Kutatua tatizo la ajali nchini kutokana na uharibifu au kufeli breki, LATRA waweke kikomo cha umri wa mabasi na malori kuruhusiwa kuwa barabarani

Kutatua tatizo la ajali nchini kutokana na uharibifu au kufeli breki, LATRA waweke kikomo cha umri wa mabasi na malori kuruhusiwa kuwa barabarani

Synthesizer

Platinum Member
Joined
Feb 15, 2010
Posts
12,699
Reaction score
22,598
Kuna mahali nilisoma kwamba unapoendesha gari yenye umri zaidi ya miaka 15 kwenda safari ya mbali, umri wa hiyo gari unaweza kuchangia wewe kupata ajali. Yaani, kadiri gari ilivyo ya umri mkubwa ndivyo ambavyo ina uwezekano mkubwa wa kupata hitilafu na kusababisha ajali hata vifo.

Tanzania ni mojawapo ya nchi duniani utashangaa kuna malori na mabasi yenye umri wa miaka zaidi ya 30, lakini bado yanatumika barabarani. Imefika wakati ambapo serikali kupitia LATRA iweke sheria kwamba kwa mabasi, gari yeyote yenye umri zaidi ya miaka 10 haipaswi kutumika tena kubeba abiria. Kwa malori, gari yeyote yenye umri zaidi ya miaka 20 lisiruhusiwe tena kutembea barabarani

Tukifanya hivi tutaepusha ajali nyingi zisizopaswa kutokea. Haya malori na mabasi yanayofeli breki kila wakati mara nyingi ni machakavu ya zamani ambayo mifumo yake imeanza kufeli, na wamiliki wanaunga unga tu ili kuyaweka barabarani. Yatolewe barabarani na kuuzwa kama vyuma chakavu.

Kuna nchi duniani gari yenye umri zaidi ya miaka 10 hairuhusiwi kutembea barabarani, na katika nchi hizo hutasikia hata siku moja ajali eti lori lilifeli breki na kuua watu

Na ikiwezekana, hizi basi za China za Yutong na Zetong sijui, zisiruhusiwe kuwa barabarani kwa safari za mikoani kama zina umri wa zaidi ya miaka mitano
 
SUMATRA? 2025?

Upo nyuma sana ya muda!
 
Mkuu
.
Sasa Hivi SUMATRA Haipo


Tuna LATRA, TASAC

LATRA Unahusika Na Usafiri Wa Nchi Kavu
TASAC Inahusika Na Usafiri Wa Majini, Bahari, Maziwa, Mito
 
Mkuu
.
Sasa Hivi SUMATRA Haipo


Tuna LATRA, TASAC

LATRA Unahusika Na Usafiri Wa Nchi Kavu
TASAC Inahusika Na Usafiri Wa Majini, Bahari, Maziwa, Mito
Asante sana. Sina basi wa lori wala boti hivyo sijui haya mambo
 
Kuna mahali nilisoma kwamba unapoendesha gari yenye umri zaidi ya miaka 15 kwenda safari ya mbali, umri wa hiyo gari unaweza kuchangia wewe kupata ajali. Yaani, kadiri gari ilivyo ya umri mkubwa ndivyo ambavyo ina uwezekano mkubwa wa kupata hitilafu na kusababisha ajali hata vifo.

Tanzania ni mojawapo ya nchi duniani utashangaa kuna malori na mabasi yenye umri wa miaka zaidi ya 30, lakini bado yanatumika barabarani. Imefika wakati ambapo serikali kupitia LATRA iweke sheria kwamba kwa mabasi, gari yeyote yenye umri zaidi ya miaka 10 haipaswi kutumika tena kubeba abiria. Kwa malori, gari yeyote yenye umri zaidi ya miaka 20 lisiruhusiwe tena kutembea barabarani

Tukifanya hivi tutaepusha ajali nyingi zisizopaswa kutokea. Haya malori na mabasi yanayofeli breki kila wakati mara nyingi ni machakavu ya zamani ambayo mifumo yake imeanza kufeli, na wamiliki wanaunga unga tu ili kuyaweka barabarani. Yatolewe barabarani na kuuzwa kama vyuma chakavu.

Kuna nchi duniani gari yenye umri zaidi ya miaka 10 hairuhusiwi kutembea barabarani, na katika nchi hizo hutasikia hata siku moja ajali eti lori lilifeli breki na kuua watu

Na ikiwezekana, hizi basi za China za Yutong na Zetong sijui, zisiruhusiwe kuwa barabarani kwa safari za mikoani kama zina umri wa zaidi ya miaka mitano
Hehehe!!!
 
1739629646288.png


Hii ni post ya Mwana JF
 
Kuna vyanzo vingi vya ajali nchini kwetu moja wapo ni hilo la uchakavu wa hayo magari.

Lakini kuna miundombinu, yaani barabara zetu hazilingani na wingi wa magari kwa sasa.

Sasa hapo angalia yale malori ya zamani yanvyokuwa safarini unakuta limeweka msururu wa magari nane mpaka kumi kwa sababu haina nguvu ya kupanda milima kwa kasi fulani matahalani ilitakiwa ipande na 30 KPH unakuta inapanda na 10/15 KPH sasa hapo tarajia gari zenye nguvu kuovateki hii innatokea kulingana na aina za madereva tulionao pia.

Chanzo kingine ni madereva wenyewe ukifatilia namna walivyopata mafunzo kama yalikuwa sahihi au ndio hayo ya mtaani.

Na hili ni tatizo la kimfumo wa usimamiaji wa utoaji wa leseni ni wazi kuna watu hawakidhi kùpatiwa leseni lakini utakuta wanazimiliki.

Kuanzishwe utaratibu wa upimwaji wa akili na ukomavu wa akili kwa madereva wote si wa commercial vehicle tuu maana madereva wa gari ndogo nao ni changamoto pia.

Wahusika wa Tanrod nao wawe wanawajibishwa kwa uzembe wa kutorekebisha maeneo yenye hali ya hatari na hizi zimeshaleta ajali nyingi sana ila lawama zinaenda kwa madereva pekee.
 
Kwenye maroli na mabasi kiwekwe kigezo cha lazima yaje na mifumo ya usalama kama Hydraulic Retarder, Hill climbing assistance, ABS, Lane departure assistance, trailer anti rolling system.

Kwenye basi za kichina wanaleta zikiwa na Eddy Current Electric Retarder ambayo ufanisi si mkubwa na ikipita sehemu zenye maji magnetic field hazifanyi kazi. Hapo dereva anategemea Foot brake tu. Kwenye roli wanatumia engine stopper wakati sasa technology ni Hydraulic Retarder ndio ina ufanisi mkubwa.

Basi na roli zote za China haziji na Hill climbing assistance na lane departure warning system. Ikiwekwa sheria ya lazima gari iwe na hizi features lazima muagizaji aweke option kwa mtengenezaji, hizo trucks na Bus za China kwenye Europe market wanapeleka na safety features hizo
 
Utasikia wakikwambia chuma injini ya scania Marcopolo hii usiione hivi bodi tu hii.
 
Back
Top Bottom