Tatizo si kupika kidogo, inawezekana wako wengine jikoni lakini ustaarabu ni kuhakikisha kilichotokea mezani kila mtu amepata na nyongeza ni ziada.Sijui ni ulafi au Uzungu, wewe kama umepika wachache si shida ni yako? kwanini usiweke kwenye sahani na mkashea hasa kwenye upande wa mboga? Hivyo vipande vitatu ni vya gram ngapi kila kimoja? Chakula cha manung'uniko bhana mwisho mtu anigwe na mfupa kisa jicho la usuda la kuchukua samaki mmoja (tena kagawanywa vipande vitatu) mwenye gram 400.
Kwani haufahamu siku hizi chakula ni mboga, YAANI MBOGA INAKUWA KUBWA ZAIDI YA WALI/UGALI?
Wewe unasema tu kwakuwa ni mwanaume, ila kuna wageni siyo wastaarabu kabisaa, na hapo ndo unaanza kuona mama mwenye nyumba mbaya kumbe mbaya wewe ambaye hujatumia ustaarabu kuto jali wengine vitu vinaenda kwa bajeti tena samaki walivyo bei halafu hawagawikagi unakuta watoto wanaambulia macho ya samaki kisa wewe mgeniMtoa mada punguza roho za njaa , wanawake vyakula vinawapaga stress.
Chakula kingi kwani kesho hutakula?!Watu wa Dar acheni uchoyo kwanini msipike chakula kingi?..ndo mana mnakufa kwa stress mana moyoni mmejaza kila aina za uchoyo.
#MaendeleoHayanaChama
Sent from my SM-A207F using JamiiForums mobile app
Kuna wengine wanachonokoa pua wakati wa kula
Ova
[emoji1][emoji1][emoji1]Kuna mgeni nimemwambia "Jisikie upo Nyumbani"
Kachinja Kuku wangu!
Hahah natania.......ila kwel bi mkubwa wangu sis watoto wa kiume alikua anatuoverload mda wa kula sana...
Absolutely right,My dear Sky Eclat
Ndio maana siku zote wazazi huwa wanashauriwa kuwa wanakula meza moja na watoto wao ili wawafundishe TABLE MANNERS ikiwamo kuwafikiria wengine na hata namna ya kutafuna chakula.
Inawezekana hao wageni ndio wale waliopelekwa boarding wakiwa bado wadogo sana (darasa la tatu) wakakosa muda wa kufundishwa tabia njema na wazazi/walezi wao.
Watu wengi wanatafuna Kama nguruwe sio mbuzi, mtu anatafuna mpaka nyumba ya nne wanasikia.Absolutely right,
Kuacha Table manner viko vingi vya kuchunguza na kuwafunza wenetu.
Nimewahi kununiwa na staff mwenzangu baada ya kumrekebisha kuhusiana na uchakuaji(utafunaji) mbovu wa chakula.
Ni tabia mbaya kutafuna Kama mbuzi,hufungi mdomo pia unaongea.
Naona umeamua kutusema sisi akina mabula na maduhuUnakaribishwa chakula kwenye familia, mabakuli makubwa ya chakula na mbogamboga yanawekwa kati kati. Inakuja wakati kila mtu ajiwekee chakula anachopenda.
Mezani mpo nane. Wewe ni mtu wa tatu kujiwekea chakula, utamsikia shemeji leo umenipatia kweli, hawa samaki ndiyo ugonjwa wangu. Anachukua vipande vitatu pasi kufikiria watano wanaomsubiri watapata samaki.
Ustaarabu ni kuchukua chakula kidogo, subiri round ya kwanza iishe. Kama ulipenda sana samaki unaweza kujiongezea katika round ya pili kama watakuwa wamebaki. Wakati huo ndiyo unaweza kusema kama hakuna anaeongeza ninatongeza hawa samaki maana hiki ndiyo chakula ninachokipenda, leo shemeji umenipatia.
Kuna wengine anakula huku anashika smart phone yake mezani anaangalia messages. Jamani hao wanaokutumia hawawezi kusubiri mpaka umalize kula na wenzako? Kama una ujumbe wa muhimu sana deal la mahela unaweza kuwataarifu wenyeji wako kuwa kuna ujumbe ninautegemea lakini ni ustaarabu kuachana na simu wakati mko mezani.
Sahihi kabisa mkuuAbsolutely right,
Kuacha Table manner viko vingi vya kuchunguza na kuwafunza wenetu.
Nimewahi kununiwa na staff mwenzangu baada ya kumrekebisha kuhusiana na uchakuaji(utafunaji) mbovu wa chakula.
Ni tabia mbaya kutafuna Kama mbuzi,hufungi mdomo pia unaongea.
Sawa mkuuWengine si boarding bali ni malezi mabaya, kama wale wababa wapenda kuoa oa hawanaga muda wa kula na watoto wao muda wote wanawaza vimada
Kabisa mkuu....na unawekaje samaki 8 exactly na idad ya wageni buana....weka misamaki yakutosha kama una wagen usibanieNdiyo maana leo huli bali unafukia, kumbe ulishazoeshwa na bi mkubwa wako kufukia, wewe hufai kukaribishwa na Sky Eclat, unafaa uje nyumbani kwangu ili uwe overloaded.[emoji1787]