Kutoka kwenye Utajiri mpaka kuishi kwenye lindi la umasikini!

Mwaka 1999 kuna Bus la Nbs na Tabora boys unaenda na kurudi home, maana yake Tabora Boys ilikuwa Day School au siyo
 
Duh, dunia hii jamani dah
 
Mwaka 1999 kuna Bus la Nbs na Tabora boys unaenda na kurudi home, maana yake Tabora Boys ilikuwa Day School au siyo
It's the brain work to find fault, mistake,error, negative,danger etc so no wonder.

So Kama amedanganya si uachane naye ama akuhakikishie Kama Ni ukweli itaongeza namba yoyote kwa maisha yako,ama kipato chako?

Na je story una uhakika gani Kama Ni ya kutunga ama uwongo ama ukweli,tangiapo ikiwa ukweli,uwongo ama kutunga wewe itakusaidia Nini ama kupunguza nini. Is there anything you wanna trade with this story?
 
Dude, why all of these? I was just wondering if NBS company was existing with such a name and Tabora boys School was a day school by then,je kuna tatizo kwenye hilo mkuu?
 
Dude, why all of these? I was just wondering if NBS company was existing with such a name and Tabora boys School was a day school by then,je kuna tatizo kwenye hilo mkuu?
Mtu hawezi andika yote sahihi. Kuna kampuni zipo tokea zamani mno. Mie nimejitambua nayaona mabasi ya Zachary Peter,kimotco nimempanda so no wonder.mie sio wewe Bali Ni Aina ya ubongo tulio nao hata mie ninao Ila sio your personality. Yaani ndio nature ya ubongo wetu yaani kila binadamu
 
Wewe una matukio zaidi ya Umughaka na wenzake kina Gabby
 
Sehemu ya 11
Nilikaa pale makuburini, na muda uliyoyoma sana nikaamua kusubiri muda uzidi kusonga maana niliona hapa ndio salama yangu.

Kausingizi kalinipitia kidogo nikaja kuamshwa na wanga waliokuja kufanya yao makaburini, wao hawajiona ila mimi nimewaona. Nikaamka kuwafata ili kujua natokaje tokaje hapa, naona wao pia wananikimbia kwa hofu sijui walihisi mfu kafufuka au vp.

Nikaendelea kujibana na vituko viliendelea nikaona busara nisisumbue tena watu nkaja kamatwa hivo nilijiongeza kusubiri adhana ilie ili niende uelekeo huo huo. Macho nayo yalikuwa mazito ila adhana niliisikia nami nilifata uelekeo huo huo mpaka Masjid pale nikajiziguzisha maeneo yale na kwakuwa mabomba yapo nilinawa. Mida ya sala ilivyoisha nikiwa na hang hang mitaa hiyo kwa kutosomeka nilisikia stori watu wanapiga. Yameuawa wote, mengine yamekatwa, yule muarabu haingiliki wale wameyakanyaga. Nikajua hapa kishanuka

Kulipambazuka na stori kubwa town ilikuwa ni hiyo ukipita vijiweni au stendi watu wanasimuliana. Hapo sina hata ndururu (sina hela) nikawaza naondokaje huu mkoa wa Kigoma.

Nikaenda stendi kuzengea zengea nikamwona konda ananichangamkia, nikamuuliza unaenda wapi jomba? Akasema Kasulu! Nikamwambia namimi naenda huko huko ila sina nauli msaada namimi ntapiga debe, akasema sawa kwanza fanya usafi ufagie ndani ya gari hilo utoe taka zote ukamwage.

Nikafanya kama nilivoambiwa, gari lilikuwa kwenye kilo abiria walivyojaa likaondoka njiani mambo yalikuwa mengi sana ila nilifika Kasulu na kuanza kufanya kazi za day worker sokoni.

Na kulala ilikuwa ni kambi popote nilikaa kama wiki mbili kisha nikaondoka na kwenda kibondo maeneo Twabagondozi ambako huko napenyewe ni vibarua vya mtaani tu.

Huko nilibahatika kupata rafiki anaitwa Ulokoze, huyu naye tulizoeana na katika kupiga soga za hapa na pale aliniambia mishe kuu kwa huku nikuteka magari au mabasi utaweza?

Nikawaza nikaona hizo mishe ni ndogo ndogo sana nikamwambia hamna za hela ndefuu? Akasema labda wewe utupe sisi uzoefu wetu ni huku Kibondo mpaka Kasulu. Nikamuuliza silaha ipo? Akasema hana ila kuna mtu anayo nikitaka inapatikana. Nikamwambia basi hamna shida tuliachana na baada ya siku 3 alinifata na kuniambia wanaenda chimbo, yaani kutesa rizki za watu. Mi nikamwambia hizo za pesa ndogo achana nazo naendelea kusoma mazingira. Wao walienda na walifanikiwa kweli kutesa rizki.

Alivyorudi nikamwambia anifanyie mpango wa silaha kuna chimbo naenda namimi kutesa rizki. Tulienda nae nikachukua silaha na kuondoka jioni nikampitia nikamwambie twende kuna hela za kutosha, tulipofika mitaa ya Kanyamhela yeye alikuwa anaendesha pikipiki mimi nyuma amenipakia nilimpiga na kitako cha bunduki kwa nguvu pikipiki iliyumba tukaanguka wote chini, nikamsogeza pembeni ya barabara na kurudi kule kule kwake nikamvamia mkewe nakuwapora hela zote ambazo zilikuwa kama milioni 1 na chenchi kidogo.

Mimi nikaamua sasa kukimbia na ile silaha niliitupa. Hapo ni usiku ukumbuke.

Je? Nini kitaendelea usikose kufuatana nami hadi mwisho.
 
Kwanini mnaleta vistori vya kipumbavu ambavyo havina kichwa wala miguu, eti itaendelea nani alikulamisha uilete huku. Shenz.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…