Kutoka kofia ya barghashia ya Nyerere 1964 hadi msalaba wa William Lukuvi 2014

Kutoka kofia ya barghashia ya Nyerere 1964 hadi msalaba wa William Lukuvi 2014

Dini sio wala haijawahi kuwa issue Tanzania.., matatizo ni ya watu kama nyie mnayoifanya kuwa issue. Mnapandikiza chuki baina ya watu..., Hivi mtu akishikia bango sasa hivi kwamba waarabu walitutesa watu weusi na kutuchukua kama watumwa kipindi kile (kwa kuwaambia wajukuu zake) hapo atakuwa amejenga au ameongeza nini ?

Issue isiwe Nyerere alifanya nini ili kudumisha au kubomoa bali ni wewe unafanya nini na unachofanya kinajenga au kubomoa.

Kutokana na ujinga wetu chepe ukiliita chepe yatakukuta tu ukitaka uwe in safe side wewe liite kijiko kikubwa tu.
 
Masuala ya dini yatawatafuna sana! Acheni chuki zenu! Wengi wetu dini hizi ni mapokeo tu! Wengine wamekuwa Waislam kwa sababu ya Wazazi, Wengine wakristo kwa sababu hizo hizo! Japo wapo waliobadili au walikuwa wapagani wakachagua dini mojawapo!

Sioni mantiki ya watu kung'aka na mambo ya dini wakati UNDUGU wetu wote ni mmoja! Na bado, hii dhambi ya ubaguzi itaendelea kututafuna tu, hatutaishia hapa!

Kwa sababu hata CCM na CDM wengi humu wenye misimamo, kwenye hii thread wanasupport kwa kuwa kuna harakati za Kiislam hapa!
 
Mzee mohamed said.. una undugu na shekhe ponda? naona mmegawana majukumu.. wewe unatumia maandishi.. yeye anatumia majukwaa..na tindikali.. ila mwenzio anakubalika kuliko wewe.. je una mpango wa kubadilisha mbinu.. ili uwe kama mwenzio shekhe ponda?

Kanyigo,
Sheikh Ponda Issa Ponda ni ndugu yangu na rafiki yangu kipenzi.

Hayo mengine ulosema sioni kama kuna tija yoyote itapatikana
kwa mimi kukujibu.
 
Mkianza itikadi/dini ndio mzizi wa matatizo mengi makubwa duniani, dini ndio zimeua zaidi duniani. Wakati huohuo zinadai zinaondoa dhuluma, zinahimiza upendo nk. Hivyo tuwe makini sana, tusi shadidie haya maitikadi tuliyokopeshwa na wakoloni.

Tuache misimamo ya kidini lasivyo tunaelekea kuuwana kama imani za dini zinavyohalalisha (kwa mlango wa nyuma) ukatili huo huku zikitoa ganzi kwa mtendaji kujiona yeye ni shujaa kiimani (kitu ambacho hakijawahi kutokea, hakipo ila eti kinatarajiwa!!).

Dini ni kitu duni sana kwasababu unaweza kubadili yoyote kila dakika, lakini ukiwa wewe ni Mtanganyika huwezi kubadili kirahisi hivyo. Sanasana utaambiwa eg Mmarekani mwenye asili ya Africa, Uafrika wako hautoki.

Hivyo tupiganie Tanganyika yetu kwa upendo
 
Haki ya Mungu mzee Mohamed Said wewe ni mtu muhimu sana katika taifa hili. Wewe umesaidia wengi kulifahamu taifa lao na siasa za nchi hii. Kina Tundulisu ni ufinyu wa shukrani tu lakini wangepaswa kuku acknolodge kwa kuwapa ukweli wa historia ya taifa lao na kuuweka wazi bungeni.
 
Last edited by a moderator:
Hiyo magwiji wa historia wanauwezo wa kukusimamisha-mara ya mwisho ulijiumauma sana na hatimae ukakaa kitako- walikwambia nakala mpya ya kitabu chako itabidi ufanye mabadiliko makubwa

Jackline1,
Naomba kwa hisani yako nipatie majina ya hao ''magwiji wa historia'' kwa kuwa
sikumbuki kitu kama hicho unachoeleza.

Ila ninachojua ni kuwa Prof. James Giblin wa Chuo Kikuu Cha Iowa na Mkuu wa
Idara ya Historia alinialika chuoni kwake na nilitoa mhadhara.

Nilipomaliza ile nakwenda kukaa Prof. Jonathan Glassman wa Idara ya Historia
Northwestern University, Evanston Chicago akanidaka akaniomba mada ile ile
nende nikaiwasilishe chuoni kwake.

Mada yangu ilikuwa, ''Islam and Politics in Tanzania.''

Hawa ni wasomi makini na wamesoma kitabu changu na kuandika ''review.''
Hicho kitabu changu ulichokitaja hawa wanakisomesha kwenye vyuo vyao.
 
Naongea kama muislamu........
Naomba MODS MUNINUKUU.
Sioni fahari Kuwa muislamu.
Waislamu(sio uislamu) ni moja kati ya matatizoya msingi katika taifa letu.
Mnahubiri(kinyume na uislamu) uadui na utengano zaidi ya upendo na mshikamano..
Ni wanafik (kinyume na uislamu).
UAMSHO( WAISLAMU) mnaua viongozi wa dini na kuchoma makanisa(kinyume na uislamu).
Bado MNA akili ya KITUMWA ya kudhani MUARABU ndio MTU bora(wakati ndio mtenda dhambi mkubwa)
Nawashauri tuu ndugu zangu katika imani (waislam) kama mnataka taifa LA kiislamu basi HAMIENI OMAN.... Kwani si kuna ndugu zenu wanaowafadhili.
Serikali 3 au ya NKATABA haipo hata mdhikiri mkiwa watupu

Wewe boya unadhani kujifanya muislamu ndio kutasaidia kuficha ukweli? Badala ya kumkemea Lukuvi unajifanya kuleta unafiki hapa. Muislamu gani hata hujui lengo kuu la uislamu.
 
Haki ya Mungu mzee Mohamed Said wewe ni mtu muhimu sana katika taifa hili. Wewe umesaidia wengi kulifahamu taifa lao na siasa za nchi hii. Kina Tundulisu ni ufinyu wa shukrani tu lakini wangepaswa kuku acknolodge kwa kuwapa ukweli wa historia ya taifa lao na kuuweka wazi bungeni.

Chamviga,
Mimi bahati yangu ni kuwa walionizaa ndiyo walioasisi harakati hizi.
Mtu yoyote angekuwa kwenye nafasi yangu na yeye angeyajua
haya pengine hata kunishinda.

Mfano, kuwa Karume alilala nyumbani kwa mmoja wa wazee wangu
siku ya kuamkia mapinduzi kwa wakati ule 1964 wala haiukuwa siri na
wala hakuna aliyedhani hili jambo litakuja kuwa muhimu kiasi hiki siku
zijazo.
 
Unaposhindwa kujenga hoja huwa unatafuta defensive mechanism kukataa ukweli.kama mchango wa waislam katika nchi hii hutaki kusikia. na kuutambua basi utambue kila kitu katika uislam ni ibada.

vilevile utambue nyerere hakujifunza kuvaa kibaghashe katika jamii ya wagalatia wa butiama.Bali katika jamii ya kiislam ya pwani.Kama umesoma fasihi au literature usingesumbuka na Titles katika uandishi husymbolize nini?

Vitu vidogo vidogo visible vinakuhofisha kuwa vinajenga attention kwa majority,unataka vitumike vitu vikubwa vikubwa ambavyo haviko visible(Ambiguity) na vijenge attention kwa minority.Nini lengo la uandishi.Je tamaduni za kibaraghashe ni za wagalatia?

Mpaka sasa hujajenga hoja zaidi ya kuchambia style ya uwasilishaji wa ujumbe na maneno yalitumika huku ukidhihirisha ufamu wako katika fasihi ya uandishi upo chini sana.

Whats the content message aliyowasilisha Sheikh Muhammed Said.Please Critisize that with Facts and Logic

Shukran Sana Sheihk Muhammed Said.
Unadhani facts na logics ni vile vifurahishavyo moyo na wako na kusisimua ufahamu wako?
Facts na logics pia hupelekea utaharuki kama, na wakati mwingi kuumia na hata kulia.
Kusoma peke yake niliyoyaandika haitakusaidia, jaribu kutafakari.
Kuhusu nani mchango wa waislam katika kuleta uhuru hili halipo katika mtiririko wa maandisho yangu, umelipenyeza kwa style uitakayo, bahati mbaya kwako ni kuwa huweza kunipata ni cheze katika level yako, mimi si wa aina ya malumbano ya kidini.
Ninaangalia ukamilifu wa mtu kuanzia kwa mtu mweenyewe, matendo yake na kuishia kwa mtu mwenyewe wala simuangalii mtu kwa dini yake.
Nakushauri: endelea kupitia pitia post za wachangiaji wengine, unaweza ukaokoteza walio tayari kwa malumbano ya kidini, siyo mimi.
Imani ya mtu si sehemu ya jukumu langu.
I'm sorry, but I have to tell you all these.
 
Notradamme,
Soma kisa hiki hapo chini:

...baada ya kuongea na mimi nikamuuliza swali,''Umejuaje kama mimi
ni Musilam? Dalili zipi zimekujulisha kuwa mimi ni Muislam?

Yule bwana akanijibu kuwa, ''Mimi nilikuwa napita nje ya hii ''telephone
booth'' na mazungumzo niliyokuwa nasikia ni ya upande mmoja tu na
nilikusikia kwanza ukizungumza Kiingereza kisha Kiswahili.

Nikajiambia lazima nisubiri hapa nje nimuone huyu kijana.
Jinsi ulivyokuwa unaongea ilinidhihirikia kuwa lazima mtu huyu atakuwa
Muislam...''

Hiki ni kisa changu na mtu mmoja kimji kidogo nje ya London kinaitwa
Tilbury.

Huyu bwana alinisikia nikizungumza na akajua kuwa mimi ni Muislam na
akawa na hamu ya kuzungumza na mimi.

Notredamme,
Mimi sikujui lakini nina hakika wewe si Muislam.
Najuaje?

Maneno yako hayakuelekea.
Ila sielewi kwa nini unajinasibisha na Uislam.

Sielewi kipi unakiona hakikukaa vyema kwenye imani yako kiasi cha kujitoa.

Nakupa kisa kingine.

Niko ndani ya tram Alexandria natoka Ramala Station nakwenda kwangu
Saint Stefano.

Behewa zima limejaa Waarabu.
Mswahili ni mimi peke yangu.

Mzee mmoja wa Kimisri akaniuliza kama mimi ni Muislam nikamjibu, ''Alhamdulilah.''
Hakuridhika akataka nimpe ushahidi.

Nikamuuliza, ''Ushahidi gani unataka nikupe?''
Akasema, ''Nisomee Qur'an.''

Nikasoma Surat Fatha.

Akacheka akasema hiyo sura mtu yoyote anaweza kuisoma akanambia, ''Nisomee
kitu chochote katikati ya mashaf.''

Behewa zima limenizunguka kutaka kujua kama kweli huyu mtu mweusi ni Musilam.
Ukitembea duniani utajifunza mengi sana.

Watu wengi hawajui zaidi ya pale wanapoishi.
Hawa Wamisri wanadhani dunia nzima wako Waarabu na Waislam ni Waarabu tu...

Nikamsomea kitu kutoka katika Qur'an nikaanza...''...ila ghasaki layli wa Qur'an l'fajr...
hawakuniachia nimalize behewa zima llilinyanyua mikono huku wakipiga kelele,
''Alhamdulilah, Alhamdulillah...''

Notradamme,
Jitulize nahisi wewe ni kijana mdogo sana.
Tulia ujifunze.

Nami nakuombea dua Allah akupe ilm na akulete katika Uislam.
Amin.

Notradamme,
Ikiwa wewe ni Muislam nakupa changamoto hiyo aya hapo juu niwekee maneno
yaliyotangulia.


Maalim Mohamed Said,

Umesomeka kwa undani ulo mwingi mno, ndugu yetu kipenzi!

Nimeipenda mno hiyo bayana yako!

Lakini hilo gunia la miba ulomtwisha nalo huyo dogo ajiitae ati "notradamme",hawezi asilan kulitua! Daah! Teeh! Teeh! Teeh!

Labda mpaka kesho ndo atamudu kurejea hapa jamvini...tena labda asaidiwe na yule Mchungaji Mwanakijiji, alokua bingwa wa malumbano ya kidini dhidi ya akina Ustaadh Mazinge pale viwanja vya Jangwani!?

Awali ya yoote...hivi Muislam gani ataweza kujiita "notradamme"/Notre dame in French, aka Our Lady Virgin Mary...or "Madonna" in Italian!? Duuh!

Tupamoja kwa yoote!

Ahsanta sana.
 
Mkuu hebu acha kujidhalilisha, kama tayari wewe unaona kilichosemwa ni pumba basi ungeanza wewe kumsahihisha halafu hao wengine watakuja.kama huna masahihisho basi nyamaza. Mimi binafsi kama sina nijualo juu ya jambo nakaa kimya kujifunza.

nakubaliana na ww kama huna la kusema ni bora unyamaze ili ujifunze-jambo jingine tusiwape watu ukuu hata kama hawastahili
 
Chamviga,
Mimi bahati yangu ni kuwa walionizaa ndiyo walioasisi harakati hizi.
Mtu yoyote angekuwa kwenye nafasi yangu na yeye angeyajua
haya pengine hata kunishinda.

Mfano, kuwa Karume alilala nyumbani kwa mmoja wa wazee wangu
siku ya kuamkia mapinduzi kwa wakati le 1964 wala haiukuwa siri na
wala hakuna aliyedhani hili jambo litakuja kuwa muhimu kiasi hiki.

Mzee Mohamed Said wewe sina shaka na wewe kuhusu ukweli wa haya unayozungumza. Wewe ni muislamu ma sio nduguzo twajua uongo gharama yake ni nini mbele ya Allah siku ya malipo.
 
Last edited by a moderator:
tunashukuru kwa mchango wako mohamed said...allah atakulipa
 
Tukubali ya kuwa Lukuvi katonesha donda.
Ni shame kwa waziri wa sera anekwenda kanisani na kuisemea serikali ya kuwa hatuiachii znz.
Anawasema hawa wasumbufu sana
Hatuwezi kuwachia hawa95% ni waislam wataunda islamic state.
Haya maneno leo miaka 50 ?
Tena wiki ijao ndio sherehe?
Hii hoja sio ya kukejeliwa na kutoa kashfa na dharau.
Japo kuna matatizo ya udini kama Mohamed Said anavoenesha lakini kwa wazirii kuisemea serikali ya kuwa hatuiachii znz hii ni hatari na ametibua waislam.
Jee muslims watanganyika na znz kuna sababu yoyote ya kujudhuria sherehe hizi ambazo kumbe lengo lake sasa ni official ni uislam?
 
Last edited by a moderator:
Unadhani facts na logics ni vile vifurahishavyo moyo na wako na kusisimua ufahamu wako?
Facts na logics pia hupelekea utaharuki kama, na wakati mwingi kuumia na hata kulia.
Kusoma peke yake niliyoyaandika haitakusaidia, jaribu kutafakari.
Kuhusu nani mchango wa waislam katika kuleta uhuru hili halipo katika mtiririko wa maandisho yangu, umelipenyeza kwa style uitakayo, bahati mbaya kwako ni kuwa huweza kunipata ni cheze katika level yako, mimi si wa aina ya malumbano ya kidini.
Ninaangalia ukamilifu wa mtu kuanzia kwa mtu mweenyewe, matendo yake na kuishia kwa mtu mwenyewe wala simuangalii mtu kwa dini yake.
Nakushauri: endelea kupitia pitia post za wachangiaji wengine, unaweza ukaokoteza walio tayari kwa malumbano ya kidini, siyo mimi.
Imani ya mtu si sehemu ya jukumu langu.
I'm sorry, but I have to tell you all these.

Huhitaji kua bias katika facts and logic ili umfurahishe mtu.ukweli siku zote huumiza.kipi kilicho kuumiza na kukuliza tukupe maneno ya kukupoza.

mchango wa waislam katika uhuru wa nchi hii umesingiziwa ni mtiririko wako tena dah!

Unaangalia ukamilifu wa mtu kuanzia mtu mwenyewe.Huku ni kuattack personality ya mtu. "Dont judge a book by its cover" deal with the content.

malumbano ya kidini ndio mind set inayokuzuia kusoma historia ya uislam Tanzania.

Imani ya dini si sehemu ya jukumu lako.U should Claim that Mtu anachoamini ndicho humsukuma kufanya maamuzi afanyayo.Do u belive in killing Albinos for wealth?

Your welcome.
 
Haki ya Mungu mzee Mohamed Said wewe ni mtu muhimu sana katika taifa hili. Wewe umesaidia wengi kulifahamu taifa lao na siasa za nchi hii. Kina Tundulisu ni ufinyu wa shukrani tu lakini wangepaswa kuku acknolodge kwa kuwapa ukweli wa historia ya taifa lao na kuuweka wazi bungeni.

Umesema kweli bwana chamviga, Ms hapa jukwaani kaleta elimu kubwa sana, na mungu hawafichi Wanafiki maneno ambayo MS anayasema hapa wanayapinga kwa nguvu zote lakini ndio hayo wanayatumia kwenye bunge lao la katiba,

Hongera sana Mwalimu Mohammed Said
 
Last edited by a moderator:
Naongea kama muislamu........
Naomba MODS MUNINUKUU.
Sioni fahari Kuwa muislamu.
Waislamu(sio uislamu) ni moja kati ya matatizoya msingi katika taifa letu.
Mnahubiri(kinyume na uislamu) uadui na utengano zaidi ya upendo na mshikamano..
Ni wanafik (kinyume na uislamu).
UAMSHO( WAISLAMU) mnaua viongozi wa dini na kuchoma makanisa(kinyume na uislamu).
Bado MNA akili ya KITUMWA ya kudhani MUARABU ndio MTU bora(wakati ndio mtenda dhambi mkubwa)
Nawashauri tuu ndugu zangu katika imani (waislam) kama mnataka taifa LA kiislamu basi HAMIENI OMAN.... Kwani si kuna ndugu zenu wanaowafadhili.
Serikali 3 au ya NKATABA haipo hata mdhikiri mkiwa watupu

Dugu,
Mtafute Max Shimba atakupa dini ambayo huenda ukaona fahari kujivunia. Au Kiranga.

Kwa nini umeamua kubakia katika uislamu? Nani anakulazimisha?

Kumbuka Mungu anaweka kumbukumbu ya yote unayoyasema na unayoyafanya,Kwa siri au dhahiri.Unaelewa kuwa Mungu ni hakimu.

Wanaotaka taifa la kiislamu wahamie Oman. Kwa nini nawe usihame? Unachokitaka wewe ni nini?

Wewe unataka serikali ngapi? Kwa sababu zipi?

Lini uliingia katika Uislamu? Je uislamu wako uliupata Oman?
 
Maalim Punjab wewe semea kweli kabisa Maalim Mohamed Said elimisha watu huyu jinga kuja jamba jamba hovyo..


Wewe vipi laumu Maalim Mohamed Said yeye kusemea mambo ya Zanzibar kwa sababu yeye penda Tanganyika. Wewe kama taka Tanganyika rudi basi pigania free sovereign Zanzibar. Impossible Tanganyika to annex Zanzibar and call it Tanganyika. You learn history from him sio that been cooked at Pengo's Altart and Chuo ya Kivukoni.
gombesugu bhai
 
Mzee mohamed said.. una undugu na shekhe ponda? naona mmegawana majukumu.. wewe unatumia maandishi.. yeye anatumia majukwaa..na tindikali.. ila mwenzio anakubalika kuliko wewe.. je una mpango wa kubadilisha mbinu.. ili uwe kama mwenzio shekhe ponda?

Wewe una undungu na Lukuvi?
Lukuvi anamwaga radhi kanisani na bungeni na wewe JF.Lini mtabadiishana majukumu?
 
Back
Top Bottom