Kuongezeka kwa ubaguzi wa kiuchumi, kieneo na ukabila nchini Tanzania

Kuongezeka kwa ubaguzi wa kiuchumi, kieneo na ukabila nchini Tanzania

Wewe kumbe una reasoning ndogo mno,majumba yaliyo vijijin Kilimanjaro huez fananisha n'a popote Kijiji tz ,ni Sawa na kuifananisha dar na New-York kwa kigezo kuwa dar pia kuna ghorofa nadhani umeelewa
Awali ni awali tu
Popote kivipi? Inaonekana hujatembea Tanzania vizuri. Ninyi kuzeni Kilimanjaro au wilaya za Wachagga(natoa Mwanga na Same kwa wapare, hawana sifa sana), kwa watu wasiofahamu. Kwa sisi tuliofika kila wilaya huna la kutudanganya.
 
Una umri gani wewe? Upendeleo ulikuwepo miaka yote. Nahisi kuna watu upendeleo umewatega mgongo ndo maana wanalia lia! Walipopendelewa wakasema ni haki yao. tulieni nchi inyooke.
Maendeleo kwa pande zote za nchi ni muhimu. Hivyo hakuna upendeleo ila sasa maendeleo yanafika sehemu zilizosahaulika.
 
Kumbe hujui lolote kuhusu história ya Uhuru pole sana hujui hata nyerere nauli za kwenda un alifadhiliwa na boss aikael mbowe enz hizo?
Huwajui kina nsilo swai? Una miaka umri gani kwanza?
Waliomfadhili ni wengi sana akiwemo na msukuma John Rupia. Kwa historia ndugu yangu hunikamati
 
Serikali lipeni madeni yaliyohakikiwa.
Kweli kuna wanaoumia sana katika utawala huu bila sababu za msingi.
 
Kuna mchagga ametajirika tukamfahamu kwa sababu ya kahawa? Kahawa ilikuwepo na bado ipo Kagera, Mbeya, Songwe(Mbozi) na Arusha. Utasema Arusha Wamasai na Waarusha hawakuwa na elimu ya kutumia kahawa kutajirika na pengine Wanyiha. Hiw about Wanyakyusa wa Mbeya, Wahaya wa Bukoba? Mengi amepata utajiri kwenye kahawa na kufanya biashara Kenya? Shirima wa precision ametajirikia Kahawa?
Kuna matajiri wakubwa na wa Kati tofautisha hiyo kwanza
 
Popote kivipi? Inaonekana hujatembea Tanzania vizuri. Ninyi kuzeni Kilimanjaro au wilaya za Wachagga(natoa Mwanga na Same kwa wapare, hawana sifa sana), kwa watu wasiofahamu. Kwa sisi tuliofika kila wilaya huna la kutudanganya.
Mikoa ambayo sijafika Tanzania hii Ni mwili tu
Hakuna vijiji vyenye majumba makali kuzid UCHAGANI
Mchaga anaonaga fahari mno kujenga nyumban,kuna maeneo Tanzânia hii mtu akijenga nyumba ya bati tu lazma ajipange maana atapigwa ndumba(Nina mifano hai)
Nbs hawakuwa wajinga walipotoa ripoti ya Kilimanjaro kuongoza makaz bora vijijin
 
Kuna matajiri wakubwa na wa Kati tofautisha hiyo kwanza
Matajiri wa kati wapo wenye asili ya kila mkoa. Wapo Wakinga wa Njombe, Waha wa Kigoma, Wajita na Wakurya wa Mara, Wahaya wa Bukoba, Wasukuma wa LZ, kwa hiyo sio wachagga tu wenye matajiri wa kati. Hata wanyiha wa Mbozi wana matajiri wa kati. Sio wivu lkn acheni sifa za kizamani.
 
Kuna mchagga ametajirika tukamfahamu kwa sababu ya kahawa? Kahawa ilikuwepo na bado ipo Kagera, Mbeya, Songwe(Mbozi) na Arusha. Utasema Arusha Wamasai na Waarusha hawakuwa na elimu ya kutumia kahawa kutajirika na pengine Wanyiha. Hiw about Wanyakyusa wa Mbeya, Wahaya wa Bukoba? Mengi amepata utajiri kwenye kahawa na kufanya biashara Kenya? Shirima wa precision ametajirikia Kahawa?

nadhani hukuchukua muda kuisoma kwa utulivu hoja yangu. mimi sikulenga kwenye matajiri wakubwa kama kina Anthony Diallo, Shirima, n.k, bali nimelenga kwa wananchi wa kawaida wa maeneo mbalimbali hapa nchini. na katika hoja yangu nimesema eneo ambalo halina zao la biashara lenye bei nzuri mara nyingi huwa halifaidiki kutokana na uwekezaji wa serikali ktk eneo hilo.

somo la hali ya kiuchumi ya maeneo mbalimbali hapa Tanzania nililipata wakati niko sekondari. nimebahatika kusoma ktk SHULE KONGWE za serikali na nilikutana na wanafunzi toka maeneo mbalimbali ya Tanzania. katika shule kongwe kulikuwa na utaratibu wa kuchukua wanafunzi toka mkoa mmoja kwa wingi kila mwaka. kulikuwa kuna mwaka wanakuja wanafunzi wengi toka mkoa kama Singida, mwaka mwingine watatoka Kilimanjaro, unaofuata Kigoma, n.k n.k.

sasa katika observation yangu niliweza kujua mkoa gani una changamoto za kiuchumi na umasikini kuliko mkoa mwingine kwa kuangalia hali za kiuchumi na mahitaji za wanafunzi waliokuwa wanaletwa kila mwaka shuleni kwetu. nakuhakikishia ukichukua random sample ya mtoto wa Kyela, Tandahimba, Manyoni, Maswa, Vunjo, n.k utaweza kujua eneo gani lina changamoto ya kiuchumi kuliko lingine. Na ukichunguza zaidi utajua kwamba changamoto hizo za kiuchumi zinatokana na uwepo au kutokuwepo kwa ZAO LA BIASHARA lenye bei nzuri, linalolipa, ktk eneo husika.

cc MzalendoHalisi, luambo makiadi
 
Matajiri wa kati wapo wenye asili ya kila mkoa. Wapo Wakinga wa Njombe, Waha wa Kigoma, Wajita na Wakurya wa Mara, Wahaya wa Bukoba, Wasukuma wa LZ, kwa hiyo sio wachagga tu wenye matajiri wa kati. Hata wanyiha wa Mbozi wana matajiri wa kati. Sio wivu lkn acheni sifa za kizamani.
Unajikanyaga mwenyewe hata haieleweki hoja yako Ni ipi
 
nadhani hukuchukua muda kuisoma kwa utulivu hoja yangu. mimi sikulenga kwenye matajiri wakubwa kama kina Anthony Diallo, Shirima, n.k, bali nimelenga kwa wananchi wa kawaida wa maeneo mbalimbali hapa nchini. na katika hoja yangu nimesema eneo ambalo halina zao la biashara lenye bei nzuri mara nyingi huwa halifaidiki kutokana na uwekezaji wa serikali ktk eneo hilo.

somo la hali ya kiuchumi ya maeneo mbalimbali hapa Tanzania nililipata wakati nasoma shule. nimebahatika kusoma ktk shule kongwe za serikali na nilikutana na wanafunzi toka maeneo mbalimbali. katika shule kongwe kulikuwa na utaratibu wa kuchukua wanafunzi toka mkoa mmoja kwa wingi kila mwaka. kulikuwa kuna mwaka wanakuja wanafunzi wengi toka mkoa kama Singida, mwaka mwingine watatoka Kilimanjaro, unaofuata Kigoma, n.k n.k.

sasa katika observation yangu niliweza kujua mkoa gani una changamoto za kiuchumi na umasikini kuliko mkoa mwingine kwa kuangalia hali za kiuchumi na mahitaji za wanafunzi waliokuwa wanaletwa kila mwaka shuleni kwetu. nakuhakikishia ukichukua random sample ya mtoto wa Kyela, Tandahimba, Manyoni, Maswa, Vunjo, n.k utaweza kujua eneo gani lina changamoto ya kiuchumi kuliko lingine. Na ukichunguza zaidi utajua kwamba changamoto hizo za kiuchumi zinatokana na uwepo au kutokuwepo kwa ZAO LA BIASHARA lenye bei nzuri, linalolipa, ktk eneo husika.

cc MzalendoHalisi, luambo makiadi
Simple and clear,Kama Kuna atakaebisha hapa basi atakuwa yupo field kufanya "thesis" ya PhD ya ubishi
 
Kamwe nashindwa kupita kimyakimya kwenye mada kama hii inayosononesha moyo.

Wakati huo huo, karibu kila mtu anaimba "Tano Tena", kama utani vile!

Sijui nchii imepatwa na janga gani.

Ni kama wote tumepigwa ganzi tusitambue ni nini hasa kinatokea.

Mimi sijui ni nani atakayekuja kututapisha sumu hii tuliyoonjeshwa sasa, ili taifa letu liendelee kuwa taifa lenye mshikamano kama aliouacha Mwalimu Nyerere.

Eeenh, sasa Mwalimu hata anasimangwa. Wale watoto nao wamekuwa kama mazuzu vile, wanatafuta ulaji, wanapoukosa wanaambiwa sababu ni kuwa baba yao hakufanya kitu nyumbani kwao!
Ukosefu wa taasisi imara ni matokeo ya kukosekana katiba ya wananchi, ambayo leo ukiongea kuihitaji, ni sawa na uhaini. Ipo siku kizazi kijacho kita asi. Kwa sasa ni maandalizi ya uasi huo, na yana andaliwa na watawala kwa kuminya kidogo kidogo uhuru wa wananchi.
 
Hii ni kansa inayotafuna nchi kwa sasa waliokua wasemaji wamezibwa kidomo, bunge linakoroma kabisa na ndo linataka kuongeza miaka ya kutawala.

Hofu yangu ni kua utawala huu jmeweka jiwe la msinhi la ukabila na ukanda.Raisi ajaye atafanya kila jitihada kupendelea kwake na hatojali vipaombele vya taifa. Ubaguzi wa wazi kabisa jnafanyika na hakuna kiongozi yeyote anayekemea.
Siku itakuja matenda yake tutayavuna

Ni kweli kabisa mkuu hii dhambi n mbaya sna kamwe haitotuacha yan akija wa kusini sa Hivi lazima apendelee kusini na mikoa jiran ya kusini na Amin !!Amin!!nakwambia Watu wa kanda ya ziwa hawatokaa waaminike tena kupewa hii nchi sababu wameshaonesha dhana ya Ubaguzi na Ukanda ulopitiliza
 
Ni kweli mkuu ila hivi karibuni umepita mto wami? ukaona utatuzi wa tatizo lililokula maisha ya watanzania wengi linavyoshughulikiwa?
Je hapo ni kanda ya ziwa?
Mh.Mkapa alipofanya bidii ya kuifungua mtwara toka kifungo cha kuwa kisiwa kwa sababu ya miundombinu ya barabara wengi tulimpongeza,hatukusema anajenga kwao bali tulifurahia ukombozi wa wenzetu wa mtwara.

Ikumbukwe kwamba kivuko hicho cha busisi waliowahi kufika hapo watakubaliana na mimi kuwa kinachofanyika sasa hivi
kilitakiwa kufanyika miaka mingi iliyopita na bahati nzuri watanzania tupo huru kwenda kuishi popote ili mradi huvunji sheria za nchi,Mtanzania akiona sehemu fulani imeboreshwa zaidi anaruhusiwa kwenda huko akaishi na kujipatia mahitaji yake.
Mikoa iliyosahaulika inapokumbukwa tuwe wavumilivu kama na wao walivyotuvumilia wakati kwetu kunaendelezwa.

Lakini kwa nini mapato ya kutoka mikoa yote yanapopatikana yapelekwe kanda ya ziwa? Je Unadhani hapo tunagawana vyema kweli keki ya nchi ? Issue syo wami wala mtwara wala dsm walau kila litokanalo na eneo husika lingetumika kuboresha sehem husika ndo mana umaskin hauishi tunajenga mavitu ya kufurahisha lakin ukiangalia kwa kiasi kikubwa hayasaidii,Najua kama una mdogo wako hajaajiriwa wewe hujaongezwa mshahara alafu unafurahia upanuzi wa uwanja mkubwa chatle ilihal kuna uwanja wa mwanza

Tatizo hata kama ww ni mzazi usioneshe kumpendelea sana Mwanao mmoja kuliko wengine utaharibu.
 
Watu wa kanda ya ziwa hawatokaa waaminike tena kupewa hii nchi sababu wameshaonesha dhana ya Ubaguzi na Ukanda ulopitiliza
Huoni nawe unatumbukia katika dhambi ile ile anayofanya aliyepo madarakani sasa?

Kwa nini uhukumu watu wa eneo zima, badala ya huyo anayeonyesha mabaya? Una maana waTanzania wote toka kanda ile hawafai?

Kwani Mwalimu Nyerere naye alitokea kanda hiyo au sio?
 
nadhani hukuchukua muda kuisoma kwa utulivu hoja yangu. mimi sikulenga kwenye matajiri wakubwa kama kina Anthony Diallo, Shirima, n.k, bali nimelenga kwa wananchi wa kawaida wa maeneo mbalimbali hapa nchini. na katika hoja yangu nimesema eneo ambalo halina zao la biashara lenye bei nzuri mara nyingi huwa halifaidiki kutokana na uwekezaji wa serikali ktk eneo hilo.

somo la hali ya kiuchumi ya maeneo mbalimbali hapa Tanzania nililipata wakati nasoma shule. nimebahatika kusoma ktk shule kongwe za serikali na nilikutana na wanafunzi toka maeneo mbalimbali. katika shule kongwe kulikuwa na utaratibu wa kuchukua wanafunzi toka mkoa mmoja kwa wingi kila mwaka. kulikuwa kuna mwaka wanakuja wanafunzi wengi toka mkoa kama Singida, mwaka mwingine watatoka Kilimanjaro, unaofuata Kigoma, n.k n.k.

sasa katika observation yangu niliweza kujua mkoa gani una changamoto za kiuchumi na umasikini kuliko mkoa mwingine kwa kuangalia hali za kiuchumi na mahitaji za wanafunzi waliokuwa wanaletwa kila mwaka shuleni kwetu. nakuhakikishia ukichukua random sample ya mtoto wa Kyela, Tandahimba, Manyoni, Maswa, Vunjo, n.k utaweza kujua eneo gani lina changamoto ya kiuchumi kuliko lingine. Na ukichunguza zaidi utajua kwamba changamoto hizo za kiuchumi zinatokana na uwepo au kutokuwepo kwa ZAO LA BIASHARA lenye bei nzuri, linalolipa, ktk eneo husika.

cc MzalendoHalisi, luambo makiadi
Bado observation haijitoshelezi. Kanda ya ziwa ambayo ni subject katika mada hii ina pamba kama zao la biashara. Kusini wana korosho kama zao kuu la biashara lakini kanda hizo 2 zinatajwa kama kanda mbili maskini kabisa nchi hii.
 
Huoni nawe unatumbukia katika dhambi ile ile anayofanya aliyepo madarakani sasa?

Kwa nini uhukumu watu wa eneo zima, badala ya huyo anayeonyesha mabaya? Una maana waTanzania wote toka kanda ile hawafai?

Kwani Mwalimu Nyerere naye alitokea kanda hiyo au sio?
Hakuna ubaguzi wowote uliofanywa na serikali ya awamu ya 5. Wao wanalilia dominance.
 
Wakati ule uchagani mnapewa upendeleo wa wazi wazi lami hadi vichochoroni,msuya anajimegea umeme hadi migombani usangi huko,sisi wa mtwara wakati kuiona lami hadi uende Daslam,mliishia kutucheka na kutuona malofa,kutudharau na kutubagua kwa kutuita "watu wa kusini" sasa hivi kibwengo kawatia gunzi kunako mnapiga piga mayowe,pumbavu kweli tulieni,malipo ni hapa hapa duniani.

Wewe unajiingizia dole unajitekenya unajichekesha mwenyewe[emoji23][emoji23][emoji23] hivi unadhan maendeleo ya watu wa kask yameletwa na serikali? Labda nkupe mfano mwaka 2019 baada ya serikal kutokujishughulisha kwa chochote ktk jimbo la Vunjo wakazi wote wa vunjo tunaoishi nje ya jimbo na nje ya Tz tulichanga jumla ya Tsh 200,000/= na kutaka kufanya ujenzi wa barabara ya Lami lakin serikali kupitia Kamati ya ulizi na usalama kwa kumtumia DC Kipi warioba wkatumika kuzima zoezi hilo

Na jumla ya zaid ya Tsh 4.2 Bill ilipatikana tukataka kuweka kipande cha Lami Serikal ikaona aibu wakaizima na Kamati ya Harambee ilikua n ya Mbunge James Mbatia Wachungaji Mapadri Madiwani Pamoja na Wananchi wenyewe sasa ww jikunee wee jitekenyee alafu Ujicheke hapo tuambie km tunategemea serikali ya jiwe na wapiga domo kaya wake watuletee maendeleo tulishaamka kitambo
 
Hakuna ubaguzi wowote uliofanywa na serikali ya awamu ya 5. Wao wanalilia dominance.
Sielewi una maana gani.
1. "Hakuna ubaguzi wowote uliofanywa na serikali ya awamu ya 5"? Ubaguzi au upendeleo wa kieneo kidogo katika kanda nzima? Sijaona kama Mara, Simiyu,Shinyanga na hata Kagera wanatofauti yoyote na mikoa mingine isiyokuwa ya kanda ya ziwa. Hata Geita yenyewe sioni kuwa imefaidika sana; ila Chato ni tofauti.

Katika nafasi za ajira serikalini, sijui; lakini je katika nafasi za uongozi katika taasisi na ngazi za juu serikalini kama mawizara, kuna upendeleo huko?

2. "Wao wanalilia 'dominance""? Wao, akina nani? Dominance ya kitu gani?
 
Bado observation haijitoshelezi. Kanda ya ziwa ambayo ni subject katika mada hii ina pamba kama zao la biashara. Kusini wana korosho kama zao kuu la biashara lakini kanda hizo 2 zinatajwa kama kanda mbili maskini kabisa nchi hii.

pamba iliathiriwa vibaya na kuvunjwa kwa vyama vya ushirika vya kanda ya ziwa. uzalishaji wa korosho uliangushwa na azimio la arusha na zoezi la operation vijiji la miaka ya 60 na 70. Na kwa mazao hayo mawili serikali isipokupa bei nzuri imekula kwa mkulima. adui wa kanda ya ziwa na kanda ya kusini ni serikali za chama cha mapinduzi. nashangaa hapa wananchi wamelewa propaganda kwamba adui wa watu wa kusini au kanda ya ziwa ni wachagga au watu wote wa "kaskazini."

katika post yangu nyingine nilizungumzia suala la biashara na mpaka wa Tanzania na Kenya jinsi unavyowafaidisha wananchi wa kilimanjaro. mkulima wa kahawa asipopata bei nzuri Tanzania anaweza kutorosha kahawa yake akauza Kenya. Vivyo hivyo kwa mkulima wa Kahawa wa Bukoba anavyoweza kutorosha kahawa yake akapeleka Uganda. Sasa ukija kwa ndugu zetu wa kanda ya ziwa hawana advantage hiyo.

Kanda ya kusini ina mpaka ambao sio mzuri kibiashara. Kwa muda mrefu mpaka wa Tanzania na Msumbiji kulikuwa na vita vya ukombozi, na sasa kuna changamoto ya ugaidi. Sasa ukija kwenye mpaka wa Tanzania na Kenya kumekuwa na stability ya muda mrefu, na Kenya ndio jirani wa Tanzania mwenye uchumi mzuri kuliko majirani wote. Hata wewe ukiambiwa ukafanye biashara mpakani, utachagua mpaka wa Tanzania na nchi gani?

sijui ndugu yangu una umri gani, lakini nakushauri utafute habari za operation vijiji na jinsi ilivyoathiri uchumi wa wananchi wa kusini. zipo habari za mpaka wananchi kushambuliwa na wanyama wakali kama simba na chui ktk vijiji vipya walivyokuwa wanahamishiwa. azimio la arusha na operation vijiji lilisababisha kuanguka kwa kilimo cha mazao ya korosho na mkonge.
 
pamba iliathiriwa vibaya na kuvunjwa kwa vyama vya ushirika vya kanda ya ziwa. uzalishaji wa korosho uliangushwa na azimio la arusha na zoezi la operation vijiji la miaka ya 60 na 70. Na kwa mazao hayo mawili serikali isipokupa bei nzuri imekula kwa mkulima. adui wa kanda ya ziwa na kanda ya kusini ni serikali za chama cha mapinduzi. nashangaa hapa wananchi wamelewa propaganda kwamba adui wa watu wa kusini au kanda ya ziwa ni wachagga au watu wote wa "kaskazini."

katika post yangu nyingine nilizungumzia suala la biashara na mpaka wa Tanzania na Kenya jinsi unavyowafaidisha wananchi wa kilimanjaro. mkulima wa kahawa asipopata bei nzuri Tanzania anaweza kutorosha kahawa yake akauza Kenya. Vivyo hivyo kwa mkulima wa Kahawa wa Bukoba anavyoweza kutorosha kahawa yake akapeleka Uganda. Sasa ukija kwa ndugu zetu wa kanda ya ziwa hawana advantage hiyo.

Kanda ya kusini ina mpaka ambao sio mzuri kibiashara. Kwa muda mrefu mpaka wa Tanzania na Msumbiji kulikuwa na vita vya ukombozi, na sasa kuna changamoto ya ugaidi. Sasa ukija kwenye mpaka wa Tanzania na Kenya kumekuwa na stability ya muda mrefu, na Kenya ndio jirani wa Tanzania mwenye uchumi mzuri kuliko majirani wote. Hata wewe ukiambiwa ukafanye biashara mpakani, utachagua mpaka wa Tanzania na nchi gani?

sijui ndugu yangu una umri gani, lakini nakushauri utafute habari za operation vijiji na jinsi ilivyoathiri uchumi wa wananchi wa kusini. zipo habari za mpaka wananchi kushambuliwa na wanyama wakali kama simba na chui ktk vijiji vipya walivyokuwa wanahamishiwa. azimio la arusha na operation vijiji lilisababisha kuanguka kwa kilimo cha mazao ya korosho na mkonge.
Mazao mengine yote yaathiriwe na ujamaa lakn kahawa haikuathirika? Kwanini?
Sababu pekee ambayo ingeweza kunishawishi mkoa wa Kilimanjaro kuwa mbele kuliko mikoa mingine ni tabia yao ya kurudi nyumbani, kujenga nyumbani, yaani kutolowea huko anakoenda kutafuta maisha. Tabia ambayo makabila mengine ya kaskazini mwa Tanzania tumeiga/tunaiga.
Huwezi kusema wachagga ni wasomi kuliko wahaya au wakerewe au wanyakyusa. Au ukasema wachagga wana hela saana kuliko wakinga. Tofauti ni hiyo tu ya kupenda kwao. Makabila yote yakipenda kwao, vijiji vya Tanzania kote vitapendeza.
 
Back
Top Bottom