Kupaua nyumba (Makadirio ya gharama)

Kupaua nyumba (Makadirio ya gharama)

mkuu hata mm mwenyewe nimeshutuka kabisa nikasema hiyo bei nitawezaje na mm ingawaje ndo kwanza niko katika msingi wa nyumba kwa hali ya mtanzania wa wakawaida inakuwa ngumu best hiyo bei aliyoitaja huyo mkuu
usihofu mama, iko namna hii,

Nyumba ina sehemu kuu 3
sehemu ya kwanza ni msingi
sehemu ya pili ni boma na
sehemu ya tatu ni paa

kati ya hizo sehemu kuu 3 sehemu ya msingi na sehemu ya paa ni part 2 zinazohitaji umakini sana na zinakuwa na gharama kubwa kidogo,

sehemu ya paa ni part inayotumia skilled labour na ni sehemu yenye risk,
mbali ya swala la kiufundi, paa kwenye nyumba ndo linaweza kubadilisha nyumba iwe nzuri au iwe mbaya,

sasa natoa mfano tu wa nyumba ndogo ya vymba 3 vya kulala, sitting room, dining, kitchen na store jumlisha veranda zote za mbele na nyumba, chukulia mfano hiyo nyumba ina jumla ya ukubwa wa 140sqm,
kutegemea na aina (design) ya hiyo ramani na paa lake labda paa lina ukubwa wa 270sqm

mahitaji ya kupaua mfano wa hiyo nyumba yapo kama ifuatavyo.
1), mbao za dawa, hasa mbao nzuri ni za SAO HILL, kama bati litatumika la Industrial Trough (I.T) (hilo ni bati la migongo mipana, manake mbao za papi hazitakuwa nyingi kama mbao za makenchi, hapo kwa SAO HILL ukubwa wa nyumba kama hiyo (tunayo'assume) jaribu kutenga pesa isiyopungua 3m za mbao tu

2), Bati kama nilivyoainisha hapo juu ni I.T mfano na running meter ni 270 , kwa mabati ya ALAF ya IT gauge 28 wanauza kwa meter moja 13500/= kupitia agent, bila agent ni 13800/= manake ni kwamba bati tu hapo litagharimu karibia 4m

3), kofia na valley labda zipo jumla 40, kofia moja wanauza 21,000/= (hizo ni kofia zenye urefu wa 3m,
manake kofia na valley zinaweza kugharimu karibia milioni moja

4), mengineyo kama misumari ya kupigia makenchi, misumari ya bati, usafiri vyote kwa pamoja weka milioni 1

5), ufundi (tafuta local fundi) labda akakufanyia kwa bei ya 2m,
ila ukumbuke local fundi akija anaagalia nyumba imejengwaje na anabuni tu namna paa litakavyokuwa na si kwa kuffuata ramani inaonyeshaje, tarajia makosa mbali mbali hapo, ila pia na ushauri atakaokuwa anakupa local fundi ujue unaweza kukugharimu wewe baadae nakubaki kulalamika kuwa nilishauriwa hivi na fundi,

kwa maelezo zaidi ni'PM email yako ntakutumia sample za ramani na budget zake na ukipenda unaweza kuzitembelea kama upo hapa dar, au mwanza, arusha na moshi,
 
Daah! nimependa udadavu wako zumbe.
hiyo kwa tofali za saruji sio? vp kwa tofali za choma?
hahaha, mkuu hapo ni udadavuaji wa paa tu, paa halijalishi sana kama umejenga kwa tofari za saruji au za kuchoma, cha msingi nyumba ni imara na inaweza kubeba uzito wa paa, unless unapaua kwa kutumia vigae vyetu vile manake wakati wakujenga boma lazima ufikirie na uzito wa kigae kitakachokaa juu,

nyumba nyingi zinaanza kupiga nyufa mara tu baada ya kumaliza kupaua, hiyo inasababishwa na kupiga hesabu vibaya kwenye msingi
 
usihofu mama, iko namna hii,

Nyumba ina sehemu kuu 3
sehemu ya kwanza ni msingi
sehemu ya pili ni boma na
sehemu ya tatu ni paa

kati ya hizo sehemu kuu 3 sehemu ya msingi na sehemu ya paa ni part 2 zinazohitaji umakini sana na zinakuwa na gharama kubwa kidogo,

sehemu ya paa ni part inayotumia skilled labour na ni sehemu yenye risk,
mbali ya swala la kiufundi, paa kwenye nyumba ndo linaweza kubadilisha nyumba iwe nzuri au iwe mbaya,

sasa natoa mfano tu wa nyumba ndogo ya vymba 3 vya kulala, sitting room, dining, kitchen na store jumlisha veranda zote za mbele na nyumba, chukulia mfano hiyo nyumba ina jumla ya ukubwa wa 140sqm,
kutegemea na aina (design) ya hiyo ramani na paa lake labda paa lina ukubwa wa 270sqm

mahitaji ya kupaua mfano wa hiyo nyumba yapo kama ifuatavyo.
1), mbao za dawa, hasa mbao nzuri ni za SAO HILL, kama bati litatumika la Industrial Trough (I.T) (hilo ni bati la migongo mipana, manake mbao za papi hazitakuwa nyingi kama mbao za makenchi, hapo kwa SAO HILL ukubwa wa nyumba kama hiyo (tunayo'assume) jaribu kutenga pesa isiyopungua 3m za mbao tu

2), Bati kama nilivyoainisha hapo juu ni I.T mfano na running meter ni 270 , kwa mabati ya ALAF ya IT gauge 28 wanauza kwa meter moja 13500/= kupitia agent, bila agent ni 13800/= manake ni kwamba bati tu hapo litagharimu karibia 4m

3), kofia na valley labda zipo jumla 40, kofia moja wanauza 21,000/= (hizo ni kofia zenye urefu wa 3m,
manake kofia na valley zinaweza kugharimu karibia milioni moja

4), mengineyo kama misumari ya kupigia makenchi, misumari ya bati, usafiri vyote kwa pamoja weka milioni 1

5), ufundi (tafuta local fundi) labda akakufanyia kwa bei ya 2m,
ila ukumbuke local fundi akija anaagalia nyumba imejengwaje na anabuni tu namna paa litakavyokuwa na si kwa kuffuata ramani inaonyeshaje, tarajia makosa mbali mbali hapo, ila pia na ushauri atakaokuwa anakupa local fundi ujue unaweza kukugharimu wewe baadae nakubaki kulalamika kuwa nilishauriwa hivi na fundi,

kwa maelezo zaidi ni'PM email yako ntakutumia sample za ramani na budget zake na ukipenda unaweza kuzitembelea kama upo hapa dar, au mwanza, arusha na moshi,


Kwa gharama hizo sidhani Kama watu wangejenga....
 
Kwa gharama hizo sidhani Kama watu wangejenga....
mkuu wewe ulijenga kwa gharama kiasi gani? itakuwa poa kama utaweka na picha ya hiyo nyumba,

labda tu niwatoe wasi wasi wanaotaka kujenga kwamba, kama una kiwanja na nikikubwa kiasi, na unaishi nyumba ya kupanga vyumba viwili, bora jenga hivyo vyumba viwili na upaue kwa bati la kawaida ili uhamie kwako, wakati upo kwako tafuta sasa hela ya kujenga nyumba unayoota kichwani.

shida moja ya client wengi wanapenda vitu vizuri lakini hawaafikiani na bei,

kwa mfano tu anayeishi kwenye nyumba yake masaki hana tofauti na anaishi kwenye kibanda chake cha vyumba viwili mpiji magohe,

mfano mwingine taa (bulb) kazi yake kutoa mwanga lakini kuna bulb ya jero na taa mpaka za laki 7, tofauti ya jero na laki 7 kwa kazi moja ya kutoa mwanga sijui unanipata?
 
mkuu wewe ulijenga kwa gharama kiasi gani? itakuwa poa kama utaweka na picha ya hiyo nyumba,

labda tu niwatoe wasi wasi wanaotaka kujenga kwamba, kama una kiwanja na nikikubwa kiasi, na unaishi nyumba ya kupanga vyumba viwili, bora jenga hivyo vyumba viwili na upaue kwa bati la kawaida ili uhamie kwako, wakati upo kwako tafuta sasa hela ya kujenga nyumba unayoota kichwani.

shida moja ya client wengi wanapenda vitu vizuri lakini hawaafikiani na bei,

kwa mfano tu anayeishi kwenye nyumba yake masaki hana tofauti na anaishi kwenye kibanda chake cha vyumba viwili mpiji magohe,

mfano mwingine taa (bulb) kazi yake kutoa mwanga lakini kuna bulb ya jero na taa mpaka za laki 7, tofauti ya jero na laki 7 kwa kazi moja ya kutoa mwanga sijui unanipata?

Mkuu nimejenga Sana mijengo ya maana Kama mitatu lakini sijawahi mlipa Fundi zaidi ya laki 8 na gharama kubwa ninayokumbuka kuwahi kutumia ni 5 M
 
Mkuu nimejenga Sana mijengo ya maana Kama mitatu lakini sijawahi mlipa Fundi zaidi ya laki 8 na gharama kubwa ninayokumbuka kuwahi kutumia ni 5 M
mkuu fafanua kidogo, ulijenga wapi hiyo mijengo ya maana? na ilikuwa wakati gani? utatutendea haki kama utatuma hata picha moja tu kati ya hiyo mijengo mitatu uliyojenga na kumlipa fundi laki 8, hiyo 5m uliyotumia uliitumia katika part gani ya ujenzi?
 
Kupaua nyumba ya sqm 156 Mbao jumla 220 * 7000=154000 Bati za Alafu za kawaida zenye rangi(Migongo midogo) ft 10 pcs 100 @17000=1700000, Misumari ya bati 20kg @2500=50000, Misumari nch 6 kg 15 3000=45000, Misumari nch 5 kg 10@3000= 30,000. Labour charge 1200000. Hapo tunatumia mbao za kawaida ambazo hazijatibiwa lakini tunapaka oil chafu kwaajili ya kuzuia mchwa. Hizi gharama nimelipa nyumba yangu ipo Iringa manispaa, kama utahtaji nipm nikuunganishe na mafundi. Jumlisha mwenyewe.
 
Last edited by a moderator:
asante sana mkuu kwa kunifafanulia na kunieleza kiundani zaidi nitawasiliana nawe
usihofu mama, iko namna hii,

Nyumba ina sehemu kuu 3
sehemu ya kwanza ni msingi
sehemu ya pili ni boma na
sehemu ya tatu ni paa

kati ya hizo sehemu kuu 3 sehemu ya msingi na sehemu ya paa ni part 2 zinazohitaji umakini sana na zinakuwa na gharama kubwa kidogo,

sehemu ya paa ni part inayotumia skilled labour na ni sehemu yenye risk,
mbali ya swala la kiufundi, paa kwenye nyumba ndo linaweza kubadilisha nyumba iwe nzuri au iwe mbaya,

sasa natoa mfano tu wa nyumba ndogo ya vymba 3 vya kulala, sitting room, dining, kitchen na store jumlisha veranda zote za mbele na nyumba, chukulia mfano hiyo nyumba ina jumla ya ukubwa wa 140sqm,
kutegemea na aina (design) ya hiyo ramani na paa lake labda paa lina ukubwa wa 270sqm

mahitaji ya kupaua mfano wa hiyo nyumba yapo kama ifuatavyo.
1), mbao za dawa, hasa mbao nzuri ni za SAO HILL, kama bati litatumika la Industrial Trough (I.T) (hilo ni bati la migongo mipana, manake mbao za papi hazitakuwa nyingi kama mbao za makenchi, hapo kwa SAO HILL ukubwa wa nyumba kama hiyo (tunayo'assume) jaribu kutenga pesa isiyopungua 3m za mbao tu

2), Bati kama nilivyoainisha hapo juu ni I.T mfano na running meter ni 270 , kwa mabati ya ALAF ya IT gauge 28 wanauza kwa meter moja 13500/= kupitia agent, bila agent ni 13800/= manake ni kwamba bati tu hapo litagharimu karibia 4m

3), kofia na valley labda zipo jumla 40, kofia moja wanauza 21,000/= (hizo ni kofia zenye urefu wa 3m,
manake kofia na valley zinaweza kugharimu karibia milioni moja

4), mengineyo kama misumari ya kupigia makenchi, misumari ya bati, usafiri vyote kwa pamoja weka milioni 1

5), ufundi (tafuta local fundi) labda akakufanyia kwa bei ya 2m,
ila ukumbuke local fundi akija anaagalia nyumba imejengwaje na anabuni tu namna paa litakavyokuwa na si kwa kuffuata ramani inaonyeshaje, tarajia makosa mbali mbali hapo, ila pia na ushauri atakaokuwa anakupa local fundi ujue unaweza kukugharimu wewe baadae nakubaki kulalamika kuwa nilishauriwa hivi na fundi,

kwa maelezo zaidi ni'PM email yako ntakutumia sample za ramani na budget zake na ukipenda unaweza kuzitembelea kama upo hapa dar, au mwanza, arusha na moshi,
 
Ukishapata makadirio basi nakukaribisha nikuuzie mbao kwa BEI YA JUMLA mkuu....Kwa maelezo zaidi piga 0655656565
 
Nyie mnafanya masikhara na paa,jamaa yuko sahihi kabisa,mi nimegonga paa imekula karibu mil 22,nyumba ya mita 17 kwa 21,nimepiga bati ya Kigae ya Jeshini mbao tu imekula 8M,Bati 6M,kofia 1.2 M,Misumari special ya Bati 0.7M,Misumari ya kawaida ya mbao 0.5M,Kofia na Valley 1.2M,Usafiri na Vibarua kwenye mbao,bati,kofia na valley jumla 1M,Ufundi 2.8M.

Msilalamike sana upauaji unategemea mambo mengi kwa mfano ukubwa wa nyumba,aina ya bati,idadi ya mbao,ramani ya paa etc,kwa mfano mtu aliyepiga bati la kawaida,bati la migongo mipana,bati la kigae na kigae hawa lazima watofautiane bei,vilevile bei ya mbao na ufundi wa bati la kigae na bati la kawaida haiko sawa bati la kigae linakula mbao nyingi zaidi,ukubwa wa nyumba ya sqm 140 hauwezi kuwa na gharama sawa ya upauaji na nyumba ya sqm 240, vilevile ramani za paa nyingine ni very complicated kwamba upauaji wake ni mgumu sana hauwezi kuwa bei sawa na mgongo wa tembo,sijui kama mnanielewa?ila kama hamkubali sio kesi nadhani kuna ambao wanaweza kunielewa hata kwa mbali sina la ziada ni hayo tu.
 
Nyie mnafanya masikhara na paa,jamaa yuko sahihi kabisa,mi nimegonga paa imekula karibu mil 22,nyumba ya mita 17 kwa 21,nimepiga bati ya Kigae ya Jeshini mbao tu imekula 8M,Bati 6M,kofia 1.2 M,Misumari special ya Bati 0.7M,Misumari ya kawaida ya mbao 0.5M,Kofia na Valley 1.2M,Usafiri na Vibarua kwenye mbao,bati,kofia na valley jumla 1M,Ufundi 2.8M.
Msilalamike sana upauaji unategemea mambo mengi kwa mfano ukubwa wa nyumba,aina ya bati,idadi ya mbao,ramani ya paa etc,kwa mfano mtu aliyepiga bati la kawaida,bati la migongo mipana,bati la kigae na kigae hawa lazima watofautiane bei,vilevile bei ya mbao na ufundi wa bati la kigae na bati la kawaida haiko sawa bati la kigae linakula mbao nyingi zaidi,ukubwa wa nyumba ya sqm 140 hauwezi kuwa na gharama sawa ya upauaji na nyumba ya sqm 240,vilevile ramani za paa nyingine ni very complicated kwamba upauaji wake ni mgumu sana hauwezi kuwa bei sawa na mgongo wa tembo,sijui kama mnanielewa?ila kama hamkubali sio kesi nadhani kuna ambao wanaweza kunielewa hata kwa mbali sina la ziada ni hayo tu.
Mkuu nimekuelewa vzr sana vipimo vyako na vyangu vinakaribiana sana pesa ya fundi ameniambia 2,5m gharama Zote vifaa na fundi 20m
 
Mkuu nimekuelewa vzr sana vipimo vyako na vyangu vinakaribiana sana pesa ya fundi ameniambia 2,5m gharama Zote vifaa na fundi 20m

Nashukuru kaka kama umenielewa watu wanapeana Moyo humu wanaweza kukopa hela wapaue wakaishia katikati,nyumba ya kupaua kwa 5M hapa Dar sijui itakuwa ya aina gani siipatii picha.
 
Achen kudanganyana kuna mafund wazur wanapaua nyumba kama hyo 1m..nlmtumia mmoja arusha
 
Bati ya alaf red...nyumba kubwa tu...sema nlmsafrsha toka mwanza na alnconect mhndi
 
Ni pm namba yako nikupe cost na benefits za kuezeka kwa kutumia light steel gauge
 
Kwa hiyo fundi anapojenga msingi ni muhimu ajue uzito wa paa?
 
Back
Top Bottom