Kutoka kwenye Utajiri mpaka kuishi kwenye lindi la umasikini!

Kutoka kwenye Utajiri mpaka kuishi kwenye lindi la umasikini!

Sehemu ya 3

Baada ya kufika Tarakea kwa shangazi aliniunganisha na mmeru mmoja baba wa makamu wa huko Kenya eneo moja linaitwa Oloitoktok kwa watu wa Rombo na maeneo ya jirani wanapafahamu hapo elimu ndio ilikuwa ishanipiga sandakalawe. Huyo mmeru alikuwa na mke na watoto wawili mke wake ni jamii ya Wakamba maeneo ya Taveta.

Nilianza kuuza duka la mahitaji ya nyumbani biashara kwa kweli ilikuwa nzuri ila kila huyo mwanamke wa Kikamba akija alikuwa na mtindo wa kuchukua pesa na kusema atarudisha ila harudishi, akija mumuwe anakana katakata hajachukua hivyo nakatwa mshahara wangu.

Sa nyingine ananipa nguo nivae yeye alikuwa anauza mitumba ikifika mwisho wa mwezi nakatwa kwenye mshahara wangu hata ukigoma kununua anasema nimekupa bure upendeze mwanangu ila tarehe ya salary ikifika nalimwa panga. Hicho kitu kilikuwa kinaniuma sana. Ikanibidi nimwambie mumewe ambaye ndio bosi wangu, kwa kweli maisha hapo Loitoktok niliyaona machungu sana maana nakumbuka msosi alikuwa hanipi mpaka mumewe arudi jioni ndio nakula, bado nilikuwa nasingiziwa kuwa nasumbua watoto wake nyakati za mchana, ile vita na mwanamke wa Kikamba ilinishinda ikabidi nikubali yaishe nikaomba kuondoka sikupewa hata mia kwani niliambiwa sidai kitu na bado nimesababisha hasara nyingi sana.

Ikanibidi niondoke hapo nakuelekea maeneo ya Taveta ambapo nilikutana na wafanyabiashara wengi sana watanzania ambao walikuwa wakileta maparachichi na ndizi kuja huu upande wa Kenya. Niliwaomba msaada maana hapo sasa nilikuwa nimeshaishiwa nikapandishwa kwenye Beckford ile kama kumbukumbu ziko sawa kwa nyuma kule, gari lilisafiri breki yake moshi mjini nikaambiwa tumefika.

Kwa hapo Moshi nilikuwa mgeni maana ni mjini hivo sio mzoefu. Nilizungaka huku na huku nikadakwa kwa kosa la uzururaji na kuambiwa mimi ni chokoraa, haswa kwa wakati huo machokoraa waliaminika kutenda uhalifu sana kwa Moshi.

Nilikaa ndani, na kila polisi wakinihoji ndugu wakwapi mimi nasema sina. Nilikaa kwa siku 3 nikaachiwa baada ya afande mmoja kusema angenichukua niende Mererani kwenye biashara yake kuuza maji maeneo ya Kazamoyo.

Niliuza maji kwa kutumia punda na hapo kwa kweli nilikuwa na hasira sana na maisha na niliona msaada sina tena maana ndugu wamenitenga na hata wadogo zangu sikuwajulia hali zao. Ile biashara kwa pale Mererani ilikuwa na hela maana nilikuwa nakaa kwa huyo afande na mke wake pia alikuwa askari ila wa magereza.

Nikaja kupata dili la kupeleka maji migodini huko, ila shida ikawa kwenye malipo ya hela mpaka shimo liteme ndio ulipwe na sa nyingine urushwe na bosi haelewi ni mtata sana, kuna muda anakushushia kipigo kizito sana ukichelewesha hela na huna pakwenda kushtaki anakuambia wazi wazi.

Nikaachana na hiyo kazi nikaingia kwenye uana polo na kwa nyakati hizo migodi ya Tanzanite ilikuwa inatema sana madini haswa mgodi wa Ray** na Lemak**. Ila kiujumla nilishindwa na haswa kutokana na kula msoto sana na magonjwa ya tumbo haswa typhoid ni kitu cha kawaida.

Na kwa nyakati hizo tofauti na sasa ilikuwa hulipwi hela ila mawe yakipatikana tajiri anachukua chake ndio na nyie mpate mgao ila inategemea na makubaliano.

Wengi sana tulienda na tulishindwa na wapo waliofanikiwa tukiwaona. Hivo nilipata kampani ya watu wa Ngarenaro nikaungana nao kwenda Arusha kujaribu bahati tena huko!

Je? Nini kitaendelea usikose kufuatana nami hadi mwisho.
 
Kumbe rombo ni Kwa ovyo mkuu. Maji mpaka mtoni 😅😅😅
Mto unapita nyumbani sio kwamba ya bomba hamna. Natokea msituni yani nimepakana na beacon ya serikali. .

Ila nina eneo nilipew huku chini Keni (mwai) karibu na Kenya huko na kweli maji pande hizo hakuna.

Ila hata hapa dar kuna sehemu kibao tu kuna shida ya maji😀
 
Sehemu ya 4

Nilifika Arusha na maisha yangu yalianza rasmi ambapo nilikuwa nakaa maeneo ya Ngarenaro Oysterbay na geto jingine lilikuwa Ungalimited. Hiyo nakumbuka ilikuwa mwaka 2002 ambapo shughuli kubwa pale chuga ilikuwa ni wizi.

Hao ambao nilikuwa nao mmoja ni Mmeru na wawili ni Waarusha. Hivyo kwa kipindi hicho kwa sababu mimi nilikuwa mdogo nilikuwa napewa kazi ya unyokaa. Yaani kuchumpa dirishani na kuzama ndani kuangalia vya maana nakuiba.

Nyakati za mchana tulikuwa Tuderee maeneo ya Kilombero na kuwapiga watu finga kuchomoa wallet zao mfukoni. Hayo ndio yalikuwa maisha ukishtukiwa mtu akiita mwizi basi sisi tunakimbilia kule mtoni hakuna anayekuja na hupati msaada maana kipindi hicho kwa pale maeneo ya Kilombero mgeni ukiibiwa wenyeji hawakusaidii.

Biashara hiyo ikaendelea nikaanza kuuza bangi na mirungi ambayo ilikuwa inalipa sana maana kama gomba wachanjaji walikuwa wengi. Na stimu zetu ilikuwa lazima utumie kuberi au ugoro unachanganya kwenye mbege.

Siku ya Jumapili mchana nikiwa maeneo ya soko mjinga naangalia mamangulo ni mkware mmoja, nilifatwa na jamaa wawili wakaniambia wana maongezi na mimi na mimi bila hiyana nilikubali. Hivyo tuliondoka hapo na kuelekea Mianzini ukiwa unataka kutokea Sakina.

Huko niliwakuta wale wenzangu hivyo tukapewa msuko na ramani nzima ya kwenda kupiga tukio kwa Bensonii tajiri mmoja wa vifaa vya simu maredio tv camera n.k

Sisi tulikuwa 4 kundi letu na wale jamaa kundi lao walikuwa watatu. Msuko wa hiyo ramani ni lazima mmoja ajifanye ni mteja ile mida ya jioni, mwingine atakuwa na pikipiki aina ya baja akiangalia uelekeo wa kwenda mawingu na mwingine atakuwa na gari ambayo itakuwa uelekeo wa kwenda Kilombero na wa mwisho yeye atakuwa na pikipiki nayo baja yeye uelekeo wake na mjini kati. Kumbuka tuko 7 waliobaki watatu kazi yao ni silaha tu.

Kutokana na umbo langu kuwa dogo niliambiwa niwe mteja na kwakuwa English najua hivyo nitavaa nipendeze siku ya tukio na hela ntakuwa nayo ya shopping. Wengine waliingia kwenye mazoezi ya kupigwa msasa namna ya kuchezea pikipiki na gari. Mafunzo yakiendelea huku pia namimi nikiendesha shughuli zangu za kimagendo na uwizi.

Ilipita miezi miwili siku ya Alhamisi tulikubaliana kuwa leo ndio ile siku ya kuushinda umasikini, hivyo tulipeana moyo na kwa mtu mwenye uwoga maana ulikuwepo tulitumia bangi na kuberi ili kuondoa uwoga. Tulikaa pamoja tukikumbushana majukumu yetu na kiongozi ambaye tulimuita jombaa, yeye alikuwa ana imani sana huku akisema hakuna kushindwa jambo.

Muda ulienda na ilipotimu saa 8 tulianza kujisogeza eneo la tukio taratibu huku wale wa vyombo vya usafiri wakikagua njia na kuangalia mapai wamekaa eneo gani foleni ya magari ikoje na mizunguko ya watu.

Majira ya sa 9 tulipewa vidonge aina ya benzodiazepine kwaajili ya kutuliza wenge kichwani. Nilitoka kwenye gari nimevaa jeans na tshirt nikaingia ndani kwa muhindi kwa nia ya kununua camera. Ile nikiwa nachagua chagua naonyeshwa na ufanisi wake nilisikia mlio wa bunduki hapo ndani paa! Wote laleni chini!

Je, Nini kitaendelea usikose kufuatana nami hadi mwisho.
 
20230314_155549.jpg

Poker hilo ndio daraja na mto Nduruma, umeaua sana
 
Back
Top Bottom