Kunena kwa lugha ni nini? Na nini hutokea pale mtu anaponena kwa lugha?

Kunena kwa lugha ni nini? Na nini hutokea pale mtu anaponena kwa lugha?

Ni upotoshaji tu na ukanjanja wa kuwapiga noti watu wenye imani haba na kutoelewa mafundisho yaliyoandikwa kwenye Biblia...
Ok nimekuelewa, je hiki wanachofanya walokole ni nini? Maana mpaka watoto hunena hayo mambo wasiyoyaelewa. Na ni walokole karibua wote duniani.

Kama sio mapepo, ni kitu gani kinawafanya waumini kuanza kuongea lugha isiyoeleweka ambayo hata wao hawaielewi? Kuna mechanism gani?
 
Daah nilitaka jana kuileta mada hii kinagaubaga. Leo umetupia swali kuhusu kunena kwa lugha.

Kwa ufupi ni;
1. Ishara ya kwamba mtu kapokea Roho mtakatifu (Mungu ameweka makazi ndani ya mtu)
Mark. 16:17

2. Kunena kwa lugha ni kuomba kwa lugha za malaika ambayo ina nguvu na haiwezi kuzuiliwa na pepo au nguvu yoyote ya giza
1.kor 14:2

Inatosha , nikipata mda taleta mada.

Pia kunena kwa lugha kuna kwa namna 2.

1. Kuhutubu (kutabiri) hii lazima mnenaji au mtu mwingine atafsiri.

2. Kunena kwa lugha ili mtu ajijenge yeye mwenyewe, hii haina haja ya kutafsiriwa maana ni siri ya mtu mbele za Mungu wake
 
Hiyo ni dalili kubwa ya magonjwa ya akili inaitwa HALLUCINATION
Ukiona unasikia sauti za ajabu pasi na kujua nini kinazungumzwa basi ni ndio kiataalamu inaitwa Shizophrrnia
Kimsingi asilimia kubwa ya walokole hamnazo kuna mmoja hapa jirani alizimia kisa hajala siku 3 kisa yesu kamtokea kamwambia afunge siku 5 jiulize wee unamjua yesu kweli kama sio ukichaaa ni nini yaan usile siku 5 hawa walokole wana magonjwa ya akili na asilimia kubwa ni wanawake
Kama ni ugonjwa (schizophrenia) kwanini uwatokee walokole tu?

Kwanini hatusikii watu wa dini zingine wakinena kwa lugha?

Au huo ugonjwa unawachagua walokole tu?
 
Ok nimekuelewa,,,je hiki wanachofanya walokole ni nini? Maana mpaka watoto hunena hayo mambo wasiyoyaelewa. Na ni walokole karibua wote duniani.

Kama sio mapepo, ni kitu gani kinawafanya waumini kuanza kuongea lugha isiyoeleweka ambayo hata wao hawaielewi? Kuna mechanism gani?
Ni ubabaishaji Pro-max, wakubwa wanatudanganya ila watoto wanachofanya ni copy and paste ya kile wanachoona wakubwa wao wanafanya.
 
Baadhi ya walokole niliowauliza hili swala wanasema wanapokuwa wananena hata hawajitambui wanaomba nini. Yani sio kwamba wanafupisha maneno kama unavyosema bali ni kama wanaingiliwa na nguvu inayoongea mambo ambayo hata wao hawayaelewi, kuyaelewa ni mpaka baadae waombe Mungu awafunulie.
Kama unajua kusoma hamna sehemu nimesema wanafupisha Maneno. Andika opinions bila kuweka justifications zisizokuwepo.
Kila mlokole atasema anavyoweza. Ila uhalisia yale tunaita ni maneno beyond. Mpaka inakua kama unatamka tu kufikisha unachofikiria kichwani. Haitokei bla sababu pia wamekudanganya.
 
Lazima wawe vichaa kwa sababu wana abudu kitu ambacho si kweli kwao na wengi wao ni matapeli.
Mkuu pole sana. Hiyo imani yako na wewe umeletewa na ukaaminishwa kwamba hiyo ndo imani ya kweli hata wakristo nao wanaamini ukristo ni njia ya kwenda mbinguni hivyo basi usisimame mahali ukausema upande mwingne kwa ubaya na maneno kedekede ilihali wewe hiyo yako pia umeikuta

Kuna msemo unasema."DEVIDE AND RULE"
Ukiuelewa huu hutabishana na watu kuhusu ima i zao
 
Mkuu pole sana. Hiyo imani yako na wewe umeletewa na ukaaminishwa kwamba hiyo ndo imani ya kweli hata wakristo nao wanaamini ukristo ni njia ya kwenda mbinguni hivyo basi usisimame mahali ukausema upande mwingne kwa ubaya na maneno kedekede ilihali wewe hiyo yako pia umeikuta

Kuna msemo unasema."DEVIDE AND RULE"
Ukiuelewa huu hutabishana na watu kuhusu ima i zao
Na hii ya dini waliitumia sana wazungu!Kwenye kitabu cha waefeso enyi watumwa watiini mabwana zenu kama kumtiii Kristo(Yesu)!
 
Ni upotoshaji tu na ukanjanja wa kuwapiga noti watu wenye imani haba na kutoelewa mafundisho yaliyoandikwa kwenye Biblia...
Kumbe wale Wasabato Masalia walikuwa sahihi , maana walitaka waende Ulaya kama Ureno, Ufaransa ,uingereza wakahubiri wakati wao wanaongea Kiswahili tu
 
Kwa Ulokole wangu na kumtumikia Mungu kwa miaka 8 Kanisa TAG huku Nyakatuntu Keisho Karagwe.

Kunena kwa Lugha, ni Karama ya Roho Mtakatifu ambayo huitoa kwa mwanadamu kama karama zingine za unabii, matendo ya miujiza na uponyaji, neno la hekima n.k 1 Korintho 12:1-12 inaeleza wazi kuhusu hizo karama
kiongozi umeelezea kwa ufasaha sana na kwa sehemu kubwa kwenye mada hii kuna watu mapandikizi ya shetani yapo kwa ajili ya upotoshaji kwa hali na mali
 
kiongozi umeelezea kwa ufasaha sana na kwa sehemu kubwa kwenye mada hii kuna watu mapandikizi ya shetani yapo kwa ajili ya upotoshaji kwa hali na mali
Ni sahihi, humunJF ni kupinga, juponda na kudharau kila kitu cha kiroho. Wengi ni agents tu tumalaswa kuwa na misimamk yetu alafu tuchukuliane nao tu.
 
Kwa Sasa Kuna waislam 1.8 billion duniani (Tuassume wote ni dhehebu lako)...Dunia Ina watu bilioni 8.

Kwahyo Sasa Kuna watu bilioni 6.2 duniani ni vichaa Kwasababu wanaabudu vitu visivyo vya kweli?
Ndio mkuu
 
Ninapenda kujua mitazamo yenu juu ya Hawa watu kunena kwa lugha
Chief mleta mada, Afrocentric

Mimi sipo mbali na maelezo ya mshamba_hachekwi hayo yaliyohusisha hypnosis na ecstacy.

Zamani hizoo watu ili waongee na Mungu huku Afrika na kwingineko kama Amazon (huku bado wanaendelea nnaona). Lakini pia ma Rastafarians kuna kitu wote hawa wanafanya kinashabihiana;

Wanatumia kilevi fulani kitakatifu 'sacred' kuweza kujiweka hali ya kuishusha akili ya mbele yenye kujizuia na kujitambua na kuruhusu akili na sehemu nyingine za ubongo zijitawale. Wanaruhusu hisia na subconscious mind vijiachie.

Pombe inaweza kusaidia kufanikisha hilo
Bhangi husaidia kufanikisha
Uyoga, mizizi, majani na hallucinogens mbalimbali husaidia sana kufanikisha hilo.

Pia sherehe hizi huambatana na ngoma na sherehe na kufunga vitakavyosaidia kuwahisha mchakato na kuushikilia 'maintain it'. Hao wanaolewa kwanza huweza kukaa hata siku tatu wanawasiliana tu na roho.

Subconscious mind ndiyo huhusika zaidi ndiyo maana wanawasilisha kihisia mawazo yao ya ndaaaani kabisa (communicating deeply desires with ones' God) na tuseme tu kuhusu kusikia Mungu anawasikia na kuwaelewa ile deeeply kabisa. Hapo zinawasiliana will kwa Will, utashi kwa Utashi mkuu.

Ni kwa nini basi maneno hayaeleweki ama kukosa muunganiko maalumu. Kumbuka cerebrum ndiyo hutumia mantiki kuwasilisha wazo. Lakini ikizimwa data au ikafifia basi wazo, haja na hisia huwasilishwa kwa namna ambayo mwanadamu mwingine hatang'amua maana kanuni za jamii za lugha hazijatumika hakuna tena inhibition kamilifu.

Turudi kwa walokole; walokole hunena kwa lugha, huongea hisia na haja zao za ndani kabisa. Ni kweli wanasali na wanawasilisha mawazo yao ya ndani kwa Mungu wake. Man to God.
Wao wamejifanyia ama self hypnosis ama kiongozi wao mwenye mamlaka juu yao kawahakikishia kwamba hicho kitu kinawezekana(wameunda constructs kwamba ni kweli mtu anaweza ongea na Mungu kwa njia hizo), na pia wamesaidiwa na nyimbo na vyombo ngoma na muziki kuifikia hali hiyo. Ni kuongea na Mungu as far as hao wawili wanahusika yaani subconscious ya mtu na superconscious ya Mungu.

Bandugu, chukulieni tu kama mama na mwanaye. Mtoto akikua kidogo anaweza sema 'mama, taka, kula' akaeleweka na mama ake na watu wote.
Au akalia na mama ake akaelewa na watu wachache wakaelewa.
Au akazubaa tu na hapo ni mama ake anauemjua vizuri, aliyemlea ndo atamuelewa hisia zake. Mama anaweza kujua mtoto kilio hiki anaumwa, au amechoka, au ni usingizi, njaa etc.... same concept
 
Mkuu hiyo haikuwa dhana halisi ya kunena kwa lugha, na ukitaka kujua kuwa hawa wajuba ni wababaishaji kwanini wote wawe wanatamka maneno yaleyale au yanakaribisna?

Ingekuwa ni kweli tungekuwa tunawasikia kwa lugha tofauti mara leo Mwamposa kakibomoa Kichina, hatujakaa vizuri Lusekelo anatapika Kireno kabla hatujapoa Mwingira anatupeleka Moscow anabonga Kirusi, wakati tunajiuliza nchi imekumbwa na jambo gani huku Gwajima anatiririka Unyola wa kufa mtu mpaka tujihisi labda tupo Madrid.
Umeichukulia kimwili ndio maana

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mungu hayupo.

Kunena kwa lugha ni Uwendawazimu na Uwehu.

Sawa na mtu aliyepandwa na Malaria kichwani.

Mnenaji wa lugha hana tofauti na mgonjwa wa Malaria iliyopanda kichwani.
 
Huja automatic ukiwa deep in prayer hasa ile prayer ys sauti
 
Back
Top Bottom