Kuna siri gani kwenda Pre-Season nje ya nchi kwa timu masikini?

Kuna siri gani kwenda Pre-Season nje ya nchi kwa timu masikini?

Pre-season kingekuwa kipindi cha wachezaji wapya wa kigeni (kama wapo) kuja tanzania kuzoea hali ya hewa, hali ya viwanja na vyakula kabla ya msimu kuanza rasmi. Hovyo kabisa kusajili mchezaji mgeni na kumpeleka uturuki badala ya kumtembeza kule ihefu, singida, kiwangwa na Geita ambako ligi itachezwa. Yaani hiyo inaitwa macho komchuzi mkono koubwabwa. Think globally and act locally. Hata timu za ulaya zinaweka preseason kwenye nchi zenye hali ya hewa, viwanja na standard sawa na kwao ambako ligi itakwenda kuchezwa.
Ingekuwa ndo Yanga anakwenda Uturuki kufanya pre season ungeandika yote haya ??
 
Ingekuwa ndo yanga anakwenda uturuki kufanya pre season ungeandika yote haya ??
Ningeandika pia, maana najua yanga haina hata uwanja wa kupigia pushup wachezaji, lakini pia ina wachezaji wapya wa kigeni ambao ingekuwa fursa yao kuja nchini mapema na kuzoea hali ya hewa, vyakula na viwanja kabla ya ligi kuanza.
 
Timu ilikwenda Dubai na Robertihno, je matokeo yake baada ya kurudi tz mnayajua? mnayakumbuka?
 
Hizi timu mbili Ni dili kwa magabachori Ni mwendo Wa utakatishaji fedha haramu ukienda undercover kuna madudu we usione juu tuu
 
Unaonaje kama hiyo pesa ndogo unayosema ingewekezwa kwenye ununuzi wa matofali ya kujenga uwanja wa club au hostel za wachezaji au ununuzi wa vifaa vya kisasa kwenye gym za timu? wasiwasi ndo akili.
Unawapangia wewe ni nani? Siyo hata mshabiki wa timu, achilia mbali kuwa mwanachama ila unataka wafanya mambo kulingana na matakwa yako. Hii ni ajabu sana.
 
Kaka hakuna logic ya timu zetu "maskini" kuweka kambi nchi za nje, kuhusu
1. hali ya hewa: Tanzania ina aina zote za hali ya hewa za dunia hii (DSM, Bagamoyo, Makambako, Mufindi, Arusha, Karatu, Shinyanga, Kagera, Mbeya, Handeni,nk). Hata hivyo hali ya hewa ya preseason lazima ifanane na ile ya mashindano (ligi)
2. Viwanja vizuri: Preseason lazima ifanyike kweye viwanja vinavyofananafanana na viwanja vitakavyotumika kwenye mashindano (ligi husika). Unaenda ulaya kwenye viwanja vizuri halafu mechi utacheza manungu na majaliwa stadium wapi na wapi.
3. Swala la mazoezi ni swala endelevu kwenye msimu wote. Huwezi kwenda kufanya mazoezi kwenye vifaa ambavyo hutakuwanavyo wakati wa mashindano msimu mzima, sio kweli. Yaani ufanye mazoezi kule Uswis kwa wiki 3 tu yatakayodumu kwa mchezaji kwa msimu mzima kule tanzania, hii sio kweli.
4. Kuwa na fedha: Hii nayo sio kweli, timu zetu zinashindwa kusajili wachezaji wazuri sokoni kwasababu hazina fedha na kuwanunua na kuwalipa mishahara.

TRA, Uhamiaji na wadau wengine:
1. Kagueni kwelikweli mifuko na mabegi ya wachezaji, benchi la ufundi na viongozi wakati wa kwenda na kurudi preseason nje ya nchi.
2. Tikiseni mipira yooote wanayoenda na kurudi nayo safarini, msione haya kuipasua randomly michache kati ya hiyo.

3. timu na wachezaji wafuate taratibu zote sa kusafiri nje ya nchi.
Kweli mkuu na waturuki wanapenda Bangi si mchezooo.
 
Eti timu zetu!,, zipi hizo ?.. lini utopolo mlikwenda nje ya nchi mkafanya pre season ukiachana na ile mliyolipiwa na waarabu,, kila mwaka excuse ile ile eti mda hautoshi, mlikuwa hamjui kuwa kuna pre season kabla ya msimu mpya kuanza ?..

Ifike wakati utopolo muelewe kuwa simba sio level yenu, kwa Tanzania ni Azam na Simba tu zenye misuli ya kifedha na uwezo wa kufanya watakalo,, hatuwezi kuwa sawa na timu inayotegemea kuuza magodoro iweze kujiendesha.. nadhani kwa sasa mmeelewa tuliposema bajeti yetu ya msimu ujao ni B23 tulikua tuna maanisha.

IKIUMA CHOMOA
nyie mnasafirisha ngada za mhindi tu hamna lolote...
 
Unawapangia wewe ni nani? Siyo hata mshabiki wa timu, achilia mbali kuwa mwanachama ila unataka wafanya mambo kulingana na matakwa yako. Hii ni ajabu sana.
kwahiyo ni timu ya mazombie? tunaandika haya kwakuwa huenda dawa za kulenya kwa vijana wetu zinapitia mlango huu, na madini yetu na pembe za faru wetu vikaondokea mlango huuhuu. Wasiwasi ndio akili bro, nothing more nothing less.
 
Kweli mkuu na waturuki wanapenda Bangi si mchezooo.
Waturuki wako karibu na Afghanistan, Pakistan, nk ziliko ngada. Wasiwasi ndio akili. Kwanini timu haziendi nchi kama Israel na nyingine ambazo ngada hazipatikani kwa urahisi? Kwanini ni uturuki, dubai, tunisia, morocco, brazil, Colombia, nk?
 
Hizi ni dili za watu kujipatia marupu rupu ya ziada koo haliwezi kukwepeka, watasema hawana hela ya kumsajili mchezaji wa milion 500 lakini wanaenda pre season ya milion 700.

Kumbe kuna 10% zao kwenye pre season ni tofauti na usajili ambapo hawana 10%
 
Hii safari ya simba ime wauma sana, hususani baada ya kutangaziwa kuwa kikundi chao cha masela kitabakia kigamboni
Msimu uliuopita Yanga alinangwa hivi hivi kwa kubakia Kigamboni wakati Simba akienda nchi zaidi ya mbili katika pre season lakini mwisho wa siku aliyebakia Kigamboni ndiye aliyebakia hadi fainali mashindano ya CAFCC, bingwa wa NBC premier league, na bingwa wa Azam Federation cup. Endeleeni kujivunia pre season tu
 
Hizi ni dili za watu kujipatia marupu rupu ya ziada koo haliwezi kukwepeka, watasema hawana hela ya kumsajili mchezaji wa milion 500 lakini wanaenda pre season ya milion 700.

Kumbe kuna 10% zao kwenye pre season ni tofauti na usajili ambapo hawana 10%
Mwisho wa siku wanasajili akina Akpan, sawadogo, okwa, dejan kwa bei ndogo kabisa na kumpa Ahmed Ally awapake mafuta wauzike kwa mashabiki.
 
kwahiyo ni timu ya mazombie? tunaandika haya kwakuwa huenda dawa za kulenya kwa vijana wetu zinapitia mlango huu, na madini yetu na pembe za faru wetu vikaondokea mlango huuhuu. Wasiwasi ndio akili bro, nothing more nothing less.
Kwa hiyo umekaa hapo unahofu Shomari Kapombe anatorosha pembe za ndovu na hayo yote unaamini yanasubiri wakati wa pre-season tu ila msimu mzima timu zinaposafiri ikiwemo Yanga hauna wasiwasi? Wewe hauna wasiwasi, bali una upungufu wa maarifa ukichanganya na wivu.
 
Umejenga hoja nzuri sana mkuu, Uandishi wako pia ni mzuri.

Natamani tungekuwa na WATU wa aina yako kwa wingi hapa jukwaani ukiondoa wale WAJINGA wanaojaza Seva za Jamii forum.

Nikienda kwenye hoja Moja kwa Moja
Timu zinahusishaa na ubebaji WA magendo kama vile madawa ya KULEVYA, Heroin Cocain Bangi nk.

Mara nyingi Timu zimekuwa hasikaguliwi uwanja WA Ndege wameamua kutumia huo mwanya kubebe PODA.

Wanasingizia
1. Hali ya HEWA nzuri..
2. Uwepo wa viwanja vizuri vya Mazoezi.
3. Kuwepo kwa Facilities zote za mazoezi.
4.kuwa na Fedha kwa VILABU nk

ZILAANIWE TIMU ZOTE ZENYE TABIA ZA KISHENZI KAMA HIZI.

MAMLAKA AMKENI.
Sina hakika na mwendelezo wa hili baada ya kipindi Hali hii iliposhamiri kushitukiwa na serikali. Enzi za Abbas Gulamali na Azim Dewji hii Hali ilikuwa juu Sana. Timu iliweza kusafiri na mipira 30 ya mazoezi wakirudi Wanarudi na mipira mipya 30. Mambo yalikuwa mengi kipindi hicho cha Giza Ila sijui kama mpaka Leo bado wanaendelea.
Nikija Kwa hoja ya mleta Uzi kuhusu timu kwenda nje huku ikishindwa kusajili Wachezaji wazuri Kwa hela kubwa, nadhani hili amelijibu mwenyewe. Safari za pre-season zinadhaminiwa na Mtu Kwa malengo na faida yake ya kibiashara. Kwa hiyo anayemlipa Mpiga Ngoma ndiye anayechagua wimbo.
 
Umejenga hoja nzuri sana mkuu, Uandishi wako pia ni mzuri.

Natamani tungekuwa na WATU wa aina yako kwa wingi hapa jukwaani ukiondoa wale WAJINGA wanaojaza Seva za Jamii forum.

Nikienda kwenye hoja Moja kwa Moja
Timu zinahusishaa na ubebaji WA magendo kama vile madawa ya KULEVYA, Heroin Cocain Bangi nk.

Mara nyingi Timu zimekuwa hasikaguliwi uwanja WA Ndege wameamua kutumia huo mwanya kubebe PODA.

Wanasingizia
1. Hali ya HEWA nzuri..
2. Uwepo wa viwanja vizuri vya Mazoezi.
3. Kuwepo kwa Facilities zote za mazoezi.
4.kuwa na Fedha kwa VILABU nk

ZILAANIWE TIMU ZOTE ZENYE TABIA ZA KISHENZI KAMA HIZI.

MAMLAKA AMKENI.
Yaweza kuwa kweli
 
Ningeandika pia, maana najua yanga haina hata uwanja wa kupigia pushup wachezaji, lakini pia ina wachezaji wapya wa kigeni ambao ingekuwa fursa yao kuja nchini mapema na kuzoea hali ya hewa, vyakula na viwanja kabla ya ligi kuanza.
Basi kaa kimya ya simba hayakuhusu dili na utopolo walioabakia kigamboni
 
Back
Top Bottom