Kuota mambo ya shule ni nini tafsiri yake?

Kuota mambo ya shule ni nini tafsiri yake?

Kuota ndoto za shule wakati ulishamaliza shule kitambo kabisa ni jambo baya kabisa na linaashiria kurudishwa nyuma katika maisha kwa namna ya kishirikina. Hapa nilipo napambana na jambo hili kwa maombi manake nimekuwa nikiona mipango yangu mingi ikiburugika na kuchelewa. Ndoto hizi huambatana na kuchelewa katika mafanikio ya mtu kwani mtu anakuwa amerudishwa nyuma au kuwekewa stop kichawi. Shughulika sana na jambo hili ni serious problem la sivyo ni vigumu kutoka kimaisha.
Wandugu hivi hii ishu ya kuota mambo ya shule mara kwa mara huwa ina maana gani kiroho!??

Nimekua nikiota ndoto kua nipo shule eidha o'level au advance na mara chache primary na chuo ila za o'level na advance ni kama kila siku tu.

Mwanzo nilikua napuuza lakini naona sasa inakua too much, karibu kila siku naota nipo shule mara nafanya pepa, nasubiri matokeo, nipo class nasoma, napiga story na wana yani zile moments nlizokua nafanya skuli ila zinakua advanced. Kama ni pepa linaweza kua gumu sana au jepesi sana.

Kuna tafsiri yoyote juu ya hizi ndoto??

Personally naonaga kawaida, may be kazi zetu zinahusu mambo innovative, kila muda tunasoma

Hiyo hali hata mimi ninayo sana, kila mara naota nipo shule. Ila kwa muono wangu naona labda kwa sababu tangu nimemaliza shule life langu halijatulia, msoto mkali so pengine subconsciously ubongo unakuwa unajaribu kunipa relief kwa kunikumbusha moments za shule kwa sababu hicho ndo kipindi sikuwa na changamoto nyingi za kimaisha au pengine ubongo kifikra unatamani siku zirudi nyuma ili nibaki kuwa mtoto kama sehemu ya kutafuta solution ya hali ya sasa.

Naona ni kama nafsi ipo kwenye denial state kuhusu hali ya sasa.

Still fighting.

Nasubiri majibu ya hili..or assumptions juu ya ndoto za namna hii

Na mimi huwa naota pia , tena naota nafanya pepa gumu sioni hata swali la kujibu, au naota nimechelewa kuingia kwenye chumba cha mtihani, nilishawahi kuota sina calculator hivo nikashindwa kusolve maswali kabisa na huwa roho inauma hadi nikishtuka hivi kwamba ilikua ni ndoto ndiyo nashukuru na kupata amani, sijui ni nini tafsiri yake 🤔

Mtu unaota
  • Umechelewa kwenye chumba cha mtihani na wenzio wameshaanza muda mrefu
  • Mtihani hauendi kwako ila kwa wengine wanafanya
  • Kufeli au kuchelewa kwenye interview
 
mimi nakumbuka nilikuwa naota ni kama nimechelewa mtihani..lakin nikawa nakumbuka ni mbona nishafika chuo lazima iwe nilifaulu hapo bado nipo usingizi basi naignore nikiwa usingizini
 
Sasa kama ni hivi, kwanini basi mtu usiote maisha na mazingira mengine ya nyuma ambayo siyo shule?

Yani kwanini iwe shule tu?
Ni swala la kiroho,ndy maana wire waliotoa ushuhuda wameonges kuhusu shule pekee,Hawaoti randomly maanake kuna kitu ambacho ni cha kiroho kinawafanya watu wote wajihisi ndoto ni Ile ile na mazingira ni yale Yale ya mtihani
 
Wandugu hivi hii ishu ya kuota mambo ya shule mara kwa mara huwa ina maana gani kiroho!??

Nimekua nikiota ndoto kua nipo shule eidha o'level au advance na mara chache primary na chuo ila za o'level na advance ni kama kila siku tu.

Mwanzo nilikua napuuza lakini naona sasa inakua too much, karibu kila siku naota nipo shule mara nafanya pepa, nasubiri matokeo, nipo class nasoma, napiga story na wana yani zile moments nlizokua nafanya skuli ila zinakua advanced. Kama ni pepa linaweza kua gumu sana au jepesi sana.

Kuna tafsiri yoyote juu ya hizi ndoto??
Ni jambo la kawaida kuota ndoto za shule kwasababu ni kipindi ambacho umetumia muda mrefu wakati unakua na ni kipindi ambacho Ubongo wako ulikuwa unajifunza vitu vingi sana.
Binafsi sidhani kama ni tatizo, hizo imani za kiroho kama wanazosema watu wengine ni masuala ya kiimani na kila mtu ana uhuru wake wa kuamini ila sidhani kama yana mashiko sana.
Mimi binafsi nmeshaota sana na hata last month tu nimeota nataka kufanya mtihani wa form IV mimi nlishafanya huu mtihani lakini ni zamani sana 2005 (ndo mwaka niliomaliza form IV) akanambia rudi nyumbani, na hakuna kitu kilichonitokea as of now.
Kingine mtoa mada inawezekana unaota sana ndoto za shule kama unajiandaa kufanya program za masomo iwe kujiendeleza ngazi za elimu au mafunzo ya muda mfupi kwahiyo Ubongo unajaribu kurecall matukio ya nyuma enzi unasoma
 
Hii hali nilidhani ni mimi pekeangu, nimeshangaa kuona tupo wengi kwakweli.

Kuna siku huwa naota yamebaki masaa machache kuingia kwenye mtihani, wakati huo sijafanya maandalizi yoyote ya mtihani huo, kitu ambacho ni tofauti sana na maisha yangu ya shule ambapo ilikuwa ni lazima nifanye maandalizi mapema.

Ipo ndoto nyingine ile unapewa karatasi ya mtihani, unakuta mtihani ni mgumu balaa, unakutana na maswali ambayo kamwe hayaonekani Kama umewahi jifunza kuhusiana na hayo maswali.

Kama walivyosema wengine, unakuta paper ina maswali mengi ambayo muda wake ni Kama masaa matatu, lakini unajikuta umebakiwa dakika 30 na hujajibu swali lolote.

Nilikuwa najiuliza mbona hizi ndoto zinajirudia, lakini leo nimepata mwanga kidogo.
 
Kuna mtaalam mmoja nilimuuliza baada yakuandamwa sana na ndoto za primary na O-level wakati huko nilishatoka kitambo sana na hata vyuo pia ni long nilisha maliza. Aliniambia kuna jamaa wanapambana ili nisisonge mbele kimaisha. Nikapotezea.... ila sasa nahisi kama kuna ukweli fulani.
 
Kwa wale wote ambao wanaota wapo shule au wanafanya mtihani au mazingira yoyote ya shule hii ni ishu ya kiroho na jibu ni hili hapa;

Inakukumbusha kwamba kuna Jambo ulikuwa unalifanya na sasa either umeliacha au umeamua kupotezea,so kiroho unakumbushwa kulirudia maana Lina manufaa sn kwako endapo utafanikisha

Tupo duniani,na dunia ina mambo mengi sn ambayo shetani anapenda tusifanikiwe,so unapoota hivi maana yake ni Yule mtu wa ndani anakukumbusha kuirudia Ile njia(Jambo) ambayo umeiacha,na sasa ni km imeota majani..Kaa tafakari ni Jambo gani ambalo haujalikamilisha na sasa linakuhitaji ulirudie..Na pengine ndy Jambo ambalo lingeweza kuyabadilisha maisha yako endapo utaamua kukomaa nalo Ila negative false ( shetani) anataka usifanye hiko kitu

Satoh Hirosh

Mimi niliacha shule kidato cha pili kutokana na matatizo ya kifamilia. Sasa hapa kama umenipa truth, sijui inakaaje hapo?
 
Hii hali nilidhani ni mimi pekeangu, nimeshangaa kuona tupo wengi kwakweli.

Kuna siku huwa naota yamebaki masaa machache kuingia kwenye mtihani, wakati huo sijafanya maandalizi yoyote ya mtihani huo, kitu ambacho ni tofauti sana na maisha yangu ya shule ambapo ilikuwa ni lazima nifanye maandalizi mapema.

Ipo ndoto nyingine ile unapewa karatasi ya mtihani, unakuta mtihani ni mgumu balaa, unakutana na maswali ambayo kamwe hayaonekani Kama umewahi jifunza kuhusiana na hayo maswali.

Kama walivyosema wengine, unakuta paper ina maswali mengi ambayo muda wake ni Kama masaa matatu, lakini unajikuta umebakiwa dakika 30 na hujajibu swali lolote.

Nilikuwa najiuliza mbona hizi ndoto zinajirudia, lakini leo nimepata mwanga kidogo.

Nina miaka 10 sasa naota hizi ndogo.
 
Mshana Jr changia neno hapa.
Hili tumeshalijadili sana hapa na lina tafsiri ya moja kwa moja kiroho kwamba kuna jambo/mambo uliyaanza na hujayamaliza hivyo unakumbushwa kiroho kuyamaliza

Mengine huwa ni ahadi ulizoshindwa kuzitimiza ama kumaliza, nadhiri, madeni, mipango ya maendeleo, mipango ya maisha na sometimes hata visasi
 
Hili tumeshalijadili sana hapa na lina tafsiri ya moja kwa moja kiroho kwamba kuna jambo/mambo uliyaanza na hujayamaliza hivyo unakumbushwa kiroho kuyamaliza

Mengine huwa ni ahadi ulizoshindwa kuzitimiza ama kumaliza, nadhiri, madeni, mipango ya maendeleo, mipango ya maisha na sometimes hata visasi
Kwangu naona kuna nadhiri niliweka sijamalizia, kuna uhusiano wowote na watu kupambana usipate maendeleo?
 
Kwanini kutokamilisha jambo huhudishwa na shule?
Miaka 20 ya mwanzo ya mwanadamu imejaa mafunzo ya msingi
Kuhusu ujuzi
Kuhusu mahusiano
Kuhusu imani nk
Katika hayo mafunzo kuna mafunzo ya KIADA na mafunzo ya ZIADA.. mafunzo ya kiada huwa na kikomo na haya ndio roho hudili nayo
Roho haina ziada .. Roho ni timilifu hivyo hutenda kwa ukamilifu.. Ukamilifu wa hatua yoyote rasmi ya mafunzo na elimu ni nyaraka ya kidunia iitwayo CHETI.. Na cheti hutolewa baada ya kufanya mtihani/mitihani ama kushiriki mafunzo fulani

Utaenda sekondari kwakuwa ulimaliza darasa la saba na kupata cheti baada ya kufanya mtihani.. Kufaulu ni jambo lingine hapo. Hali huwa hiyo hiyo mpaka elimu ya juu kabisa
Kwa muktadha huo basi usipokamilisha jambo lolote kiroho litakurudisha nyuma ulikotoka kwenye elimu na maarifa uliyopata kama kichokoo cha kukupa taarifa uyatimize yakupasayo kufanya hivyo
Unaweza kusahau vyote lakini sio elimu yako na hatua zote za mitihani na ufaulu ulizopitia
 
Kwangu naona kuna nadhiri niliweka sijamalizia, kuna uhusiano wowote na watu kupambana usipate maendeleo?
 
Nitajaribu kujibu kwa kadiri ya uwezo wangu na uelewa wangu.

1.KUOTA UKO SHULE

Kwa tafsiri ya kawaida kabisa ni hivi, tunapeleka watoto shule ili kuwaandaa kwa ajili ya maisha yao ya baadae hivyo TAFSIRI ya mojawapo ya SHULE kwenye NDOTO ni MAANDALIZI.

Hivyo kuota kuwa upo shuleni,TAFSIRI mojawapo ni kuwa KUNA MAANDALIZI (FULANI) ambayo unapewa ALERT kuwa unapaswa KUYAFANYA kwenye specific area ya MAISHA yako..

Au hii yaweza kuwa alert unapewa kuwa Kuna maandalizi fulani ambayo ulipaswa kuyafanya na hukuyafanya na ndio sababu ya ww kukwama mahala fulani fulan kwenye maisha yako hivyo unapewa sign kwamba SHTUKA na chukua hatua ili UTOKE HAPO ULIPONASA

NB:Kibarua sasa ni hiki
NI WAJIBU WAKO KUJUA kujua ni wapi hapo ulipokwama na NI AINA GANI YA MAANDALIZI UNAPASWA KUJIANDAA for future au ulipaswa kujiandaa na hukujiandaa.

2. KUOTA UKO DARASA FULANI AU LEVEL FULANI (primary/secondary/high school au chuo)

Kwa tafsiri niliyosema kwamba Shule ni maandalizi hapo juu basi TAFSIRI ya kuota upo darasa gani au level gani, hii maana yake ni KIWANGO CHA MAANDALIZI unachohitaji KWA HATUA ILIYO MBELE YAKO (future),AU ili uvuke kufika unakopaswa KUWEPO sasa (PRESENT) au ili UTOKE ULIPONASA ambapo ndio sababu ilio ku hold usipige hatua hadi leo (PAST) (kimaisha kiafya kijamii kicheo kiroho kimahusiano kiuchumi nakadhalika inategemeana tu na MKWAMO wako)

Hivyo kuota uko darasa au level ambayo kimsingi ulishapita yaweza kuwa tafsiri kuwa u need to fix something in you past.Uli pita level hiyo lakin kuna eneo katika eneo hilo hukufanya sawa sawa now it has become ur stambling block so get rid of it first uendelee na maisha mana kwa hapo ulipo maandalizi yale kwenye level ile uliopita hayakua sawa sawa.FIX UR PAST TO UNLOCK UR CURRENT OR FUTURE SITUATION

Ukiota uko LEVEL ya JUU ambayo HUJAFIKA BADO mfano umeota uko high school na wakat elim yako ni secondary au unaota uko Diploma au Degree chuo wakati elim yako ni High school uliishia au unaota uko masters au Phd wakati ulifanya Degree tu basi TAFSIRI yake ni MAANDALIZI unayoyahitaji for FUTURE which just yet and on the way TO COME / HAPPEN TO YOU. Hivyo unahitaji maandaliz ya juu ambayo kwasasa HUNA na usipojiandaa basi UTAKWAMA au UNACHOPASWA KUPATA / KUEPUKA for your FUTURE'S SAKE itakula kwako.


3. KUOTA UNAFANYA MTIHANI.
Tafsiri ya mtihani ni KIPIMO CHA MAANDALIZI uliojiandaa nayo. Unaweza ota uko shule tu na hakuna mtihani maana yake unahitajintubkujiandaa lakin unaweza ota uko shule UNASOMA NA BAADAE KUNA MTIHANI, sasa basi;

ukiota unafanya mtihani maana yake ili utoke hapo ulipo au ili ufanikiwe unapokwenda huhitaji tu kufaya maandalizi ili kuvuka maandalizi hayo unayopaswa kufanya YATAPIMWA ,ili kupata GO AHEAD kwenye suluhisho unalohitaji.

3A. KUOTA SOMO UNALOFANYIA MTIHANI
Kwa tafsiri ya shule kama maandalizi na darasa/level uliopo kuwa Kiwango cha maandalizi basi kuota unafanya mtihani wa somo FULANI tafsiri moja wapo ya hii kitu ni AINA YA MAANDALIZI UNAYOHITAJI. hivy ukiona unaota sio tu uko shule bali uko level flan na pia unafanya mtihani tena mtihani wa somo fulani maana yake ndoto hii inakuwa MORE SPECIFIC kukusaidia kujua EXACTLY what you are supposes to DO TO PREPARE URSELF.It is ur task to find WHAT WHEN HOW.

3B. KUOTA UNAFANYA MTIHANI MGUMU SANA AUBWA KAWAIDA AU MWEPESI

Tafsiri iko wazi..Huu ni ugumu au wepesi wa JARIBU /TEST that is ahead of you..Kwamba kipimo utakachopimwa kitakua ndani ya uwezo au nje ya uwezo wako kulingana na maandalizi uliofanya.

3C.KUOTA UME FELI AU UMEFAULU
Hii nadhan kwa maelezo marefu niliotoa hapo juu nadhani itakuwa HOMEWORK rahis tu kujiongeza
Na maranyingine unaota mpaka MARKS ULIZO SCORE.

4.KUOTA UKO DARASANI NA WATU WENGINE UNAOWAJUA AMBAO KIMSINGI WALIKUTANGULIA KUSOMA ILA UNAOTA UKO NAO DARASA MOJA AU MNAFANYA MTIHANI MMOJA AU MKO SHULE MOJA.

Hii nadhan ukielewa maelezo yangu haponjuu utaweza kujua maanda yake nini

5. KUOTA UKO DARASA HILO/ LEVEL HIYO MARA KWA MARA.
Pia waweza kuta unaona unafanya mtihani huo mara kwa mara au uko shule hiyo hiyo mara kwa mara..Hii pia ina maelezo yake na kwa kiasi unaweza ukajiongeza mwwnyewe kw maelezo marefu niliokwisha tangulia kuyatoa hapo juu.

6. MSISITIZO.
Ukiona unaota ndoto hiz mara kwa mara basi USIPUUZIE chukua hatua .

Kwasababu gani?
Kwasabau simetimes SIO KILA NDOTO ya kuwa nayo SERIOUS maana ndoto zingine huja kwa sababu umewaza sana jambo au kwasababubu ya shughul na mambo kuwa mengi so mind ina mix mafile lakin sometimes ndoto yaweza kuwa inatoka kwa Mungu/mungu unayemwamini wewe ili kukuonya na kukupa ONYO au TAHADHARI about future au ALERT wapi umekwama ili UTOKE.

ni hayo. Am open for critisism.
Eyce Carleen Mshana Jr Pascal Mayalla to yeye Vishu Mtata financial services
 
Wandugu hivi hii ishu ya kuota mambo ya shule mara kwa mara huwa ina maana gani kiroho!??

Nimekua nikiota ndoto kua nipo shule eidha o'level au advance na mara chache primary na chuo ila za o'level na advance ni kama kila siku tu.

Mwanzo nilikua napuuza lakini naona sasa inakua too much, karibu kila siku naota nipo shule mara nafanya pepa, nasubiri matokeo, nipo class nasoma, napiga story na wana yani zile moments nlizokua nafanya skuli ila zinakua advanced. Kama ni pepa linaweza kua gumu sana au jepesi sana.

Kuna tafsiri yoyote juu ya hizi ndoto??
Uliota kwa muda gan sasa week au siku kadhaa zimepita tafsir yake unakumbushwa kuna jambo linakuitaj wewe utatue haraka sanaa kwa kutumia akili kwan kuna sehem linafanyika kwa siri sanaaa mimi nilikua na mgonjwa wa sukar alikua hatumii dawa na anakula vitu vya sukar kwa sir niliota hii ndoto kama week hiv kumbe ilikua ishara ya kunikumbusha wajibu wangu kufuatilia mgonjwa akafariki kumbe alikua anakunywa soda kila siku kimya kimya
 
Back
Top Bottom