Uchaguzi 2020 Kutoka viwanja vya CCM, Lindi: Membe atangaza nia ya Urais!

Uchaguzi 2020 Kutoka viwanja vya CCM, Lindi: Membe atangaza nia ya Urais!

Mojawapo ya maajabu ya dunia ni Tanzania kuwa na viongozi ambao hawajitambui na hawana sifa kabisa za kuwa viongozi lakini ndio viongozi/mawaziri wetu. Mtu mzima anautaka urais ili amfurahishe Nyerere???? Huu ni ulimbukeni na usanii uliopitiliza. Membe huna sifa hata kidogo ya kuwa rais wa Tanzania, kwa mtizamo wangu kwa mtizamo ulionao hata kuwa kiongozi wa mtaa ni shida.
 
JF
Jana kwa !maranyingine tena tumeshudia kituko kingine kwa wanachama wa chama cha watia nia kutoka CCM wakiendelea kutuimbia nyimbo zisizona chembe chembe ya ukweli hata kidogo. Membe katika ubora wake alidai kutembelea kaburi la Mwalimu Butiama na kumuomba mwalimu amsaidie kuvaa vyatu v alivyomwachia Mwinyi, mwinyi kumwachia Mkapa na baadae JK. Sina hakika kama Mwalimu wetu mpendwa alimjibu au kumfukuzia mbali. AIBU!!!!.

Moja ya sababu alioitoa kwa nini anataka kuvivaa hivyo viatu nikwamba vyatu hivvyo bado ni vipyaaaaaa kama alvyoviacha Mwalimu.
Toka jana nimekuwa nikijiuliza kama kweli hvi viatu ni vipya au la. Anaposema viatu ni vipya basi tunategemea kuona vitu alivyoviacha mwalimu vikiendelea kwepo au vikiboreshwa na kuwa imara zaidi.
Kwangu mimi viatu kundelea kuwa vipya basi napata maana mbili; moja ni kwamba viatu havikutumika kabisaa toka mwalimu avivae mara ya mwisho na la pili nikwamba viutu vya mwalimu havipo tena bali viatu alivyoviona membe ikulu sio vilee vya mwalimu bali ni vingine vimeunuliwa vipya kutoka china, vikapakwa kiwi na kuwekwa kona moja hapo ikulu ili kuonyeshea wageni wa i***** kama membe ili kuwazuga.

Mh. Membe hivi uliviona vile vya mwalimu kweli???, siamini mimi!

Kama kweli viatu vya mwalimu vipo basi hatutegemei kuona mafisadi wakidunda mtaani.

Mwalimu hakuacha UFISADI ulokithiri kila kona na kila idara ya serikali, kuanzia magogini kwenyewe mpaka manyumbani kwetu. Kwa ufisadi huu hvi ni kweli viatu vya mwalimu bado vipya??au mheshimiwa haamini kwamba ufisadi umeshatafuna viatu hadi kamba za kufungia viatu.

Kingine kama viatu ni vipya basi tunategemea kuona Azimio la Arusha likiendelea au hata likiboreshwa na kuwa imara zaidi. Basi kwa hili nalo mheshiwa kawa kipofu kabisaaaa na haoni. Watu wamekuwa vipofu kiasi kwamba hawaoni hata aibu kudanganya saa sita mchana kweupeeeee. AIBU GANI HII!!!,

Viwanda alivyojenga mwalimu viko wapi Mh. Membe?? Au unaposema viatu vya mwalimu bado vipya unamaanisha vile vya na 9 vya Bata???, sijaelewa mimi!!. Kila kitu alichoacha mwalimu kimeharibiwa vibaya isipokuwa mipaka ya nchi.

Kwa imani yangu vile vya mwalimu kwanza havikutoshi labda uvikate katikati ili mvivae wawili wewe pamoja na mbuge wangu Wasira. Mkifanya collabo labda mtakaribia karibia namba ya mwalimu.

Nawasilisha
 
Nilisikiliza hotuba ya Hon Membe kwa mshangao. Hivi kweli wewe baada ya kuwa wa mwisho mwisho kutangaza nia ulishindwa kujiandaa vizuri kama Rais mtarajiwa? Unatafutaje Urais kwa kuongea na mtu aliyekufa miaka 16 iliyopita? Sasa ni wazi kwamba hata albino na wazee wataendelea kuuwawa kwa utaratibu huu. Hon Membe hotuba yako pia ilipwaya sana hata kuliko ya Kingwangala, Mwigulu na January ambae anaonekana kujipanga vizuri, angalau kwa kuandaa hotuba nzuri na mtiririrko. Tulitaka kusikia sera lakini hatukuona Hon Membe. Ni wazi kwamba utawalea watoa rushwa. Kuwa usalama wa Taifa au jeshini mbona wengi tu walikuwepo hata Rais Kikwete mwenyewe na Hon Pinda, lakini zaidi tunataka kusikia umeshafanya nini kama msingi wa sisi kukuamini utafanya nini mbele. HUJANISHAWISHI HATA KIDOGO KAMA WEWE NI PRESIDENTIAL MATERIAL!
 
Hili jiwe limetupwa gizani,naona kuna mtu lishampata
 
Chama chetu hakibadili jina Tokea ASP ,TANU mpaka CCM.Kuna wengine wamezunguka wakaja na UKAWA, tumegundua ujanja ujanja sio UKAWA bali UKIWA.
 
Duh sasa Nyerere afurahie yeye kuwa rais, halafu Makongoro afurahiwe na nani? CCM bwana kila mtu anataka kusafiria nyota ya Nyerere

Hili limeniacha hoi.
Hayo ndiyo mawazo ya Raisi Mtarajiwa.
Tunaletewa Richmond yeye akiwa Waziri wa Mambo ya Nje alisaidia nini mpaka Kampuni ya Kitapeli kuvuga Serikali Mzima tena anajidai eti Shushu mzoefu.

 
ndo nimetoka kumsikiliza mtangaza nia Bernad membe kaongea kwa kujivuna weee eti aliongea na NYERERE kaburini naye kampa ruksa
.. kwa kumaliza katuomba tumsindikize kwenye jumba kubwa lile jeupe zuri pale baharini... dah eti tumsindikize se tulale nje ye ndani...
 
Back
Top Bottom