Uchaguzi 2020 Kutoka viwanja vya CCM, Lindi: Membe atangaza nia ya Urais!

Uchaguzi 2020 Kutoka viwanja vya CCM, Lindi: Membe atangaza nia ya Urais!

Ebu twendeni taratibu na swala hli, Tutazame upande wa pili wa shilingi. Kwa nini watu mnafikiri Membe hafai? Ana mapungufu gani kama kiongozi na kwa nini watu mnafikiri Mwigulu amefanya vizuri kuliko Membe katika kuweka nia!. NIA ni kitu gani?

Hivi kati ya wagombea wote wa CCM kuna mmoja ambaye nyie mnafikiri ni bora zaidi ya wengine? na kwa nini?
Mapungufu ni mengi, kwanza kaonekana hakujipanga in the first place, kama hakujipanga kwa speech muhimu kama hii unategemea ajipange akiwa ikulu?

Kama umesikiliza Membe hajataja vipaumbele vyake tofauti na watiania wengine kama Wassira, Mwigulu nk waliokuwa wanataja kama ni vitano au vinne, mfano hakuzungumzia chochote kuhusu elimu, afya, maji nk.

Technical errors, sehemu kama hiyo hakutakiwa kuuabudu ushirikina waziwazi hadi kaita mzee wa kufanya zindiko kwenye mkutano, vile vile tumemsikia akisema alikwenda kwenye kaburi la Nyerere na kuongea naye, really?

Pili hatunzi kumbukumbu vizuri, kasema atagombea uchaguzi wa 2010, pia kasema tangu uhuru wapinzani wamekuwa wakishindwa uchaguzi wengine wameshindwa mara tano, hii ni kuonesha hakuwa anajua alichokusudia kukisema.
Tatu, personal attacks, kwa mtu mwenye diplomasia kama yeye hakutakiwa aende too personal.

Nne, pale alikuwa anatangaza nia alitakiwa kuwaomba wana CCM wampe ridhaa na sio kupambana na UKAWA kwa vile Ukawa sio wajumbe wa NEC ya CCM, alitakiwa kuelewa kwa kipindi hiki maadui (competitors) wake sio UKAWA ni watiania wa CCM ambao leo wanafika 22.

Amejikita kwenye eneo moja la ushirikiano wa Tanzania na nchi za nje huku masuala yanayowagusa wananchi wa kawaida akiyapa nafasi ndogo au kuyaacha kabisa.
 
Raisi wa TFF au wa wapi? Huyu jamaa tunajua anabebwa na Jumba kuu, ila either Chama kitavunjika au jamaa atafika hata round ya pili
Kwa vyovyote vile CCM wote wana makundi na wamejipanga kwa plan ABC kwa hiyo nachosema kati ya wote walokwisha weka NIA Membe ni mbora zaidi yao wote kutokana na yeye mwenyewe na Experience yake haswa katika sehemu hizi mbili 1. Ushirikiano wa Kimataifa na 2. Usalama wa Taifa unampa nafasi ya juu zaidi ya wote.

Vinginevyo yalobakia ni maneno matupu kwani sera na Ilani ya chama ndio utamaduni wa CCM miaka yote. Yeyote atakaye chaguliwa atafuata ILANI ya chama aidha kuendeleza miradi iliyokwisha pitishwa au mipya. Tumeandikiwa na kupangiwa mipango ya maendeleo ya Millenium hadi 2025 baada ya kuiweka nchi rehani na mkoba walobeba wagombea wote. Ndio maana unayaona mambo yalopitishwa toka mwaka 2000 bado yanaendelea kutimizwa kwa awamu, tofauti zao ni jinsi ya usimamizi na utekelezaji tu. Kwa hiyo tusidanganywe na mgombea sijui ataimarisha ELIMU wakati fedha hawana wala hawajui watazipata wapi wanasubiri wafadhili na wahisani.
 
Dada leo tumbo vipi? Umepata nafuu? Watanzani wenzangu, please please Say No No to third term of 4th Regime. No to uncle , no to project ya Jumba Kuu aka Membe, no to ukabila. Jamaa alivyojikita kwenye ukabila utadhani alikuwa anaonba ridhaa ya kugombea Udiwani

Naona unabwabwaja na kuhororoja bila mpango, Ukawa wenyewe wapo hapa wanagombania wagombea wa CCM, wewe uko usingizini?
 
Naamini mnapenda kupata mrejesho kama mtu wenu ame-impress au la - sasa jibu ni kuwa amepwaya:

1. Kwanza shughuli yenu imekosa ubunifu,mmeiga kila kitu kutoka shughuli ya Mzee mzima iliyofanyika Arusha tar.30/5/2015,kubalini tu kuwa EL is the pace-setter and the agenda-setter

2. Mwenyekiti wenu wa Mkoa mzee Mchopa ametutangazia kuwa Membe nae ameanza safari ya Matumaini,hii ni failure ya communication within - watu wa karibu kabisa hawaelewi mnachofanya na kwamba safari yenu inahusu nini

3. Mmeiga pia style ya Lowassa kupiga nyimbo za Capt.Komba kabla ya kuzungumza,ndo maana mtu wenu alipostuka akaamua kuimba nyimbo za kienyeji,hahahaha

4. Naamini pia kwa sasa mnatafuta ndege ya kukodi na kwa hakika kwa kuwa hamkujipanga mapema,mtakopa sana hela na mwisho wa kampeni mtakuwa na madeni makubwa mno,na natabiri mtafaruku ndani ya kambi.

POLENI NDUGU ZANGU KAZI YA KUTAFUTA URAIS NGUMU MNOOOO!
 
Membe Ama Bakari Hafai Kabisa
Yaani Anataka Kuwalinda Marais Wanaoiba Mali Ya Umma

Albino Wanakufa Halafu Anasema Dawa Anayo
Kwanini Muda Huu Bakari Yupo Serikalini Asiiwape Dawa Wauaji Ili Ndugu Zetu Albino Wasiuwawe
 
Rais ni mmoja tu ni lowasa wengine ni wasindikizaji tu
Naamini mnapenda kupata mrejesho kama mtu wenu ame-impress au la - sasa jibu ni kuwa amepwaya:

1. Kwanza shughuli yenu imekosa ubunifu,mmeiga kila kitu kutoka shughuli ya Mzee mzima iliyofanyika Arusha tar.30/5/2015,kubalini tu kuwa EL is the pace-setter and the agenda-setter

2. Mwenyekiti wenu wa Mkoa mzee Mchopa ametutangazia kuwa Membe nae ameanza safari ya Matumaini,hii ni failure ya communication within - watu wa karibu kabisa hawaelewi mnachofanya na kwamba safari yenu inahusu nini

3. Mmeiga pia style ya Lowassa kupiga nyimbo za Capt.Komba kabla ya kuzungumza,ndo maana mtu wenu alipostuka akaamua kuimba nyimbo za kienyeji,hahahaha

4. Naamini pia kwa sasa mnatafuta ndege ya kukodi na kwa hakika kwa kuwa hamkujipanga mapema,mtakopa sana hela na mwisho wa kampeni mtakuwa na madeni makubwa mno,na natabiri mtafaruku ndani ya kambi.

POLENI NDUGU ZANGU KAZI YA KUTAFUTA URAIS NGUMU MNOOOO!
 
Mapungufu ni mengi, kwanza kaonekana hakujipanga in the first place, kama hakujipanga kwa speech muhimu kama hii unategemea ajipange akiwa ikulu?

Kama umesikiliza Membe hajataja vipaumbele vyake tofauti na watiania wengine kama Wassira, Mwigulu nk waliokuwa wanataja kama ni vitano au vinne, mfano hakuzungumzia chochote kuhusu elimu, afya, maji nk.

Technical errors, sehemu kama hiyo hakutakiwa kuuabudu ushirikina waziwazi hadi kaita mzee wa kufanya zindiko kwenye mkutano, vile vile tumemsikia akisema alikwenda kwenye kaburi la Nyerere na kuongea naye, really?

Pili hatunzi kumbukumbu vizuri, kasema atagombea uchaguzi wa 2010, pia kasema tangu uhuru wapinzani wamekuwa wakishindwa uchaguzi wengine wameshindwa mara tano, hii ni kuonesha hakuwa anajua alichokusudia kukisema.
Tatu, personal attacks, kwa mtu mwenye diplomasia kama yeye hakutakiwa aende too personal.

Nne, pale alikuwa anatangaza nia alitakiwa kuwaomba wana CCM wampe ridhaa na sio kupambana na UKAWA kwa vile Ukawa sio wajumbe wa NEC ya CCM, alitakiwa kuelewa kwa kipindi hiki maadui (competitors) wake sio UKAWA ni watiania wa CCM ambao leo wanafika 22.

Amejikita kwenye eneo moja la ushirikiano wa Tanzania na nchi za nje huku masuala yanayowagusa wananchi wa kawaida akiyapa nafasi ndogo au kuyaacha kabisa.
Mkuu labda nikuulize hivi. Kweli wewe unategemea Lipumba na Dr.Slaa wasimame kuweka nia kama wagombea wa UKAWA, kisha kila mmoja ajieleze tofauti na ILANI ya UKAWA watakuwa wamejenga hoja ya msingi? Yaani Mbatia akiongea vizuri kuliko Dr.Slaa au Lipumba itakupa moyo zaidi na Mbatia ama jinsi unavyowafahamu wagombea hawa nani mwenye uwezo zaidi?

Nimepitia maandishi ya mleta mada hapo juu sikuona kosa zaidi ya mtu aloweka nia tu. Kumbuka kila alozungumza kasema Vipaumbele vyake ataanza na nini wakati hakuna kati yao alosema fedha zitatoka wapi? Atakata wapi ili awezeshe wapi. Hizi zote ni porojo tupu kwa mtu asokuwa na kitu maana waswahili wengine wamejaaliwa mdomo lakini utekelezaji ni mashoga.

Mipango yote ya Maendeleo ya CCM yanategemea mikopo na mpango wa maendeleo tulopewa na IMF na Marekani Millenium sijui hadi huko 2025, kwa hiyo hakuna mjuzi pale, wote wameisha pangiwa (copy and paste) umchague Membe au Mwigulu tofauti zao ni nani kweli ataweza kusimamisha utawala wa sheria katika nchi hii ama kuleta kweli mageuzi..

Unapotia tia onyesha wewe ndiye mgombea uliye tayari kupambana na Upinzani, Unatazama mbele sio kilicho mfukoni maana kuweka nia una uhakika kwa kiwango kikubwa cha kupita..
 
Unavyo sema ukawa
Zungumzia habari nyingine ukawa mziki mnene ccm hamuwezi sibili tiingie kwenye kampeni.
 
Akiteuliwa kugombea, picha itamsaidia kumpa kura za wamama.Nakumbuka ata chuo sie tusiokuwa "presentable" tulikuwa tunadisadvantage kwenye angle hiyo maaba viumbe wetu hawa kitu cha kwanza walikuwa wanangalia muonekano wa mtu.Mitaani, vijijini na uswahilini ndio usiseme.
ina maana wasira hapati kitu.
 
ccm wote ni majanga tu, ila point moja aliyoongea ni kuwa mkitaka kumjua mgombea msafi ni nani, angalia watu wanaomzunguka ni kina nani!! na nyingine ni kuwa yeye hana magunia ya pesa ya kugawa.
 
wooooteee wanaotangaza nia hawajamfikia makongoro nyerere

A philosophical man.. yah, huyu Nerere jr.aliweza kuteka hadhir yake kwa mpangilio na ukizingatia yeye alikuwa anaflow tu bila karatasi wala kinote book, empty handed ila bado ameita unchallenged,ngoja tusubiri akiamua kuandika point zake sijuhi hawa jamaa watakimbilia wapi.
 
Kwa vyovyote vile CCM wote wana makundi na wamejipanga kwa plan ABC kwa hiyo nachosema kati ya wote walokwisha weka NIA Membe ni mbora zaidi yao wote kutokana na yeye mwenyewe na Experience yake haswa katika sehemu hizi mbili 1. Ushirikiano wa Kimataifa na 2. Usalama wa Taifa unampa nafasi ya juu zaidi ya wote.

Vinginevyo yalobakia ni maneno matupu kwani sera na Ilani ya chama ndio utamaduni wa CCM miaka yote. Yeyote atakaye chaguliwa atafuata ILANI ya chama aidha kuendeleza miradi iliyokwisha pitishwa au mipya. Tumeandikiwa na kupangiwa mipango ya maendeleo ya Millenium hadi 2025 baada ya kuiweka nchi rehani na mkoba walobeba wagombea wote. Ndio maana unayaona mambo yalopitishwa toka mwaka 2000 bado yanaendelea kutimizwa kwa awamu, tofauti zao ni jinsi ya usimamizi na utekelezaji tu. Kwa hiyo tusidanganywe na mgombea sijui ataimarisha ELIMU wakati fedha hawana wala hawajui watazipata wapi wanasubiri wafadhili na wahisani.
Kubwa zaidi watu tunadhani pale ni sehemu ya kumwaga sera wakati kimsingi pale ni sehemu ya kutangaza nia tu... haya maneno mengi ni mbwembwe tu kwa kuwa E.L alianza kwa staili hiyo! Pale Membe na wengine kama yeye hawatafuti ridhaa ya Watanzania bali ridhaa kutoka kwa wana-CCM, hivyo basi, kwa hatua hii, wanakotakiwa kujimaliza ni ndani ya vikao vya CCM na sio kwenye mikutano ya kutangaza nia! Na hata hii mkikutano ya kuoneshwa LIVE wala haikuwa na sababu lakini kv kuna mtu ameanza, hakuna aliye tayari kuachwa nyuma! Candidate awe na sera bora kuliko zote lakini, mathalani, ikiwa moja wapo ni kuvunja Muungano, CCM hawawezi kukupitisha lakini kama ingekuwa ni wakati wa kutangaza sera kwa wananchi huenda sera hiyo ingekupa kura!! Wakishatoka kwenye vikao vya CCM, nikiwa na maana kwa yule atakayepitishwa kama ndie mgombea rasmi, ndipo sera zao sasa zitakuwa wazi kwa Watanzania! Na kimsingi, zinakuwa sio sera zake tena bali ni sera za CCM!!
 
Mkuu labda nikuulize hivi. Kweli wewe unategemea Lipumba na Dr.Slaa wasimame kuweka nia kama wagombea wa UKAWA, kisha kila mmoja ajieleze tofauti na ILANI ya UKAWA watakuwa wamejenga hoja ya msingi? Yaani Mbatia akiongea vizuri kuliko Dr.Slaa au Lipumba itakupa moyo zaidi na Mbatia ama jinsi unavyowafahamu wagombea hawa nani mwenye uwezo zaidi?

Nimepitia maandishi ya mleta mada hapo juu sikuona kosa zaidi ya mtu aloweka nia tu. Kumbuka kila alozungumza kasema Vipaumbele vyake ataanza na nini wakati hakuna kati yao alosema fedha zitatoka wapi? Atakata wapi ili awezeshe wapi. Hizi zote ni porojo tupu kwa mtu asokuwa na kitu maana waswahili wengine wamejaaliwa mdomo lakini utekelezaji ni mashoga.

Mipango yote ya Maendeleo ya CCM yanategemea mikopo na mpango wa maendeleo tulopewa na IMF na Marekani Millenium sijui hadi huko 2025, kwa hiyo hakuna mjuzi pale, wote wameisha pangiwa (copy and paste) umchague Membe au Mwigulu tofauti zao ni nani kweli ataweza kusimamisha utawala wa sheria katika nchi hii ama kuleta kweli mageuzi..

Yawezekana Dr Slaa na Prof Lipumba wasimzidi Mbatia kwa kupangilia mawazo yao vizuri wanapowasilisha hoja lakini bado hoja zao zitakuwa nzito,zenye facts na zinazoshawishi.At least hawatachanganya mambo kama alivyofanya Mr Bernard C. Membe kwamba wanatangaza kugombea urais mwaka 2010 au vyama vya Upinzani vimezowea kushindana na kushindwa tangu tupate uhuru mpaka sasa. Aidha ameapa kupambana na ugaidi nchini,is he serious? Hivi terrorists anawajua?Wapi wamelipua Tanzania? Huyu kama akiwa rais anaweza kuvunja rekodi za Mulugo (Waziri wa Elimu wa zamani) aliyedai kwamba Muungano wa Tanzania unatokana na Tanganyika na Zimbabwe. Hatutake tuaibike huko nje ya nchi kwamba rais wetu amechanganya mambo ktk hotuba yake flani,please!
 
yangu masikio na macho kuona nini kitajiri kwa sasa sina haja ya kupoteza nguvu zangu kuzungumzia hili!
 
Back
Top Bottom