Kunena kwa lugha ni nini? Na nini hutokea pale mtu anaponena kwa lugha?

Kunena kwa lugha ni nini? Na nini hutokea pale mtu anaponena kwa lugha?

Siamini katika kunena kwa lugha, maana huwezi kuzungumza kitu ambacho huwezi kutafsiri, mitume wakati wanaenda kusambaza injili walipewa karama ya kuzungumza lugha ya wakazi wa eneo husika na sio lugha ambayo kwa sasa si wewe wala mkazi wa eneo husika anaejua

Hivi ni lugha gani ambayo ina maneno yasozidi hata 10 as a matter of fact, nahisi matano tu mengi ni mwendo wa RABASHABAKA. . .

Ikiwa yapo maneno mengine mtanifuta nipo paaale mniite jina lolote maadam limpendezalo Mungu

Nashukuru imani yangu haina hayo masuala, wala kuabudu masanamu, wala kuambiwa baadae ntapewa 70 ilhali huyu mmoja ananitosha, wala kusujudia miungu watu kwa gia ya maji na mafuta

Mi ni Dua kwa Mungu mmoja kupitia kwa mkombozi wetu Masihi, kushika siku saba ya Juma, kusambaza upendo na kupiga vita chuki na kuyashika yote niliyoamriwa.
 
Kunena kwa lugha ni lugha ya kiroho ambayo huja automatic na hakuna awezaye kuimiliki...

Sent using Jamii Forums mobile app
Nilihisi Mshana Jr atakuwa mbobezi kwenye hili kumbe, hakuna anayejua yote! Kasome biblia yako vzr kunena kwa lugha inaanzia kushuka kwa roho siku ya pentekoste na inaonyesha bayana ya kuwa waliokuwa wananena walinena kwa lugha za kibinadamu ambazo wao walikuwa hawazijui kabla, mfano msukuma aaze kuongea kiitaliano ambacho hakuwa kujifunza mwanzo huku akitaja ukuu wa Mungu! Na. Mfaransa aanze kuongea kiangaza, kisha muangaza ashangae mbona anaongea maneno ya ukuu wa Mungu kwa lugha yake??? Swali zile robo shaka shaka ni lugha gan? Kule ni kupuyanga tuh hakuna roho wa hivyo
Ref :matendo ya mitume 2:1-13
 
Ni upotoshaji tu na ukanjanja wa kuwapiga noti watu wenye imani haba na kutoelewa mafundisho yaliyoandikwa kwenye Biblia.

Wajanja ndiyo hupita humo na kukunja noti kiulaini kabisa kupitia uposhaji unaofanywa na makanisa ya leo yanoyojiita ya kiroho.

KUNENA KWA LUGHA KULIANZAJE KIHISTORIA?
Ukisoma kwenye Biblia kunena kwa lugha kulitokea siku ya Pentekoste ( Yaani siku ya Hamsini baada ya Kupaa kwa Yesu).

Katika maandiko tunaona kuwa ujumbe wa neno la Mungu ulikuwa umepokelewa katika jamii moja lakini dhima ilikuwa ni ujumbe huu usambae Ulimwenguni kote. Yaani kwa mfano, tuchukulie kwamba ujumbe wa neno la Mungu ulifikia Tanzania ambapo lugha inayotumika kwa mawasiliano ni Kiswahili, lakini ujumbe wa neno la Mungu ulitakiwa ufike Djibout, Malawi, DRC, Ethiopia na kwingineko Ulimwenguni ambapo hata hawakijui Kiswahili.

KULITOKEAJE?
Kunena kwa lugha kulitokea kwa wale Mitume sio kwa kubadili na kuacha kutumia lugha zao za asili au walijifunza lugha za Mataifa waliyoenda kuhubiri, la hasha, bali walitumia lugha zao za asili lakini waliokuwa wakihubiriwa waliupata ujumbe kwa kuusikia kwa lugha zao wenyewe.

Yaani tukirejea katika huo mfano hapo juu, ni kwamba, wewe Petro Mtanzania ukiwa unazungumza Kiswahili chako sanifu kabisa lakini unawahubiria watu wa DRC na wao wanasikia ujumbe unaowapa kupitia lugha wanayoielewa wao mfano, Kilingala, au Kifaransa.

Kwahiyo ni kama leo hii baada ya kuja teknolojia Uhutubie pale UN lakini wawakilishi wa Oman wanakusikia unaongea Kiarabu kilichonyooka, au Ujumbe kutoka Rome unaona unagonga kile Kilatini chenyewe kabisa, au wajumbe kutoka Brazil wanaona unakibomoa kireno ipasavyo.

Na kwa njia hiyo ndivyo ujumbe wa neno la Mungu ukaweza kuenea Ulimwenguni kote na maandiko kuweza kutafsiriwa katika lugha mbalimbali kulingana na sehemu ujumbe wa neno la Mungu unapelekwa

UPOTOSHAJI WA MAKANISA YA LEO YANAYOJIITA YA KIROHO:
Viongozi wengi wa hayo Makanisa hawaijui dhana ya kunena kwa lugha kwa mapana yake, na kama wanafahamu basi wanatumia ujinga wa waamini wao kufanya upotoshaji wa Makusudi kwa Maslahi yao binafsi.

Ukienda kwenye Makanisa ya leo yanayojiita ya kiroho yamejaa upotoshaji juu ya dhana hii ya kunena kwa lugha kwa kukuta hao viongozi wa makanisa hayo wanaongea lugha ambazo hata waumini wao hawazielewi nini wakimaanisha au ujumbe gani unatolewa kupitia matamshi hayo.

Nachelea kusema usikute hata wao hawajui ni kitu gani wanaongea na wala hawajui hiyo lugha gani wanatamka.

NB: Kunena kwa lugha sio kama kupandisha mashetani na kuongea vitu visivyoeleweka, bali ni njia iliyowatukia Mitume katika zama hizo ili neno la Mungu liweze kufika mahali pote Ulimwenguni.

Kwa ulimwengu wa sasa sidhani kama hiki kitu bado ni applicable.
Umenena vyema !👏🏾
 
Matapeli wana lugha zisizotafsirika kwenye kamusi yoyote ile ... Wakimaliza kunena lugha zao utasikia shika sadaka yako.. Na wanakondoo wanajipuputisha walivyo navyo wakirudi nyumbani ni kwenda kununua mafuta ya mia mbili na kupika ugali dagaa wa free (mchana hadi jioni) huku wamenyanyua mikono ya nabii kwa 50k ..
 
Unaweza ukawa na elimu,pesa na bado ukawa kichaa,We unavyowaona walokole wako sawa.
Maana ikiwa tumerukwa na akili zetu, ni kwa ajili ya Mungu; au ikiwa tunazo akili zetu timamu, ni kwa ajili yenu.
2 Kor 5:13 SUV
 
Ni mfumuko mkubwa wa hisia ndani ya muda mfupi(religious ecstasy) unaosababishwa na hypnosis inayoletwa na ile hali ya umakini kwenye ibada, mchanganyiko wa nyimbo za kuabudu, kusifu na kusali kwa muda mrefu unaleta huo umakini.

Pia kuna tatizo la kiakili linaitwa frontal lobe epilepsy, linasababisha mtu kuhisi mchanganyiko wa hisia nyingi ndani ya muda mfupi, visababishi flani vikiwepo.

Uthibitisho kwamba kunena kwa lugha ni uongo ni kwamba imegundulika wanaonena kwa lugha, yale matamshi wanayotamka yana silabi zinazofanana na lugha zao za kawaida, hivyo sio lugha mpya wanaongea bali wako kwenye hali flani ya kihisia inayofanya washindwe kuongea vizuri.

Nimejaribu kuelezea nnachokijua, mnisamehe vitu vingine sijui kiswahili chake nimeandika hivyo hivyo tu
Sawa mkuu
 
Nilihisi Mshana Jr atakuwa mbobezi kwenye hili kumbe, hakuna anayejua yote! Kasome biblia yako vzr kunena kwa lugha inaanzia kushuka kwa roho siku ya pentekoste na inaonyesha bayana ya kuwa waliokuwa wananena walinena kwa lugha za kibinadamu ambazo wao walikuwa hawazijui kabla, mfano msukuma aaze kuongea kiitaliano ambacho hakuwa kujifunza mwanzo huku akitaja ukuu wa Mungu! Na. Mfaransa aanze kuongea kiangaza, kisha muangaza ashangae mbona anaongea maneno ya ukuu wa Mungu kwa lugha yake??? Swali zile robo shaka shaka ni lugha gan? Kule ni kupuyanga tuh hakuna roho wa hivyo
Ref :matendo ya mitume 2:1-13
Kunena kwa lugha ni tendo la kiroho lisilo na tafsiri yoyoye iwayo yote katika ulimwengu! Ni tendo la ndani mno na haliji kwa siku moja wala kwa kupanga
Kadiri unavyokuwa na usafi wa kiroho.. Uchaji wa kiimani na usadifu wa maombi kuna viwango vya kiroho na kiimani unajiona kabisa unapanda..

Na pindi unapoingia kwenye maombi kuna hali fulani hivi hukuvaa na kujikuta unahama kutoka ulimwengu huu na kuingia ulimwengu mwingine mwepesi na mng'avu sana.. Hapo ndio kuna maneno hukutoka bila utashi wako na bila kujua unaongea nini.. Lakini unakuwa na hakika MOJA tu si maneno ya kujitungia wala ya kidunia ni maneno yenye lugha yenye uhai na una i feel kabisa..

Nilishaishi katika wokovu kwahiyo ninalifahamu hili kwa hakika[emoji1545]

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wakuu,

Hapa duniani Kuna Imani nyingi, Kuna watu ambao hawaamini Mungu (atheists), Kuna waislam,Kuna wabudha. Kuna wakatoliki,wasabato na Kuna hawa wahusika wenyewe (walokole na wengineo).

Ninapenda kujua mitazamo yenu juu ya Hawa watu kunena kwa lugha.

Je ni Mungu au sio?

A) Wanaosema ni Mungu (walokole nk.)
Mechanism ikoje? Ukiwa unanena unajisikiaje? Je unajielewa unachosema?Nani anacontrol mdomo wako?Unapanga cha kuomba? Kuna faida gani?

B) Wanaosema si Mungu
Mechanism ikoje? Ni kweli wananena au usanii tu? Je nini hufanyika pale? Kwanini walokole wengi waumini wa kawaida tu nao wanene? Kuna siri gani nyuma ya kunena kwa lugha? Je wanajitambua au wanatawaliwa na nguvu nje ya akili Yao? Ni nguvu gani hiyo? Nini huendelea kwenye ubongo wa mtu pale anaponena kwa lugha?(mental state)

Uhakika Bro Mshana Jr Tate Mkuu adriz Che mittoga Walker Water Smotor Surya FaizaFoxy KENZY Mcqueenen Kiranga mwakabonao CAPO DELGADO Blood of Jesus
Hamna lolote ni usanii tu..rakashobayatattaaaaa yayyyy
 
Dini zinavituko sana, Utakwepa kunena kwa lugha utakutaha na Kuabudu Sanamu, utakwepa sanamu utakutana na mademu 70 yani ni usanii na Urofa mtupu mara maji ya upako na ujinga mwingine. Afu hapo ubakuta jitu zima na midevu yake anafuata older za kitoto/kike.
Umrsahau mito inayotiririka Konyagi,Amarura ,Safari,Balimi, Kimpimu na Wanzuki!
 
Wakuu,

Hapa duniani Kuna Imani nyingi, Kuna watu ambao hawaamini Mungu (atheists), Kuna waislam,Kuna wabudha. Kuna wakatoliki,wasabato na Kuna hawa wahusika wenyewe (walokole na wengineo).

Ninapenda kujua mitazamo yenu juu ya Hawa watu kunena kwa lugha.

Je ni Mungu au sio?

A) Wanaosema ni Mungu (walokole nk.)
Mechanism ikoje? Ukiwa unanena unajisikiaje? Je unajielewa unachosema?Nani anacontrol mdomo wako?Unapanga cha kuomba? Kuna faida gani?

B) Wanaosema si Mungu
Mechanism ikoje? Ni kweli wananena au usanii tu? Je nini hufanyika pale? Kwanini walokole wengi waumini wa kawaida tu nao wanene? Kuna siri gani nyuma ya kunena kwa lugha? Je wanajitambua au wanatawaliwa na nguvu nje ya akili Yao? Ni nguvu gani hiyo? Nini huendelea kwenye ubongo wa mtu pale anaponena kwa lugha?(mental state)

Uhakika Bro Mshana Jr Tate Mkuu adriz Che mittoga Walker Water Smotor Surya FaizaFoxy KENZY Mcqueenen Kiranga mwakabonao CAPO DELGADO Blood of Jesus

Kunena kwa Lugha au Glossolalia let me talk on 3 persepectives...

Kisayansi/Afya..

Kunena kwa lugha au Glossolalia kisayansi inakuwa associated na Magonjwa ya Afya ya Akili kama Schizophrenia ,Bipolar na mania...

Kwa sababu Mtu yoyote anayejiona kama anaongea na mtu Mwingine ambaye hamuoni na anaona kama anamuona huku akimwambia vitu visivyoeleweka yeye akiamini Vinaeleweka hiyo 2⁰ Mania au bipolar na huenda ikawa schizophrenia kabisa kwa Visual na mind halucination..

Na haipingiki ukija kwangu unanena kwa lugha nakuchoma Haloperidol za kutosha ili urudi sawa...

Kibiblia na kidini
Haipingiki kwamba Kunena kwa lugha ni karama ya roho ila yenye utaratibu wake katika kuifanya Uataratibu huo umewekwa kwenye 1 wakorintho 14..

Paulo anasema kuwa ziko sauti Nyingi duniani na zote zina maana... 1 Wakorintho 14:10
Screenshot_20231010-080211.png


Na utaratibu aliuweka mzuri kwamba ukitaka kunena kwa lugha basi Wanene wachache na wengine watafasiri kinenwacho.. 1 Wakorintho 14:27-28
Screenshot_20231010-080734.png


Wanachokifanya walokole Ndo kitu Paulo Amekiita kama Wazimu kwenye 1Wakorintho 14 :23-25
na anasisitiza Bora kutoa Hotuba ila sio Kuzungumza lugha isiyoeleweka...
Ieleweke kwamba neno Lililotumika hapo kama wajinga ni
Screenshot_20231010-081749.png


Sasa najua unaweza ukaja ukasema neno kuhusu Wajinga wanapoingia...
Sasa hii ni tafsiri kwa lugha ya Kingereza...

Screenshot_20231010-082959.png


Na pia unaweza ukaona katika Lugha ya Kigreek fungu hilo ni...

"Εἰ οὖν συνέλθῃ ἡ ἐκκλησία ὅλη ἐπὶ τὸ αὐτὸ καὶ πάντες γλώσσαις λαλήσουσιν, εἰσέλθωσιν δὲ ἰδιῶται ἢ ἄπιστοι, οὐκ ἐροῦσιν ὅτι μαίνεσθε; εἰ δὲ πάντες προφητεύουσιν, εἰσέλθῃ δέ τις ἄπιστος ἢ ἰδιώτης, ἐλέγχεται ὑπὸ πάντων, ἀνακρίνεται ὑπὸ πάντων, τὰ κρυπτὰ τῆς καρδίας αὐτοῦ φανερά γίνεται, καὶ οὕτως πεσὼν ἐπὶ τὸ πρόσωπον αὐτοῦ προσκυνήσει τὸν Θεὸν, ἐξαγγέλλων ὅτι ὄντως ὁ Θεὸς ἐν ὑμῖν ἐστιν"

sasa neno " ἰδιώτης" ambalo Kiswahili wametafsiri kama Mjinga lina maana ya Mtu asiyejua,layman ama Mtu kutoka Sehemu nyingine au outsid...

My take kuhusu Kunena kwa lugha kwenye biblia naconclude kama Paulo alivyoconclude tu kwenye hilo 1 Wakorintho 14:36

Screenshot_20231010-084010.png


Na PERSPECTIVE YA MWISHO NI WALE WAFATA MKUMBO..
 
Back
Top Bottom