Kuna umuhimu wa kuripoti JKT kwa wahitimu wa Form 6?

Kuna umuhimu wa kuripoti JKT kwa wahitimu wa Form 6?

Think wisely, Miezi mi3 ni michache sana. Kama hauna cha msingi cha kufanya nyumbani na una afya yako njema, nenda huko. Ni kuzuri kuna faida utajua siku ya mwisho. pia kuna advantage ya cheti utakachopata kitakusaidia kwenye mbele huko.
 
Watoto wa sasa hivi ni lonyolonyo sana, nashauri mbunge litunge sheria iwe ni lazima kwenda JKT.

Kiukweli mnatusikitisha sana Toto lipo high school bado linasimamiwa na wazazi hawezi hata kujisimamia.

Kizazi hiki bila kukipitisha jeshini tunaandaa msiba mkubwa kwa Taifa.
Nakubaliana na wewe kabisa mkuu, pia kama utaratibu huu ni kuwajengea vijana uwezo wa kizalendo pamoja na utambuzi wa skills mbalimbali za maisha basi nashauri usiwe na mazingira ya kiubaguzi kwani sio wote wanaomaliza huenda bali wengi wao huwa ni school candidates na sio PC. Unawezaje kuona SC anafaa kujiunga na JKT halafu PC asifae ilihali wote ni vijana wa kitanzania. Pili napata tabu kujua ni utaratibu upi ulitumika kutambua kuwa wanaostahili kwenda jkt kwa mujibu wa sheria ni hawa waliomaliza six pekee? Kwa nini kama lengo ni jema serikali isiweke utaratibu unaogusa kundi kubwa la vijana na iwe ni lazima labda mtu mwenye matatizo? Naomba nimalizie kwa kusema kwamba binafsi naliona kundi linalofaa kujiunga jkt kwa mujibu wa sheria ni hawa wanaomaliza kidato cha nne na iwe hivyo kwa wote kabisa kabisa.
Sababu ni kama zifuatazo:-

1/. Utagusa kundi kubwa sana la vijana.

2/. Kutokana na mazingira ya sasa, utakuwa umeokoa vijana wengi kwa kuwafanya wakakamavu na kuwaondolea hali ya urojourojo ikumbukwe kwamba siku hizi mfumo wa maisha umebadilika vijana wengi wamezoeshwa maisha mwendokasi kwa hiyo kusubiria wamalize kidato cha sita wanakuwa wameshakubuhu.

3/. Ni kundi ambalo lina muda mrefu wa kukaa jkt bila kuwaza mambo mengine kwani huwa kuna gap kubwa kutoka kumaliza shule, matokeo kutoka, selection na kujiunga na ngazi nyingine za elimu. Na hapa utakuwa umeokoa au umenusuru watoto wengi dhidi ya mambo kurupushi ya mtaani mfano kuolewa kabla ya kufikia malengo, na mengine yenye kufanana na hayo.

4/. Kundi hili kubwa mara baada ya kumaliza mafunzo hayo, nina imani vijana wetu hawatabaki kama walivyoingia na hatimae nchi itakuwa ina vijana wengi wanaojitambua.

NB. SERIKALI ISIOGOPE GHARAMA.
 
Hebu mwenye kufahamu tovuti ya JKT yenye kuonyesha majina ya waloitwa Jeshini,maana hii ya www.jkt.go.tz haipatikani,au siyo ya jeshi la kujenga taifa ?
 
Habari zenu Wana JF,

Naomba msaada kufahamu madhara ya kuacha kuripoti wito wa kujiunga na JKT kwa wale waliomaliza A level.

Je, cheti cha kumaliza mafunzo ya JKT huwa kinahitajika kwa ambaye anataka kufanya maombi vyuo vikuu vya Serikali kama UDSM, Tanzania Institute of Accountancy na IFM, kwa mfano?

Lakini la ziada: kama mhusika hatafanya maombi ya mkopo kupitia HESLB ataathirika namna gani?

Asanteni kwa msaada.
Unauliza haya maswali Ili usiende JKT dogo??
 
Nakazia hoja 100%.
Ewe kijana, kama utabahatika kupitia uzi huu nakushauri NENDA Karipoti JKT.
Manufaa ya kupitia Jeshini hayako wazi kivile na ndo maana wapo wachangiaji hapa wanasema(wanadai) ni kupoteza muda. Sio kupoteza muda hata kidogo.
Hebu fikiria ww kama kijana unatakiwa uwe jasiri, mvumilivu, ngangari, mbunifu, mwenye kuthubutu na mwenye kujisimamia - Kule JKT hayo utayapata na utakuja kugundua hilo baadaye utakapokuwa tayari umeshamaliza Jeshi na uko mitaani au kwenye ajira binafsi au kwenye Mashirika yasiyo ya kiserikali au hata Serikalini.
Usikubali ushauri wa hao ambao hawakupita huko na ndo hao Laini-laini(Nyoronyoro) anashindwa hata kutembea kwa miguu Km 3 eti ni mpaka apande boda.

Njoo na cheti chako cha JKT na mimi na hiki kitambi changu lakini ntakuponda vbya mno.

Hakuna faida yyte kwend JKT,Usimtishe dogo
 
Nakazia hoja 100%.
Ewe kijana, kama utabahatika kupitia uzi huu nakushauri NENDA Karipoti JKT.
Manufaa ya kupitia Jeshini hayako wazi kivile na ndo maana wapo wachangiaji hapa wanasema(wanadai) ni kupoteza muda. Sio kupoteza muda hata kidogo.
Hebu fikiria ww kama kijana unatakiwa uwe jasiri, mvumilivu, ngangari, mbunifu, mwenye kuthubutu na mwenye kujisimamia - Kule JKT hayo utayapata na utakuja kugundua hilo baadaye utakapokuwa tayari umeshamaliza Jeshi na uko mitaani au kwenye ajira binafsi au kwenye Mashirika yasiyo ya kiserikali au hata Serikalini.
Usikubali ushauri wa hao ambao hawakupita huko na ndo hao Laini-laini(Nyoronyoro) anashindwa hata kutembea kwa miguu Km 3 eti ni mpaka apande boda.
Yajayo yanafurahisha
 
Huko JKT watoto wanakwenda kupotezea muda na kutumikishwa bila sababu za msingi. Mimii mdogo wangu au mwanangu hawezi kwenda huko na hakuna mtu atakayemzuia kuingia Chuo Kikuu. Waache ujinga wa kuwatesa watoto wa watu makusudi.

Ukimpeleka mtoto wako wa kike JKT atat*mbw* achakae. Na wa kiume akirudi hajawa shoga mshukuru Mungu. JKT ni ushuzi tu sijui kwanini wanang'ang'aniza watoto wa watu waende kuharibiwa kwenye hayo makambi ya uovu. Mungu anawaona.
Yana ukweli hayo usemayo????
 
Mimi nilichaguliwa lakini sikwenda, madhara niliyoyapata Ni kushindwa kuapply kazi Kama za ujamiaji nk. Ila Mimi pia Ni mkakamavu sikuona sababu ya kwenda JKT
 
Kupita JKT haimaniishi utapata faida zozote sema kutokana na umasikini wa pesa na fikra wazazi huwapeleka watoto wao jkt ili angalau wabaatishe nafasi za majeshi Kama ulinzi , police ,jwtz nk .


Na sio kila Mtu anayekwend jkt atapata hizo nafasi za majeshi.
jkt kwa mujibu ( kupitia form six miezi3) haina faida yoyote maana hata magereza, polisi wanakataa wele wenye cheti cha jkt kwa mujibu wanataka wale waliojitolea kwa miaka kazaa juzi tu hapa ajira za vyombo vya ulinzi zimetoka wale wote wenye vyeti vya kwa mujibu wamepigwa chini
 
Nakazia hoja 100%.
Ewe kijana, kama utabahatika kupitia uzi huu nakushauri NENDA Karipoti JKT.
Manufaa ya kupitia Jeshini hayako wazi kivile na ndo maana wapo wachangiaji hapa wanasema(wanadai) ni kupoteza muda. Sio kupoteza muda hata kidogo.
Hebu fikiria ww kama kijana unatakiwa uwe jasiri, mvumilivu, ngangari, mbunifu, mwenye kuthubutu na mwenye kujisimamia - Kule JKT hayo utayapata na utakuja kugundua hilo baadaye utakapokuwa tayari umeshamaliza Jeshi na uko mitaani au kwenye ajira binafsi au kwenye Mashirika yasiyo ya kiserikali au hata Serikalini.
Usikubali ushauri wa hao ambao hawakupita huko na ndo hao Laini-laini(Nyoronyoro) anashindwa hata kutembea kwa miguu Km 3 eti ni mpaka apande boda.
Una fikra za kimasikini sana.
Huo muda unaopoteza kulima bustani bora ukawe machinga
 
KUNA UMUHIMU SANA KUNA KUSAIDIA KUPATA MARAFIKI WAPYA AMBAO BADAE NDO WAMBANGA WA WANAO ....UMEELEWAA JICHANGANYE NA WATU
 
Kama mwanao hana kazi ya muhimu anayofanya hapo nyumbani ni heri aende jkt, usiweke matarajio kua akienda jkt ndio atapata ajira, hapana.
Sema itamsaidia kuona maisha kwa namna tofauti, mimi nilivomaliza kidato cha sita wazazi wangu walinikomalia niende jkt, Na kweli nilienda na nimejifunza mengi nimekutana na watu wengi, tumelima sana, kufyatua matofali,kuchoma mkaa kupanda miche ya maparachichi,kwata,kua mkakamavu na mvumilivu, imenifundisha kidogo kuhusu silaha leo nina abc zake,kubwa kabisa imetengenezea mtandao mkubwa sana nimepata marafiki wengi,
Haya mambo yote nisingeyajua kama nisingeenda ningeishia kucheza magame kwenye ps nyumbani na kufukuzia mahousegirl.Kwa sababu sikua na kazi yoyote ya kufanya mda huo zaidi ya kula ugali wa baba.
Ndio maana mnaitwa wajinga na wapumbavu.
Hayo yote ulitakiwa fundishwa na waliokuzaa
 
Mkuu tuache siasa tuseme ukweli, Kama hhna ndoto za kujiunga jeshi kwenda Jkt ni kupoteza muda.

Hivi kijana wa miaka 19 aliyemaliza kidato cha 6 nini atakwenda kujifunza ambacho hajajifunza nyumbanibjwao kwa miaka yote tangu anazaliwa.

Hivi hujaona watoto wa darasa la pili wanahudumia wateja madukani na magengeni au hata barabarani wakizungusha mboga? Utajifunza kilicho kwenye familia yako automatically.

Hata hivyo enzi hizi siyo za kujivunia kwenda kujifunza eti kuchoma mkaa, kufyatua matofali, n.k... na ukifuatlia siyo kwamba elimu hutolewa labda ya kilimo bali wanatumika tu km mashine za uzalishaji.

Mazoezi yenyewe ukirudi mtaani wiki mbili tu yashapotea.

Tuache uzamani, mambo ya miaka ya 70 yamekwishapitwa na wakati.
Achana na hao wapumbavu, jeshi kwa Tz halina maana. Hakuna uzalendo unafundishwa kwa miezi 3
 
Kijana, nenda JKT.
Siku zitakuja mbeleni, very soon, kuna fursa zitatokea na kwa makusudi kabisa, watasema aliyepita JKT ana "added advantage"
Hakuna madhara ya kupitia JKT, bali kuna faida.
Siku za mbeleni zipi wakati kuna kundi kubwa la wasio na ajira na wamepita huko?
Watu wasipoteze muda wao kwenda jiahangaisha
 
Ulonyolonyo mmeuanzisha nyie wazazi wa sasa wa dotcom....hakuna wazazi vilaza kama nyie yaani ni jukumu la mwingine....halafu eti ndio muwapeleke JKT, kwa nini upeleke nyolo JKT kaa nalo mwenyewe...maanza enzi zetu hakukua na nyolo kama hawa wenu ambao mnawalea kama mayai mkiamini ndio mapenzi....mtoto sio kuku kusema utakuja umle ....huyu ni binadam ambaye tunategema kesho aweze kujitegema na kuyatawala mazingira yake.
Mbona kuna kundi kubwa la wasiojua kusoma na kuandika wa zama hizo kuliko zama hizi?
 
Back
Top Bottom