Kutoweka uzalendo kwa nchi: CCM haiwezi kuepuka lawama

Kutoweka uzalendo kwa nchi: CCM haiwezi kuepuka lawama

Kwa Tanzania kuna uhusiano mkubwa sana kati ya Uzalendo, Ujinga na Umasikini.
 
Uzalendo ni Dini kama zilivyo imani nyengine_na nisumu kwa wapumbavu
 
Nimeona niandike kipande kidogo kinachohusu uzalendo.

Mara nyingi unaweza kutana na mtu akisema uwe mzalendo, wengine hata wakidiriki kutumia neno hili kinyume kabisa.

Ipo hivi, uzalendo kwa kingereza ni "patriotism" mzalendo ni patriotic, uzalendo maana ya kiulimwengu (universal meaning) ni mapenzi ya mtu kwa taifa lake ,pamoja na jamii inayomzunguka yaani

*Patriotism is the feeling and expression of love for one’s home country, along with a feeling of unity with those who share those feelings*

Mapenzi kwa nchi au Taifa lako hutofautiani nchi na nchi ,Lawrence W.Reed katika andiko lake la *True meaning of patriotism* ,anasema mapenzi kwa nchi yako sio kupenda milima,mito,maziwa,misitu,hali ya hewa sababu hata nchi zingine zina milima na mabahari,mito na misitu.

Anasema Mapenzi ya nchi yako sio kutetea serikali sababu hata nchi zingine zina serikali ,na pia serikali huingia na kutoka, ni sawa leo uzalendo wako ni kusifu na kuamini katika serikali ya Bush ,siku Bush akitoka madarakani? Je na uzalendo wako utakuwa mwisho?

Uzalendo ni mapenzi kwa nchi au Taifa lako,huwezi kutokea kupenda kitu bila sifa (Sababu),merits zinazokufanya uwe (attached to ).

Ni sawa mapenzi katika familia yako (Marital fedelity),una mpenda mke wako sababu ya tabia zake,na historia yenu mlipotokea hivyo utaendelea kupambana muwe pamoja bila kuvurugwa na yeyote.

Mapenzi ya nchi yako ni tofauti na mapenzi ya mtu mwingine katika taifa lake sababu ya tofauti ya historia ya taifa hilo na watu wake, tamaduni,mila ,misingi na desturi mliyopokea kutoka kwa waasisi wa taifa lenu (national fathers).

Hivyo basi uzalendo ni kupenda nchi yako ,sio kwa sababu ya milima na bahari ,ni kwa sababu ya misingi hiyo,historia ya watu wa taifa hilo na nchi yenyewe na tamaduni yake na watu wake.Sio kuishia hapo tuu, kazi nyingi ni kulinda misingi hiyo ,storia hiyo ,watu hao na maslahi yao dhidi ya mtu yeyote anaye hatarisha kuivuruga awe wa nje au wa ndani.

Lawrence Reed anasema ,marekani ukitaja tuu misingi iliyopo katika azimio la Uhuru wa marekani (American declaration of Independence) ndio kitovu cha uzalendo wa watu wa marekani.Mule kuna storia ya taifa lao,watu wao,na misingi ya waasisi wao (Civic virtues)ambayo mingi imeingizwa katika katiba ambayo hulindwa kwa namna yeyote.

Tanzania sisi tuna misingi (Values na civic virtues) na tamaduni iliyoaminiwa na tuliyoachiwa na waasisi wetu (Nyerere na viongozi wengine).

Kama amani,umoja,usawa na haki, upendo na msingi mingine aliyotuachia ipo katika katiba ya TANU au Azimio la Arusha , Binadamu wote ni sawa,uhuru wa mawazo, kufanya kazi kwa bidii,heshima kwa kila mtu,usawa, Demokrasia , misingi mingine aliyoiamini waliyo iamini iliingia katika katiba , misingi hii ndiyo imekuwa ikitumiwa na watangulizi na viongozi wengine hadi hivi sasa katika kudumisha taifa letu na maendeleo yetu.

Hivyo uzalendo ni kupenda nchi kwa kuhakikisha misingi hii inadumishwa ,watu wake wanaishi vyema pia hata kujitolea kwa niaba ya watu ili waishi vyema kuwasaidia au kuwasemea na kuwasimamia.Mzalendo ni anayehakikisha misingi yote tuliyoachiwa ina dumishwa na kuheshimiwa ,stori ya uhuru wetu na huru tulio achiwa unaimarika bila kutikiswa na watu wa aina yeyote wa nje au wa ndani .

Ndio maana kuna uzalendo wa kikatiba unaitwa *Constitutional patriotism* uzalendo wa kuheshimu na kuilinda katiba, *Jurgen Habermas* ameelezea vyema sana dhana hii,hivyo yeyote atakaye heshimu na kuilinda katiba na sheria zingine huyo pia ni mzalendo.

Watu watakaotimiza misingi hii kwa kikamilifu hao watakuwa wazalendo wa taifa lao haswa na watakao timiza majukumu yao ya kutetea na kusifia serikali na mamlaka hao watakuwa wafuasi haswa.


Shukrani sana.

Abdul Nondo

abdulnondo10@gmail.com
 
Mimi tangu zamani sijawahi kuwa na uzalendo kwa nchi hii iliyojaa dhuluma na unafiki wa kupindukia. Kwa kuwa naamini tupo wengi, ndio maana nimefungua uzi huu kwa ajili ya wale raia ambao hatuna uzalendo hata kidogo ndani ya nchi hii ya kusadikika na ya kipumbavu.

Hivi unakuwaje mzalendo katika nchi ambayo baadhi ya watu wanakula na kusaza ilhali wengine wakifa kwa njaa? Utakuwaje mzalendo ktk nchi ambayo watu wanauawa ovyo na "watu wasiojulikana" na serikali wanatoa majibu ya kujisaidia haja kubwa?

Naawalika wenzangu wasiokuwa wazalendo tukutane kwenye kijiwe hiki ambapo tutakuwa tunapeana mbinu za hapa na pale za kutorudi nyuma ktk jambo hili.

Naahidi kutokuwa mzalendo hadi naingia kaburini kwa kuwa siwezi kukubali kuungana na wapumbavu wachache wanaofaidi rasilimali za taifa kwa 101% wakati wengine wakiishi maisha ya kijela.

Naungana na mzalendo mwenzangu, Cyprian Musiba, kutetea maslahi mapana ya wanyonge dhidi ya maslahi finyu ya kikundi kidogo cha wachumiatumbo wanaoogelea kwenye neema wakati mamilioni ya watanzania wakiteseka. Kamwe tusikubali hawa kupe mamboleo waiue nchi huku tukiwa tumekaa kimya. Tupambane ima faima mpaka kieleweke.
 
Matabaka yapo nchi zote duniani na watu kuuwawa kupo karibia nchi zote.

Infact uki-peep your nose in other people's affairs unakula za uso.

Si USA si Russia si China si Kenya
 
Lazima ujue dhana ya uzalendo kwanza ni nn? yawezekana ww ni mzalendo namba moja kuliko hao waliopo madarakani hasa kwa hoja zako hapo juu, propaganda za wanasiasa na hasa wa awamu hii wamekuwa wapotoshaji wakubwa ktk kuudadavua huu msamiati uzalendo
 
1. Hujawahi kuwa mzalendo
2. Mwisho una sema unaungana na mzalendo mwanzako
tubebe lipi sisi tusiokuwa na upande
Inaonesha jinsi WaTz tusivyojitambua. Daima tunaota!
 
Ata ukimpa mtu au mama yako hela ya matumizi ndio uzalendo ukitii sheria bila shuruti ndio uzalendo na wewe ni mzalendo
 
Mimi nina uzalendo na nchi yangu isipokua tu huyu mdudu anayeitwa si si emu! Angetokea mtu wa kumuua huyu kirusi, hakika huyo angebakia milele kama shujaa wa Taifa na watanzania tungetembea vifua mbele.
 
Back
Top Bottom