Kuna siri gani kwenda Pre-Season nje ya nchi kwa timu masikini?

Kuna siri gani kwenda Pre-Season nje ya nchi kwa timu masikini?

kavulata

JF-Expert Member
Joined
Aug 2, 2012
Posts
13,778
Reaction score
14,214
Tanzania hakuna timu tajiri, timu nyingi kama sio zote hazina misuli ya fedha za kusajili wachezaji wazuri sana na mabenchi ya ufundi class ya juu. Timu nyingi zinashindwa kuwalipa makocha na wachezaji signing fees zao na mishahara kwa wakati, wachezaji hawana bima na hazina viwanja vyao wenyewe. Kwa ujumla timu zetu zinaendeshwa kwa kubangaiza huku na kule; kwa maneno ya kimpira timu zetu ni feeder clubs kwa timu za kanda nyingine Afrika kutokana na umaskini wao.

Kwanini ni rahisi mno timu zetu kwenda kuweka kambi nje ya nchi lakini ni vigumu kusajili wachezaji wazuri, kulipa mishahara mikubwa ya wachezaji na benchi la ufundi au kujenga uwanja? Majibu ni mengi sana, mojawapo ya majibu hayo ni kwamba kuna uhusiano mkubwa sana kati timu kwenda pre-season za nje ya nchi na sababu za mtu kukubali kuidhamini timu.

Sina ushahidi kamili, lakini pre-season hizi za hivi zina uhusiano mkubwa na biashara za magendo (smuggling), madawa ya kulevya au ukwepaji ushuru kwa kutumia jina la timu, wachezaji na benchi la ufundi. Akili ya kawaida tu haiwezi kuamini kwamba timu zetu zina fedha nyingi za kwenda kuweka kambi nje nchi lakini hazina fedha za kusajili wachezaji wazuri wa kuleta mataji.

Jeshi la uhamiaji na wadau wengine hebu tegeni mitego ya kunasa matunda ya pre-season za nje ya nchi kwa timu mbovu kabisa uwanjani na zinazolalamika kuwa hazina pesa za kulipa wachezaji, makocha, kusajili na kujenga viwanja vyao. Mnaweza kugundua chocholo za uovu kwenye hizi safari.
 
Umejenga hoja nzuri sana mkuu, Uandishi wako pia ni mzuri.

Natamani tungekuwa na WATU wa aina yako kwa wingi hapa jukwaani ukiondoa wale WAJINGA wanaojaza Seva za Jamii forum.

Nikienda kwenye hoja Moja kwa Moja
Timu zinahusishaa na ubebaji WA magendo kama vile madawa ya KULEVYA, Heroin Cocain Bangi nk.

Mara nyingi Timu zimekuwa hasikaguliwi uwanja WA Ndege wameamua kutumia huo mwanya kubebe PODA.

Wanasingizia
1. Hali ya HEWA nzuri..
2. Uwepo wa viwanja vizuri vya Mazoezi.
3. Kuwepo kwa Facilities zote za mazoezi.
4.kuwa na Fedha kwa VILABU nk

ZILAANIWE TIMU ZOTE ZENYE TABIA ZA KISHENZI KAMA HIZI.

MAMLAKA AMKENI.
 
Tanzania hakuna timu tajiri, timu nyingi kama sio zote hazina misuli ya fedha za kusajili wachezaji wazuri sana na mabenchi ya ufundi class ya juu. Timu nyingi zinashindwa kuwalipa makocha na wachezaji signing fees zao na mishahara kwa wakati, wachezaji hawana bima na hazina viwanja vyao wenyewe. Kwa ujumla timu zetu zinaendeshwa kwa kubangaiza huku na kule; kwa maneno ya kimpira timu zetu ni feeder clubs kwa timu za kanda nyingine Afrika kutokana na umaskini wao.

Kwanini ni rahisi mno timu zetu kwenda kuweka kambi nje ya nchi lakini ni vigumu kusajili wachezaji wazuri, kulipa mishahara mikubwa ya wachezaji na benchi la ufundi au kujenga uwanja? Majibu ni mengi sana, mojawapo ya majibu hayo ni kwamba kuna uhusiano mkubwa sana kati timu kwenda pre-season za nje ya nchi na sababu za mtu kukubali kuidhamini timu. Sina ushahidi kamili, lakini pre-season hizi za hivi zina uhusiano mkubwa na biashara za magendo (smuggling), madawa ya kulevya au ukwepaji ushuru kwa kutumia jina la timu, wachezaji na benchi la ufundi. Akili ya kawaida tu haiwezi kuamini kwamba timu zetu zina fedha nyingi za kwenda kuweka kambi nje nchi lakini hazina fedha za kusajili wachezaji wazuri wa kuleta mataji.

Jeshi la uhamiaji na wadau wengine hebu tegeni mitego ya kunasa matunda ya pre-season za nje ya nchi kwa timu mbovu kabisa uwanjani na zinazolalamika kuwa hazina pesa za kulipa wachezaji, makocha, kusajili na kujenga viwanja vyao. Mnaweza kugundua chocholo za uovu kwenye hizi safari.
Eti timu zetu!,, zipi hizo ?.. lini utopolo mlikwenda nje ya nchi mkafanya pre season ukiachana na ile mliyolipiwa na waarabu,, kila mwaka excuse ile ile eti mda hautoshi, mlikuwa hamjui kuwa kuna pre season kabla ya msimu mpya kuanza ?..

Ifike wakati utopolo muelewe kuwa simba sio level yenu, kwa Tanzania ni Azam na Simba tu zenye misuli ya kifedha na uwezo wa kufanya watakalo,, hatuwezi kuwa sawa na timu inayotegemea kuuza magodoro iweze kujiendesha.. nadhani kwa sasa mmeelewa tuliposema bajeti yetu ya msimu ujao ni B23 tulikua tuna maanisha.

IKIUMA CHOMOA
 
Tanzania hakuna timu tajiri, timu nyingi kama sio zote hazina misuli ya fedha za kusajili wachezaji wazuri sana na mabenchi ya ufundi class ya juu. Timu nyingi zinashindwa kuwalipa makocha na wachezaji signing fees zao na mishahara kwa wakati, wachezaji hawana bima na hazina viwanja vyao wenyewe. Kwa ujumla timu zetu zinaendeshwa kwa kubangaiza huku na kule; kwa maneno ya kimpira timu zetu ni feeder clubs kwa timu za kanda nyingine Afrika kutokana na umaskini wao.

Kwanini ni rahisi mno timu zetu kwenda kuweka kambi nje ya nchi lakini ni vigumu kusajili wachezaji wazuri, kulipa mishahara mikubwa ya wachezaji na benchi la ufundi au kujenga uwanja? Majibu ni mengi sana, mojawapo ya majibu hayo ni kwamba kuna uhusiano mkubwa sana kati timu kwenda pre-season za nje ya nchi na sababu za mtu kukubali kuidhamini timu. Sina ushahidi kamili, lakini pre-season hizi za hivi zina uhusiano mkubwa na biashara za magendo (smuggling), madawa ya kulevya au ukwepaji ushuru kwa kutumia jina la timu, wachezaji na benchi la ufundi. Akili ya kawaida tu haiwezi kuamini kwamba timu zetu zina fedha nyingi za kwenda kuweka kambi nje nchi lakini hazina fedha za kusajili wachezaji wazuri wa kuleta mataji.

Jeshi la uhamiaji na wadau wengine hebu tegeni mitego ya kunasa matunda ya pre-season za nje ya nchi kwa timu mbovu kabisa uwanjani na zinazolalamika kuwa hazina pesa za kulipa wachezaji, makocha, kusajili na kujenga viwanja vyao. Mnaweza kugundua chocholo za uovu kwenye hizi safari.
Wauza ngada.
 
Kiongozi huko kwnye pre season ndo znakopatikana hizi pesa kidogo za kuendesha team ,hvi viingilio vya mlangoni hakuna kitu pale ,but kikubwa sisi mashabiki tunapenda sana kuona timu ikifanya vizuri na kuchukua makombe,mengine wala hatufikirii wala kuyajadiri
 
Huu ni wivu wa kimaskini na ukosefu wa maarifa. Kwani unadhani kwenda Uturuki kuweka kambi ni kiasi gani?

Nakumbuka Simba walipoenda Dubai watu walikuwa wanaleta gharama za kutisha wakati gharama za ile kambi ni za kawaida tu na kwa timu iliyo na utaratibu wa kawaida tu wa kifedha hawawezi kushindwa kufanya kitu kama hicho.

Kusajili mchezaji wa gharama kubwa unahitaji zaidi ya signing fee, unahitaji uweze kumlipa mshahara mkubwa pia, hili wengi mnasahau. Ongeza maarifa kabla haujaanza kutuhumu watu na taasisi bila kuwa na ushahidi.
 
Kama kusafiri tu kwenye mechi za Caf mnapanda ndege za abiria na mnakwenda kimafungu ndo mtaweza kwenda pre season nje ya nchi mkae wiki tatu ?
wafadhili wetu wanalalamika muda wote kuwa wanapata hasara kubwa, je, kwenda kupiga kambi nchi ya kigeni kunapunguzaje hasara hizo?
 
Huu ni wivu wa kimaskini na ukosefu wa maarifa. Kwani unadhani kwenda Uturuki kuweka kambi ni kiasi gani?

Nakumbuka Simba walipoenda Dubai watu walikuwa wanaleta gharama za kutisha wakati gharama za ile kambi ni za kawaida tu na kwa timu iliyo na utaratibu wa kawaida tu wa kifedha hawawezi kushindwa kufanya kitu kama hicho.

Kusajili mchezaji wa gharama kubwa unahitaji zaidi ya signing fee, unahitaji uweze kumlipa mshahara mkubwa pia, hili wengi mnasahau. Ongeza maarifa kabla haujaanza kutuhumu watu na taasisi bila kuwa na ushahidi.
Hii safari ya simba ime wauma sana, hususani baada ya kutangaziwa kuwa kikundi chao cha masela kitabakia kigamboni
 
Umejenga hoja nzuri sana mkuu, Uandishi wako pia ni mzuri.

Natamani tungekuwa na WATU wa aina yako kwa wingi hapa jukwaani ukiondoa wale WAJINGA wanaojaza Seva za Jamii forum.

Nikienda kwenye hoja Moja kwa Moja
Timu zinahusishaa na ubebaji WA magendo kama vile madawa ya KULEVYA, Heroin Cocain Bangi nk.

Mara nyingi Timu zimekuwa hasikaguliwi uwanja WA Ndege wameamua kutumia huo mwanya kubebe PODA.

Wanasingizia
1. Hali ya HEWA nzuri..
2. Uwepo wa viwanja vizuri vya Mazoezi.
3. Kuwepo kwa Facilities zote za mazoezi.
4.kuwa na Fedha kwa VILABU nk

ZILAANIWE TIMU ZOTE ZENYE TABIA ZA KISHENZI KAMA HIZI.

MAMLAKA AMKENI.
Kaka hakuna logic ya timu zetu "maskini" kuweka kambi nchi za nje, kuhusu
1. hali ya hewa: Tanzania ina aina zote za hali ya hewa za dunia hii (DSM, Bagamoyo, Makambako, Mufindi, Arusha, Karatu, Shinyanga, Kagera, Mbeya, Handeni,nk). Hata hivyo hali ya hewa ya preseason lazima ifanane na ile ya mashindano (ligi)

2. Viwanja vizuri: Preseason lazima ifanyike kweye viwanja vinavyofananafanana na viwanja vitakavyotumika kwenye mashindano (ligi husika). Unaenda ulaya kwenye viwanja vizuri halafu mechi utacheza manungu na majaliwa stadium wapi na wapi.

3. Swala la mazoezi ni swala endelevu kwenye msimu wote. Huwezi kwenda kufanya mazoezi kwenye vifaa ambavyo hutakuwanavyo wakati wa mashindano msimu mzima, sio kweli. Yaani ufanye mazoezi kule Uswis kwa wiki 3 tu yatakayodumu kwa mchezaji kwa msimu mzima kule tanzania, hii sio kweli.
4. Kuwa na fedha: Hii nayo sio kweli, timu zetu zinashindwa kusajili wachezaji wazuri sokoni kwasababu hazina fedha na kuwanunua na kuwalipa mishahara.

TRA, Uhamiaji na wadau wengine:
1. Kagueni kwelikweli mifuko na mabegi ya wachezaji, benchi la ufundi na viongozi wakati wa kwenda na kurudi preseason nje ya nchi.
2. Tikiseni mipira yooote wanayoenda na kurudi nayo safarini, msione haya kuipasua randomly michache kati ya hiyo.

3. timu na wachezaji wafuate taratibu zote sa kusafiri nje ya nchi.
 
Eti timu zetu!,, zipi hizo ?.. lini utopolo mlikwenda nje ya nchi mkafanya pre season ukiachana na ile mliyolipiwa na waarabu,, kila mwaka excuse ile ile eti mda hautoshi, mlikuwa hamjui kuwa kuna pre season kabla ya msimu mpya kuanza ?..

Ifike wakati utopolo muelewe kuwa simba sio level yenu, kwa Tanzania ni Azam na Simba tu zenye misuli ya kifedha na uwezo wa kufanya watakalo,, hatuwezi kuwa sawa na timu inayotegemea kuuza magodoro iweze kujiendesha.. nadhani kwa sasa mmeelewa tuliposema bajeti yetu ya msimu ujao ni B23 tulikua tuna maanisha.

IKIUMA CHOMOA
sawa hatujasema msiende, lakini tunasema mkaguliwe kwelikweli kila pahala. Haiwezekani timu inakutia hasara lakini kambi iwe ulaya. Wasiwasi ndio akili.
 
Kiongozi huko kwnye pre season ndo znakopatikana hizi pesa kidogo za kuendesha team ,hvi viingilio vya mlangoni hakuna kitu pale ,but kikubwa sisi mashabiki tunapenda sana kuona timu ikifanya vizuri na kuchukua makombe,mengine wala hatufikirii wala kuyajadiri
utashangaa familia moja tu hiyohiyo, kabila moja tu hilohilo miaka nenda rudi ndo wanaipenda hizi timu, kuna nini hapa? ni kweli wanazipenda sanabhizi timu au ni kama lubricant tu?
 
Huu ni wivu wa kimaskini na ukosefu wa maarifa. Kwani unadhani kwenda Uturuki kuweka kambi ni kiasi gani?

Nakumbuka Simba walipoenda Dubai watu walikuwa wanaleta gharama za kutisha wakati gharama za ile kambi ni za kawaida tu na kwa timu iliyo na utaratibu wa kawaida tu wa kifedha hawawezi kushindwa kufanya kitu kama hicho.

Kusajili mchezaji wa gharama kubwa unahitaji zaidi ya signing fee, unahitaji uweze kumlipa mshahara mkubwa pia, hili wengi mnasahau. Ongeza maarifa kabla haujaanza kutuhumu watu na taasisi bila kuwa na ushahidi.
Hivi ninyi mnadhani Kina Gharib na Mo ni wajinga kama ninyi? Wenzenu wanatumia fedha lakini wanajua wanachopata kama return. Japokuwa timu haziwangizii fedha direct lakini kwa kujihusisha na hizo timu wanapata faida nyingi mno. Hawa watu wanatumiwa na watawala kushika raia masikio na in return wanaachiwa kufanya makandokando yao wanayotaka. Ona sasa raia wote wameshikwa utumwa wa akili kwenye Yanga na Simba huku watu wanafanya yao kuchuma kupitia raslimali za nchi.
 
Huu ni wivu wa kimaskini na ukosefu wa maarifa. Kwani unadhani kwenda Uturuki kuweka kambi ni kiasi gani?

Nakumbuka Simba walipoenda Dubai watu walikuwa wanaleta gharama za kutisha wakati gharama za ile kambi ni za kawaida tu na kwa timu iliyo na utaratibu wa kawaida tu wa kifedha hawawezi kushindwa kufanya kitu kama hicho.

Kusajili mchezaji wa gharama kubwa unahitaji zaidi ya signing fee, unahitaji uweze kumlipa mshahara mkubwa pia, hili wengi mnasahau. Ongeza maarifa kabla haujaanza kutuhumu watu na taasisi bila kuwa na ushahidi.
Unaonaje kama hiyo pesa ndogo unayosema ingewekezwa kwenye ununuzi wa matofali ya kujenga uwanja wa club au hostel za wachezaji au ununuzi wa vifaa vya kisasa kwenye gym za timu? wasiwasi ndo akili.
 
Hii safari ya simba ime wauma sana, hususani baada ya kutangaziwa kuwa kikundi chao cha masela kitabakia kigamboni
Pre-season kingekuwa kipindi cha wachezaji wapya wa kigeni (kama wapo) kuja tanzania kuzoea hali ya hewa, hali ya viwanja na vyakula kabla ya msimu kuanza rasmi. Hovyo kabisa kusajili mchezaji mgeni na kumpeleka uturuki badala ya kumtembeza kule ihefu, singida, kiwangwa na Geita ambako ligi itachezwa. Yaani hiyo inaitwa macho komchuzi mkono koubwabwa. Think globally and act locally. Hata timu za ulaya zinaweka preseason kwenye nchi zenye hali ya hewa, viwanja na standard sawa na kwao ambako ligi itakwenda kuchezwa.
 
Hivi ninyi mnadhani Kina Gharib na Mo ni wajinga kama ninyi? Wenzenu wanatumia fedha lakini wanajua wanachopata kama return. Japokuwa timu haziwangizii fedha direct lakini kwa kujihusisha na hizo timu wanapata faida nyingi mno. Hawa watu wanatumiwa na watawala kushika raia masikio na in return wanaachiwa kufanya makandokando yao wanayotaka. Ona sasa raia wote wameshikwa utumwa wa akili kwenye Yanga na Simba huku watu wanafanya yao kuchuma kupitia raslimali za nchi.
ongeza sauti
 
Back
Top Bottom