Uchaguzi 2020 Kutoka viwanja vya CCM, Lindi: Membe atangaza nia ya Urais!

Uchaguzi 2020 Kutoka viwanja vya CCM, Lindi: Membe atangaza nia ya Urais!

inaonesha humu kuna kundi kubwa la wale waliokodiwa mabasi kwenda sheikh amri abeid.
 
Yawezekana Dr Slaa na Prof Lipumba wasimzidi Mbatia kwa kupangilia mawazo yao vizuri wanapowasilisha hoja lakini bado hoja zao zitakuwa nzito,zenye facts na zinazoshawishi.At least hawatachanganya mambo kama Mr Bernard C. Membe kwamba wanatangaza kugombea urais mwaka 2010 au vyama vyama vimezowea kushindana na kushindwa tangu tupate uhuru mpaka sasa. Aidha ameapa kupambana na ugaidi nchini,is he serious? Hivi terrorists anawajua?Wapi wamelipua Tanzania? Huyu kama akiwa rais anaweza kuvunja rekodi za Mulugo (Waziri wa Elimu wa zamani) aliyedai kwamba Muungano wa Tanzania unatokana na Tanganyika na Zimbabwe. Hatutake tuaibike huko nje ya nchi kwamba rais wetu amechanganya mambo ktk hotuba yake flani,please!
Mkuu taratibu, twende kwa mpango maana siwezi kuamini kwamba Mbatia anaweza washinda Lipumba na Dr.Slaa kwa kutia nia halafu ukasema afadhali watakuwa wamezungumza facts!..FACTS zipi hadi washindwe na huyo Mbatia atakuwa amesema nini. Ukishindwa ina maana hukuweza kuwaridhisha wananchi kwisha..

Kifupi, Hali ya Usalama nchini ni tete na usitazame tu magaidi (terrorists) Kina Al - Shabab, wapo magaidi wa ndani kama umesahau wakimbizi wa Rwanda na Burundi awamu ya kwanza ya JK. Majambazi wa kupora na kuiba majumbani all are terrorist. Kuna maswala ya Zanzibar na Bara, Waislaam na Wakristu akipitishwa rais mzigo, mkuu wangu itakula kwetu.

Mimi simpambi lakini ndivyo navyoona hadi sasa hivi watu watatu, Yeye, Mwigulu na Makongoro wana ukomavu katika baadhi ya sehemu. Makongoro ni CCM Asilia, sijui kama ataweza badilisha watu walokwisha batizwa Ubepari, Mwigulu kaandaliwa vema na Membe anayo experience zaidi yao wote sehemu nyeti ktk kutazama uwezo na sifa za mgombea Urais.

Binafsi yangu leo, bora mtu anayezungumzia mambo ya ndani na sheria kuliko yule anaye ahidi Maendeleo wakati kisha pangiwa anafanya nukuu tu. Nani baina yao aloahidi nje ya Mipango ya maendeleo tulokwisha pangiwa hadi 2025 nakala hii HAPA Je, huyo muweka nia wa CCM ataandika yake kinyume cha kupangiwa?.Atapata wapi fedha za kuanzisha miradi hiyo kama sio kodi juu zaidi kwa wananchi..
 
Mkuu labda nikuulize hivi. Kweli wewe unategemea Lipumba na Dr.Slaa wasimame kuweka nia kama wagombea wa UKAWA, kisha kila mmoja ajieleze tofauti na ILANI ya UKAWA watakuwa wamejenga hoja ya msingi? Yaani Mbatia akiongea vizuri kuliko Dr.Slaa au Lipumba itakupa moyo zaidi na Mbatia ama jinsi unavyowafahamu wagombea hawa nani mwenye uwezo zaidi?

Nimepitia maandishi ya mleta mada hapo juu sikuona kosa zaidi ya mtu aloweka nia tu. Kumbuka kila alozungumza kasema Vipaumbele vyake ataanza na nini wakati hakuna kati yao alosema fedha zitatoka wapi? Atakata wapi ili awezeshe wapi. Hizi zote ni porojo tupu kwa mtu asokuwa na kitu maana waswahili wengine wamejaaliwa mdomo lakini utekelezaji ni mashoga.

Mipango yote ya Maendeleo ya CCM yanategemea mikopo na mpango wa maendeleo tulopewa na IMF na Marekani Millenium sijui hadi huko 2025, kwa hiyo hakuna mjuzi pale, wote wameisha pangiwa (copy and paste) umchague Membe au Mwigulu tofauti zao ni nani kweli ataweza kusimamisha utawala wa sheria katika nchi hii ama kuleta kweli mageuzi..
Mkuu, kwa taarifa tu Tanzania huwa tunachagua mtu(rais) atakayewakilisha chama huwa hatuchagui chama kama UK. Sasa kama mtiania huyo hana anachopanga kuanza nacho kama alivyo Membe kuna haja gani ya kumfikiria kuwa rais.

Kama wagombea hawana sera na vipaumbele vyao kuna haja gani ya kuwa na watiania wengi ndani ya CCM si wangemteua mwenyekiti wao tu akawakilisha chama kupambana na mgombea kutoka UKAWA.

Tofauti na CCM UKAWA nao wana utaratibu wao wa kumpata mgombea, hata kama watakuwa na sera na ilani moja itawalazimu kuwaita wagombea watakaojitokeza waeleze vipaumbele vyao.

Mfano...ilani ya UKAWA kwenye sera iko kama ifuatavyo, 1. Elimu 2. Afya 3. Miundombinu nk, itabidi waangalie mgombea A ana vipaumbele vipi kwenye sera ya Elimu je ataanza na kujenga madarasa au yeye ataanza na mishahara ya walimu nk, je B yeye anasemaje kwenye sera ya Miundombinu anaona kipi muhimu kujenga reli au barabara na ana mipango gani. Kwa hiyo hata kama chama kina sera na ilani yake lazima kiangalie kitafit most na mgombea yupi.
 
Mkuu, kwa taarifa tu Tanzania huwa tunachagua mtu(rais) atakayewakilisha chama huwa hatuchagui chama kama UK. Sasa kama mtiania huyo hana anachopanga kuanza nacho kama alivyo Membe kuna haja gani ya kumfikiria kuwa rais.

Kama wagombea hawana sera na vipaumbele vyao kuna haja gani ya kuwa na watiania wengi ndani ya CCM si wangemteua mwenyekiti wao tu akawakilisha chama kupambana na mgombea kutoka UKAWA.

Tofauti na CCM UKAWA nao wana utaratibu wao wa kumpata mgombea, hata kama watakuwa na sera na ilani moja itawalazimu kuwaita wagombea watakaojitokeza wajieleze vipaumbele vyao.

Mfano...ilani ya UKAWA kwenye sera iko kama ifuatavyo, 1. Elimu 2. Afya 3. Miundombinu nk, itabidi waangalie mgombea A ana vipaumbele vipi kwenye sera ya Elimu je ataanza na kujenga madarasa au yeye ataanza na mishahara ya walimu nk, je B yeye anasemaje kwenye sera ya Miundombinu anaona kipi muhimu kujenga reli au barabara na ana mipango gani. Kwa hiyo hata kama chama kina sera na ilani yake lazima kiangalie kitafit most na mgombea yupi.
Unachokosea mkuu wangu ni kusema tanzania tunachagua MTU ukasahau kwamba huyo mtu hupangiwa ILANI na chama chake. Hivyo vipaumbele vyake ni porojo tupu maana masikini hana kupanga jambo hupangiwa.

Kwa hiyo unachanganya kutazama mazuri yanayokufaa tu wakati hutazami hali halisi ya vyama na sababu za kufukuzwa watu wasiofuata misimamo ya chama. Kweli sisi huchagua MTU na sio chama kwa hiyo Membe hatafuti kura yako bali ameweka nia ili kupata hizo saini za wafadhili wake. Tofauti na mfumo wa nchi nyingine wagombea wote tayari wana uhakika wa wadhamini toka mikoa yao ama sehemu walokwisha pitia, kwa hiyo hatua ya pili ni kupita ngazi za chama tu na kuna vigezo vyake sio swala la Sera wala vipaumbele ila nani anauzika?.

Hivyo mgombea huchaguliwa kwa sababu anakubalika na wananchi kwa sura na tabia zake maana kumbuka JK alikataa hata midahalo na Dr.Slaa na bado akashinda!. Kwa hiyo yeyote atakaye simama kwa jina la CCM ndiye atakaye tangaza SERA na ILANI ya chama dhidi ya Upinzani kwa kutoa ahadi tu, lakini leo huko ndani watashindania nani atakuwa mwakilishi mzuri wa CCM kwa kufuata vigezo vya Wadanganyika kama mnavyotaka hadi sasa ambavyo ni UNAFIKI, Atakaye kuwa MNAFIKI zaidi ndiye atakaye shinda, watu kama Muhongo na Lowassa!.
 
Mkandara

Sikiliza vipaumbele vya January Makamba sikumsikia Membe akitaja hata kimoja.

1. kukuza kipato cha uchumi cha mtu mmoja mmoja.
2. huduma bora za uhakika za kijamii
3. utawala bora, utawala wa haki
4. usimamizi wa uchumi ma benki, TRA, na mashirika ya umma nk.
5. kudumisha amani
 
Ccm hakuna jipya watu ni wale wale sera zilezile tusitarajie manadiliko yoyote kutoka kwa hawa jamaa, tubadilishe tuweke chama kingine kwani sio dhambi.. Tanzania miaka 50 hakuna mabadilko ya maana rasilimali zinaisha nchi inageuka jangwa na bado nchi masikin...
 
Tofauti na CCM UKAWA nao wana utaratibu wao wa kumpata mgombea, hata kama watakuwa na sera na ilani moja itawalazimu kuwaita wagombea watakaojitokeza waeleze vipaumbele vyao.
Hapo kwenye RED ndicho pia wanachofanya CCM! Utafika wakati wote hawa wataitwa mbele ya vikao vya CCM kuelezea vipaumbele vyao... kimsingi, wakati wa kutangaza nia hawalazimiki kufanya hivyo! Pale inatosha kabisa kuitisha tu Press Conference ukatangaza nia, biashara inaisha na kusubiria hatua nyingine!
 
UKAWA tunaheshimu hadhi ya cheo cha rais sio CCM ambao wamekifanya kama sehemu ya kujifunzia siasa hadi watoto wa shule wa miaka 20 nao wametangaza.


Wanaeshimu urais wapi! democrasia changa na mfumo wa kidictatar na kifalme unaowanyanyasa nafsi, kibabu kimengangani tangaza nia uone.
 
tangu waanze kutangaza nia membe leo ameharibu.
1.hajaeleza dira dhidi ni historia yake.
2.kutukana wapinzani wakati hajapitishwa bado na cc .
3.ameshindwa kuwa na hoja sahihi zaidi ya kueleza tambo za rushwa bila kuzifahamu sheria za rushwa .
4.kuivua nguo serikali wakati yeye ni mmoja wapo.
5.kueleza habari za kaburi la nyerere wakati makongoro analala juu ya kaburi la baba yake.
5.amefeli kuelezea kwanini awe yeye na si mwingine.
6.pia amejishushia hadhi pale aliposema kawa kiongozi wa ccm tangu enzi za nyerere,mwinyi,mkapa ila hakuwahi kuwa hata balozi wa ccm wa nyumba kumi means viongozi wa awamu tatu hawakumuamini .busara angekaa kimya angetangazia nia chumbani akiwa yeye na mke wake.
Kweli amekosa washauri wa kumweleza cha kusema ? Na waandishi wa hotuba mlishindwa kumwandikia ya msingi zaidi ya ngoma za kimwela?,
ndio maana nasema leo mh membe umetia aibu kweli hotuba ya kuwania urais uzungumzie "ukiwa rais utakataza pombe kwa wanaume wanaowanywea watu" kweli membe uko serious hata huyo shemeji hawezi kukubeba kwa style hii .hotuba yako haukuipanga ktk mtindo wa nini cha kufanya kwa tanzania ijayo ndo maana ulikuwa ukisema nani kama membe watu kimya.
Tunakushauri kaa pembeni maana huwezi kujenga hoja zenye mantiki na mashiko.
Ahsante
twalb zubeir
fbi .


ccm futa membe futa lowasa,hawafai wapenda bifu za kijinga,wapenda mitandao na urafiki usio na tija kwa masikini, hawajiamini ndo maana wanaweka watu wa kuwapamba hadi kwenye mitandao.
 
baada ya ccm kukataza watangaza nia kushiriki mdahalo ndo nikaelewa kuwa membe ndo chaguo la ccm.wanajua udhaifu wake ndo maana walijua ataaibika

mkuu mdahalo upo kwa watangazani nawaurumia wengine maana vigezo vilivyo wekwa ni aibu.mfn

1,hotuba inayoeleweka
2,nusu ya takwimu za hotuba yako zitoke kichani sio kukopy hadi kumta,
3 muda masaa 3
4,mtiririko uaoeleweka sio kurudi hoja na maneno,
yaani acha kabisa iko burudani

 
Mkandara

Sikiliza vipaumbele vya January Makamba sikumsikia Membe akitaja hata kimoja.

1. kukuza kipato cha uchumi cha mtu mmoja mmoja.
2. huduma bora za uhakika za kijamii
3. utawala bora, utawala wa haki
4. usimamizi wa uchumi ma benki, TRA, na mashirika ya umma nk.
5. kudumisha amani
Atakuzaje? Nini maana ya huduma bora ama utawala bora ikiwa hazisemi sheria gani atazipitisha. Ndio hayo ya Cyberbill badala ya kutaja specific crimes, sheria inasema matumizi mabatya ya Mitandao.. Ni yapi hayo? oooh hapo tena utawasikia sijui Bulling! kwani walishindwa nini kuandika Bulling katika mitandao ndio crime! badala yake tunaona sheria inayotaka kumlinda Lowassa na mafisadi isiwe kigezo cha kuwabomoa.

Labda nikwambie ukweli, January Makamba nilimpenda kwa sababu ya exposure yake lakini ilipofika swala la kodi za simu, mara kaingia katika hii Cyberbill ili kumlinda Lowassa kiana huku tukiaminishwa ni team tofauti inanipa picha kwamba pengine he bet his chances as plan B itakavyokuwa japo EL anataka yeye tu na kama sio yeye basi hakuna mwingine..

Kwa hiyo, hii habari ya kutangaza sijui nitafanya hivi ama vile wakati unaomba nia ni kujaribu kuleta siasa za nchi za magharibi ambako rais ana wajibu mkubwa wa kujitofautisha katika Vipaumbele vyake akionyesha fedha zitatoka wapi na atakata mambo gani kutokana na bajeti inayotegemewa na wataalam wa mambo hayo wakayajadili.
 
kubwa zaidi watu tunadhani pale ni sehemu ya kumwaga sera wakati kimsingi pale ni sehemu ya kutangaza nia tu... Haya maneno mengi ni mbwembwe tu kwa kuwa e.l alianza kwa staili hiyo! Pale membe na wengine kama yeye hawatafuti ridhaa ya watanzania bali ridhaa kutoka kwa wana-ccm, hivyo basi, kwa hatua hii, wanakotakiwa kujimaliza ni ndani ya vikao vya ccm na sio kwenye mikutano ya kutangaza nia! Na hata hii mkikutano ya kuoneshwa live wala haikuwa na sababu lakini kv kuna mtu ameanza, hakuna aliye tayari kuachwa nyuma! Candidate awe na sera bora kuliko zote lakini, mathalani, ikiwa moja wapo ni kuvunja muungano, ccm hawawezi kukupitisha lakini kama ingekuwa ni wakati wa kutangaza sera kwa wananchi huenda sera hiyo ingekupa kura!! Wakishatoka kwenye vikao vya ccm, nikiwa na maana kwa yule atakayepitishwa kama ndie mgombea rasmi, ndipo sera zao sasa zitakuwa wazi kwa watanzania! Na kimsingi, zinakuwa sio sera zake tena bali ni sera za ccm!!


mkuu nimekubali! Ktk siku ambayo nimeingia humu na kukuta logic sms ni hii yako,nadhani kuna kitu cha ziada unacho kichwani,hivyo ndivyo ilitakiwa kuwa,mpaka sasa nimemuona 1, ambaye amekuja na style yake wengine ni viraza tu kukopi na kupest hadi sumu,nikisema
magufuli anawazidi wote, watu wanabisha,asante sana kwa ufafanuzi huo.
 
baada ya ccm kukataza watangaza nia kushiriki mdahalo ndo nikaelewa kuwa membe ndo chaguo la ccm.wanajua udhaifu wake ndo maana walijua ataaibika

mkuu mdahalo upo kwa watangazani nawaurumia wengine maana vigezo vilivyo wekwa ni aibu.mfn

1,hotuba inayoeleweka
2,nusu ya takwimu za hotuba yako zitoke kichani sio kukopy hadi kumta,
3 muda masaa 3
4,mtiririko uaoeleweka sio kurudi hoja na maneno,
yaani acha kabisa iko burudani

 
Healing of the nation and party needs to be part of the process. Hatuchagui mwenyekiti wa chama kama watia nia wengine walivyosema katika vipaumbele vyao
 
Ndugu yetu Bernard Membe ameanza safari ya matumaini

Source:Mzee Mchopa -M/kiti wa CCM mkoa Lindi 7/06/2015
 
Back
Top Bottom