Uchaguzi 2020 Kutoka viwanja vya CCM, Lindi: Membe atangaza nia ya Urais!

Uchaguzi 2020 Kutoka viwanja vya CCM, Lindi: Membe atangaza nia ya Urais!

ccm inajitahidi kujitangaza kama chama kupitia watangaza nia.

bado sijamwona msafi ambaye anakidhi urais, wote walewale
 
Wakuu,


Mtakumbuka juzi wakati anatagaza nia pale Lindi, Bernard Membe alishindwa kujieliza au kujenga hoja za maana za kushawishi wana-CCM wenzake ili waweze kumpitisha kuwania Urais, kuna taarifa mpya kwamba, Tayari amishatonywa kuwa ndiye atakayeteuliwa ndiyo maana alikuwa anaongea utadhani tayari amishapitishwa kugombea Urais au tayari ni Rais, vile vile, Bernard Membe alionekana kutokuwa makini na tukio lenyewe pale aliposema anagombea Urais mwaka 2010 badala ya 2015 na kurudia zaidi ya mara 4 sentensi hii, pia alikosa umakini na kutokujua dhamira ya tukio la siku hiyo ambapo lilikuwa ni mahsusi kwa ajili ya kutangaza nia na kuwaomba wanaCCM wenzake wamuunge mkono..yeye akaenda zaidi hadi kwa Ukawa....

Kwa kweli Bernard Membe ni dhaifu sana labda viongozi wa Juu wa CCM wanapenda mtu kama huyu ndo awe mgombea wao lakini kama wpo serious basi Makongoro Nyerere, Magufuli, Mwigulu, Mwandosya, Mhongo au wasira au January wanafaa.
 
Si unajua mtu akisoma sana kujieleza inakua ngumu ila vitendo ndio mwenyewe we subiri aingie pale mjengoni DUME LA KIMWERA. Wamekaa
 
wakati mc akimkaribisha joji khama kwenye jukwaa kuongea kwenye mkutano wa kutangaza nia amenukuliwa ''joji khama ndo alikua akitumwa na mwlimu kwenda kufuatilia mipango ya mapinduzi''

hv we unamjua george kahama huyu ambaye alikuwa waziri wa kwanza tz lakin kaiba kipindi cha mkapa kajenga kiwanda cha baiskeli za vilema canada, naye rushwa asidanganye, familia yake iko uko , kadanganya wana karagwe mpaka basi
 
wakuu,


mtakumbuka juzi wakati anatagaza nia pale lindi, bernard membe alishindwa kujieliza au kujenga hoja za maana za kushawishi wana-ccm wenzake ili waweze kumpitisha kuwania urais, kuna taarifa mpya kwamba, tayari amishatonywa kuwa ndiye atakayeteuliwa ndiyo maana alikuwa anaongea utadhani tayari amishapitishwa kugombea urais au tayari ni rais, vile vile, bernard membe alionekana kutokuwa makini na tukio lenyewe pale aliposema anagombea urais mwaka 2010 badala ya 2015 na kurudia zaidi ya mara 4 sentensi hii, pia alikosa umakini na kutokujua dhamira ya tukio la siku hiyo ambapo lilikuwa ni mahsusi kwa ajili ya kutangaza nia na kuwaomba wanaccm wenzake wamuunge mkono..yeye akaenda zaidi hadi kwa ukawa....

Kwa kweli bernard membe ni dhaifu sana labda viongozi wa juu wa ccm wanapenda mtu kama huyu ndo awe mgombea wao lakini kama wpo serious basi makongoro nyerere, magufuli, mwigulu, mwandosya, mhongo au wasira au january wanafaa.

ikulu si sehem ya kuuza sura
 
Jana niliwasha TV nikajaribu kumsikiliza anavyoongea kuhusu kutia nia kwake ilibidi nibadili Station zaidi alipokuja kugusia suala la Muungano "alisema ole wake mtu atakaekuja kujaribu kuugusa muungano''

Nikawa najiuliza maswali ivi hati miliki ya Muungano wa Tanzania ipo bara? kwanini anasema ivi kabla hajashika hayo madaraka?

Pia alitahadharisha kwa kukikusudia chama cha wananchi CUF kule Zanzibar na matokeo ya Uchaguzi ''Kwamba CUF kila uchaguzi wanaibiwa kura alisema akiwa yeye Rais atakomesha CUF kuja na madai hayo'' Nikawa najiuliza ni kwanini Membe anaumizwa na siasa za Zanzibar na yanayotokea Zanzibar na aahidi kuforce kulazimisha watu wasiseme neon hata kama kuna dhulma?

Lakini Jengine baya zaidi alisema akimaanisha Chama cha CUF Zanzibar, alisema utawala wake atakomesha uongozi wa kifalme akimaanisha eti Maalim Seif tokea 1992 kwa upinzani anagombania yeye urais na hakuna mbadala. Nikawa najiuliza ivi Membe kumbe kwa kiasi kikubwa kumbe anamchukia maalim seif?

Ivi Membe hajuwi kwamba kuendelea kwa kugombania maalim seif kwa CUF ni ridhaa ya wana CUF wa Zanzibar? Lakin hata kama yeye hili linamuuma huwa anaumizwa na nini kuhusu Zanzibar?

Nimemtafakari sana nikagundua lazima atakuja na ajenda za siri kuhusu Zanzibar. nimelinganisha na saivi wakati ni Waziri wa mambo ya nje mambo mengi ambayo ni maslahi kwa Zanzibar huwa anaweka mkono hataki ku-sign jambo lolote ambalo litaleta maslahi kwa Zanzibar.

Mfano mzuri tena juzi alipokuja Patrice Culvert Zanzibar alitaka kijengwe chuo Zanzibar cha kufundishia mpira kwa kids ambao baadae waweze kulichezea Taifa amekataa ku-sign amesema ata-sign lakini chuo kijengwe Tanzania Bara badala sharti hilo Culvert amekataa alijibu kwamba yeye interest yake kijengwe Zanzibar Membe na jopo lao walikataa (hii niliipata kwa mtu wangu wa karibu ambaye anafanya kazi Tours alikuwa akimtembeza huyu Patrice Cluvert sehemu mbalimbali za utalii Zanzibar.

Wagombea nafasi wengine wengi nimewasikiliza kwa makini sana lakini sikuona chembe ya dalili kama za huyu Membe ni afadhali ya JK mara 1000 zaidi.

Kwenu Wadau.
 
"Katika karne hii ya sayansi na teknolojia baba mtu mzima bado anaamini anaweza kuupata urais wa nchi kwa nguvu za giza kwa kuitumia mizimu? Ukisikia kuchanganyikiwa ndio huku! Kinachofuata ni kuokota makopo, ukingoja safari yako ya mwisho".... Mwalimu Mkuu.... Pascally Mayega... Tanzania Daima.... 10.6.2015...
 
Hahahahaha kamkana mpk ndugu yake chezea urais wewe
 
hahaaaaaaaaa...kawa chizi...!!! Chezea Lowassa...!!!😂😂😂😂
 
Ni Jumapili Tu Iliyopita Ulionyesha Udhaifu Mkubwa Huu Ambao Nauweka Hapa Hadharani

Kuonyesha PAPARA Anapozungumza.


Kujawa Na SHAUKU.


Ameshindwa Kuhimili MIHEMUKO Ya Kisiasa.


Amekuwa Na Kauli Za KIBABE Na VITISHO Haswa Kwa Wanaume Dhidi Ya Kuwatesa Wake Zao.


Anayajua Ya NJE ( ULAYA ) 85% Na 15% Ya Tanzania.


Amejawa Na VISASI Na Hana Tofauti Na Arch Rival Wake Lowassa Na Visasi Vyao Vinaonekana Wazi Usoni.


Ana Matatizo au Udhaifu Mkubwa Wa ARTICULATION Kila Azungumzapo.


Mjivuni.


Hana Convincing Skills.


Ni Mtu Wa MLIPUKO ( Body Language Yake Ina Majibu Rahisi Kwetu Kuliko Ayasemayo ).


Alipashwa Kufanya COUNTERING Kwa Lowassa Ambaye Ndiye Mshindani Wake Mkuu Baada Ya Kumtangulia Wiki Moja Iliyopita Lakini AKAFELI ( Namaanisha HAKUJIANDAA Vizuri Kwa Event Yake Ya Lindi ).


Team Yake ( Team MEMBE ) Imemwangusha Kwa 85% Kivipi? Kuna Mahala Alionyesha Kuwa Kumbe Hata Yeye Ana Matatizo Ya KIAFYA Kama Ambavyo Wanamsingizia Mpinzani Wake Lowassa Kwa KUKOHOA Mara 3 Ktk Intervals Tofauti Mithili Ya Mgonjwa Wa Kifua Kikuu Na Nilidhani Watu Wake Wa Protocal Hili Wangeliona Mapema Kwa Kucheza Na Psychology Ya Watu Na Kuliwahi Ili Kufunika Huu Udhaifu Lakini Walichelewa Na Kuonyesha Jinsi Gani Walivyo MAPOPOMA WALIOTUKUKA Hivyo Kupelekea Kuwapa MTAJI Mwingine Maadui Zake Kisiasa Na Kitendo au Hali Ile Ilimuharibia Sana.


Kuna Nonsenses Nyingi Alizizungumza Ambazo Zilikuwa Ni Very Irrelevant Kulingana Na Tukio Zima Kwa Mfano Kuna Wakati Alisema Kuwa Atahakikisha Kuwa Akiwa Rais Basi WANARIADHA Watakuwa Na HATI MILIKI ( Wakati Alitakiwa Kusema au Kumaanisha WASANII Ndiyo Atawapigania Hati Miliki Zao ), Pili Kitendo Cha Kumwita Mzee Wa KIMWERA Kutambika Mbele Ya Ile Kadamnasi Kulionyesha Udhaifu Mkubwa Na Kutudhihirishia Kuwa Ni MSHIRIKINA Na Anaabudu Ndumba Na Kitendo Cha Kusema Kuwa Ameongea Na Nyerere Kaburini Na Akamjibu Ni Vitu Vya Kipuuzi Kusema Mbele Ya Intellectuals.


Alizungumza Kwa Dakika 51:12 Japo Kwa Content Yake Nzima Dakika 45 Tu Zingemfaa Na Angeeleweka Vizuri Tu.


Kutumia Jina Na Ueledi Wake Ktk Taasisi Nyeti Ya SSIT Hakukuwa Na Maana Wala Umuhimu Na Sana Sana Ameidhalilisha Taasisi Na Kufanya Sasa Watu Pengine Waanze Kuwa Na Jicho La HUSUDA ( Hasi ) Juu Ya Idara Hiyo Nyeti Ktk Nchi Hii Na Kitendo Chake Hicho Kinaweza au Pengine Kitasababisha Kuigawa Idara Kitu Ambacho Ni Hatari Mno Kwa Maslahi Ya Taifa Letu Na Nch Yetu.



Sasa Nikujua Kuwa Team Yake ( Kamati ) Labda Itakuwa Ilifanya Assesment Ya Tukio Zima ILI Kumshauri Aweze Kufanya Vizuri Ktk Mchakato Wake Jana Tena Kaja Na SARAKASI Nyingine Ambayo Ndiyo IMENISAIDIA Sasa Kuujua Vizuri Udhaifu Wake Mara Baada Ya Kusema Kuwa " Kama Jina Lake Likikatwa Basi Atamuunga Mkono Mgombea Mwingine Mzee Mwandosya ) Kwa Macho Na Akili Za MAPOPOMA WALIOTUKUKA Anaweza Akaeleweka ILA Kwa Wenye AKILI Zao Na UPEO Wao Amejichoresha Na Kujiangusha.

Team Membe Humu Wamekuwa Wakimponda Lowassa ILA Bila UNAFIKI Wala SANIFU Huku Nikijua Kuwa Hata Lowassa Mwenyewe Hawezi Kuwa Rais Wetu Lakini Kama Pangekuwa Na Nafasi Ya Best Loser au Wild Card Na Ningewekewa Nichague Nani Aingie Kati Ya Mzee Lowassa au Mzee Membe Ili Kupambana Na Akina Magufuli, Muhongo, Jaji Augustino Ramadhan Na Makongoro Nyerere Ambao Nina Uhakika 100% Kuwa Watakuwepo ktk Top 5 Mimi Ningemchagua Mzee Edward Ngoyai Lowassa Aingie Kwa Nafasi Hiyo Ya Best Loser au Wild Card Na Siyo Mzee Bernard Camillius Membe. Lowassa Anamzidi Membe Kwa Vitu Vingi Sana Na Haswa Ktk Upande Mzima Wa Strategies.

Namalizia Kwa Kusema ( I Stand To Be Corrected ) Kuwa Ewe Baba Cecilia, Richard Na Dennis ( Mzee Membe ) Huna SIFA Na HUTOSHI Kuwa CCM 2015-2020 Presidential Flag Bearer Period.
 
Mkuu washauri stategists wake. Naamini wanapita humu.
 
CCM CCM inakufa CCM, inakufa kifo kibaya, kifo cha ganzi, ganzi linaanzia miguuni, hatimae mikono inaukana mwili, mwili hatimae utaikana roho.....heri kufa kifo chema
 
Kosa kubwa na lisilosameheka kwa Membe ni kuwasema vibaya wapinzani.
 
haiwezekan eti membe anasema akiwa rais nyerere atafurahi.......... hatutaki rais wa kufurahisha wafu sisi na wala wafu hawapigi kula kama unataka kuwafurahisha wafuate hukohuko...... mwalimu amefanya mengi makubwa hadi tukamaliza miaka hamsini ya uhuru ,sasa tunamtaka rais wa kutusaidia kujenga taifa kwa miaka mingine hamsin.............membe acha unafiki mngekuwa mnampenda mwalimu msingezika azimio lake la arusha na kuleta la zanzibar enz za zidumu fikra za mwalimu imepitwa na wakati.....kutuletea mawazo ya mwalimu 2015 ni kutudhalilisha we are in capitalist world and we are not static.......... hoja za huyu alikataliwa na mwalimu kwa hiyo hafai ,siyo hoja acha watanzania wa 2015 waamue wao wenyewe..................membe ametudhalilishaaaa
 
  • Thanks
Reactions: PPM
Wakuu hivi team imekosa kabsa washauri



TEAM MEMBE! TEAM MEMBE!

Naomba ieleweke kuwa ni vigumu kuwa Rais wa nchi hii bila kutumia mizimu ya baba wa Taifa Hayati J. K. Nyerere.

Mwl nyerere alikaa Ikulu kwa zaidi ya miaka ishirini mizimu yake ikikubali hakuna wa kukuzuia kuingia Ikulu na ndiyo maana mgombea wetu aliweka wazi kabisa mahusiano yake na mizimu ya mwalimu.

Narudia kusema mizimu ya mwalimu ni lazima itupeleke Ikulu na wala hatutanii na kamwe hatutounga mkono mgombea yeyote kama tulivyosema MBEYA. Alichokisema mgombea wetu Mbeya kumuunga mkono prof Mwandosya kama jina lake litakatwe ilikuwa ni mbinu ya kupata wadhamini eneo husika

Mizimu haijawahi kushindwa na hasa mizimu yenyewe ya Baba wa Taifa.

Membe akiwa Rais kila mwisho wa mwezi tutakuwa tunaenda kutambika musoma kama shukrani kwa mizimu yetu

Lazima tuelewe kuwa Rais anayeongoza kwa kutumia mizimu atakuwa na uwezo mkubwa wa ki maamuzi na ki utendaji
SISI KWETU MIZIMU KWANZA KWA MAENDELEO YA NCHI YETU
 
Back
Top Bottom