Kura ya Maoni: Muundo upi wa Muungano unafaa?

Kura ya Maoni: Muundo upi wa Muungano unafaa?

Muundo upi wa Muungano unafaa?

  • Serikali 1

    Votes: 81 23.3%
  • Serikali 2

    Votes: 22 6.3%
  • Serikali 3

    Votes: 241 69.5%
  • Sijui

    Votes: 3 0.9%

  • Total voters
    347
  • Poll closed .
Jamani mnaotaka serilaki zaidi ya moja hebu tafakarini kwa undani zaidi. Tunachohitaji ni muungano wa kweli kweli na siyo serikali zisizokuwa na tija. Wapi duniani kuna serikali zaidi ya moja kwenye nchi moja. Worst senario itakuwa Kufufua serikali ya Tanganyika na kwa masikitiko makubwa kuzika serikali ya Tanzania.
 
wanajf kwa mda mrefu sasa kuelekea utungaji wa katiba mpya kumekuwa na mjadala mkali kuhusu muungano wetu uwe wa muundo upi sasa ningependekeza tuwe na kura ya maoni hapa jf kuhusu muundo wa muungano, upi ni muundo sahihi?

1.serikali moja.
2. Serikali mbili.
3.serikali tatu.


N:b ukiweza kutoa sababu za muundo wa muungano unaoutaka itakuwa vizuri zaidi

baada nyerere kuivamia zanzibar january 1964 , aliwakamata mawaziri wote pamoja na waziri mkuu wa zanzibar na kuwafunga jela za tanganyika , kabla ya huo aliouita muungano

jee hapa kuna muungano wa nchi mbili au huu ni uvamizi

tunataka kuifanya haramu kuwa ni halali ??

Hii kitu haiwezi kuwa milele ,

tanganyika iwaombe radhi wazanzibari na kuwaachia waangalie wenyewe wafanye nini na sio kukaa dodoma na kujipakazia katiba mpya
 
Jamani mnaotaka serilaki zaidi ya moja hebu tafakarini kwa undani zaidi. Tunachohitaji ni muungano wa kweli kweli na siyo serikali zisizokuwa na tija. Wapi duniani kuna serikali zaidi ya moja kwenye nchi moja. Worst senario itakuwa Kufufua serikali ya Tanganyika na kwa masikitiko makubwa kuzika serikali ya Tanzania.

Hali ya kisiasa ilivyo, hilo unalolisema haliwezekani kwa sasa!
 
Jamani mnaotaka serilaki zaidi ya moja hebu tafakarini kwa undani zaidi. Tunachohitaji ni muungano wa kweli kweli na siyo serikali zisizokuwa na tija. Wapi duniani kuna serikali zaidi ya moja kwenye nchi moja. Worst senario itakuwa Kufufua serikali ya Tanganyika na kwa masikitiko makubwa kuzika serikali ya Tanzania.

Tatizo kubwa ni kuwa muungano huu unaonekana kama wa asp na tanu na sasa ccm.
Si muungano wa wananchi.tumesukumwa na upepo tu madaam tumo basi hatuna budi.
Lakini ni kitu cha kulazimishana na ccm kwa kiasi kikubwa wanaitumia ccm au asp znz kuendelea wanachotaka wao. Na sio kinachokubalika pande zote mbili.
Ukweli hakuna tena kuaminiana hasa upande wa znz wamekosa imani .
Utaona hili vurugu huko dodoma looote zaidi ni kuhusu muungano.
Katiba imekua ndii muungano.
Mambo mengine kuhusu haki za binadamu. Usawa.muundo wa serikali.
Uchaguzi
Ardhi
Haki ya kulindwa
Haki ya elimu
Haki ya afya
Haki ya kuishi na kuabudu
Nguvu za rais
Teuzi za rais
Na mengineyo yote watu hawana habari nayo ila muungano.
Hakika upande mmoja hayo mambo niliyotaja hapo juu kwa wazanzibari wengi hayawahusu.wao wana katiba yao .
Mnaona kizungu mkuti cha katiba?
 
Kilichopendekezwa na wananchi ni muundo wa serikali 3 na tume imetenda haki.
Sababu yangu ni kwamba, hata sasa muundo unaofanya kazi ni muundo wa serikali tatu.

1.serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.
2.Tawala za mikoa , na serikali za Mitaa(Tanganyika)
3.serikali ya jamhuri ya muungano wa Tanzania.

Kimsingi rasmu imejaribu kuweka hadharani kila kitu.Mungu akubariki sana Warioba
 
Serikali 2 ndo mpango mzima! Tukiendekeza 3 Serikali ya Muungano itakuwa haina hata ardhi (ardhi si suala la Muungano) na itakuwa ombaomba kwa nchi washirika kwa kuwa haina vyanzo vya mapato vya kwake!
Vipi kama Suala la Ardhi likirejeshwa kua la Muungano utaafiki Serikali 3?
 
baada nyerere kuivamia zanzibar january 1964 , aliwakamata mawaziri wote pamoja na waziri mkuu wa zanzibar na kuwafunga jela za tanganyika , kabla ya huo aliouita muungano

jee hapa kuna muungano wa nchi mbili au huu ni uvamizi

tunataka kuifanya haramu kuwa ni halali ??

Hii kitu haiwezi kuwa milele ,

tanganyika iwaombe radhi wazanzibari na kuwaachia waangalie wenyewe wafanye nini na sio kukaa dodoma na kujipakazia katiba mpya

Mkuu wewe unapendekeza Muungano wa Serikali ngapi??
 
Serikali moja ndo utakuwa muungano wa kweli, ikishindikana basi serikali 3...kwani Tanzania ilitokana na nchi mbili zilizo huru so zinaitajikana kuonekana zote au kuwa na nchi moja, kuliko sasa Tanganyika haionekani wakati Zanzibar inaonekana
 
Liwalo na liwe. Mimi hata ziwe nchi kumi serikali moja hakuna shida coz hata sifaidiki nao kwa lolote zaidi zaidi ya hasara tu.
 
Sawa mzee tumekuelewa ila haliwezi kutekelezeka maana hawa jamaa wanapenda short cut na kuridhishana kwingi bila kufuata misingi

M. M. Mwanakijiji

Bunge la Katiba linaweza kujikuta linatumia fedha nyingi na muda na mwisho likakwama kwenye suala la Muundo wa Muungano kwenye sura ya sita ya rasimu ya Katiba. Lakini hili peke yake si sababu kubwa ya mimi kupendekeza kuwa kabla ya kwenda mbali na kupitia vifungu vingine vya rasimu hiyo wajumbe waamue kwanza suala la muundo wa Muungano kwanza. Kuna sababu moja kubwa.


Rasimu ya Katiba ilivyo sasa imeandikwa na kupangwa ikiwa imedhania (assume) kuwa kutakuwepo na Serikali tatu. Kwamba Ibara zake nyingi na muundo wake umefikiria kuwa Bunge la wananchi watakubali uwepo wa serikali tatu na kuridhia mfumo wa Shirikisho lenye nchi mbili na serikali tatu – Serikali ya Tanganyika, Serikali ya Zanzibar na Serikali ya Muungano.

Kutokana na ukweli huo basi suala la uwepo wa Tanganyika na vyombo vyake vya kiutawala – Mahakama, Baraza la Wawakilishi, Waziri Mkuu (Rais wake) ni la muhimu zaidi kuliko kuendelea na mchakato huu ulivyo sasa. Bunge halipaswi kuendelea na kupitia vifungu vingine vya rasimu bila kuamua kwanza aina ya muundo wa Muungano – kama ni Serikali Mbili, Moja au Tatu kama inavyopendekezwa.

Pande Mbili Zinazokinzana
Hadi hivi sasa ni wazi kuwa upo upande mmoja unaotaka kuendelea kwa mfumo wa Serikali Mbili na wapo wale ambao wanapendekeza mfumo wa Serikali Tatu. Sasa, vyovyote itakavyokuwa kuna matokeo mawili yanayowezekana:

Moja, Wanaotaka Serikali mbili – wengi wakiwa ni wana CCM – wakashinda na hivyo rasimu ya Katiba ni LAZIMA ifanyiwe marekebiso makubwa na Bunge la Katiba ili kuondoa vipengele vinavyozungumzia muundo wa serikali tatu;

Pili, wanaotaka Serikali Tatu – wapo wana CCM na wapinzani – wakashinda na hivyo rasimu ya Katiba kuweza kuendelea bila mabadiliko makubwa ya kimuundo. Hata hivyo kukubalika kwa serikali tatu kutalazimisha mchakato huu wa Katiba ulilvyo sasa usitishwe kwani kwa maoni yangu – na kwa unyenyekevu nayatoa – Bunge hili Maalum la Katiba halipaswi kujadili rasimu ya Katiba ya Muungano bila wawakilishi kutoka vyombo na wananchi wa Tanganyika.

Nini kifanyike basi?


  1. Baada ya Mwenyekiti na Makamu wake kupatikana na wajumbe wote kuapishwa na baada ya taratibu zote za mwanzo kuwa tayari basi badala ya kuanza kupitia ibara za kwanza za Katiba ambazo hazina utata sana napendekeza wajumbe waende moja kwa moja kwenye moyo wa rasimu – Muundo wa Muungano. Hili liamuliwe kabla kwenda kuamua mambo mengine – kama ni serikali mbili au tatu lijulikane mapema kwani ibara nyingine zote (ukiondoa zile za mwanzo) zinasimama na kuanguka na Sehemu ya Sita ya rasimu ya Katiba.
  2. Endapo itapitishwa Serikali Tatu basi Bunge la Katiba lisitiswe kwa muda (indefinitely) hadi pale ambapo Tanganyika itakapokuwa na Katiba yake, Bunge lake na wawakilishi wake ambao wataingia kwenye Bunge la Katiba. Ikumbukwe hadi hivi sasa hakuna wawakilishi wa Tanganyika wa aina yoyote wakati Zanzibar ina wawakilishi wake.
  3. Baada ya Bunge Maalum kuridhia uwepo wa Serikali ya Tanganyika basu Bunge la kawaida liitishwe mara moja na kufanyia marekebiso Katiba ya sasa chini ya Ibara ya 98 ili kuruhusu kuundwa kwa serikali ya Tanganyika na vyombo vyake; mabadiliko hayo ya Katiba yaridhiwe na Baraza la Wawakilishi kwa mujibu wa Katiba.
  4. Mabadiliko hayo ya Katiba ya sasa yaweke utaratibu wa wananchi wa Tanganyika kutunga Katiba yao na kufanya uchaguzi wao mkuu ili kujipatia viongozi wake wa kitaifa na wawakilisi; uchaguzi huo ufanyike mapema mwakani ambapo viongozi wote wa kitaifa watapatikana wakiwemo wa Bunge wa Bunge la Tanganyika (sijui litaitwa Baraza la Wawakilishi au Seneti sijui)
  5. Wakati wananchi wa Tanganyika wanafanya mchakato wa kurudisha serikali yao na vyombo vyake vyote (pamoja na alama zake za kitaifa, wimbo wa taifa, bendera n.k) Mchakato wa Katiba Mpya wa hivi sasa utakuwa umesitishwa.
  6. Baada ya Serikali ya Tanganyika kurudi basi suala kubwa la kwanza ambalo litahitaji kuamuliwa ni kama tunahitaji kuendelea kuwa Muungano. Hili litafanyika kwa kupigwa kwa kura ya maoni pande mbili za Muungano – na endapo kila upande utapata angalau asilimia 60 ya wapiga kura kukubali Muungano basi hatua za kuendelea kuandika Katiba Mpya itabidi zifuatwe; kinyume chake utaratibu wa utengano ufanyike ili hatimaye kupatikane mataifa mawili jirani ambayo yatakuwa na uhuru kamili yakidumisha ushirikiano wa kimataifa wan chi jirani.
  7. Endapo wananchi wa Tanganyika na Zanzibar watataka uwepo Muungano basi Baada ya Serikali ya Tanganyika kurudi na kuanza kazi, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania atavunja Baraza la Mawaziri la sasa na kuzingatia mabadiliko yale ya Katiba (namba 3 hapo juu) kuingiza katika Serikali ya Muungano wa wakilishi kutoka Serikali ya Tanganyika kwa ajili ya masuala ya Muungano na hivyo kupunguza ukubwa. Hili linaweza kuwa rais kufanyika chini ya Rais Kikwete ambaye atasimamia serikali ya mpito kuelekea uundwaji wa Katiba Mpya na Uchaguzi Mkuu Mpya mwishoni mwa mwaka 2015.
Kama kutakuwa na Utengano basi Rais Kikwete atakuwa ni Rais wa Mwisho wa Tanzania iliyoungana na atasimamia serikali ya mpito na makubaliano ya mambo mbalimbali kabla ya Tanganyika na Zanzibar kuachana kuelekea uchaguzi mkuu wa kila nchi. Uwepo wa Serikali ya Tanganyika utasimamia maslahi ya Tanganyika katika kuelekea Utengano huo.

  1. Kama kutakuwa na Muungano wa Serikali tatu basi Bunge Maalum la Katiba liitwe wakati Sheria yake ikiwa imefanyikwa mabadiliko makubwa ya kimfumo ili liakisi uwepo wa Serikali na Wawakilishi kutoka Tanganyika na kutoka hapo mchakato wa Katiba Mpya Muungano uanze upya ili kuhakikisha Katiba Mpya inapatikana kwa njia nzuri zaidi.

Naamini kuendelea na mchakato huu ulivyo sasa bila kuamua masuala haya makubwa ni kujaribu kukwepa kiini cha mgogoro. Wajumbe hawawezi kuendeleea kujadili mambo mengine kabla ya kuamua aina ya Muungano utakaokuwepo; kama utakuwepo. Naamini na napendekeza kuwa waamue kwanza suala la muundo wa Muungano kwani ni kutoka hapo ndiyo mambo mengine yataeleweka.

Napendekeza.
 
:majani7:Kisayansi na ukweli Muundo wa serikali tatu ndio unafaa kwa sasa . Maadamu Zanzibar hawataki Muungano wa serikali moja hatuna namna nasi ni kuwa naTanganyika yetu tuking'ang'ania serikali mbili hakika Muungano utavunjika.
 
Me serikali moja ndiyo mpango mzima, halafu kusiwe na mikoa bali majimbo that means zanzibar itambulike kama jimbo la visiwani ikiwa na count ya inguja na pemba.
 
Serikali mbili kwetu mzigo hizo tatu si ndo pasua kichwa kabisa

Hapana mkuu!! Serikali 3 ni bora zaidi kuliko hizi 2. Na gharama zitapungua sana! Wachambuzi walikokotoa wakaona ni bora 3
 
33333333333333333333333333333333333333333333333333333333333333333333333333333333333333333333333333333333333333333333333333333333333333333333333333333333333333333333333333333333³³³³³³
 
baada nyerere kuivamia zanzibar january 1964 , aliwakamata mawaziri wote pamoja na waziri mkuu wa zanzibar na kuwafunga jela za tanganyika , kabla ya huo aliouita muungano

jee hapa kuna muungano wa nchi mbili au
Hii kitu haiwezi kuwa milele ,

tanganyika iwaombe radhi wazanzibari na kuwaachia waangalie wenyewe wafanye nini na sio kukaa dodoma na kujipakazia katiba mpya

kwa wale tunao amin umoj ni nguvu,hatuwez kufuata mawazo ya kipumbavu km hayo.nchi za ulay zinajiuunga pamoja na utajir wao.so mawazo ya kibaguzi ya watu wachache km nyia,kamwe hatuwez kuyafanyia kazi
 

Huyu hawajui wa znz.
Wa znz hawataki kuvunja muungano . Wanachotaka ni uhuru zaidi ili nchi yao ifaidike na mahusiano na wengine bila kubanwa na masharti ya mungano.
Wawe huru katika katika mambo kiuchumi sarafu mikopo na misaada bila ya kubanwa na masharti ya muungano.
Tumeona miaka 50 namna gani uchumi wa znz ulivo poromoka kutokana na muundo wa muungano. Mfumo wa muungano ndio sababu kubwa ya kuanguka uchumi wa znz ma bila kupata msaada wa maana kutika serikali ya mungano kujikwamua.
Wakati tanganyika ikisaidiwa kujikwamua kiuchumi toka wakati wa mwinyi mkapa na sasa kikwete mazungumzo yote na mashirika ya fedha nje kama world bank IFC au IMF
Tanzania imefanya mazungumzo na mashirika haya kwa niaba ya tanganyika na wamesaidia sana kukwamua uchumi wao kwa kupewa ushauri na fedha . Katika masharti yale tanganyika ilikubali masharti magumu ili kupata kupata misaada hio kutoka mashirika ya fedha.
masharti hayo ni kubinafsisha makampuni na mashirika ya umma,
Kufungulia njia makampuni ya nje kuwekeza
Kubinafsisha ma benki
Na kubwa zaidi ambalo ulikua ni mwiba mkali ni lazima wakubali kushusha thamani ya fedha ya Tanzania.
Kutokana na hali ngumu walokua nayo serikali ya tanganyika ndani ya muungano walikubali kuumeza mwiba huo na kukubali kushusha thamani ya shilingi .
Kabla ya masharti haya USD $ 1 =Tshs 20 tu. Hii imekwenda mpaka sasa ni shs 1630.
Na hali ya uchumi na uwezo wa SMZ wakati huo haikua mbaya ulikua mzuri tu wa kujiweza.
Serikali ya mungano kwa niaba ya mambo ya tanganyika wakapokea misaada mikubwa na mikopo baada ya kukubali masharti ya IMF na World Bank.
Nini kilitokea ? Wakati tanganyika ikifaidika na misaada hio, Zanzibar ndio mwanzo wa kuanza kuporomoka uchumi wake .wao hawakupata fidia yoyote kutokana na Tanganyika kukubali kushuka kwa Shilingi.
Bajeti yake ilianza kuharibika mfumuko wa bei ukuwa juu bei ya mafuta ukawa juu . Wakati tanganyika ikipata misaada kujikwamua zanzibar ikaachwa kufa kabisa kiuchumi.
Muundo wa sasa wa muungano hauruhusu znz kuingia katika mikataba mashauriano au kupata misada kuwa na mahusiano yoyote na mashirika ya fedha au mashirika ya kimataifa kama FAo ,Unicef,UNdp,IMF au hata Comminwealth,OIC au hata mashirika ya mahusiano na umoja wa visiwa vya Indian Ocean !!
Hivyo mfumo uliopo haufai kabisa. Utakua unafaa kama kuna nia ya kuimaliza zanzibar kiuchumi na kuifanya wawe mafukara wa kutupwa.
Nadhani sote nia yetu tunapenda kuona Tanzania bara inaendelea na kusonga mbele na pia tunapenda kuona Zanzibar nao wanaendelea kiuchumi na sio tegemezi.
Kutaka serikali 3 sio kuvunja muungano ni njia nzuri ya kuumarisha kukiwa na njia njema .
Kuwa na serikali tatu sio sababu ya kuanza kuchochea chuki, sio sababu ya Tanganyika kuwabana wazanzibari na kadhalika.
Haubadili mahusiano yetu bali kuleta mfumo mzuri zaidi utaoboresha mahusiano na uchumi wetu.
Huyu mheshimiwa ametaja kuhusu ardhi na wafanyabiashara wa znz walioko walioko bara ni kweli wa znz wapo Bara na wanafanya kazi na biashara lakini wanasaidia kujenga uchumi wa bara na sio znz. Kiserikali znz haifaidiki chochote hakuna hata anaeweka akiba yake katika benki ya znz
Na pia huyu mheshimiwa ni katika watu wa kuogopwa kama ukimwi ni mbaguzi,mchochezi ndio maana maoni yake ameleta upemba na uunguja.
Hasemi kuwa Tanzania bara walotaka serikali 3 ni 66% ila yeye ameona wapemba tu. Ni Racist mkubwa.na hawa ni katika wale ambao serikali ya muungano inapoteza fedha nyingi kuwaweka madarakani ikadhaniwa kuwa wataendelea kuulinda muungano kwa porojo na propaganda.ukweli tanganyika haihitaji kupoteza fedha kuwa na mamluki kutoka znz eti waunge mkono muungano hata kama unaizika znz na kuwafanya omba omba.vibaraka hawa wanazidisha tu ari na morari ya wa znz kuuchukia muungano.
tuufanye muungano huu uwe wa wananchi na wananchi wataupenda na wataulinda , hakutakua na sababu kwa serikali ya bara kuwalinda na kuweka vubaraka kama hawa huku ikigharamika bure.hawa wanapigania matumbo yao na ndio walio influence CCM kuweka msimamo wa serikali 2 japo kwa gharama ya 66% ya watanzania bara waliotaka serikali 3.
Serikali tatu ndio suluhisho la kupata muungano wenye nguvu zaidi.
Hata wakati wa apartheid kule afrika ya kusini walikuwapo waafrika na waliojifanya wazalendo sana lakini walikubali mfumo ule wa kibaguzi .wakakubali kuwa viongozi wa zile bantustans. Na walikubali kupewa uhuru wa hizo bantustan na kupewa "urais" mimi namfananisha huyu seif khatib na buthelezi aliepewa kaji urais wa wazuli !!!
 
Back
Top Bottom