Kuna umuhimu wa kuripoti JKT kwa wahitimu wa Form 6?

Kuna umuhimu wa kuripoti JKT kwa wahitimu wa Form 6?

JKT kupoteza muda tu na kutesa vijana wetu wameshachoka na mitihani hata hawajapumzika waend tena kulima huko na kukimbiakimbia, hao wa kujitolea tu hawawaajiri wanazeekea makambini na kurejea mitaani.
Binafsi sioni faida ya kwenda huko, labda kama una ndoto na jeshi unaweza kwenda ukapata connection otherwise piga chini, chuo utaenda tu.
Hujamjibu swali lake, bali umetoa fikra zako.
 
Mkuu, Sio dharau ila sababu, faida na madhara ya kujiunga au kukataa kujiunga na Taasisi, yao hao vijana wataenda kuyajua huko mbele kwa mbele.
Aidha kijana anatakiwa kujiandaa kwa hali zote za Heri na Shari sio anakaa tu kulemaa-lemaa hapo mtaani kazi ni kulalamika kila siku na kujishaua eti amesoma hadi form six. Akienda jeshini atashangaa anawakuta wenzake maafande wamesoma hadi form seveni na ndo watakaomhenyesha.
Wameshaanza kuomba pesa za kununulia simu, acha waende wakajifunze maisha sio kunenepeana na kujaza mashavu bila sababu, ngoja waende wakajifunze hata kutumia mabumu yao watakapoanza vyuo
 
Aisee! We unaweza kuwa ni mtu hatari sana unataka kulea vijana kama mayai. Kumbuka wahenga walisema "Kijana ni maji ya moto lakini hayachomi nyumba" tena wakasema "samaki mkunje akingali mbichi"
Umeona kijana wako eti anaenda kuteswa?? amechoka na mitihani??? wanaenda kulima na kukimbiakimbia?? Yaani Hutaki kijana wako achangamke, ajue kujipambania maisha na uhai wake, akutane na vijana wenzake wamkaramshe(Wamwondoe ulofaulofa) ajifunze kutii amri na pia kufanya maamuzi binafsi n.k. Sasa wewe umeamua kijana wako unamrembaremba na kumpetipeti hapo nyumbani? Majuto ni mjukuu. Nimemaliza.
Mkuu tuache siasa tuseme ukweli, Kama hhna ndoto za kujiunga jeshi kwenda Jkt ni kupoteza muda.

Hivi kijana wa miaka 19 aliyemaliza kidato cha 6 nini atakwenda kujifunza ambacho hajajifunza nyumbanibjwao kwa miaka yote tangu anazaliwa.

Hivi hujaona watoto wa darasa la pili wanahudumia wateja madukani na magengeni au hata barabarani wakizungusha mboga? Utajifunza kilicho kwenye familia yako automatically.

Hata hivyo enzi hizi siyo za kujivunia kwenda kujifunza eti kuchoma mkaa, kufyatua matofali, n.k... na ukifuatlia siyo kwamba elimu hutolewa labda ya kilimo bali wanatumika tu km mashine za uzalishaji.

Mazoezi yenyewe ukirudi mtaani wiki mbili tu yashapotea.

Tuache uzamani, mambo ya miaka ya 70 yamekwishapitwa na wakati.
 
Habari zenu Wana JF,

Naomba msaada kufahamu madhara ya kuacha kuripoti wito wa kujiunga na JKT kwa wale waliomaliza A level.

Je, cheti cha kumaliza mafunzo ya JKT huwa kinahitajika kwa ambaye anataka kufanya maombi vyuo vikuu vya Serikali kama UDSM, Tanzania Institute of Accountancy na IFM, kwa mfano?

Lakini la ziada: kama mhusika hatafanya maombi ya mkopo kupitia HESLB ataathirika namna gani?

Asanteni kwa msaada.
Kijana, nenda JKT.
Siku zitakuja mbeleni, very soon, kuna fursa zitatokea na kwa makusudi kabisa, watasema aliyepita JKT ana "added advantage"
Hakuna madhara ya kupitia JKT, bali kuna faida.
 
Watoto wa sasa hivi ni lonyolonyo sana, nashauri mbunge litunge sheria iwe ni lazima kwenda JKT.

Kiukweli mnatusikitisha sana Toto lipo high school bado linasimamiwa na wazazi hawezi hata kujisimamia.

Kizazi hiki bila kukipitisha jeshini tunaandaa msiba mkubwa kwa Taifa.
Ulonyolonyo mmeuanzisha nyie wazazi wa sasa wa dotcom....hakuna wazazi vilaza kama nyie yaani ni jukumu la mwingine....halafu eti ndio muwapeleke JKT, kwa nini upeleke nyolo JKT kaa nalo mwenyewe...maanza enzi zetu hakukua na nyolo kama hawa wenu ambao mnawalea kama mayai mkiamini ndio mapenzi....mtoto sio kuku kusema utakuja umle ....huyu ni binadam ambaye tunategema kesho aweze kujitegema na kuyatawala mazingira yake.
 
Habari zenu Wana JF,

Naomba msaada kufahamu madhara ya kuacha kuripoti wito wa kujiunga na JKT kwa wale waliomaliza A level.

Je, cheti cha kumaliza mafunzo ya JKT huwa kinahitajika kwa ambaye anataka kufanya maombi vyuo vikuu vya Serikali kama UDSM, Tanzania Institute of Accountancy na IFM, kwa mfano?

Lakini la ziada: kama mhusika hatafanya maombi ya mkopo kupitia HESLB ataathirika namna gani?

Asanteni kwa msaada.

Majibu

No1

Cheti Cha JKT hakina uhusiano na maombi ya chuo na hakiambatanishwi

Ila kinaweza kikahitajika wakati wa kuomba baadhi ya kazi



No 2

Kama mwanafunzi hatatuma maombi ya mkopo kupitia HESLB hatapata mkopo

(Inatakiwa muwe mnajiweza kiuchumi)
 
Nakazia hoja 100%.
Ewe kijana, kama utabahatika kupitia uzi huu nakushauri NENDA Karipoti JKT.
Manufaa ya kupitia Jeshini hayako wazi kivile na ndo maana wapo wachangiaji hapa wanasema(wanadai) ni kupoteza muda. Sio kupoteza muda hata kidogo.
Hebu fikiria ww kama kijana unatakiwa uwe jasiri, mvumilivu, ngangari, mbunifu, mwenye kuthubutu na mwenye kujisimamia - Kule JKT hayo utayapata na utakuja kugundua hilo baadaye utakapokuwa tayari umeshamaliza Jeshi na uko mitaani au kwenye ajira binafsi au kwenye Mashirika yasiyo ya kiserikali au hata Serikalini.
Usikubali ushauri wa hao ambao hawakupita huko na ndo hao Laini-laini(Nyoronyoro) anashindwa hata kutembea kwa miguu Km 3 eti ni mpaka apande boda.

Unachokiongea ni sahihi labda kwa vijana wanaotumikia JKT mkataba wa miaka 2+, ila sio kwa hawa vijana wanaokwenda miezi mitatu (mujibu wa sheria).

Mwisho wa siku uvumilivu, ujasiri, kujisimamia na uthubutu kama ulivyotaja ni mambo yanayojengwa kwa muda mrefu sana na kwa hatua mbali mbali kuanzia ngazi ya familia, jamii n.k huko kwingine kama jkt ni kupiga msasa tu
 
Umuhimu wa Cheti cha JKT ni pale utakapotaka kuomba kazi zinazohusu maswala ya ulinzi maana utatakiwa kuambatabisha cheti cha kuhitimu mafunzo ya jkt, mfano wa kazi nikama ifuatavyo;-

Polisi
Jwtz
Uhamiaji
Magereza
Takukuru (hawa huwa hawasemi ila wanazingatia pia) na;
Vyombo vingine vya ulinzi na usalama ama kazi zinazohusiana na ulinzi..


Kuhusu kuomba vyuo/chuo na mkopo wa elimu ya juu cheti cha jkt hakihusiki kwenye maombi yako ya vyuo wala maombi ya mkopo.

Lakini kama umepata nafasi ya kwenda mafunzo nakushauri nenda maana utafurahia sana na hautakuwa na chakupoteza!

Kila la kheri!
 
Je, cheti cha kumaliza mafunzo ya JKT huwa kinahitajika kwa ambaye anataka kufanya maombi vyuo vikuu vya Serikali kama UDSM, Tanzania Institute of Accountancy na IFM, kwa mfano?
Nenda JKT kijana, hicho cheti kina umuhimu wake hata kama sio kwa kufanya application ya chuo
 
Habari zenu Wana JF,

Naomba msaada kufahamu madhara ya kuacha kuripoti wito wa kujiunga na JKT kwa wale waliomaliza A level.

Je, cheti cha kumaliza mafunzo ya JKT huwa kinahitajika kwa ambaye anataka kufanya maombi vyuo vikuu vya Serikali kama UDSM, Tanzania Institute of Accountancy na IFM, kwa mfano?

Lakini la ziada: kama mhusika hatafanya maombi ya mkopo kupitia HESLB ataathirika namna gani?

Asanteni kwa msaada.
Huko JKT watoto wanakwenda kupotezea muda na kutumikishwa bila sababu za msingi. Mimi mdogo wangu au mwanangu hawezi kwenda huko na hakuna mtu atakayemzuia kuingia Chuo Kikuu. Waache ujinga wa kuwatesa watoto wa watu makusudi.

Ukimpeleka mtoto wako wa kike JKT atat*mbw* achakae. Na wa kiume akirudi hajawa shoga mshukuru Mungu. JKT ni ushuzi tu sijui kwanini wanang'ang'aniza watoto wa watu waende kuharibiwa kwenye hayo makambi ya uovu. Mungu anawaona.
 
Back
Top Bottom