Kuna uhusiano gani kati ya Pesa, Umasikini na kelele

Hata nyumba za ibada wanokoswali maskini zimejaa kelele.

Dalili mojawapo ya umaskini ni kupenda kelele. Ndio maana soko kubwa la vyombo vya kupaza sauti liko Africa. Imagine watu wanafit subwoofers kwenye bodaboda! Nyumba ya ibada isiyojaa hata watu hamsini lakini utakuta PA system yao inatia mji wote taharuki.

Anyway. Kwangu mimi, viwango vya sauti vinawiana inversely na viwango vya akili. Akili kubwa, sauti ndogo. Akili ndogo, kelele mingi.
 
Mkuu uko vizuri. Hii imekaa vzr.
Naona kuna uhusiano mkubwa kati ya stress za ufukara na makelele.
 
😁😁 mpunguze kelele
😂😂 Sema una point usikilizwe kuna uhusiano kati mental disability na makelele, kuna sehemu kama hotel au maofisi tulivu watu wanaoingia hata anavyoingiq na tembea yake tu unaona huyu sio wa hapa au huyu wa mitaa flani
 
😂😂 Sema una point usikilizwe kuna uhusiano kati mental disability na makelele, kuna sehemu kama hotel au maofisi tulivu watu wanaoingia hata anavyoingiq na tembea yake tu unaona huyu sio wa hapa au huyu wa mitaa flani
Hata muhudumu anajua hiki kichwa hakichelewi kusepa na kandambili na Taulo za Hotelini. Ukitoka tu wanakagua kabla hujafika mbali.😁😁
 
Hata muhudumu anajua hiki kichwa hakichelewi kupndoka na kandambili na Taulo za Hotelini. Ukitoka tu wanakagua kabla hujafika mbali.😁😁
😂Tumezoea kulala guest zina kandambili za mguu mmoja na kataulo cha kiswazi
 
Ila wabongo tunapenda sana kelele.

Mf. Huwezi kuta bar hawapigi mziki mkubwa.

Huwezi kuta watu wakiangalia mpira bila kubishana.

Kila mara wanataka muongee ongee tu.


Kwenye dala dala kelele,

Maofisini kelele.

Masokoni ni makelele kila mahali.

Kiufupi bongo hakuna utaratibu wa lolote huwa tunajiendea tu.

Ukitaka kujua tupo disorganised mno, toka nje ya nchi halafu urudi utasikitika namna tunavyoishi.

Ila hivyo hivyo maisha yanakwenda.
 
Masikini=makelele=uchawi=roho mbaya=unafiki.
 
kwenye siasa huwezi sema ni kelele lazima ccm na chadema watoe sera zao alafu tuchuje ila maskini ni kweli wana makelele unakuta libodaboda lina makelelee alafu kafungulia mziki kwa sauti ya juu!
 
Tajiri manunuzi yake siyo ya rejareja huwa ananunua jumla huwez mwekea viduka, au grocery, au genge.....hawanunui mafuta ya kula ya vibaba, wala kiberiti cha mia, wala wembe wa mia 2.

Kwa Tajiri huenda malls na supermarket kununua jumla...
hata mimi kuna baadhi ya vitu ndivyo hununua kidogo, ila mchele mafuta ya kula, sabuni za kufulia na kuogea, unga wa ugali na baadhi ya mahitaji nachukua vya kutosheleza mwezi mmoja, inapowezekana hata zaidi ya mwezi.
Ila mimi sio tajiri. Nina maisha ya kawaida tu.
.
.Hata baadhi ya matajiri hununua bidhaa kwenye masoko ya hayahaya, wengine hutumia wafanya kazi wao.
 
Kweli mkuu.
 
Unavielementi vya utajiri, utafika mbali. Jitahidi tu usiwe na kelele 😃😃
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…