Kupatwa kwa jua Jumatatu 8 Aprili 2024

Kupatwa kwa jua Jumatatu 8 Aprili 2024

Tukio la kupatwa kwa jua hutokea wakati mwezi unasimama kikamilifu kati ya Dunia na jua, na kuzuia mwanga wa jua kufika duniani.
Mamilioni ya watu kote Amerika Kaskazini watapata fursa ya kushuhudia tukio la kipekee la asili siku ya Jumatatu wakati kupatwa kamili kwa jua kutaonekana kutoka sehemu za Mexico, Marekani na Kanada.Kupatwa kwa jua kabisa kutafanya anga kuwa nyeusi kwa dakika chache (Picha)
Kupatwa kamili kwa siku ya Jumatatu kutaonekana kutoka sehemu za Mexico, Marekani na Kanada.

Itaingia katika bara la Amerika Kaskazini huko Mazatlan, katika jimbo la kaskazini-magharibi mwa Meksiko la Sinaloa, saa 11:07am saa za ndani (18:07 GMT). Itatoka barani kwenye pwani ya Atlantiki ya Newfoundland, Kanada, saa 5:16 jioni kwa saa za ndani (19:46 GMT).

images - 2024-04-08T140114.947.jpeg


Nchini Marekani, kupatwa kwa jua kutaingia katika jimbo la Texas saa 1:27pm kwa saa za ndani (18:27 GMT) na kuondoka Maine saa 3:35pm kwa saa za ndani (19:35 GMT).

Katika majira hayo kwa upande wa Tanzania itakuwa usiku hivyo haitawezekana kushuhudia tukio hilo.Tukio lijalo la kupatwa kwa jua (partial solar eclipse) ambalo Tanzania itashuhudia ni tarehe 2 August 2027 na Total solar eclipse ikitarajiwa kutokea tena tarehe 9 April 2100.

65136eb61c099d0019ad2098.jpeg
 
Saa mbili usiku, huku itakuwa usiku kwa hiyo hatutaweza kuona.Ila huko Marekani. Mexico na Canada baada ya masaa kadhaa wataanza kuona
duh! Kumbe sie tanzania hatutaona hiyo eclipse ikitokea, tusubiri hadi mwaka fula mwezi na jua vitakapokutana katika njia moja.
 
Asantee Sana Mama SAMIA kwa kuwezesha jua likamatwe na Mwezi kwakweli unafanya kazi kubwa sana
 
Umezaliwa baada ya 2000?
Kuna raisi wa awamu ya 3 alituletea hilo tukio Mubashara kabisa, tukauziwa mpaka miwani ya kuangalizia, Mbeya ndo walilifaidi tukio kwa 100%
Enzi hizo uchawa ulikuwa sio shughuli rasmi?
 
Ayatolah ameanza kutangaza kuwa Allah anaionya USA kwahiyo Mashia wote Waswali sunna.
 
Na wale washenzi WA Kizayuni wanatarajia kuchinja ng'ombe mwekundu na kufanya rituals za kuanza harakati zao za kishenzi za kujenga third temple , au hekalu na kuondoa msikiti wa Alaqsa hapo Temple mount Jerusalem na tunajua maandiko ya dini zote yanasema nini kuhusu hii issue
 
Kuna kitu kitu kibaya kinatokea duniani huu mwaka 2024 kabla ya kuisha , najua kuna watu mtajoke ,ila hii kitu ni serious ,na kuna issues nyingi zinatokea huu mwaka kwa pamoja ,hii sio coincidence ya bure
 
Back
Top Bottom