Kushika sana dini kunaweza kukupeleka kubaya. Rafiki yangu aliacha kazi ya Ualimu baada ya Mkuu wa Shule kumtaka anyoe ndevu

Kushika sana dini kunaweza kukupeleka kubaya. Rafiki yangu aliacha kazi ya Ualimu baada ya Mkuu wa Shule kumtaka anyoe ndevu

Dini ya kweli ni ipi na dini ya uongo ni ipi?
sifa za dini ya kweli;
1.Ni lazima ieleze ukweli juu ya maumbile
2,Ni lazima iwe na kanuni na Sheria zinazoendana na maumbile yote
3,Ni lazima itosheleze mahitajio ya mwanadamu ya kimwili na kiroho
4,Ni lazima iwe na mfumo wa maisha uliokamilika
5,iwe ya walimwengu wote na nyakati zote
6,Ni lazima ianishe na kusimamia haki zote za mwanadamu


kinyume chake dini isiyo na sifa hizo maanayake haijitoshelezi na ya uongo
 
Ni jirani yetu huko nyumbani kwetu, pia kuna kaurafiki kwa mbali baina yetu. Likizo sometimes tulikuwa tunajisomea pamoja kwakuwa tulikuwa darasa moja.

Jamaa akawa teacher wa Serikali baadaye. Sasa nasikia walimu wana miiko mingi kutokana na mazingira yao ya kazi, sometimes wanakuwa walezi.

Sasa jamaa hakuacha sunnah ya Mtume akafuga ndevu vizuri. Mkuu wa shule akamwambia Mr nyoa hizo ndevu hii shule ni secular, jamaa akakataa.

Alipoona anazidi kuhimizwa kunyoa uchebe na sometimes kutishiwa kufutwa ajira akamwahi boss wake akaandika 24 hrs resignation letter, mkuu wa shule akaipitisha, na Mkurugenzi akamaliza kazi.

Jamaa sasa kwa moyo mweupe analima kijijini. Kaka yake aliyemsomesha wamegombana baada ya jamaa kupiga kalamu chini lakini anasema hawezi kurudi.
Nahisi jamaa alikua tu ameichoka hiyo kazi akapata kisingizio [emoji28][emoji28]
 
sifa za dini ya kweli;
1.Ni lazima ieleze ukweli juu ya maumbile
2,Ni lazima iwe na kanuni na Sheria zinazoendana na maumbile yote
3,Ni lazima itosheleze mahitajio ya mwanadamu ya kimwili na kiroho
4,Ni lazima iwe na mfumo wa maisha uliokamilika
5,iwe ya walimwengu wote na nyakati zote
6,Ni lazima ianishe na kusimamia haki zote za mwanadamu


kinyume chake dini isiyo na sifa hizo maanayake haijitoshelezi na ya uongo
1. Ukweli wa maumbile! how?

Ni maumbile yote kwa ujumla kuanzia ulimwengu ulivyo na viumbe or..
 
Safi sana! Kupelekeshwa si jambo jema! Halafu mimi nadhani kuna mambo inabidi tukubali kuwa yamepitwa na wakati.

Kwanza mihutasari inaandaliwa ikiwa na lengo miongoni mwa malengo ni kuthamini utamaduni wa jamii. Haya niambie ni utamaduni gani wa mtanzania ambao ndevu ni marufuku? Au je hakuna utamaduni wa watanzania miongoni mwa jamii ambao ndevu kwao ni jambo muhimu miongoni mwa yenye umuhimu? Majibu utapata kwamba hakuna kuheshimu utamaduni wa watanzania bali kuutweza na kuufutilia mbali!

Pili ndevu ni swala la kimaumbile na imekuwa fasheni kwa watu wengi sasa. Haya na tuambiwe wakina Rick Ross na Roma Mkatoliki ile fasheni yao ya ndevu ina madhara gani kwa jamii. Propaganda ya ugaidi imeharibu kila kitu na bahati mbaya viongozi wetu hawataki kabisa kushtuka na ndiyo maana hata vazi la taifa bado ni kigugumizi hadi leo!

Siyo ndevu tu, mimi sioni mantiki ya kumzuia mtu (mwalimu) kuvaa jinsi, msuli, kanzu, shuka, malapa, kobazi, katambuga, dera, mgolore, tisheti na mavazi mengine eti kwa kigezo cha maadili ya utumishi. Mbona mavazi hayo ndiyo mavazi ya wanajamii wetu tena watu wa heshima tu wanavaa huko kwenye jamii sasa kwanini huku iwe nongwa!?

Wenzenu walizuia zamani kwa sababu zilizoendana na mazingira ya wakati huo nyinyi badala muangalie mazingira ya wakati wetu tulionao, bado mnatumia hukumu ya kale kwa mazingira ya sasa
 
Sio kweli kuwa kushika Sana dini kunaweza kukupeleka kubaya ila kwa dini zile za uongo(ambapo mafikio yake ni jahanam,huko ndiko kubaya kuliko kote)!
kinyume cha kushika Sana dini ya kweli (uislam) ndiko kunakupeleka kuzuri(Jannah)ambapo ndipo mafikio mazuri kabisa ya mwanadamu.
Allah atuongoze katika njia sahihi na tusife ila tumekuwa waislam kamili!
Acha bana.. dini ya ukweli, dini ya uongo... Uthibitisho "Trust me bro"
 
Huyo jamaa alikuwa sahihi , kufuga ndevu kuna tatizo gani.?


MTU mweusi haelewi nini nini !! MTU Kama imani yake inamwambia hivyo kufuga ndevu ni sunah basi muacheni afuge tu.


Mashuleni sahivi kuna masomo ya dini wanakuja mashekh na maustadhati kufundisha na wamefuga ndevu na hatusikii kelele.
 
Wengi wa namna hii huishia kwenye makundi ya ugaidi ama maisha yakiwachapa huishia kujuta na kuachana na dini.

Mimi kuna jamaa tulisoma nae chuo Mwaka wa pili akaacha kwa sababu kama hizohizo, aliporudi kitaa kakaa kama miaka miwili ngoma ikawa tight akili zikamrudi akaanza kutafuta opportunity ya kurudi chuo Ardhi
Bora alipata msaada wakurudi chuo wengine wamepotea kwakweli Mungu atusaidie
 
1. Ukweli wa maumbile! how?

Ni maumbile yote kwa ujumla kuanzia ulimwengu ulivyo na viumbe or..
Ukweli kuhusu maumbile,nn lengo la mwanadamu kuwepo Duniani,lengo,dhima
na maumbile ya vyote vilivyomo mfano mbingu,ardhi,nyota,wanyama,mimea n.k
 
Ukweli mchungu.
Mod hakujua kusoma wala kuandika mpaka anakufa, na wafuasi wake Wana litambua Hilo,
Lakin mod amewatrick Kwa kuwaogopesha Sana watu, it was psychological manipulation
Jahanamu kuchomwa Moto milele, jahna mabikira kama wote + Mito ya pombe
 
Mkuu inategema na Madhahab Gani?
Niliwahi kuwa Salafiya.na Answar pia..
Usipofuga Ndevu hata swafu ya Mbele ya Swala utaisikia tu utapelekwa safu ya Nyuma..
Na utapigwa Vijembe na kuitwa mwanamke..

Kuna hadithi Nyingi wanazo za kuhalalisha wasemacho kuwa Ni sunna Zenye Faradhi ndani..
Kama hujawahi kuwa hilo dhehabu huwezi kunielewa
Mimi ndo wange niponda mawe😃😆
 
Back
Top Bottom