Kuna Tofauti kubwa ya wadau wa upinzani wa Kaskazini na sehemu nyingine

Kuna Tofauti kubwa ya wadau wa upinzani wa Kaskazini na sehemu nyingine

Kamundu

Platinum Member
Joined
Nov 22, 2006
Posts
7,823
Reaction score
10,857
Nashangaa mpaka leo bado CCM na viongozi wa Serikali hawajajua tofauti ya wapinzani wa kaskazini na wa sehemu nyingine kama Kigoma au Mbeya

Huku Arusha, Kilimanjaro na Tanga tatizo kubwa sio barabara au madarasa ya shule. Ni sehemu ambayo ilikuwa na barabara nyingi za lami na shule nyingi ukilinganisha na sehemu nyingine lakini kulikuwa na wapinzani wengi.

Hivyo Rais Samia anavyoringia barabara na kujidanganya kwamba watu wamebadilika sio kweli watu wako vilevile.

Jamii ya huku Kaskazini tatizo lao na Serikali ni kwamba Serikali imekuwa kikwazo kikubwa kwa biashara. Serikali imeingilia biashara za madini kuwa na mpangilio, tozo biashara za utalii na hoteli. Lakini hii mikoa ya mipakana haipendi kusumbuliwa kwenye biashra za mpakani kama kuuza mahindi, vitunguu na kupita kwa magari.

Kwa ufupi watu wa Kaskazini wanataka Serikali ambayo ni pro-business na yenye mazingira mazuri ya biashara.

Wengi wa Kaskazini wanaamini vitu vingi wanaweza kufanya bila serikali lakini wanataka serikali isiwe vikwazo.

Upinzani wa sehemu nyingine kama Kigoma ni kutokana na serikali kuwasahau na kuona kama vile wenyewe hawapewi maendeleo kama barabara, reli, mazao yao, na ziwa Tanganyika. Lakini Mbeya nayo ni hivyo hivyo ni maendeleo ya barabara na maji ndiyo tatizo.

Hivyo Rais Samia kwenda Arusha na kuongea kuhusu maji kuliko biashara ni kutokujua jamii ya Kaskazini

Ili kutoa ukabila nijitambulishe mimi mwenyewe. Mimi nimekulia Arusha na Baba Mpare na Mama Mchagga hivyo nimechanganya kama wengine wengi
 
Nashangaa mpaka leo bado CCM na viongozi wa Serikali hawajajua tofauti ya wapinzani wa kaskazini na wa sehemu nyingine kama Kigoma au Mbeya

Huku Arusha, Kilimanjaro na Tanga tatizo kubwa sio barabara au madarasa ya shule. Ni sehemu ambayo ilikuwa na barabara nyingi za lami na shule nyingi ukilinganisha na sehemu nyingine lakini kulikuwa na wapinzani wengi.

Hivyo Rais Samia anavyoringia barabara na kujidanganya kwamba watu wamebadilika sio kweli watu wako vilevile.

Jamii ya huku Kaskazini tatizo lao na Serikali ni kwamba Serikali imekuwa kikwazo kikubwa kwa biashara. Serikali imeingilia biashara za madini kuwa na mpangilio, tozo biashara za utalii na hoteli. Lakini hii mikoa ya mipakana haipendi kusumbuliwa kwenye biashra za mpakani kama kuuza mahindi, vitunguu na kupita kwa magari.

Kwa ufupi watu wa Kaskazini wanataka Serikali ambayo ni pro-business na yenye mazingira mazuri ya biashara.

Wengi wa Kaskazini wanaamini vitu vingi wanaweza kufanya bila serikali lakini wanataka serikali isiwe vikwazo.

Upinzani wa sehemu nyingine kama Kigoma ni kutokana na serikali kuwasahau na kuona kama vile wenyewe hawapewi maendeleo kama barabara, reli, mazao yao, na ziwa Tanganyika. Lakini Mbeya nayo ni hivyo hivyo ni maendeleo ya barabara na maji ndiyo tatizo.

Hivyo Rais Samia kwenda Arusha na kuongea kuhusu maji kuliko biashara ni kutokujua jamii ya Kaskazini

Ili kutoa ukabila nijitambulishe mimi mwenyewe. Mimi nimekulia Arusha na Baba Mpare na Mama Mchagga hivyo nimechanganya kama wengine wengi

Wenda uko wrong. Ingekuwa hivyo mbona hizo 560 B zilizotolewa hazijapigiwa kelele. Ziende hizohizo zikatolewe kanda ya ziwa ungesikia makelele ya kufa mtu.

Tatizo la huko kaskazini ni kutaka kujifanya mifano ya nchi kwamba barabara ya rami hadi vijijini migombani, hamna nyumba ya tembe. Lakini wakijaribu kunyanyua kwingine angalau kuwe kuwe ni vita kali maana you are threatening their dominance .

Haja ya wana kaskazini ni kuwa na serikali yenye upendeleo maalum kwao yani kwamba bila hivyo hata ufanye nini unajisumbua tu kwao.
 
Wenda uko wrong. Ingekuwa hivyo mbona hizo 560 B zilizotolewa hazijapigiwa kelele. Ziende hizohizo zikatolewe kanda ya ziwa ungesikia makelele ya kufa mtu.

Tatizo la huko kaskazini ni kutaka kujifanya mifano ya nchi kwamba barabara ya rami hadi vijijini migombani, hamna nyumba ya tembe. Lakini wakijaribu kunyanyua kwingine angalau kuwe kuwe ni vita kali maana you are threatening their dominance .

Haja ya wana kaskazini ni kuwa na serikali yenye upendeleo maalum kwao yani kwamba bila hivyo hata ufanye nini unajisumbua tu kwao.
Sio kweli Mku.
Uhalisia uendane na mazingira kwani wafufue zao la kahawa
 
Kwa ufupi watu wa Kaskazini wanataka Serikali ambayo ni pro-business na yenye mazingira mazuri ya biashara.

Wengi wa Kaskazini wanaamini vitu vingi wanaweza kufanya bila serikali lakini wanataka serikali isiwe vikwazo.
👍
 
Nashangaa mpaka leo bado CCM na viongozi wa Serikali hawajajua tofauti ya wapinzani wa kaskazini na wa sehemu nyingine kama Kigoma au Mbeya

Huku Arusha, Kilimanjaro na Tanga tatizo kubwa sio barabara au madarasa ya shule. Ni sehemu ambayo ilikuwa na barabara nyingi za lami na shule nyingi ukilinganisha na sehemu nyingine lakini kulikuwa na wapinzani wengi.

Hivyo Rais Samia anavyoringia barabara na kujidanganya kwamba watu wamebadilika sio kweli watu wako vilevile.

Jamii ya huku Kaskazini tatizo lao na Serikali ni kwamba Serikali imekuwa kikwazo kikubwa kwa biashara. Serikali imeingilia biashara za madini kuwa na mpangilio, tozo biashara za utalii na hoteli. Lakini hii mikoa ya mipakana haipendi kusumbuliwa kwenye biashra za mpakani kama kuuza mahindi, vitunguu na kupita kwa magari.

Kwa ufupi watu wa Kaskazini wanataka Serikali ambayo ni pro-business na yenye mazingira mazuri ya biashara.

Wengi wa Kaskazini wanaamini vitu vingi wanaweza kufanya bila serikali lakini wanataka serikali isiwe vikwazo.

Upinzani wa sehemu nyingine kama Kigoma ni kutokana na serikali kuwasahau na kuona kama vile wenyewe hawapewi maendeleo kama barabara, reli, mazao yao, na ziwa Tanganyika. Lakini Mbeya nayo ni hivyo hivyo ni maendeleo ya barabara na maji ndiyo tatizo.

Hivyo Rais Samia kwenda Arusha na kuongea kuhusu maji kuliko biashara ni kutokujua jamii ya Kaskazini

Ili kutoa ukabila nijitambulishe mimi mwenyewe. Mimi nimekulia Arusha na Baba Mpare na Mama Mchagga hivyo nimechanganya kama wengine wengi


Ukiangalia wale wapinzani Ndesamburo alikuwa mfanyabiashara, Lema alikuwa mfanyabiashara, mbowe alikuwa mfanyabiashara sehemu nyingi hasa mijini wanapenda zaidi wafanyabiashara
 
Kamundu,

maoni yako yalinishangaza kidogo mpaka niliposoma kwamba umekulia ARUSHA. kwa msingi huo inawezekana hujaishi kabisa Upareni ingawa umejitambulisha kama baba yako ni Mpare na mama yako ni Mchagga. Ungeishi Upareni inawezekana kabisa usingekuwa hapo ulipo leo kwasababu wilaya ya Same ndio wilaya inayoshika mkia ktk matokeo ya mitihani ya kitaifa ktk mkoa wa Kilimanjaro.

nakuomba umsikilize mbunge wa Same Mashariki akielezea shida na changamoto wanazozipitia wananchi wa wilaya ya Same ambayo eneo lake ni asilimia 40% ya mkoa mzima wa Kilimanjaro. Wilaya ya Same ni wilaya iliyosahaulika Tanzania, sio Kilimanjaro peke yake.

 
jamani angalieni hapa mjifunze kuhusu Kilimanjaro. Kungekuwa na maendeleo yanayosema Mbunge asingedhalilika namna hii kuomba fedha za maendeleo. Kilimanjaro ni zaidi ya mnavyoisikia.



cc MkamaP, Kamundu
 
jamani angalieni hapa mjifunze kuhusu Kilimanjaro. Kungekuwa na maendeleo yanayosema Mbunge asingedhalilika namna hii kuomba fedha za maendeleo. Kilimanjaro ni zaidi ya mnavyoisikia.



cc MkamaP, Kamundu


Kipiga magoti ni fix tu, wewe hujafika mikoa mingine utalia kwa machozi wala utoleta tena hizi video. Kuna sehemu kufika hospitali ya wilaya unachukuliwa na machela km 100 kwa miguu porini kiza ka njia kamefunikwa na miti unapita kama kwenye tunnel ukifika hizo km 100 center unachukua bajaji km 20 inakufikisha mwaloni/ziwani kisha unachukuiwa na mtumbwi masaa 6 ukifika kando ya pili unachukua tena bajaji kufika hospital. Unafika hospital unakuta hakuna daktari kuna nesi mmoja manesi watatu wa maternity leave , mgonjwa anakosa huduma anafariki unaanza upya safari.
 
Kamundu,

maoni yako yalinishangaza kidogo mpaka niliposoma kwamba umekulia ARUSHA. kwa msingi huo inawezekana hujaishi kabisa Upareni ingawa umejitambulisha kama baba yako ni Mpare na mama yako ni Mchagga. Ungeishi Upareni inawezekana kabisa usingekuwa hapo ulipo leo kwasababu wilaya ya Same ndio wilaya inayoshika mkia ktk matokeo ya mitihani ya kitaifa ktk mkoa wa Kilimanjaro.

nakuomba umsikilize mbunge wa Same Mashariki akielezea shida na changamoto wanazozipitia wananchi wa wilaya ya Same ambayo eneo lake ni asilimia 40% ya mkoa mzima wa Kilimanjaro. Wilaya ya Same ni wilaya iliyosahaulika Tanzania, sio Kilimanjaro peke yake.



Sasa ni ajabu gani kwa ubunge kuomba maji au barabara!. Na unavyosema ni ya mwisho Kilimanjaro je ni ya ngapi kitaifa? Kilimanjaro wapo juu kielemu hivyo ukiwa wa mwisho haina maana kwa Tanzania nzima unafanya vibaya. Na nilichosema mimi ni kwamba matatizo ya watu wa kasikazini ni vikwazo je wewe unajuaje kama vikwazo havijachangia kutokupata maendleo hapo Same!
 
Kamundu,

sikiliza hapa swali la Mh.Naghenjwa Kaboyoka aliyekuwa mbunge wa Same Mashariki, na swali la nyongeza alilouliza Mh.Susan Lyimo kwa niaba ya Kaboyoka. Pia sikiliza kauli ya Spika kuhusu barabara za wilaya ya Same kuanzia dakika ya 3:59.

 
Kamundu,

sikiliza hapa swali la Mh.Naghenjwa Kaboyoka aliyekuwa mbunge wa Same Mashariki, na swali la nyongeza alilouliza Mh.Susan Lyimo kwa niaba ya Kaboyoka. Pia sikiliza kauli ya Spika kuhusu barabara za wilaya ya Same kuanzia dakika ya 3:59.



Haya ni mawazo yangu ni kwanini watu wa kaskazini wengi wanapenda upinzani zaidi. Kama wewe unaamini kama hao viongozi sawa haya ni mawazo yangu tu na najua yako sawa. Watu wa kule wananielewa wengine mnaweza msinielewe
 
Kipiga magoti ni fix tu, wewe hujafika mikoa mingine utalia kwa machozi wala utoleta tena hizi video. Kuna sehemu kufika hospitali ya wilaya unachukuliwa na machela km 100 kwa miguu porini kiza ka njia kamefunikwa na miti unapita kama kwenye tunnel ukifika hizo km 100 center unachukua bajaji km 20 inakufikisha mwaloni/ziwani kisha unachukuiwa na mtumbwi masaa 6 ukifika kando ya pili unachukua tena bajaji kufika hospital. Unafika hospital unakuta hakuna daktari kuna nesi mmoja manesi watatu wa maternity leave , mgonjwa anakosa huduma anafariki unaanza upya safari.

Wilaya ya Same hakuna barabara wala umeme mpaka migombani kama ambavyo watu wamekuwa wakihubiri kuhusu Kilimanjaro.
 
Haya ni mawazo yangu ni kwanini watu wa kaskazini wengi wanapenda upinzani zaidi. Kama wewe unaamini kama hao viongozi sawa haya ni mawazo yangu tu na najua yako sawa. Watu wa kule wananielewa wengine mnaweza msinielewe
wananchi wa wilaya ya Same wanapenda upinzani kwasababu serikali za CCM zimewatenga kwa kutowapelekea huduma mbalimbali za maendeleo. muamko wa maendeleo upo juu, lakini wananchi hawaungwi mkono na serikali, na ndio chanzo cha wabunge kama Anna Malecela kukataliwa ktk uchaguzi wa 2015 na 2020.
 
Mama kila anapofika Ni barabara na zahanati na madarasa

Watu wanataka kipato Cha mfukoni kipande

Mzunguko wa biashara na kazi za kueleweka

Watu wa mijini ndio maana hawaitaki kabisa ccm wengi wanaoshabikia ccm mjini Ni wastaafu, Wanaofugwa na wajinga wajinga wasio na elimu ya uraia.
 
Sasa ni ajabu gani kwa ubunge kuomba maji au barabara!. Na unavyosema ni ya mwisho Kilimanjaro je ni ya ngapi kitaifa? Kilimanjaro wapo juu kielemu hivyo ukiwa wa mwisho haina maana kwa Tanzania nzima unafanya vibaya. Na nilichosema mimi ni kwamba matatizo ya watu wa kasikazini ni vikwazo je wewe unajuaje kama vikwazo havijachangia kutokupata maendleo hapo Same!

Kuna potential ya wanafunzi wa Same kufanya vizuri zaidi. Nyinyi mlioko nje ya Same msibweteka na sifa za jumlajumla za mkoa wa Kilimanjaro. Kwanini uone it is OK wilaya ya Same kuwa ya mwisho kielimu ktk mkoa wa Kilimanjaro miaka nenda rudi? Kwani Same ndio wana DNA ya ujinga ktk mkoa wa Kilimanjaro, au tatizo ni kukosa support ya serikali na wenzetu walioweza kutoka na kwenda kusoma nje ya wilaya ya Same?
 
Nashangaa mpaka leo bado CCM na viongozi wa Serikali hawajajua tofauti ya wapinzani wa kaskazini na wa sehemu nyingine kama Kigoma au Mbeya

Huku Arusha, Kilimanjaro na Tanga tatizo kubwa sio barabara au madarasa ya shule. Ni sehemu ambayo ilikuwa na barabara nyingi za lami na shule nyingi ukilinganisha na sehemu nyingine lakini kulikuwa na wapinzani wengi.

Hivyo Rais Samia anavyoringia barabara na kujidanganya kwamba watu wamebadilika sio kweli watu wako vilevile.

Jamii ya huku Kaskazini tatizo lao na Serikali ni kwamba Serikali imekuwa kikwazo kikubwa kwa biashara. Serikali imeingilia biashara za madini kuwa na mpangilio, tozo biashara za utalii na hoteli. Lakini hii mikoa ya mipakana haipendi kusumbuliwa kwenye biashra za mpakani kama kuuza mahindi, vitunguu na kupita kwa magari.

Kwa ufupi watu wa Kaskazini wanataka Serikali ambayo ni pro-business na yenye mazingira mazuri ya biashara.

Wengi wa Kaskazini wanaamini vitu vingi wanaweza kufanya bila serikali lakini wanataka serikali isiwe vikwazo.

Upinzani wa sehemu nyingine kama Kigoma ni kutokana na serikali kuwasahau na kuona kama vile wenyewe hawapewi maendeleo kama barabara, reli, mazao yao, na ziwa Tanganyika. Lakini Mbeya nayo ni hivyo hivyo ni maendeleo ya barabara na maji ndiyo tatizo.

Hivyo Rais Samia kwenda Arusha na kuongea kuhusu maji kuliko biashara ni kutokujua jamii ya Kaskazini

Ili kutoa ukabila nijitambulishe mimi mwenyewe. Mimi nimekulia Arusha na Baba Mpare na Mama Mchagga hivyo nimechanganya kama wengine wengi
Una hoja nzuri isipokuwa bado una ushamba unakusumbua
 
Haya ni mawazo yangu ni kwanini watu wa kaskazini wengi wanapenda upinzani zaidi. Kama wewe unaamini kama hao viongozi sawa haya ni mawazo yangu tu na najua yako sawa. Watu wa kule wananielewa wengine mnaweza msinielewe
Kimsingi hao watu wanaoitwa watu wa kaskazini wengi ni wachaga. Kwa asili wachaga ni wafanyabishara ambao sera inayowafaa ni ubepari. Ccm ni chama cha kijamaa sera ambayo ni kama inakumbatia umasikini. Kwa sababu za kihistoria na kijiografia zilivutia wazungu zaidi kukaa huko, na kuanzisha shule hatimaye wachaga wengi kupata elimu. Kijiografia eneo hilo lina rutuba, na kuna wingi wa maji hivyo lishe ya huko ni ya uhakika. Sasa ukichanganya elimu, utajiri wa asili hasa ardhi yenye rutuba na maji mwaka mzima, kisha wenyeji kuwa wafanya biashara. Huko kunawafanya kuwa tabaka lenye unafuu wa kimaisha, hivyo sera za CCM za kijamaa hao wachaga wanachukulia kama umasikini, unakuta automatically hao waitwao watu wa kaskazini hawaikubali ccm.

Ccm inatamba sana sehemu yenye umasikini na elimu duni, kwani huko hutumia ujinga wao na kuwatawala kwa hofu. Kwa sasa ccm inapata shida kutawala ndio maana inajikuta inatumia nguvu zaidi, maana kizazi hiki kimeelimika hivyo kinaweza kupambanua mambo.
 
Wenda uko wrong. Ingekuwa hivyo mbona hizo 560 B zilizotolewa hazijapigiwa kelele. Ziende hizohizo zikatolewe kanda ya ziwa ungesikia makelele ya kufa mtu.

Tatizo la huko kaskazini ni kutaka kujifanya mifano ya nchi kwamba barabara ya rami hadi vijijini migombani, hamna nyumba ya tembe. Lakini wakijaribu kunyanyua kwingine angalau kuwe kuwe ni vita kali maana you are threatening their dominance .

Haja ya wana kaskazini ni kuwa na serikali yenye upendeleo maalum kwao yani kwamba bila hivyo hata ufanye nini unajisumbua tu kwao.
Tangu lini umesikia kaskazini wamependelewa na uongozi wa nchi hii. Tangu kabla ya uhuru Nyerere alipingana na wa kaskazini na baada ya ya uhuru alifanya jitihada zote kuwarudisha nyuma watu hawa kwa mbinu nyingi ikiwa ni pamoja na kutaifisha mali zao, mashule nk. Waskazini walizuiliwa kusoma shule za serikali na walikimbilia Kenya kusoma. Leo hii hawa watu wamejaa kwenye mabiashara na sekta binafsi ambapo si rahisi kuwazuia, serikalini hawatakiwi kama wahindi halafu unasema wamependelewa! Hujui kitu.
 
Back
Top Bottom