Chizi Maarifa
JF-Expert Member
- Jul 29, 2013
- 10,931
- 24,816
Huyu dada rafiki yangu wa muda toka tukiwa chuo. Jana alipenda tuonane tuweze ongea mawili matatu sababu ilikuwa ni weekend. Nilichukuana naye tukawa sehemu tunapata viburudisho then akaomba tunapoondoka tupitie somewhere nimchukulie kuku wa kuchoma. nikasema haina shida. So we went there. Akasema haina haja ya kushuka sababu alishakunywa sana so niagize tuje tukae kwenye gari, sikuona haja ya kuzima gari nikaona niache tu gari ipo on maana sipendi kufungua vioo vumbi lisije ingia ndani. so niliacha gari AC ipo on.
Nimeenda nikaagiza na kusimamia kidogo. nikarudi kumkuta amegonga gari eti alikuwa anajaribu kugeuza kabisa. Kmbe katika kurudi nyuma amegonga gari ya watu na kupasua taa ya gari yangu na ya huyo mwingine. Nimemkuta anatokwa jasho ile mbaya haelewi cha kufanya. Namuuliza why did you do that. anasema niliona tu nigeuze gari kabisa kumbe sikuangalia vizuri nyuma sijazoea kutumia Camera.
Huyu dada kwa kweli nimeshindwa kuelewa nimfanye nini maana amenipa hasara ambayo haikuwa na sababu. Jamaa imebidi nimlipe kwa ajili ya taa nami pia nikanunue taa kwa ajili ya gari yangu. Yeye amebaki tu anakodoa macho kama mjusi aliyebanwa na mlango. hawa watu wengine sijui waliumbwa wapi. Nilienda mshusha kwake na kuondoka sina hamu naye tena. Anatuma tu text kuwa nimsamehe tuoane tuyamalize au niende kwake tukaongee. Nami sioni cha kwenda kuongea naye. Na mimi naye nina matatizo sana na madada wa na mna hii ambao hawajielewi. Naanza hata kujionea mashaka kuwa pengine sasa mimi ndo tatizo.
Nimeenda nikaagiza na kusimamia kidogo. nikarudi kumkuta amegonga gari eti alikuwa anajaribu kugeuza kabisa. Kmbe katika kurudi nyuma amegonga gari ya watu na kupasua taa ya gari yangu na ya huyo mwingine. Nimemkuta anatokwa jasho ile mbaya haelewi cha kufanya. Namuuliza why did you do that. anasema niliona tu nigeuze gari kabisa kumbe sikuangalia vizuri nyuma sijazoea kutumia Camera.
Huyu dada kwa kweli nimeshindwa kuelewa nimfanye nini maana amenipa hasara ambayo haikuwa na sababu. Jamaa imebidi nimlipe kwa ajili ya taa nami pia nikanunue taa kwa ajili ya gari yangu. Yeye amebaki tu anakodoa macho kama mjusi aliyebanwa na mlango. hawa watu wengine sijui waliumbwa wapi. Nilienda mshusha kwake na kuondoka sina hamu naye tena. Anatuma tu text kuwa nimsamehe tuoane tuyamalize au niende kwake tukaongee. Nami sioni cha kwenda kuongea naye. Na mimi naye nina matatizo sana na madada wa na mna hii ambao hawajielewi. Naanza hata kujionea mashaka kuwa pengine sasa mimi ndo tatizo.