Kuoa mwanamke masikini

Ulitaka aje kwako na nini bruh 😄
 
Yaani Mwanaume mzima niache kuangalia vitu vya maana anavyomiliki mwanamke katika mwili wake na kichwani mwake nihangaike kufuatilia umasikini au utajiri wake?
 
Sasa mnataka tuweje jamani
Tuwe maskini,tajiri, tuwe na tako, tuwe weupe, tuwe weusi, tuwe na mguu wa bia
Au tuweje jamani mbona hatuelewi????
 

Uko sahihi kiongozi, na ni ngumu sana mwanamke anaetoka kwenye familia ya kimaskini akakosa kukutwisha matatizo mengi yahusuyo ndugu zake.

Kama hutajipanga sawa sawa basi ndio litakuwa anguko lako kiuchumi kwa maana maendeleo hutayaona pamoja na hustlings zako zote..
 
Tena hata hiko kibegi hatakiwi kuja nacho. Kila kitu hukohuko tutapata
 
Unaweka kikao unawaambia mimi sintohusika katika yafuatayo.
1. Kutumikia ukoo
2. Kuletea shida za pesa zisizo namwelekeo
3. Kuacha kufanya mambo ya msingi eti hela imetumika mahali nanikwenu kila siku .
4. Nipo katika kusaidia ujenzi wa nyumba ya wazazi na kuwafungulia biashara basi . Jingine bambaneni na hali zenu je nisingeoa kwenu ingekuwaje??
 
Kweli kabisa mkuu, hilo linaboa na linakwamisha maendeleo binafsi
 
Mwanaume kamili hawezi kumpenda mwanamke kwa kigezo cha kuangalia kipato cha mwanamke, hizo tabia waachie wanawake
 
Vijana wangu wakikua nitawashauri waoe wanawake ambao hawajapishana nao sana level ya uchumi kama kigezo mojawapo.
Mwanamke masikini ni mzigo unless na wewe ni masikini basi tafuta masikini mwenzio.
 
Mtoa mada mimi naomba kufahamishwa, 'mwanamke maskini' ni mwanamke gani kabla sijasema chochote tafadhali..!!
Kuna masikini wa mali na masikini wa maarifa....
Mtoa mada kajikita kwa masikini wa mali.
Mfano familia tu ya kawaida chakula baba, umeme baba, gas baba, ujenzi baba, ada baba inshort kila kitu... mama hela mpaka abane kwenye matumizi anayoachiwa. Baba akianguka kwa lolote basi familia inaanza kuomba omba. Binafsi baba yangu alifariki during a critical time na mama yetu hajawahi tuangusha bila msaada wa mtu yeyote

Binafsi kama mwanamke nimezaa idadi ya watoto ambao hata baba yao asipokuwepo ntaweza kuwamudu bila kuwa ombaomba na kitu pekee watakosa ni uwepo wa baba tu na sio gap la uchumi liliopitiliza.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…