Kusoma sana sio kigezo cha utendaji: Nehemiah Mchechu ana degree moja

Kusoma sana sio kigezo cha utendaji: Nehemiah Mchechu ana degree moja

kinadharia ndiyo kiuhalisia siyo. Kujua unachofanya ndicho kinakupa confidence.
hiyo confidence labda bar tu na vyuoni si field.
Sasa kujua si ndo lazima shule iwe kubwa mzee.....vinginevyo utakuwa na uelewa wa kawaida tu, unaelewa kwa nini kule mahospitalini kuna baadhi ya wagonjwa huwa wanapewa rufaa kuwaona madaktari bingwa, kama swala ni utendaji tu si wangewatibu hao hao madaktari wa kawaida, kwa hiyo mchawi shule tu.....​
 
Mkuu, shule kubwa ni lazima ufanane na performance, laa sivyo huo ni ubatili mtupu.
Peformance hata la saba anaweza ku-perform, unaperform vipi kwenye swala la kitaaluma na huna shule. Unajua kwa nini mahospitalini baadhi ya wagonjwa huambiwa wakawaone madaktari bingwa, shule hapo ndo ina determine mkuu siyo hicho unachoita sijui utendaji, huna shule utabaki kufanya mazingaombwe tu.
 
Mtu

Yoyote mwenye elimu ni msomi, ila kigezo cha elimu hiyo aliyonayo/aliyoipata inaleta manufaa gani kwa kada yake au eneo lake la ubobezi, jamii inayomzunguka na nchi kwa ujumla hapo ndio huwa panazua mjadala
Upo sahihi sn wengi wanasoma ajili ya mishahara ipande na kusubiri uteuzi lakini yeye mwenyewe ukimuuliza alisoma kwa sababu zipi hajui
 
Peformance hata la saba anaweza ku-perform, unaperform vipi kwenye swala la kitaaluma na huna shule. Unajua kwa nini mahospitalini baadhi ya wagonjwa huambiwa wakawaone madaktari bingwa, shule hapo ndo ina determine mkuu siyo hicho unachoita sijui utendaji, huna shule utabaki kufanya mazingaombwe tu.
Hao madaktari wanaosahau viwembe ndani ya matumbo ya wagonjwa baada ya operation kuisha hao bila ni mabingwa?

Vp wale waliomfanyia mgonjwa operation ya kichwa badala ya mguu??
 
Hao madaktari wanaosahau viwembe ndani ya matumbo ya wagonjwa baada ya operation kuisha hao bila ni mabingwa?

Vp wale waliomfanyia mgonjwa operation ya kichwa badala ya mguu??
Kufanya operation ni shule inahusika haijalishi kuna makosa yamefanyika ya kusahau mkasi......mambo ya kibinadamu hayo.
 
Katika Kikao cha Wenyeviti na watendaji wa taasisi za Umma kinachoendelea Jijini Arusha ambacho kinaongozwa na Msajili wa Hazina Ndg. Nehemia Mchechu, katika moja ya maongezi yake amekiri ana degree moja na hana mpango wa kuongeza nyingine kwa sasa.

Amezungumza hayo baada ya kuzungumzia suala la Vyuo Vikuu kutokuwa na fedha (kulia ukata) hasa vile vikongwe kama UDSM, IFM na Mzumbe wakati wana wanafunzi wengi waliowafundisha na wapo kwenye taasisi mbalimbali ambao wanaweza kusaidia kuidhinisha fedha zitakazowasaidia kwenye masuala yao kupitia CSR etc.

Akachagiza kuwa atafanya kikao na VCs ( makamu wakuu wa vyuo) ili kujadiliana kuhusu issue tofauti ila hana mpango wa kurudi darasani kuchukua degree nyingine wasije wakamkamata bure (kupata Supplementary n.k) hii moja aliyonayo inamtosha.

Ukiangalia kwa namna historia yake ya ufanyaji kazi na wasifu alionao sasa, unaona kabisa kuwa na ma-degree mengi sio sababu ya kuwa mtendaji mzuri au mwenye sifa ya kuongoza taasisi nyeti, unaweza ukawa na degree moja na bado ukaongoza taasisi nzito na nyeti na bado ukafanya vizuri, uwezo ukiongeza na uzoefu unatosha kabisa kufanya jambo.

Anyway ni hilo tu tuendelee kupambana na kulijenga Taifa letu.
Huu ushauri awapelekee sua kwanza.

Wale jamaa kila siku hakuna hela,ikifika june unashangaa fungu linarudi hazina.
 
🤣🤣Mkuu hapana
Mie nilitoka vyema sana
Nikaamua nilitumikie taifa huku uraiani
Kuna wale Wenye pass
Hata kwenye magroup ya wasap ukichangia hoja wanareact hatari
Unagundua ni inferiority complex
Unakaa kimya,kuepusha malumbano
Basi ni fani na fani, fani yangu ya sheria, LL.B, wenye 1st Class hakuna kesi wanashinda, wenye pass, they are doing great!.

P
 
Katika Kikao cha Wenyeviti na watendaji wa taasisi za Umma kinachoendelea Jijini Arusha ambacho kinaongozwa na Msajili wa Hazina Ndg. Nehemia Mchechu, katika moja ya maongezi yake amekiri ana degree moja na hana mpango wa kuongeza nyingine kwa sasa.

Amezungumza hayo baada ya kuzungumzia suala la Vyuo Vikuu kutokuwa na fedha (kulia ukata) hasa vile vikongwe kama UDSM, IFM na Mzumbe wakati wana wanafunzi wengi waliowafundisha na wapo kwenye taasisi mbalimbali ambao wanaweza kusaidia kuidhinisha fedha zitakazowasaidia kwenye masuala yao kupitia CSR etc.

Akachagiza kuwa atafanya kikao na VCs ( makamu wakuu wa vyuo) ili kujadiliana kuhusu issue tofauti ila hana mpango wa kurudi darasani kuchukua degree nyingine wasije wakamkamata bure (kupata Supplementary n.k) hii moja aliyonayo inamtosha.

Ukiangalia kwa namna historia yake ya ufanyaji kazi na wasifu alionao sasa, unaona kabisa kuwa na ma-degree mengi sio sababu ya kuwa mtendaji mzuri au mwenye sifa ya kuongoza taasisi nyeti, unaweza ukawa na degree moja na bado ukaongoza taasisi nzito na nyeti na bado ukafanya vizuri, uwezo ukiongeza na uzoefu unatosha kabisa kufanya jambo.

Anyway ni hilo tu tuendelee kupambana na kulijenga Taifa letu.
Kwani Msechu ana nini cha ziada?
 
Wenyewe mlisema sisi manesi na wakunga twenye uzoedu wa miaka zaidi ya 15 tuna vyeti feki na tulishazoea kazi zetu kiasi tunaweza kumzalisha mtu kwa miguu bila kutumia mikono huku tuko instagrammar hatufai acheni tuu vyeti vitumike msituumize zaidi tafadhari
Hahaaa, duh! Sikutegemea hii coment, mbavu sina. 😄
 
Ni kweli hakupaswa kusema Ivo....anatuvunja moyo vijana tunaojiendeleza kielimu.Ukweli ni kuwa Kuna tofauti kubwa kati ya degree na masters, labda kama masters unayosoma unasomea vyuo ambavyo ni vya kawaida utabaki vile vile, ila Kuna value kubwa sana unaadd unaposoma masters.Ila kwa mtu mwenye position kubwa kama yake kusoma masters ni muhimu.
Ila tukumbuke pia watu kama hawa ambao wana degree moja lakini uelewa wao na competence huwa ni mkubwa,

Unaweza kuta tangu ahitimu ana practice kitu alichosomea, anafuatilia trends na mabadiliko mbali mbali yanayotokea katika kada yake au eneo lake la ubobezi, anafuatilia tafiti mbalimbali zinazofanywa katika eneo lake la kazi, na anahudhuria semina, warsha na makongamano yanayohusu sekta aliyopo hivyo uelewa wake na skills zinakuwa zinaongezeka kwa sababu ya kuongeza maarifa kila baada ya kupindi fulani baada ya kuhitimu
 
Back
Top Bottom