Kuporomoka kwa Ghorofa Kariakoo Nov 16: Waziri Mkuu aunda Tume ya watu maalumu 21 - Nov 22, 2024

Kuporomoka kwa Ghorofa Kariakoo Nov 16: Waziri Mkuu aunda Tume ya watu maalumu 21 - Nov 22, 2024

Hapo polisi wanahusika vip unajua kazi ya polisi na je unajua kazi ya jeshi la zima moto au jeshi la uwokoaji? Umekalili vibaya
Mafunzo ya ukakamavu uliyopewa utaacha mtu apoteze maisha huku unamtazama kwa sababu wewe siyo zimamoto au uokoaji? Hao raia wa kawaida wanaofanya hayo wao wamepewa mafunzo? Idiot!
 
yaani nimekuta nawaza sana kama mimi leo asubuhi nilirushwa na umeme wakati nadeki nyumba nzima ilipiga short kila kitu kimezima. sikulichukulia maanani sana ila sasa baada ya kupata taarifa ya kuporomoka nimejikuta nawaza sana. kama hao waliokutwa na umauti wameondoka na kuaga familia zao. wengine ndo walikuwa tegemezi ee Mwenyezi Mungu watie nguvu familia zao na uponye wale waliokutwa na majanga.
Aamen.
 
Asee hii n Hatari vifo visiwe vingi tu...Mali zinatafutwa.
Ila Jiji wajitathmini kwa Majengo yanayojengwa kama Uyoga hapo kariakoo sidhani kama yanafuata ubora unaotakiwa...maana Pale jengo linabeba watu wengi ongezea Uzito wa bidhaa lazima ubora wake uwe mkubwa
 
Mambo
Na mamlaka zinazohusika zipo zinapokea 10pa tu!!!Hii nchi ya kifa*l sana
Mambo mengine tuwe tunajiwajibisha ,wewe unajenga jengo bila kufuata standards ,unasubiri nani awajibike kama sio wewe kwanza kuwajibika ,kama si udumavu wa akili ni nini ?
Au hizo standards walioziweka ni wapumbavu , mtu hata mafundi anaitumia ni wahuni tu wa mitaani ,wewe unategemea nini hapo ?
 
Ni hatari sana.

Tatizo kubwa zaidi lililopo Tanzania ni kwamba Hakuna mamlaka madhubuti za kudhibiti viwango na ubora wa Majengo pamoja na ubora wa bidhaa zingine mbalimbali.
Watanzania tunaishi kwa nguvu ya Mungu tu peke yake.
Inasikitisha mno kwani bado tunalipa pia kodi ili mambo hayo yawezeshwe/yafanyike lakini wapi Kodi imeenda ; huduma na uwajibikaji sifuri.
 
Mwisho wa Mwaka una husianaje hapo?
Uzembe wetu alafu tunatafuta sababu za kijinga hautamaliza matatizo yetu..

Ukisema hivyo ina maana kila linalotokea Sababu ni mwisho wa Mwaka?.
Huzijui codes za mwisho wa mwaka siyo?
 
Polisi badala ya kujitosa kwenye vifusi naona wanazuia watu wasikaribie jengo, hivi hawa polisi zaidi ya kuzuia maandamano kuna jambo lingine wanaloweza kweli? Mishahara wanayolipwa ni ya kazi gani kama majukumu yao wanafanya raia wa kawaida wakati wao ndiyo kazi yao na vifaa wanavyo?
F..v..ck
Police Force and TISS are the Paramilitary Wings of the Ruling Party, don't you know it?
 
Mafunzo ya ukakamavu uliyopewa utaacha mtu apoteze maisha huku unamtazama kwa sababu wewe siyo zimamoto au uokoaji? Hao raia wa kawaida wanaofanya hayo wao wamepewa mafunzo? Idiot!
Sikia si kila idara ina mafunzo yake jeshi la uokoaji wale wanapewa mafunzo yote kikamifu kwaajili ya uokoaji wa matatizo mbalimbali

Polisi pia anapewa mafunzo yake kwaajili ya kazi ambazo atazifanya mda mwingi mfano jinsi ya kupambana na waarifu majambazi sugu

Hapo polisi anaweza toa msaada sawa ila sio kwa uzoefu bali ni kwakujiongeza tu ambapo ikitokea wakati anaenda kutoa msaada wa kuwaokoa hao majeruhi ikatokea shida nyingine na yeye ikaonekana ndio chanzo kesi yote inamuangukia yeye

Pia pale ikatokea watu wakalalamika wameibiwa sana na polisi walikuwepo teyari kesi imeangukia kwao na polisi kufukuzwa kazi ni chap sana

Usichojua hapo utaratibu wa kuwaokoa watu unafanyika na wanajitahidi kusaidia pia
 
Mambo
Mambo mengine tuwe tunajiwajibisha ,wewe unajenga jengo bila kufuata standards ,unasubiri nani awajibike kama sio wewe kwanza kuwajibika ,kama si udumavu wa akili ni nini ?
Au hizo standards walioziweka ni wapumbavu , mtu hata mafundi anaitumia ni wahuni tu wa mitaani ,wewe unategemea nini hapo ?
Huyo mwenye jengo Hadi anatumia hao wahuni wa mtaani mamlaka husika hazioni???
 
Mafunzo ya ukakamavu uliyopewa utaacha mtu apoteze maisha huku unamtazama kwa sababu wewe siyo zimamoto au uokoaji? Hao raia wa kawaida wanaofanya hayo wao wamepewa mafunzo? Idiot!
Wanaweza kupoteza maisha yao au wanaowaokoa kwa sababu hapo unahitajika weledi wa uokozi, kumbuka MV Bukoba 1996 ilizama kwa sababu watu wasio na weledi waliitoboa ili kuokoa watu kumbe lile ombwe lilikuwa ndio linasaidia kutomalizikia kuzaa, mamia wakafa
 
Back
Top Bottom