Kusuasua kwa harakati za ukombozi nchini ni matokeo ya uongozi dhaifu

Kusuasua kwa harakati za ukombozi nchini ni matokeo ya uongozi dhaifu

brazaj

JF-Expert Member
Joined
Jul 26, 2016
Posts
31,698
Reaction score
41,733
Kwamba hawa nao tumawapa majukwaa ya kisiasa na kuwashangilia?


Kwamba tuna hata wenye kujidhania kuwa ni wenye hoja kuliko hata wenye CV zao zinazojulikana kimataifa?
Kwamba tumefikia hatua ya kuwaacha hata wapuuzi kuwanyanyapaa wenye akili zao?

Na Bado tupo tupo tunakenua? Ama kwa hakika haya ni matokeo ya wazi ya ombwe litokanalo na uongozi ulio dhaifu. Watu aina hizi walipaswa kukemewa pasipo na kuwaonea haya.

Udhaifu, iliwaudhi mno aina za kina Yobo. Tusipende mno kusifiwa hata tusipostahili. Udhaifu si tusi, bali dhana sahihi ya ukosoaji yenye lengo zaidi la kujenga.

Kwanini wanakofanikiwa kwenye harakati zao, huko viongozi wao huhama vyama na hata wakabadili washirika bila ya unyanyapaa wa kipuuzi kama wa huku kwetu?

Laila alijiunga na KANU, akawa na Ruto, Kibaki, Kenyatta, Mudavadi, Wetangula, Musyoka, nk na matokeo yake huko mwenye nchi mwabanchi? Ila sisi tumeshindwa kuelewa kutokuwa na maadui wa kudumu kuna faida kubwa kwa nchi zaidi ya faida binafsi.

Kwetu walikuja kina Lowassa(r.i.p), Sumaye, Ngombale(r.i.p) nk ambayo ilikuwa ni hatua njema mno. Tulipiga hatua mbele kiasi gani kipindi hicho? Ni mamburula peke yao wenye kuthubutu kuyabeza mafanikio ya kipindi hicho.

Kwanini iwe dhambi kwa Mbowe, Lissu au Msigwa au awaye yote kuhamia CCM wakati wowote? Au kwa Nape, Januari, Mpina au awaye yote kuhamia CHADEMA au ACT Wazalendo? Hatuwezi kuyaweka maslahi ya nchi yetu mbele?

Utayasikia mamburula mburula, "hatumtaki huyo!" Kwani wewe ni nani ndugu? Au hata kwa CV yako ipi basi yenye kuweza kutushawishi hivyo na wengine basi?

Kwamba kama vipi mkaanzishe chenu au mhame chama? Looh! Kwanini hayo yasiwahusu ninyi?

Shughuli ni watu. Hii nchi haiwezi kukombolewa ndani ya wimbi la ujinga ndugu zangu.

Habari ndiyo hiyo.
 
Suala si kuhama chama bali kukosa ustaarabu na kuanza kuzusha tuhuma zisizo na mantiki dhidi ya uliowaacha kwenye chama ulichohama.

Huko ni kujenga au kubomoa harakati? Wewe unaona Msigwa anafanya vyema kabisa?
 
Suala si kuhama chama bali kukosa ustaarabu na kuanza kuzusha tuhuma zisizo na mantiki dhidi ya uliowaacha kwenye chama ulichohama.

Huko ni kujenga au kubomoa harakati? Wewe unaona Msigwa anafanya vyema kabisa?

Mtu anayo haki ya kusema lolote analoamini.

Kwanini kama kumeoza mngependa Msigwa aseme kupo vizuri?

Kwani kama kupo kama alivyosema si kurekebishwe?

Kwanini kupenda kusikia sifa tu hata ikibidi zisizostahili?

Angalizo: habari mbaya ni bora zaidi kwa maendeleo.
 
Punguza povu.huyo msigwa unayemtetea hana maana kwa dunia ya wastarabu.hakuna mtu anayekatazwa kusema ila sema pale ambako kuna mizania sawa yakupeana majibu.Kwasasa ilo halipo kwasababu yeye yuko kwenye kinga ya watawala ndo maana anaropoka ovyo,je na hao anaowasema wana haki sawa yakumropokea kama yeye anavyofanya?.
 
Punguza povu.huyo msigwa unayemtetea hana maana kwa dunia ya wastarabu.hakuna mtu anayekatazwa kusema ila sema pale ambako kuna mizania sawa yakupeana majibu.Kwasasa ilo halipo kwasababu yeye yuko kwenye kinga ya watawala ndo maana anaropoka ovyo,je na hao anaowasema wana haki sawa yakumropokea kama yeye anavyofanya?.

Wapi katetewa Msigwa achilia mbali povu ambalo labda ungetamani mno liwepo?

Wewe unadhani huyo mwenye safari ya Congo ndiyo ma think tank sasa wa kukisemea hiki chama na ulipo ndiyo uko kwenye kukenua kuwa katoa points mno huyo ndugu?

Kulikoni kukidhalilisha chama hivi?

Hakuna kigeni kwenye mtu kuhama chama na tungekuwa na akili, wengi tungehamia CCM wakiwamo kina Mbowe, Lissu na wengine tukawabomoe kutokea huko huko!

KANU ilikufa kwa mkakati wa Raila aliyeingia kule kwa dhamira kamili.

Muyaone hayo vipi kama upeo wa kuona si zaidi ya pia zenu?
 
Mtu anayo haki ya kusema lolote analoamini.

Kwanini kama kumeoza mngependa Msigwa aseme kupo vizuri?

Kwani kama kupo kama alivyosema si kurekebishwe?

Kwanini kupenda kusikia sifa tu hata ikibidi zisizostahili?

Angalizo: habari mbaya ni bora zaidi kwa maendeleo.
Right ya kwenda public kumsema mtu chochote unachoamini - baada ya kuhama chama?

Totally IRRATIONAL viewpoint.

Btw, you would also buy this, certainly: Dr. Mollel alipohama CHADEMA aliongea public kuwa yeye alikuwemo katika mpango wa CHADEMA kumpiga Lissu risasi.
 
Right ya kwenda public kumsema mtu chochote unachoamini - baada ya kuhama chama?

Kila mtu ana haki ya kusema anachoamini kama unavyoweza kuungana na huyo mwamba kwenye mada ukasafiri naye hadi Congo kama amekuvutia.

Totally IRRATIONAL viewpoint.

Totally IRRATIONAL to you is not necessarily to everybody.

Ustaarabu: Tusipangiane; kila mtu anawajibika na mechi zake.

Btw, you would also buy this, certainly: Dr. Mollel alipohama CHADEMA aliongea public kuwa yeye alikuwemo katika mpango wa CHADEMA kumpiga Lissu risasi.

I hope you buy this: Lissu anayo capacity ya ku appreciate na ku implement agenda ya masafa marefu yenye uwezo wa kuiangusha CCM, Raila style na ndiyo maana huko kuna vibrant Gen Z.

Zingatia:

CCM haitatolewa madarakani kijinga, above all na wajinga!
 
Wapi katetewa Msigwa achilia mbali povu ambalo labda ungetamani mno liwepo?

Wewe unadhani huyo mwenye safari ya Congo ndiyo ma think tank sasa wa kukisemea hiki chama na ulipo ndiyo ukwe kwenye kukenua kuwa katoa points mno ndugu?

Kulikoni kukidhalilisha chama hivi?

Hakuna kigeni kwenye mtu kuhama chama na tungekuwa na akili wengi tungehamia CCM wakiwamo kina Mbowe, Lissu na wengine tukawabomoe kutokea ndani!

KANU ilikufa kwa mkakati wa Raila aliyeingia kule kwa dhamira kamili.

Myaone hayo vipi kama upeo wa kuona si zaidi ya pia zenu?

..Peter Msigwa katumia haki yake kusema anachokiamini.

..Dudu Baya katumia haki yake kusema anachokiamini.

..kwa maoni yangu wote wako sahihi ktk kutumia haki yao ya kutoa mawazo.

..tulinde haki ya Msigwa, Dudu Baya, na kila Mtanzania, kutoa mawazo.
 
..Peter Msigwa katumia haki yake kusema anachokiamini.

..Dudu Baya katumia haki yake kusema anachokiamini.

..kwa maoni yangu wote wako sahihi ktk kutumia haki yao ya kutoa mawazo.

..tulinde haki ya Msigwa, Dudu Baya, na kila Mtanzania, kutoa mawazo.

Zaidi sana tujikite kwenye kuiondoa CCM madarakani kwa mbinu zote.

Uadui wa kudumu haujengi. Hilo likiwa somo kuu kutoka Kwa wenzetu waliofanikiwa kwenye vita vyao vinavyofanana na vyetu.

Kujengeka kwa a vibrant Gen Z ni mafanikio makuu ya kuiweka nchi kwa wananchi kunakotokana na viongozi kuweka maslahi ya nchi mbele.

Kuendekeza uadui wa kudumu ni upumbafu usiokuwa mfano.

Nchi si mali ya mtu na haupo u staa kwenye ukombozi!
 
Zaidi sana tujikite kwenye kuiondoa CCM madarakani kwa mbinu zote.

Uadui wa kudumu haujengi. Hilo likiwa somo kuu kutoka Kwa wenzetu waliofanikiwa kwenye vita vyao vinavyofanana na vyetu.

Kujengeka kwa a vibrant Gen Z ni mafanikio makuu ya kuiweka nchi kwa wananchi kunakotokana na viongozi kuweka maslahi ya nchi mbele.

Kuendekeza uadui wa kudumu ni upumbafu usiokuwa mfano.

Nchi si mali ya mtu na haupo u staa kwenye ukombozi!

..Demokrasia ndio salama yetu pamoja na kasoro zinazojitokeza.

..labda nisemee kidogo suala la UHAMAJI wa wanasiasa wetu.

..wanasiasa wa Tanzania uhamaji wao ktk vyama uko tofauti na uhamaji wa wanasiasa ktk demokrasia zinazopigiwa mfano.

..mwanasiasa anatakiwa kuhama chama kama atabaini chama chake kinamkwaza ktk itikadi na misimamo yake kisiasa.

..tatizo la wanasiasa wa Tanzania unaweza kukuta amejulikana na kujenga brand kutetea mambo fulani.

..Halafu mwanasiasa huyo anadai chama chake kimemkwaza, na anahamia ktk chama ambacho kinapinga mambo yote aliyojijengea sifa kuyapigania wakati wote ktk maisha yake ya kisiasa.

..kwa wenzetu mwanasiasa mhafidhina huhamia chama kingine cha kihafidhina. Ni nadra kukuta mwanasiasa mhafidhina akahamia ktk chama cha kiliberali.

..Ninachoweza kusema ni kwamba hapa Tanzania wanasiasa huwa hawahami vyama tu, bali wanachofanya ni kujikana wao binafsi, na kuyakana mambo yote waliyoiaminisha jamii, wanapohama vyao.

..Kwa kifupi, wanasiasa wa Tanzania, wanatumia ndivyo-sivyo, haki ya kujiunga, au kujitoa ktk vyama vya siasa.
 
Zaidi sana tujikite kwenye kuiondoa CCM madarakani kwa mbinu zote.

Uadui wa kudumu haujengi. Hilo likiwa somo kuu kutoka Kwa wenzetu waliofanikiwa kwenye vita vyao vinavyofanana na vyetu.

Kujengeka kwa a vibrant Gen Z ni mafanikio makuu ya kuiweka nchi kwa wananchi kunakotokana na viongozi kuweka maslahi ya nchi mbele.

Kuendekeza uadui wa kudumu ni upumbafu usiokuwa mfano.

Nchi si mali ya mtu na haupo u staa kwenye ukombozi!

..hii dhana ya " uadui wa kudumu..." ktk siasa nayo inatumika holela-holela.

..dhana hiyo huko tulikoitoa maana yake ni kwamba wanasiasa wa itikadi tofauti wanaweza kufanya kazi pamoja ktk baadhi ya mambo wanayokubaliana.

..kwa hapa Tanzania maana yake ni mwanasiasa kujikana, na kuwaacha kwenye mataa, wananchi waliokuwa naye toka mchanga mpaka anakuwa maarufu.
 
..Demokrasia ndio salama yetu pamoja na kasoro zinazojitokeza.

Kuna shutuma za muda mrefu wa kupigania demokrasia pasipokuwa demokrasia.

Si jambo la afya sana kuipuzia miito kama hiyo vyamani hata kama hatupendi kuisikia.

..labda nisemee kidogo suala la UHAMAJI wa wanasiasa wetu.

..wanasiasa wa Tanzania uhamaji wao ktk vyama uko tofauti na uhamaji wa wanasiasa ktk demokrasia zinazopigiwa mfano.

Mkuu hakuna uhamaji spesheli. Bila shaka tusipuuze pia sababu za wahamaji kwani karibu wote wana tuhuma zile zile.

..mwanasiasa anatakiwa kuhama chama kama atabaini chama chake kinamkwaza ktk itikadi na misimamo yake kisiasa.

Haya ni mawazo yako ambayo tumekubaliana tusipangiane.

Usisahau wengine wanaweza kuhamia kwingine kama mtaji wetu. Kama CCM wanaliweza hilo kwanini kwetu liwe haram?

..tatizo la wanasiasa wa Tanzania unaweza kukuta amejulikana na kujenga brand kutetea mambo fulani.

Ukiliangalia hili vyema utagundua kuwa linafanywa kuwa ni kisingizio cha kutaka kutowajibika kwa waliojitangazia ufalme chamani.

Kwamba mahakimu na washitaki ni wao!

Kauli za kuonja sumu kwa ulimi hazina afya.

Kauli za kuwahimiza wengine kuondoka au kuanzisha vyama vyao hakuwezi kuwa na afya.

Kulikoni awaye yote kuhimiza wengine kuondoka?!

..Halafu mwanasiasa huyo anadai chama chake kimemkwaza, na anahamia ktk chama ambacho kinapinga mambo yote aliyojijengea sifa kuyapigania wakati wote ktk maisha yake ya kisiasa.

Kama tulivyokubaliana Tusipangiane. Tuheshimu katiba, tusitishane na tuwajibike.

Tushindane Kwa hoja kama tunavyowaitisha CCM kufanya nasi bila mafanikio.

..kwa wenzetu mwanasiasa mhafidhina huhamia chama kingine cha kihafidhina. Ni nadra kukuta mwanasiasa mhafidhina akahamia ktk chama cha kiliberali.

Hivi ni visingizio vitupu ndugu. Raila amewahi kuwa na ushirika na hata kutofautiana na kina Moi, Kibaki, Kenyatta, Mudavadi, Wetangula, Karia, Musyoka, Ruto, nk na maisha yanasonga Hadi leo.

Matokeo yake ni hili ni hili vibrant Gen Z ambalo sisi limetushinda.

Tunaugonjwa wa kujiwekea maadui wa kudumu kama vile sisi tu wasafi ki hivyo.

Tatizo letu la hapa siyo siri, ni ujinga. Mengine tuyaonayo ni yatokanayo tu.

Ndiyo maana tuna taabu kubwa na wasomi. Ya kuwa tungependa kuwaponda wasomi. Wasomi ni engine, hawakwepeki.

Bottom line, nendeni mkasome. Elimu Haina mwisho.

..Ninachoweza kusema ni kwamba hapa Tanzania wanasiasa huwa hawahami vyama tu, bali wanachofanya ni kujikana wao binafsi, na kuyakana mambo yote waliyoiaminisha jamii, wanapohama vyao.

Kwani ni siri ndugu yangu?

Huu u sultan ndipo anguko letu lilipo.

Kwa hakika hadi tutapokuwa na chaguzi huru na za haki zenye kuanzia kwenye primaries, labda kama ilivyo kwa beberu kuanzia vyamani huko, bado tupo tupo sana.

..Kwa kifupi, wanasiasa wa Tanzania, wanatumia ndivyo-sivyo, haki ya kujiunga, au kujitoa ktk vyama vya siasa.

Natofautiana nawe kwenye hili:

CHADEMA: Bila kuwapa Makavu hakuna Katiba Mpya
 
..Raila Odinga alivyokwenda KANU hakugeuzwa kuwa kikaragosi wa watawala, na kuyakana yote aliyoyapigania ktk maisha yake ya kisiasa.

..Nashauri tutafute mfano mwingine wa kufananisha na uhamaji wa wanasiasa wa hapa Tanzania.
 
Ang
Mtu anayo haki ya kusema lolote analoamini.

Kwanini kama kumeoza mngependa Msigwa aseme kupo vizuri?

Kwani kama kupo kama alivyosema si kurekebishwe?

Kwanini kupenda kusikia sifa tu hata ikibidi zisizostahili?

Angalizo: habari mbaya ni bora zaidi kwa maendeleo.
eanza kusema akiwa bado Chadema angeeleweka vizuri !

Lakini kwa sasa anonekana ni kituko tu !
 
Shida ni kusema madhaifu ya huko ulikokua na hukuwahi kuyasema kabla lakini pia hukuonekana hata kujaribu kutaka kuyarekebisha...

Kuna mengi mabovu ya ccm aliyasema akiwa chadema, na bila shaka hatopaza sauti kusema wala kushauri hata baya moja aliloisemea ccm akiwa chadema.

Siku akihama ccm tena akienda chama pinzani, ataanza kuisemea vibaya ccm huku yale mabaya aliyokua anakisema chama pinzani akiwa ccm akiyaweka kwapani na kujifanya yuko sahihi tena..

Ni kweli wanasiasa ni waongo waongo ila isizidi sasa, inakua ujuha na upumbavu, na taifa haliwezi kupata maendeleo kwa namna hiyo.
 
..Raila Odinga alivyokwenda KANU hakugeuzwa kuwa kikaragosi wa watawala, na kuyakana yote aliyoyapigania ktk maisha yake ya kisiasa.

Kugeuzana vikaragosi hizo ni hisia binafsi ambazo kila mtu anaweza akatofautiana nawe.

Raila ni mfano mzuri sana kutulia na kuweka kituo nao, ikizingatiwa kuwa:

1. Huyu ni mwana EA mwenzetu ambako hata wanaoongea kiswahili:

Nyimbo za Tanzania zatumika kuhamasisha maandamano Kenya

2. Huyu ni katika mazingira kamili kama yetu kutokea kwenye kadhia ya chama kimoja, katiba mbaya, upinzani, maridhiano, kupata katiba mpya Hadi nchi mikononi mwa wananchi.

3. Huyu aliingia chama tawala kwenda kuwavunjilia mbali huko huko. Labda Msigwa naye ni mwanzo mzuri huo wakupiga makombora ya mbali Raila style?

4. Labda Msigwa ni mjumbe mamluki huko alikokwenda?

5. Hata kama Msigwa CCM, labda si agenda ya chadema, basi yawezekana sasa tuna la kukumbuka kwa Raila kupeleka umamluki ikibidi ikibidi?

6. Nani asiyejua CCM haitatoka kijinga wala kutolewa na wajinga.

7. Kumbe uko wapi mkakati wa kuwatoa CCM lini madarakani?

8. Katiba mpya haitapatikana mezani, kwani hata Raila hakuipata hivyo na mapambano yanaendelea:

Ukombozi kupitia masikilizano na CCM ni kupoteza muda

..Nashauri tutafute mfano mwingine wa kufananisha na uhamaji wa wanasiasa wa hapa Tanzania.

1. Kwanini ungependa kuikimbia mifano iliyoko kwenye mazingira yetu?

2. Au labda ungeweja mfano upi ambao ungedhani kuuzidi huu wa Raila na Kenya?

3. Au kwa nini ungependa usilaumiwe udhaifu wa viongozi wetu kwa kusua sua kwa ukombozi kwetu?

4. Au hata labda una lolote la kuwakosoa viongozi ving'ang'anizi hawa popote ikizingatiwa inafahamika si ajabu kwetu kuwapo na chawa wa kulipwa?

Tuzitambue tofauti za vyama vya upinzani (ACT, CHADEMA, CUF, nk) na Wanaharakati

5. Au wewe unaona Hawa ndugu halipo la kuwakosoa Kwa sabaini mithili ya malaika kutoka mbinguni?
 
Ang

eanza kusema akiwa bado Chadema angeeleweka vizuri !

Lakini kwa sasa anonekana ni kituko tu !

1. Mada umeielewa lakini au na wewe ni kama huyo ndugu mwenye kuwahi mtaa wa Congo?

2. Mada hii haimhusu Msigwa hata kidogo japo hata kama ungependa kumwongelea huyo, kwamba labda alidhani kutakuwa na mabadiliko basi na anyamaze sasa Kwa vile tu hakuwa amesema?

3. Kwamba hapo #3 kwanini huoni kama ndivyo Bado huna lolote la kuwaambia chadema Wala mheshimiwa Mbowe au awaye yote?!
 
Shida ni kusema madhaifu ya huko ulikokua na hukuwahi kuyasema kabla lakini pia hukuonekana hata kujaribu kutaka kuyarekebisha...

Kuna mengi mabovu ya ccm aliyasema akiwa chadema, na bila shaka hatopaza sauti kusema wala kushauri hata baya moja aliloisemea ccm akiwa chadema.

Siku akihama ccm tena akienda chama pinzani, ataanza kuisemea vibaya ccm huku yale mabaya aliyokua anakisema chama pinzani akiwa ccm akiyaweka kwapani na kujifanya yuko sahihi tena..

Ni kweli wanasiasa ni waongo waongo ila isizidi sasa, inakua ujuha na upumbavu, na taifa haliwezi kupata maendeleo kwa namna hiyo.

Mada hii haimhusu mtu achilia mbali Msigwa bali kusua sua kwa ukombozi wetu.

Zingatia tuna Gen Z dhaifu ikisubiria katiba mpya mezani.

Inawezekana namna gani?

Kwa maana hiyo ninalazimika kuya paste haya hapa kwako pia:

1. Mada umeielewa lakini au na wewe ni kama huyo ndugu mwenye kuwahi mtaa wa Congo?

2. Mada hii haimhusu Msigwa hata kidogo japo hata kama ungependa kumwongelea huyo, kwamba labda alidhani kutakuwa na mabadiliko basi na anyamaze sasa Kwa vile tu hakuwa amesema?

3. Kwamba hapo #3 kwanini huoni kama ndivyo Bado huna lolote la kuwaambia chadema Wala mheshimiwa Mbowe au awaye yote?!
 
..hii dhana ya " uadui wa kudumu..." ktk siasa nayo inatumika holela-holela.

Dhana ya uadui wa kudumu inaitafuna chadema kwa sababu ya kuwaendekeza wa aina ya huyo mwenda Congo kwenye mada:

Tusio na adui wa kudumu tunasimama na Dkt. Slaa

Yasome mawazo ya makamanda uchwara (imhotep) wenye vibiongo kwenye uzi huo.

..dhana hiyo huko tulikoitoa maana yake ni kwamba wanasiasa wa itikadi tofauti wanaweza kufanya kazi pamoja ktk baadhi ya mambo wanayokubaliana.

Mtamaliza bucha zote ndugu, lakini nyama ni ile Ile.

Kutokuwa na adui wa kudumu ni kule kule kokote, ambako hata tisiowapenda Kwa sura wakati wowote, hatuwezi kuwa delete milele katika harakati za ukombozi:

Kwanini Wakili Mwabukusi na wenzake wanastahili kuungwa mkono

..kwa hapa Tanzania maana yake ni mwanasiasa kujikana, na kuwaacha kwenye mataa, wananchi waliokuwa naye toka mchanga mpaka anakuwa maarufu.

Hii ni maana yako ndugu ambayo unasomeka vyema, kuwa asiye submit kwa sultan huyo hapana.

Maana duni kabisa!
 
Back
Top Bottom