Kuna tofauti kati ya VAR na Goal Line Technology

Mayu

JF-Expert Member
Joined
May 11, 2010
Posts
7,621
Reaction score
12,505
Michuano ya CCL hawatumii Goal line technology ambayo ingemaliza huu utata

CCL wanatumia VAR peke yake kusaidia kutoa maamuzi

Angalia Goal line technology ilivyotumika kwenye hii video fupi hapo chini

Utaona ni jinsi gani mpira unatakiwa uwe umeingia kwa asilimia 100 ili kuhesabika goli

So ukiangalia kwa haraka lile shuti lilikua ni kali sana kiasi kwamba unahitaji umakini kuchukua picha exactly pale mpira ulipo dunda na kurudi juu.

Ukichukua picha wakati mpira umekwisha dunda au kabla haujadunda ni lazima mpira utaonekana umevuka mstari kwa asilimia 100

Lakini ukichukua picha mpira unapodunda utaona uligusa mstari

Angalia picha hapo chini, moja mpira ulipodundia na nyingine ni mpira kabla au baada ya kudunda

Mwisho tujikumbushe kidogo kuhusu sheria inasemaje kuhusu mpira kuhesabika kuwa umeingia na kuwa goli.... ni lazima mpira wote uingie na sio asilimia 99.9.

Angalia picha za sheria za goli.

 

Attachments

  • IMG_4760.mov
    7.8 MB
Lile la jana kwenye game ya Yanga na Mamelodi ukiweka mahaba pembeni sio goli...ila watu wanaangepaste katika angel ambayo unaliona goli ila ule mpira haukuvuka mstari wote aslimia mia...ila mashabaki wamepata kichaka chao....nakumbuka hata kombe la dunia 2022 game ya spain na China utata kama huo ulikuwepo.
 
Nilijuwa unaleta video kumbe umeleta hizi takataka za kuokota mitandaoni?

Kilichomshinda refa kwenda kureview VAR ni kitu gani?
 
Macho Yako hayako sawa utakuwa na makengeza wewe!
View attachment 2955750
 
Acha ubishi ndugu yangu.
Nini kuhusu picha wakati video zote zinaonyesha mpira wote kwa 100% ulikuwa ndani.
Marefa wa jana walizingua kukataa lile goli.
Utopolo walinyongwa kihuni na sio kisoka.
 
Ficha unazi
 
Itoshe kusema huna akili!
 
Vyura wamechafukwa utaambulia matusi ya mwilini mkuu
 
Ushabiki wa waswahili unatufanya kuwa vipofu wa kuukataa ukweli hata kama tumeuona dhahiri.

Kwa kuliona hili binafsi nilishachagua kuwa neutral katika kila jambo ili niweze kuwa huru kutika kufikiri, kuona, kutenda, kusema na kusimama katika ukweli. Ndo maana sinaga utimu utimu, ambao naamini unapumbaza kwa viwango tofauti kulingana na mhusika. Kuna wanaopumbazwa sana, wastani, na wachache sana hawapumbazwi kabisa licha ya kuwa na utimu wao.

Ukweli ni kwamba bao la Aziz Ki jana halikuwa na utata wowote hata kwa macho linaonekana, ila kile kigugumizi cha matumizi ya VAR technology kilikuwa dhahiri kabisa kiasi wakati marudio yanafanyika watu wanashangilia nilikuwa nawasikitikia nikijisemea "ngoja mshangazwe".

Ukitaka uuone vema utambulisho wa mwafrika mwezeshee mazingira ya haki kuonekana dhahiri. Hatojali, badala yake ataisigina hata mchana kweupe, mbele ya kila jicho, na bila hata chembe ya soni.

In short kuna vitu Africa bado hatujawa na ustaarabu wa kutosha kuwa navyo. Mojawapo ni hizo teknolojia kama VAR. Kuna game moja niliona mwanzoni hivi wakati ndo VAR inaingia Afrika, refarii kaenda kucheck zaidi ya dakika nzima anarudi na maamuzi ya penati kuwa mchezaji kaugusa mpira kwa kiwiko wakati mikono yake ilikuwa juu na mpira ulikuwa kwa chini maeneo ya goti! Hakukuwa hata na ujirani kati ya mpira na mikono, ila mmakonde akaamua ni tuta tena kwa msisitizo wa vitendo.
 
We differ in thinking capacity and on handling things
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…