Kuna tetesi Dunia inafikia ukomo, Masiha anarudi?

Kuna tetesi Dunia inafikia ukomo, Masiha anarudi?

itakuwa ni kitendo cha kufumba na kufumbua kope/eye blink speed..cha haraka sana speed kubwa sana.

Kitajulikana kwa sababu itakuwa watu wawili wakiwa shambani wanalima mmoja atanyakuliwa mmoja ataachwa,wawili watakuwa shambani mmoja atanyakuliwa mmoja ataachwa.Watu wataarifiana kuhusu taarifa za kupotea kwa watu dunia mtaani,mkoa,nchi nzima na dunia kwa ujumla itarepotiwa watu kupotea na kuna watashuhudia nguo zimebaki watu hawapo au kama mlikuwa mnafanya jambo pamoja mnaona mtu anavanish chap si mnashuhudia na ukiuliza na kwingine habari zitatapakaa dunia nzima.
Then kuanzia hapo sasa NEEMA ILE NEEMA INAYOZUIA MABAYA ya wale watu wa Mungu ndio waliokuwa wanatulinda sisi kupitia maombi yao na uwepo wao na Mungu alikuwa anazuia mabaya yasiwapate kanisa lake watu wake na sisi tunanufaikamo,na mvua alikuwa anawanyeshea wema na sisi wabaya tunanufaikamo(wema na wabaya wote tunapata mvua.)
Na shetani na malaika zake walikuwa wanafungiwa kuzimu kwa ajili ya kuwalinda watu wake na sisi tunanufaikamo.
Na hiyo neema ipo mpaka sasa inatusubiri hata sisi wenye dhambi tutubu tuingie kuwa wamoja ya watoto wake kanisa lake kondoo wake tuache dhambi atusamehe.
BAADA YA UNYAKUO KUCHUKUA WATU WAKE...ile neema itaondolewa au itapungua ina maana wataobaki walioachwa duniani kuna baadhi watavumilia mateso ya miaka 7/2 nusu ya miaka 7 ilifupishwa kutoka 7,kama ingekuwa 7 hakuna angeweza vumilia,so watakaovumilia hata mauti yao bila kumkufuru Yesu na kumsujudia SHETANI watakao itetea imani yao wakivumilia mateso nao baada ya kufa Roho zao zitaingia mbinguni zikaungane na wale walionyakuliwa washerehekee kwa miaka 1000 toka ile siku ya unyakuo katika karamu ya watakatifu mbinguni washindi wateule.

Baada ya miaka 3.5 ya dhiki kuu...na miaka 1000 ya karamu ya watakatifu mbinguni wakati huo wenye dhambi wako kuzimu ya duniani wakiteseka .

Yesu atarudi kuhukumu ulimwengu mara ya tatu akiwa na jeshi la watakatifu na malaika.Wema PEPONI na wenye dhambi katika ziwa la moto na shetani na mapepo majini.

BAADA YA HAPO Yesu atakuwa amemaliza kazi yake aliyotumwa na Mungu Baba,KAZI GANI hiyo 1)Alishiriki kumuumba binadamu mbinguni akishirikiana na Mungu baba na Roho Mtakatifu.2)Alikuja duniani katika umbo la binadamu akasulibiwa msalabani akateswa akafanyika kafara kwa ajili ya kumkomboa mwanadamu kupitia damu yake ili kila mtu kupitia yeye aokolewe kutoka dhambi atubu dhambi,amkubali Yesu..NDIO KIPINDI TULICHOPO cha hii neema ya bure inatusibiri walioko baa,lodge,wanaowanga,wezi,waasherati,wachawi,wote tunasubiriwa na hii neema ya bure...ila hii neema ina mwisho wake tusichelewe
3)UNYAKUO ..ndio huu umekaribia...neema itaondolewa.
Asante mtumishi
 
Pia tujue hili,

Unyakuo utaanza kwanza Kisha maisha ya taabu na dhiki kuu yataanza rasmi duniani WATAKATIFU wakiwa mapumzikoni.

Baada ya miaka elfu , Yesu atakuja kuwachukua na kufufuka waliowake washindao mateso ya dhiki kuu.

Baada ya hapo ndipo ataihukumu Dunia na Ulimwengu kutupwa Ziwa la moto jehanum baada ya kuhukumu.
Imani yetu ya kikristo imejaa mikanganyiko mingi kiasi kwamba wanazuoni wakristo wenyewe kwa wenyewe hawaelewani. Hata unachoongea hapa ni mrengo wa PRE-TRIBULATION RAPTURE kwenye Teolojia. Mwingine anaamini kwenye POSTTRIBULATION RAPTURE., mwingine MIDTRIBULATION RAPTURE. Ukija kwenye Teolojia ya kikatoliki hakuna unyakuo. Na wote hao ati ni wakristo na kila mmoja anajiona ndio yuko sahihi zaidi. Na wote hao wanadai wanaongozwa na roho mtakatifu kuujua ukweli. Upuuzi mtupu. Mbona Yesu mwenyewe amesema ufalme uliogawanyika hauwezi kusimama. Achana na hizo tabiri za mwisho wa dunia ishi maisha adilifu basi yatosha. Whether the world will end tomorrow or will last forever hilo halitakusumbua. Hizo doomsday zilitabiriwa nyingi zikapita and nothing happened. Ni ujinga tu.
 
Pengine wewe bado mtoto mdogo wa 2000, ila sie wazee wako tulishaahidiwa na manabii wa kizazi kipya kuwa mwisho wa dunia ulikuwa mwaka 1978, wakachemka tena na kusema mwaka 1982 mara 1999......cha kushangaza mpaka leo bado tunapeta tu na kugawana dhambi according to dini za kuletewa.
Kweli huyu atakuwa wa kizazi cha 2000. Akina HELLEN WHITE na wenzake wa Sabato walishatabiri mwisho wa dunia karne ile ya 19 wakaangukia pua wakajaribu kubadilisha tarehe lakini holaaa. Tuache haya mambo ya kijinga.
 
Acha kujidanganya mkuu, Yesu hawez kurudi.

Tena Kwa wayahudi tulionao sahivi, watampiga Yesu makombora mpk achakae.

Bora kina Pilato walimhurumia wakamgonga misumari nchi 6 mikonini na miguuni Ila wakauacha mwili wake angalau unatambulika ukiutizama

Ila Kina Netanyau hawacheki na kima, wataulipua,kuuchakaza na kuufukia na vifusi vya Gaza.
😂😂😂😂😂😂😂😂 Kwahio Netanyahu atamnyoosha
 
Kuna mtu aliwahi kuniambia kuwa mwisho wa dunia ni pale pumzi yako inapokata. Otherwise dunia itaendelea kuwepo tu.

Naanza kumuelewa sasa.
 
Kuna taarifa za kushangaza huko USA inasemekana mwisho wa Dunia (doomsday) ni karibu mno na kizazi hiki kitashuhudia Yesu anarudi stay tuned kwa ushahidi.
Matayo 16:28
 

Attachments

  • 061392C4-ED1B-4797-B987-ABE948D4A134.jpeg
    061392C4-ED1B-4797-B987-ABE948D4A134.jpeg
    55.4 KB · Views: 1
Kuna mtu aliwahi kuniambia kuwa mwisho wa dunia ni pale pumzi yako inapokata. Otherwise dunia itaendelea kuwepo tu.

Naanza kumuelewa sasa.
Ni msemo wa mababu wa siku nyingi sana. Wewe ukifa na dunia yako imefika mwisho. Doomsday ni hadithi za kipumbavu tu. Mara sijui kuna Asteroid itaipiga dunia mwisho wa mwaka 2024! Iko wapi? Asteroids zinapita kivyao kwenye orbit zao and nothing happens. Yaani ulevi wa dini ni afadhali unywe safari lager ukalale zako. Ni uraibu mbaya kuliko uraibu mwingine wowote. Unafanywa ndondocha na una Ph.D yako uliyoisotea miaka mitano kuandika thesis😆
 
Ni msemo wa mababu wa siku nyingi sana. Wewe ukifa na dunia yako imefika mwisho. Doomsday ni hadithi za kipumbavu tu. Mara sijui kuna Asteroid itaipiga dunia mwisho wa mwaka 2024! Iko wapi? Asteroids zinapita kivyao kwenye orbit zao and nothing happens. Yaani ulevi wa dini ni afadhali unywe safari lager ukalale zako. Ni uraibu mbaya kuliko uraibu mwingine wowote. Unafanywa ndondocha na una Ph.D yako uliyoisotea miaka mitano kuandika thesis😆
😆😆😆😆😆😆 Bora safari ukiamka unakuwa mpya
 
Una akili mdogo sana ,Kurud Kwa Yesu hakutakua Kwa kinyonge na ufukara kama unavyowaza kiufukara itakua ni tukio la kutisha mnoo.. kama unadhan natania kawaulize wale walinzi pale kaburini wakati anafufuka yaan walkua kama wafu wakat Mwanaume anafufuka palikua hapatoshi ,Kwa iyo hayo mabomu ya Netenyau yenyewe yatasema Yesu amerudi ,miti itasema Yesu amerudi,mamba itakiri Yesu amerudi ,Samia,Museven,Ruto,kagame,askofu, Sheikhe ,imamu,Mufti woooote watasema Yesu amerudi kulichukua kanisa, ng'ombe wako kuku,meza kabati, vijiko, kitanda vyooote vitasema ni mwisho wa Dunia
Watu wanajua Bwana Yesu ni mnyonge hawafikiri hayupo duniani lakini Jina lake likitajwa mapepo hanatetemeka.. Sasa hawajui ni zaidi ya atakayokuja mwenyewe
 
Back
Top Bottom