Kushika sana dini kunaweza kukupeleka kubaya. Rafiki yangu aliacha kazi ya Ualimu baada ya Mkuu wa Shule kumtaka anyoe ndevu

Kushika sana dini kunaweza kukupeleka kubaya. Rafiki yangu aliacha kazi ya Ualimu baada ya Mkuu wa Shule kumtaka anyoe ndevu

Kumbe Bado haya Mambo yanaendelea?
Mi nilidhani yalikemewa yakaachwa..

Kuna Kiongozi wa Kisalafi Abu Fadhil kassim Mafuta huyu jamaa Ndo Kiongozi wao na wanamuamini sana kwa miaka mingi..Mitafaruku Mingi naona kama yye ndo aanzisha..

Ila waislamu wangepunguza Vurugu za wao kwa wao..
Yataisha tu!

Kwa mfano Qassim Mafuta huyu naye ni changamoto. Anawagawa sana watu. Kazi yake ni kuraddi tu watu. Juzi kati kamraddi Mufti Menk kwamba msimfuate. Sasa yeye ni nani?

Ndiyo maana aliulizwa; ukitoa kuraddi watu, kufuga kwako ndevu na kuvaa kanzu fupi una kipi cha maana ulichokiacha kwenye jamii? Hana! Yeye badala ya kufundisha elimu yeye anafundisha misimamo na kisha anawagawa watu. Qassim Mafuta ni mfitinishanaji tu! Hamna Sheikh pale.

Jamii ya Kiislamu hapa Tanzania licha ya kwamba walifahamu kuwa wana ikhtilafu baina yao ila waliheshimiana kwa tofauti zao. Ila tangu lilipozuka kundi la salafi/Answar sunna kila kitu kikawa tofauti, zile ikhtilaf wao wamezifanya aqida/itikadi na matokeo yake wanaleta vurugu kwenye jamii.

Laiti kama mimi ningelikuwa na mamlaka ningelipiga pini kundi la Salafi kama walivyofanya Misri. Misri ukiwa na usalafi kama wa Qassim Mafuta wanakukamata ndani.
 
Duniani kote wanafikiria namna ya kuzipata rasilimal za africa, lakini waafrika wanawaza namna ya kwenda mbinguni, hapo hapo nikaachana na usabato rasmi [emoji23]
Umetisha...[emoji38]

Ubinadamu ni kazi/Humanity is a work.
 
Katika Uislam kuna dua ya kuomba kuruzukiwa ufahamu" Ewe Mwenyezi Mungu niruzuku mimi elimu na fahamu yake". Ninachomaanisha ufahamu nao ni riziki.

Unaweza ukawa umesoma lakini ukakosa riziki ya ufahamu. Kama wengine wanavyokosa hii riziki ya maisha ijapokuwa wamesoma. Sasa kwenye dini hawa watu nao wapo.

Ukipima uchumi wa nchi ambao mhusika anaishi unachangiwa na vitu vingi. Unachangiwa na mambo ya halali na mambo yasiyo ya halali. Na uchumi huo huo pengine ndiyo unawezesha Taasisi zako za kidini ziweze kujiendesha.

Kwa mfano kama huyo jamaa mwalimu, yeye ameangalia kwenye ufugaji wa ndevu. Ila amejaribu kutafakari mshahara anaoupokea kutoka serikalini jamhuri inapata namna gani pesa mpaka yeye anapata kwa kupitia mshahara? Serikali inakusanya kodi kwenye maviwanda ya bia huko, kwenye baa n.k

Kwa hiyo mambo mengine ni ufahamu. Uislamu unakutaka uumche Mungu kadri ya uwezo wako ulipoishia. Mambo mengine ndiyo mifumo ilivyo. Bila hiyo mifumo huwezi kuishi. Mwisho wa siku unaweza ukawa gaidi sasa.
Umesema sahihi sana Mkuu, barikiwa 🙏
 
Yataisha tu!

Kwa mfano Qassim Mafuta huyu naye ni changamoto. Anawagawa sana watu. Kazi yake ni kuraddi tu watu. Juzi kati kamraddi Mufti Menk kwamba msimfuate. Sasa yeye ni nani?

Ndiyo maana aliulizwa; ukitoa kuraddi watu, kufuga kwako ndevu na kuvaa kanzu fupi una kipi cha maana ulichokiacha kwenye jamii? Hana! Yeye badala ya kufundisha elimu yeye anafundisha misimamo na kisha anawagawa watu. Qassim Mafuta ni mfitinishanaji tu! Hamna Sheikh pale.

Jamii ya Kiislamu hapa tanzania licha ya kwamba walifahamu kuwa wana ikhtilafu baina yao ila waliheshimiana kwa tofauti zao. Ila tangu lilipozuka kundi la salafi/Answar sunna kila kitu kikawa tofauti, zile ikhtilaf wao wamezifanya aqida/itikadi na matokeo yake wanaleta vurugu kwenye jamii.

Laiti kama mimi ningelikuwa na mamlaka ningelipiga pini kundi la Salafi kama walivyofanya Misri. Misri ukiwa na usalafi kama wa Qassim Mafuta wanakukamata ndani.
Ni kweli kabisa mimi Ninawajua Vizuri sana..
Ninajua Aqida zao Nimewahi kuwa Salafi, nimewahi kuwa Answar..

Hata sheikh mafuta vitabu vyake ninavyo..
Kuan hiki kimoja anaelezea kuhusu Aqida za Kisalafiya na kuwabeza wengine wasiofata Aquda yake..

Hata ukimkamata Mafufa haisaidii kitu kaacha Athari kubwa sana kwenye Jamij Kiusuly na kiitqadi sana sana utazalisha Ugaidi wa kuuana sisi kwa sisi..
Screenshot_20240313_100400_Adobe Acrobat.jpg

Screenshot_20240313_100415_Adobe Acrobat.jpg
 
Hii kitu nimesikia Sheikh mmoja leo asubuh anasema riba dhambi yake ni kubwa kuliko mtoto kuzini na mzazi wake tena sehem takatifu(alisema kwa jina la dini) mfano baba na bintiye au mama na mtoto wake wa kiume, Asee nilishangaa sana kumbe riba ni big deal.
Sote tunajua dhambi ya Uzinzi ilivyo inaogopwa, sasa ndiyo uje Uzini na Mzazi wako kweli?

Mungu aepushilie mbali, huyo sheikh atakuwa alipotoka
 
Atakuwa anakula ndevu zake sahiv kama chakula.Kuna watu wahovyo sana kutaka kulazimisha mambo yao Kila sehemu Kwa kuhisi ndiyo wenye haki kumbe ujinga TU.
No, alitakiwa apande level, awe imam kisha mufti ale kwenye chain ya iman yake sasa akaishia kuwa mfuasi tu
 
Ni jirani yetu huko nyumbani kwetu, pia kuna kaurafiki kwa mbali baina yetu. Likizo sometimes tulikuwa tunajisomea pamoja kwakuwa tulikuwa darasa moja.

Jamaa akawa teacher wa Serikali baadaye. Sasa nasikia walimu wana miiko mingi kutokana na mazingira yao ya kazi, sometimes wanakuwa walezi.

Sasa jamaa hakuacha sunnah ya Mtume akafuga ndevu vizuri. Mkuu wa shule akamwambia Mr nyoa hizo ndevu hii shule ni secular, jamaa akakataa.

Alipoona anazidi kuhimizwa kunyoa uchebe na sometimes kutishiwa kufutwa ajira akamwahi boss wake akaandika 24 hrs resignation letter, mkuu wa shule akaipitisha, na Mkurugenzi akamaliza kazi.

Jamaa sasa kwa moyo mweupe analima kijijini. Kaka yake aliyemsomesha wamegombana baada ya jamaa kupiga kalamu chini lakini anasema hawezi kurudi.
hii ni m,atokeo ya watu kushindwa kuheshimu imani za wenzao. So sad
kweli ndevu zitamfanya mtu ashindwe kufundisha
 
Sema hivi " kuwa na ndevu si lazima kwenye dini yangu".
Yule mwamba anakupa mpaka Aya kuwa bila ndevu huonji pepo.
Hekima za Ukristo:

Mshike sana elimu usimwache aende zake

Asiyefanya kazi na asile

Kila jambo muwe na kiasi

Mbumbumbu pekee ndiye ataacha kazi au shule kwa sababu za kiimani.

Ubinadamu ni kazi/Humanity is a work.
 
umesema sunna, kivipi iwe lazima? mbona mnafanya waislam wengine waonekane kituko? ndevu sio lazima kufuga japo pia haipendezi kwa (mwanaume kunyoa kabisa pakabaki kama shavu kwa mtazamo wangu)
"Marufuku kula nguruwe ISIPOKUWA njaa ikichachamaa kula nguruwe"

Ubinadamu ni kazi/Humanity is a work.
 
Angesubiri afukuzwe kwa kosa la kufuga ndevu. Huenda alikurupuka.
 
Mods naona mmeamua kuchagua kuwa upande wa mtoa hoja kusambaza sumu hii! Kwanini kwenye heading msiondoe hiyo sentensi ya kwanza ikabaki ya pili tu?
Wengine hawa hapa...[emoji2960]

Ubinadamu ni kazi/Humanity is a work.
 
Nenda Znz huko watoto wanakazaniwa Madrasa kuliko shule.

Sawaa, wanakazaniwa kusoma Madrasa na hapo hapo wanasoma secular, kwani kuna shida!

Mfungo wa Ramadhan ukikaribia au kuanza ndio mada za kukashifu Uislamu zinaanza

بِسْمِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ قُلْ يَا أَيُّهَا الْكَافِرُونَ
109:1 Al-Kafirun (The Disbelievers)
Sema: Enyi makafiri!

لَا أَعْبُدُ مَا تَعْبُدُونَ
Siabudu mnacho kiabudu;
109:2 Al-Kafirun (The Disbelievers

وَلَا أَنْتُمْ عَابِدُونَ مَا أَعْبُدُ
109:3 Al-Kafirun (The Disbelievers
Wala nyinyi hamuabudu ninaye muabudu.

وَلَا أَنَا عَابِدٌ مَا عَبَدْتُمْ
109:4 Al-Kafirun (The Disbelievers
Wala sitaabudu mnacho abudu.

وَلَا أَنْتُمْ عَابِدُونَ مَا أَعْبُدُ
109:5 Al-Kafirun (The Disbelievers
Wala nyinyi hamuabudu ninaye muabudu.

لَكُمْ دِينُكُمْ وَلِيَ دِينِ
109:6 Al-Kafirun (The Disbelievers
Nyinyi mna dini yenu, nami nina Dini yangu.
 
Nikiyakumbuka yale yaliyotokea Shakahola ya Kenya nabaki kusikitika Sana.
Imagine mtu anaacha kazi ya urubani yenye mshahara mnono anaenda kufungishwa ili afe aende mbinguni.

Kwa Kweli hapa Africa wajinga Ni wengi sana.
 
Atakuwa anakula ndevu zake sahiv kama chakula.Kuna watu wahovyo sana kutaka kulazimisha mambo yao Kila sehemu Kwa kuhisi ndiyo wenye haki kumbe ujinga TU.

Kwako wewe uliepo gizani ndio utaona ujinga, ila yupo sahihi, kilimo hakimtupi mtu endapo hutafanya ujinga
 
Sawaa, wanakazaniwa kusoma Madrasa na hapo hapo wanasoma secular, kwani kuna shida!

Mfungo wa Ramadhan ukikaribia au kuanza ndio mada za kukashifu Uislamu zinaanza

بِسْمِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ قُلْ يَا أَيُّهَا الْكَافِرُونَ
109:1 Al-Kafirun (The Disbelievers)
Sema: Enyi makafiri!

لَا أَعْبُدُ مَا تَعْبُدُونَ
Siabudu mnacho kiabudu;
109:2 Al-Kafirun (The Disbelievers

وَلَا أَنْتُمْ عَابِدُونَ مَا أَعْبُدُ
109:3 Al-Kafirun (The Disbelievers
Wala nyinyi hamuabudu ninaye muabudu.

وَلَا أَنَا عَابِدٌ مَا عَبَدْتُمْ
109:4 Al-Kafirun (The Disbelievers
Wala sitaabudu mnacho abudu.

وَلَا أَنْتُمْ عَابِدُونَ مَا أَعْبُدُ
109:5 Al-Kafirun (The Disbelievers
Wala nyinyi hamuabudu ninaye muabudu.

لَكُمْ دِينُكُمْ وَلِيَ دِينِ
109:6 Al-Kafirun (The Disbelievers
Nyinyi mna dini yenu, nami nina Dini yangu.
Hii comment niliweka kabla ya Ramadhan. Nina rafiki zangu waislamu ambao wameshaamka katika usingizi. Ukishatambua hizi dini tuliletewa utafika mbali sana. Na tambua kuwa maisha yana sheria zake na dini ina sheria zake. Sio kila sheria au utaratibu wa dini una-apply kwenye maisha. Dini inatusaidia katika malezi ili tuwe na utu(Human Dignity) tukishakuwa watu wazima. Hivi vitu sio kwa waislamu hata wakristu walokole wanaokesha makanisani usiku mzima. Sibagui ujinga, na mjinga akishaambiwa imeisha huo maana ameshakuwa alipoteleza.
 
Back
Top Bottom