Kusavaivu hadi leo hii wengi wetu bila kupigwa chale tusingetoboa

Kusavaivu hadi leo hii wengi wetu bila kupigwa chale tusingetoboa

UMUGHAKA

JF-Expert Member
Joined
Sep 1, 2021
Posts
2,753
Reaction score
12,932
Nisikuchoshe na Usinchoshe, tusichoshane!

Maisha haya ya kitanzania yaliyojaa dhiki, umasikini, roho mbaya, husda, vijicho, masengenyo na masimango ingekuwa ngumu sana kutoboa kimaisha kama wengi wetu tusingepita kwa kina karumanzira ili kuwekwa sawa.

Kila mtu anafahamu kilichompeleka kwa mganga lakini ukweli ni kwamba watu ndiyo sababu ya watu kwenda kwa waganga!.

Mara nyingi watu wanaofanya twende kwa waganga kwa ajili ya tiba ya kuweka miili sawa ni MASHANGAZI & WAJOMBA (USHANGAZINI na UJOMBANI).

Hadi leo sijafahamu ni kwanini kwenye jamii hii ya watanzania kina-Shangazi na Wajomba mara nyingi kama si zote wamekuwa na husda sana kwa watoto wa ndugu zao,yaani wapo radhi wakaroge huku na huko ili kuona mtoto wa ndugu yao hafanikiwi,na mara zote hizo wanapokuwa wakihangaika na watoto wa ndugu zao huwa wamewasahau watoto wao kwamba wanaendelea kukua na umri kuzidi kusonga, mwisho wa siku wanakuja kushituka watoto wa ndugu waliokuwa wakiwapiga vita wamefanikiwa huku mitoto yao akiendelea kugombania ugali wa mazabe hapo makwao.

Tusingechukua hatua mapema za kwenda kwa Sangoma kuwekwa mili sawa bila shaka mashangazi na wajomba wangekuwa wametumaliza zamani sana.

Kuanzia kizazi cha miaka ya 1970 hadi 1990 ukikuta mtu hana Chale kwenye mwili wake basi yawezekana hakuwa akiishi Tanzania na kama aliishi Tanzania uenda hakuwa na Mashangazi au Wajomba.

Asilimia 90% ya kizazi cha Miaka 1970 hadi 1990 wamepigwa Chale na Chale nyingi zilizopigwa kwa watu hao ni kuwekwa sawa ili mambo yanyooke baada ya kuharibiwa na Ndugu zao hasa Mashangazi na wajomba.
 
Nsikuchoshe na Usinchoshe,tusichoshane!.

maisha haya ya kitanzania yaliyojaa dhiki,umasikini,roho mbaya,husda,vijicho,masengenyo na masimango ingekuwa ngumu sana kutoboa kimaisha kama wengi wetu tusingepita kwa kina karumanzira ili kuwekwa sawa.

Kila mtu anafahamu kilichompeleka kwa mganga lakini ukweli ni kwamba watu ndiyo sababu ya watu kwenda kwa waganga!.

Mara nyingi watu wanaofanya twende kwa waganga kwa ajili ya tiba ya kuweka miili sawa ni MASHANGAZI & WAJOMBA(USHANGAZINI na UJOMBANI).

Hadi leo sijafahamu ni kwanini kwenye jamii hii ya watanzania kina-Shangazi na Wajomba mara nyingi kama si zote wamekuwa na husda sana kwa watoto wa ndugu zao,yaani wapo radhi wakaroge huku na huko ili kuona mtoto wa ndugu yao hafanikiwi,na mara zote hizo wanapokuwa wakihangaika na watoto wa ndugu zao huwa wamewasahau watoto wao kwamba wanaendelea kukua na umri kuzidi kusonga,mwisho wa siku wanakuja kushituka watoto wa ndugu waliokuwa wakiwapiga vita wamefanikiwa huku mitoto yao akiendelea kugombania ugali wa mazabe hapo makwao.

Tusingechukua hatua mapema za kwenda kwa Sangoma kuwekwa mili sawa bila shaka mashangazi na wajomba wangekuwa wametumaliza zamani sana.

Kuanzia kizazi cha miaka ya 1970 hadi 1990 ukikuta mtu hana Chale kwenye mwili wake basi yawezekana hakuwa akiishi Tanzania na kama aliishi Tanzania uenda hakuwa na Mashangazi au Wajomba.

Asilimia 90% ya kiazazi cha Miaka 1970 hadi 1990 wamepigwa Chale na Chale nyingi zilizopigwa kwa watu hao ni kuwekwa sawa ili mambo yanyooke baada ya kuharibiwa na Ndugu zao hasa Mashangazi na wajomba.
Imani tu za kishirikina zimejaa sana vichwani mwa waafrica..

Na hii ni kwasababu watu wengi hawapo bize ingekuwa wapo bize hakuna angekuwa anawaza huu ujinga.
 
Mtajuana wenyewe na mila zenu za kishirikina
Wengine huwa tunasikia tu na asilimia kubwa mna chale mpaka machoni, mgongoni na kifuani

Huwa siwafichi wala kupepesa pindi ninapoona chale lazima nihoji kwa kejeli

Sisi home ilikuwa ni marufuku kuamini haya na ilikuwa wakati mwingine tukiwa watoto mnajua watoto wanasikia mengi kwa udadisi

Sasa ikiwa tumesikia mama fulani ni mchawi basi huwa tunasubiri aingie king kwa mzee
Tunamwambia baba huyu mama mchawi daaa basi atachezea fimbo

Hapo sisi ndio anatujenga kutokuamini upumbavu huu ambao umefanya watu wengi kuwa masikini wa kutupa na sisi tusioamini ndio tunawasaidia wengi

Usipoamini ujinga huu ndio mwanzo wako wa maendeleo na fikra nzuri
Msiwafundishe haya watoto wenu kwani wataamini binadamu ndio mungu
 
Back
Top Bottom