Kupigwa billioni 75 ni ujinga au upumbavu? Tutaendelea kukubali kufanywa kichwa cha mwendawazimu hadi lini?

Nakuunga mkono na hicho ndicho nilichomaanisha kuwa tukishasaini mikataba tusije kuja baadaye kukimbilia kuvunja haraka haraka bila kutafakari madhara ya uvunjaji holela wa mikataba .Ni lazima kama tunaona kuna mahali watu wetu waliosaini walikosea na tunapata hasara kama Taifa basi yatupasa kukaa mezani na kuzungumza na upande wa pili katika kutafuta muafaka mzuri na utakaokwisha kwa amani na maridhiano yenye afya kwa pande zote mbili.

Tusivunje mikataba kwa mbwembwe halafu tukaanza kulipa kwa maumivu. Tujuwe kuwa anayeumia ni mtanzania anayebebeshwa mzigo wa kulipa fedha hizo.lakini pia tufahamu kuwa hayo malipo na hizi fedha zingeweza kutumika kugharamia shughuli mbalimbali za kiuchumi na miradi ya maendeleo.

Tujisahihishe kwa kutokurudia makosa ya aina hiyo.wasomi wetu waliopewa dhamana wana wajibu mkubwa wa kushauri kwa busara mamlaka zetu ili zinapofanya uamuzi uwe ni uamuzi ambao hautaleta athari na maumivu kwa walipa kodi siku za mbele. watumie taaluma zao kulipa Taifa faida na siyo hasara. Unaweza ukawa na lengo zuri lakini ukitumia njia za mkato ni lazima utaliumiza Taifa letu.Tusiliumize Taifa letu kwa kutoa na kufanya maamuzi yaliyo kinyume cha sheria tulizozisaini sisi wenyewe. Tukumbuke kuwa kama Taifa tumesaini mikataba mbalimbali ya kimataifa,ambayo tunawajibika kuitumikia ikiwepo kushitakiwa huko ambako watu wanasimamia sheria na vifungu vyake tu pasipo kuangalia sura ya mtu wala kesi inamhusu nani.
 
Tatizo si ujinga wetu. Mbina hilo lipo wazi kama milango ya msikitini.


Hakuna mkataba wa Kimataifa utaofuata sheria zako au zake, sheria zipo kabisa kimataifa, ndiyo maana kuna hao "arbitrators wa kimataifa.

Sheria za uchimbaji madini zipo, uchimbaji mafuta, uchimbaji gas, viwanda, wakandarasii, uwekezaji kilimo, mpaka ndoa za kimataifa zina sheria zake.

Tena hakuna kazi nyepesi kama kuwa wakili wa mikataba ya Kimataifa.
 
Wakati akina Lisu na wengine wakionya kuhusu mikataba hii mkawaita majina yote likiwemo la kutokuwa wazalendo..!!

Haya sasa 75B zimepigwa huku na wewe na mimi na wote wanaojiita wazalendo ni muathirika wa jambo hilo. 75B zimepigwa huku CCM, CDM CU etc wakiwa waathirika wa upigwaji huo.
 
Hujaliona hili kwenye DPW?
Wewe kwenye nyuzi za DPW zote umesimama kidete kwa hali sana ya juu kutetea. Je.!! ujinga tulioufanya kwenye hili hujauona kwenye DP world?

Sema tatizo nyie wengine HADI LIWAKUTE NDO MNAANZA KUELEWA WAKATI INAKUWA TOO LATE..!!

Mfano, la DPW

1.
Wapo waliolisema kidini (akina Faiza)

2. Wapo waliolisema Kizanzibar na kibara (akina makamu wa pili wa rais Zanzibar)

3. Wapo waliolisema kijinsia (akina Mongera Getrude)

4. Wapo waliolisema kisiasa ( hapa ndo wamejaa kibao)

Lakini mwisho wa siku ni kama kenge hadi damu itoke masikioni ndo anajua kuwa kaumia. We kumbuka kukamatwa kwa ndege zetu nje ya nchi mara kadhaa..!!
 
Wakati akina Lisu na wengine wakionya kuhusu mikataba hii mkawaita majina yote likiwemo la kutokuwa wazalendo..!!

Haya sasa 75B zimepigwa huku na wewe ni muathirika wa jambo hilo. 75B zimepigwa huku CCM, CDM CU etc wakiwa waathirika wa upigwaji huo.
Waonye nini wapiga porojo wale, wana tofauti gani na wajinga wengine?


Sheria za Kimataifa, uwe au usiwe na mikataba, yaleyale tu.
 
Sasa kwanini nisitetee maendeleo?


Kuna lipi baya kwenye DP World?

Kwani mabaya mangapi yameshaorodheshwa? Huyajui?

Time will tell

Utarudi hapa kuja kusifia MAKUBALIANO NJE YA MAHAKAMA kwamba ni afadhari kuliko kuendelea na kesi

FaizaFoxy, kuhusu issue ya DPW, post yako #208 ndo unachokifanya hapa. Unaendeleza ujinga ulioutaja kwenye post ile
 
Nani alimteua kwenda kushughulikia hiyo kesi?
 
Pascally tafadhali walio ingia mikataba ya ovyo sio tu watanzania ni wanachama wa chama cha mapinduzi ccm tafadhali sanaaa wstukane hao hao wapumba na wajinga.sisi wengine hatumo.
 
Ingewachwa kesi iendelee yangekuwa matrilioni tena hatulipi kwa pesa za madafu. Waliokubali wayamalize nje ya mahakama na walipe hizo tu, wamefanya la maana sana.
Mahakama ni chombo cha kutoa haki. Kama yalifanyika nje ya mahakama inaonekana haki haijatendeka
 
Unamlaumu Mkwere wakati huu uamuzi wa kijinga aliufanya Jiwe?

Una akili kweli wewe sukuma gang?

Ebu ficha huo ujinga wenu wa kushinda mazizini.
 
Wacheni kulaumu mlipoangukia na kusahau mlipojikwaa kwa kutetea na kuficha madhaifu ya Jiwe
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…