Kutoka kwenye Utajiri mpaka kuishi kwenye lindi la umasikini!

Kutoka kwenye Utajiri mpaka kuishi kwenye lindi la umasikini!

Sehemu ya 4
Nilifika arusha na maisha yangu yalianza rasmi ambapo nilikuwa nakaa maeneo ya ngarenaro oysterbay na geto jingine lilikuwa ungalimited. Hiyo nakumbuka ilikuwa mwaka 2002 ambapo shughuli kubwa pale chuga ilikuwa ni wizi. Hao ambao nilikuwa nao mmoja ni mmeru na wawili ni waarusha. Hivo kwa kipindi hicho kwa sababu mimi nilikuwa mdogo nilikuwa napewa kazi ya unyokaa. Yaani kuchumpa dirishani na kuzama ndani kuangalia vya maana nakuiba.
Nyakati za mchana tulikuwa tuderee maeneo ya kilombero na kuwapiga watu finga kuchomoa wallet zao mfukoni. Hayo ndio yalikuwa maisha ukishtukiwa mtu akiita mwizi basi sisi tunakimbilia kule mtoni hakuna anayekuja na hupati msaada maana kipindi hicho kwa pale maeneo ya kilombero mgeni ukiibiwa wenyeji hawakusaidii.
Biashara hiyo ikaendelea nikaanza kuuza bangi na mirungi ambayo ilikuwa inalipa sana maana kama gomba wachanjaji walikuwa wengi. Na stimu zetu ilikuwa lazima utumie kuberi au ugoro unachanganya kwenye mbege. Siku ya jumapili mchana nikiwa maeneo ya soko mjinga naangalia mamangulo nimkware mmoja, nilifatwa na jamaa wawili wakaniambia wanamaongezi namimi na mimi bila hiyana nilikubali. Hivyo tuliondoka hapo na kuelekea mianzini ukiwa unataka kutokea sakina. Huko niliwakuta wale wenzangu hivo tukapewa msuko na ramani nzima ya kwenda kupiga tukio kwa bensonii tajiri mmoja wa vifaa vya simu maredio tv camera n.k
Sisi tulikuwa 4 kundi letu na wale jamaa kundi lao walikuwa watatu. Msuko wa hiyo ramani ni lazima mmoja ajifanye ni mteja ile mida ya jioni, mwingine atakuwa na pikipiki aina ya baja akiangalia uelekeo wa kwenda mawingu na mwingine atakuwa na gari ambayo itakuwa uelekeo wa kwenda kilombero na wa mwisho yeye atakuwa na pikipiki nayo baja yeye uelekeo wake na mjini kati. Kumbuka tuko 7 waliobaki watatu kazi yao ni silaha tu.
Kutokana na umbo langu kuwa dogo niliambiwa niwe mteja na kwakuwa English najua hivo nitavaa nipendeze siku ya tukio na hela ntakuwa nayo ya shopping. Wengine waliingia kwenye mazoezi ya kupigwa msasa namna ya kuchezea piki piki na gari. Mafunzo yakiendelea huku pia namimi nikiendesha shughuli zangu za kimagendo na uwizi.
Ilipita miezi miwili siku ya alhamisi tulikubaliana kuwa leo ndio ile siku ya kuushinda umasikini, hivyo tulipeana moyo na kwa mtu mwenye uwoga maana ulikuwepo tulitumia bangi na kuberi ili kuondoa uwoga. Tulikaa pamoja tukikumbushana majukumu yetu na kiongozi ambaye tulimuita jombaa, yeye alikuwa ana imani sana huku akisema hakuna kushindwa jambo. Muda ulienda na ilipotimu saa 8 tulianza kujisogeza eneo la tukio taratibu huku wale wa vyombo vya usafiri wakikagua njia na kuangalia mapai wamekaa eneo gani foleni ya magari ikoje na mizunguko ya watu. Majira ya sa 9 tulipewa vidonge aina ya benzodiazepine kwaajili ya kutuliza wenge kichwani. Nilitoka kwenye gari nimevaa jeans na tshirt nikaingia ndani kwa muhindi kwa nia ya kununua camera. Ile nikiwa nachagua chagua naonyeshwa na ufanisi wake nilisikia mlio wa bunduki hapo ndani paa! Wote laleni chini!
Je? Nini kitaendelea usikose kufuatana nami hadi mwisho.

Duuuh
 
Huko ndipo lilipokuwa chimbo letu tukitokea kambi ya chupa madukani...😅😅😅
Kuelekea wapi mkuu.
Hili daraja niliwahi shuhudia ajali mbaya mnoo.
Magari 6 yaligongana...yale mafusso ya abiria ya Moshi Arusha lilining'inia darajani na abiria wanadindokea mtoni kama maembe na wanapasuka vichwa kwenye mawe ya mtoni
 
Kuelekea wapi mkuu.
Hili daraja niliwahi shuhudia ajali mbaya mnoo.
Magari 6 yaligongana...yale mafusso ya abiria ya Moshi Arusha lilining'inia darajani na abiria wanadindokea mtoni kama maembe na wanapasuka vichwa kwenye mawe ya mtoni
nilikuwa naishi maeneo hayo kwa juu wanapaita kambi ya chupa ukitaka kwenda tengeru lazima upite hapo darajani...
usiku hiace zinapandisha gharama kwenda huko tengeru kutokea mjini,
 
sema nin, nadhani hapo cha kuhuzunisha ni kupoteza wazazi wako, mali zenu kuuzwa na huyo dingi mkubwa, ndugu kutupiana mpira kwenye kukulea na manyanyaso ya chakula. Lakn kukata majani ya ng'ombe, kuwalisha, kusafisha banda na kuokota kuni sio mateso bali ni wajibu.
Nashangaa eti kazi ni mateso
 
Sehemu ya 5
Watu walilala ila yule muhindi akawa naye hajalala na mimi nilikuwa nimesimama nikijua kazi imeanza, nilisikia sauti ikisema mkate wenge mejaa, ghafla nilishtukizwa na kofi moja matata sana nyuma ya kichogo na kusindikizwa na mtama chini nilianguka mzima mzima mpaka chini na wenge lilikata kweli.

Muhindi yule bwana Bensonii naye hakutaka kukubali hivi hivi ila alitoa pesa haswa wenyewe wakisisitiza na kauli yao usitujazie nzi hapa. Na sisi wateja pia tuliibiwa na watu wakasepa.

Mimi nimeenda kuiba ila nikaibiwa kwa kweli jiji la Arusha nyakati hizo lilikuwa na ubabe sana sio mtoto, sio mwanamke, sio mzee kila mtu ni mbabe na hataki kuonewa. Polisi nao sio haba haswa kipindi hicho tukio likitokea mtakaa hadi nusu saa ndio muwaone. Mi nilitoka na sikuwaona wale jamaa zangu, ikanibidi nipige ngoko mpaka kule kambi niliwakuta na kuwahoji kulikoni?

Wao walisema mpango umefeli kuna watu wameuza ramani yao kwa genge lingine kukawa na mvutano wa hapa na pale kisha tukaachana kwa ahadi tutakutana tena siku nyingine.

Niliondoka Arusha nakwenda Rombo tena nikawakuta wadogo zangu na kuwapa zawadi kidogo kidogo, nakutaka kujua maisha yanaendaje kwa kweli malalamiko yalikuwa ni mengi haswa ukizingatia wabibi wakizeeka wanakuwa na maneno sana.

Niliwaahidi naenda mjini nakirudi basi ntawachukua twende wote mjini nao walifurahi na kuonyesha tabasamu lao ambalo kwangu lilinipa moyo sana na faraja.

Hii ilikuwa ni mwaka 2003 nakumbuka nilikuwa na moto sana wakutoboa kwenye maisha na kuwasaidia wadogo zangu hivyo dili za magendo ndio zilikuwa zina unafuu na chanel nilikuwa nishaanza kuziona.

Nyakati hizi niliungana na Mroso wa Matejoo na Palangyo wa Tengeru tuliungana na kuwa kundi moja hivo lengo letu lilikuwa ni kuendesha matukio ya ujambazi hii njia ya Arusha na Moshi haswa tukiwatarget wafanyabiashara wa madini maana walikuwa na fujo sana mjini kipindi wamepata hela na ilikuwa rahisi kuwagundua.

Tulijua kuwavizia huko Mererani ni risky sana maana nao huwa wako rafu mno katika uendeshaji na wengi wamejipanga hivyo tulibidi tujiongeze kwa kutafta wadada wawili mmoja kwa jina Mankah wa Machame Nronga na mwingine Adela Mrombo wa Mashati wote walikuwa weupe na wanalipa.

Hapa sasa tulimtafuta Kicherema yeye ni Mkenya mtaalam sana wa mambo ya madawa haya kizungu na alitupatia maji ambayo anasema ni kemikali sumu na inaweza kumzimisha mtu. Alitwambia ni nitrous oxide kwahyo hata sisi tuwe nayo makini. Tulianza kuwawinda haswa huko huko Mererani kwenye nyumba za wageni na 🍺🍻. Mara nyingi hawa wakishapiga mishondo wanakuwa na wapambe saivi ndio chawa ila kipindi hicho ni wapambe.

Nakumbuka aliingia Ima akiwa na wapambe wake akamwita meneja wa bar na kumpa hela acheze wimbo mmoja tu aliuchagua mpaka achoke. Kutokana na watoto wale wakichaga nimekaa nao pale wanaita jamaa alituma wapambe wake waje na sisi tulikuwa 5 jumla wanaume 3 na warembo 2. Hivo sisi hatukubana nao wakasema hawana hela hawa miyeyusho hivyo wakatuhama nakuhamia meza kuu ya hela.

Hapo tuliona mambo yanaenda kama tulivyopanga. Sisi tuliondoka na kwenda eneo letu kutulia tukisubiri ishara.

Je? Nini kitaendelea usikose kufuatana nami hadi mwisho.
 
Back
Top Bottom