Kupaua nyumba (Makadirio ya gharama)



mkuu cliff huu mchango wako nimeuleta na kwenye uzi huu,
itapendeza kama mods akina Invisible watapendezwa kuupandisha ujumbe huu kwenye ukurasa wa kwanza
 
Last edited by a moderator:
Asalam Ailekum wandugu,

Nahitaji mtaalam wa kunifanyia makadirio ya ujenzi wa nyumba hususan kupaua kwa kutumia bati. Nyumba ipo Kigamboni jijini Dar es Salaam.

Natanguliza Asante.


--------------------
Naongeza,gharama za kujenga paa zinategemea vitu vifuatavyo
1.aina ya paa -kama ni ya mgongo ama flat
2.roof complexity-kama uwepo wa kona nnyingi ,box zinatofautiana
3.angle ya mwinamo-
4.material tumika -mfano bati,udongo,zege,bati aina gani,vigae,biomass,nyasi....
5.gharama ya mtaalam-msanifu na fundi
6.eneo ilipo nyumba yako toka upatikanaji wa vifaa-
7.upatikanaji wa malighafi
Hivyo unapotaka kujua gharama ni lazima vitu hivi uvitafiti.Nawasilisha
 
kazi za watu hizo wamesomea chuo kikuu miaka minne....watu hao wanaitwa wakadiriaji ujenzi...kikristo wanaitwa quantity surveyors (QS)...NIKUPE NAMBA YAKE UMTAFUTE UONGEZE AJIRA KUTOKA ZILE MILIONI MOJA ZIFIKIE HATA MILIONI MOJA NA MOJA?
 
Mi ya kwangu ina vyumba 3, sitting room, dining, kitchen na vyoo viwil vya ndani. Nataka niweke bati ya m-south. Jumla ya garama itakuwa 2,540,000 tu.hizo garama ni kuanzia bati, mbao na ufundi.
Au kwa vile iko vikindu? Achwni kutisha watu ujenzi inawezekana.
 

Mkuu naomba kujua wapi unanua hizo bati za msouth? na mimi nataka kuezeka mkuu
 
Mbagala lang3 opposite na NMB ATM kuna hardware pale utapata kwa bei poa
 
njoo ofisini kwangu nitakupa ushauri mim nauza bati za rangi na treated timber ni buguruni chama, call 0713283670
 

Mkuu Zumbe, kuna ramani nimeipenda lakini ina Sq M 384, naomba nipe makadirio ya paa kwa mabati ya migongo mipana (I.T)
 
Mkuu Zumbe, kuna ramani nimeipenda lakini ina Sq M 384, naomba nipe makadirio ya paa kwa mabati ya migongo mipana (I.T)

Duu, mkuu hiyo nyumba ni kubwa si mchezo, loh, sijajua paa limekaa style gani ila hapo hazipungui running meter zaid ya 400, running meter moja ALAF ni Tshs. 13,500/=
 
Wakuu

Naomba ushauri wa level ya kuezeka paa. Fundi mwashi anasema zinatakiwa kozi mbili baada ya lintel, na muezekaji anasema zinatakiwa kozi tatu? Nani ni mkweli?

Fundi paa anadai kozi mbili zitafanya madirisha yasipendeze kwamba paa litaonekana liko chini. Fundi mwashi alojenga anasema nyumba iko juu tayari hivyo kozi tatu zitafanya nyumba isipendeze.
 
Wataalam wa hili jukwaa, kwa kuwa garama zimepanda za ujenzi, naaka kupaua nyumba yangu yenye ukubwa wa 16mx27m, nataka kutumia zile bati za kigae....hapo nahitaji mbao ngapi treated za 4x2, na 2x2? na pc ngapi za bati? fundi ninaye ila kwa wastani fundi anaweza kula ngapi kwa nyumba kama hio?
 
Bro, nimepaua recently nyumba ya 16.2 x 14.9 hapa DSM, SAOHILL treated timber ni gharama but ndipo nilipokwenda just for assurance, 4 x 2 nilichukua 180, 2 x 2 nilikosa but fundi alitaka 90 so nikaongeza 4x 2 mbao 50. Bati niiweka msouth IT 4 na niichukua 135 pcs but nadhani fundi alitaka kuniibia coz nilimbana site na siku ya mwisho zilibaki bati 28. fundi amekula 2 mil but ni msumbufu. So gharama ya mbao ilikuwa around 4.7mil, bati ni 7.2 mil,fundi 2 mil, mengineyo kama 0.5 mil. Wish u all da best
 
jamani mim nauza mbao pia ni agent wa mabati kutoka kampuni tatu Alafu, Dragon na Afrina. bati la Alaf migongo mipana gauge28 mita ni 15340,na vigae kuna aina aina tatu 28gauge ya kwanza bei ni 15812 kwa mita moja,pili ni 16166 na tatu ni 17240.Dragoni 28 gauge migongo mipana ni 12000 kwa meter na vigae 13500 kwa mita na mbao ninazo.njooni tujenge pamoja msiogope
 
Kwenye MABATI NA KOFIA mafundi huwa wanaagiza nyingi kuliko mahitaji alafu wanakula timing ukizubaa wanakwiba bati ukikaba sana wanazipiga mbili mbili :frown:
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…