaika wema waliobakia mbinguni kwa kumtii Mungu.

Muwe makini mnapotumia biblia kama reference kwani naona mapepo ulivoyacategorize hapa na jinsi unavoyaelezea ni kwa mujibu wa imani ya kiisilamu na sio biblia.
 
Pepo wanaozungumzwa kwenye biblia, au wale mapepo waliotolewa na yesu kwenye injili ni malaika wabaya, ni kundi la malaika walioasi na kufukuzwa mbinguni pamoja na shetani.

na wala hayo tunayoita mapepo (mashetani waasi) hawapo kwenye makundi kiivyo kwamba pepo la ngono, pepo la umasikini, pepo la maradhi, pepo la ulevi, pepo la kubeti nk. Ni wapo makundi mawili tu malaika waasi waliofukuzwa mbinguni pamoja na shetani na malaika wema waliobakia mbinguni kwa kumtii Mungu.

Muwe makini mnapotumia biblia kama reference kwani naona mapepo ulivoyacategorize hapa na jinsi unavoyaelezea ni kwa mujibu wa imani ya kiisilamu na sio biblia.
Hiki kifungu umekielewa lakini?
[emoji1541][emoji1541][emoji1541]
Kwa sababu ya ukweli kwamba Injili zinasimulia hadithi tofauti juu ya kutoa pepo kutendwa na Yesu, imani imeenea kuwa pepo siku zote ni nguvu hasi au za kishetani, au ni shetani mwenyewe. Walakini, haya hayapaswi kuchanganywa na mfano wa shetani.
 
Sasa MUNGU awasaidie nini tena kama wameshindwa kutumia akili aliyopatia kujitengenezea maarifa ya kujijenga vema na kuwa na maisha mazuri na sio kuwa wabangaizaji. MUNGU hakuwataka wawe hapo ni matokeo ya namna wao walikuwa wanapanga ratiba zao za kila siku.
Idadi wa watu wengi hatumuelewi vizuri Mungu na dini basi tuu. Binadamu tulipewa na Mungu akili na utahi akamaliza haya mambo mengine yote ni matokeo ya matendo yetu wenyewe wala Mungu hausiki kabisa. Watu wanaharibu misitu na vyanzo vya maji afu mwisho tunapigwa na ukame na njaa. eti tunaenda kesha kanisani kumuomba Mungu alete mvua, au tunanyoshea vidole eti tuache dhambi kisa hakuna mvua serious tunashindwa kufundishana na kuwekea sheria kali za kudhibiti mazingira afu tunakuja kumpigia kelele Mungu eti hakuna mvua.

Huo ni mfano tu, ila asilimia kubwa hayo ndio maisha na fikra zilizopo kwenye familia zetu. Tunaona dhahiri kabisa tu kinatakiwa kufanyika hiki na hiki hata kwa jasho na damu ili kuepusha matokeo mabaya, ila tunakaza mafuvu tunaenda kukesha makanisani, kwa waganga, manabii na mitume.
 
Sasa MUNGU awasaidie nini tena kama wameshindwa kutumia akili aliyopatia kujitengenezea maarifa ya kujijenga vema na kuwa na maisha mazuri na sio kuwa wabangaizaji. MUNGU hakuwataka wawe hapo ni matokeo ya namna wao walikuwa wanapanga ratiba zao za kila siku.
Wewe unawakilisha kizazi kilicholishwa kasumba kuwa there is no second chance.

Full kulaani
Full kulaumu
Maisha ni tairi lilanozunguka. Tatizo ni wapi tairi linapita
 
Hiki kifungu umekielewa lakini?
[emoji1541][emoji1541][emoji1541]
Kwa sababu ya ukweli kwamba Injili zinasimulia hadithi tofauti juu ya kutoa pepo kutendwa na Yesu, imani imeenea kuwa pepo siku zote ni nguvu hasi au za kishetani, au ni shetani mwenyewe. Walakini, haya hayapaswi kuchanganywa na mfano wa shetani.
Nimekuelewa mkuu.

Nilichotaka kusema ni hizo nguvu hasi, sio kwamba zipo kwenye makundi mfano kundi la ngono, kundi la ulevi, kundi la uvivu, kundi la umasikini nk. Ila ni kundi moja tu la malaika waasi basi na ambao walishavunjwa vujwa na kumalizwa nguvu na Yesu mwenyewe, hivyo hawana tena ubavu wala nguvu zozote juu ya binadamu kama kabla ya Yesu kuwashinda. Hivyo tukiendelea kuwatupia lawama hawa malaika waasi kwamba ndio wanaoendesha hizo nguvu hasi kwa kuwaona kama wao ndio chanzo cha kila dhambi na matatizo yote yanayomkabili binadamu ma familia zetu basi Yesu hakuna alichokifanya na ni kama hakuwahi kuja kabisa duniani maana shetani na malaika zake bado wanatamba.
 
Wewe unawakilisha kizazi kilicholishwa kasumba kuwa there is no second chance.

Full kulaani
Full kulaumu
Maisha ni tairi lilanozunguka. Tatizo ni wapi tairi linapita
Second chance ipo sio kwa kukesha kanisani na kumuomba Mungu, second chance ipo kwa kutafuta na kufumbua vyanzo vya matatizo yanayotuandama na kupambana navyo kwa kuyarekebisha hata kwa jasho na damu. Nje ya hapo Mungu hana msaada wowote maana sio kazi yake, alisha kuoatia akili na utashi akamaliza. Yanayobakia yote yatakuwa ni matokeo ya matendo ya binadamu mwenyewe either wewe mwenyewe au mwingine. Na ndio mana hata wasio-muelewa Yesu mpaka leo wanawaza Yesu alikuja duniani kumaliza matatizo yote ya mwanadamu na kumfanya aishi bila shida wala tatizo lolote.
 
Second chance ipo sio kwa kukesha kanisani na kumuomba Mungu, second chance ipo kwa kutafuta na kufumbua vyanzo vya matatizo yanayotuandama na kupambana navyo kwa kuyarekebisha hata kwa jasho na damu. Nje ya hapo Mungu hana msaada wowote maana sio kazi yake, alisha kuoatia akili na utashi akamaliza. Yanayobakia yote yatakuwa ni matokeo ya matendo ya binadamu mwenyewe either wewe mwenyewe au mwingine. Na ndio mana hata wasio-muelewa Yesu mpaka leo wanawaza Yesu alikuja duniani kumaliza matatizo yote ya mwanadamu na kumfanya aishi bila shida wala tatizo lolote.
Je wewe ndo unayeweka masharti ya second chance au ni aliyetuumba ndo huweka masharti?

Usiwe na inda wala ila ndani ya moyo unapokuwa unaangalia haya mambo. Usiwalaumu wahanga bali muombe Mungu yasikukute
 
Ni muhimu sana kufanya vetting ya kutosha kwenye kutafuta mwenza mwenye background yenye afya kiroho kwenye familia atokayo ili kuweza ku dissolve hiyo hali.. Lakini hii ni njia mojawapo tu
Hujawahi kuona kwenye familia yenye shida tangu kwa mababu, baba anachepuka na kuzaa mtoto anayekuwa tofauti na wengine na kuja kuwa mkombozi wa familia ama akawa kimeo
Nimekubali. Ukishaona historia ya mtu kiroho NI hovyo,kuachaacha wanawake,Mara alizalisha akatelekeza,kimbiaaaa
 
Back
Top Bottom