Kutumia Msalaba kama ishara ya ukristo na kanisa si sahihi

Kutumia Msalaba kama ishara ya ukristo na kanisa si sahihi

Korinto 1:18-31

Kwa sababu neno la msalaba kwao wanaopotea ni upuzi, bali kwetu sisi tunaookolewa ni nguvu ya Mungu. Kwa kuwa imeandikwa, Nitaiharibu hekima yao wenye hekima, Na akili zao wenye akili nitazikataa.
 
Hakuna utamaduni wa kiarabu unaoingiliana na uislam
Waarabu wanatumia lugha gani?? Quran inatumia lugha gani?? Wewe ukiruhusu akili yako ifanye kazi,Mungu anaongea kiarabu??

Lugha ni sehemu ya utamaduni fulani.

Waarabu walikuwa wanavaa vipi?? Waislamu vazi lao kuu ni lipi??

Mavazi ni sehemu ya utamaduni ya jamii fulani.

Ndoa za waarabu zilikuwa vipi?? Uislamu ulikuja kuziondoa mitala??

Ndoa ni sehemu ya utamaduni ya jamii fulani.

Dini ni sehemu ya utamduni

Ili ujue haya ni lazima uruhusu akili yako ifanye kazi vizuri coz usipotumia akili vizuri ndiyo bado utashikilia kuwa Quran imeshuka, imekamilika,sayansi zote zimo ndani yake kumbe zote ni propaganda.
 
Waarabu wanatumia lugha gani?? Quran inatumia lugha gani?? Wewe ukiruhusu akili yako ifanye kazi,Mungu anaongea kiarabu??
Mungu anaongea lugha gani?..ulitaka lugha gani itumike?..au telepathy?
Lugha ni sehemu ya utamaduni fulani.

Waarabu walikuwa wanavaa vipi?? Waislamu vazi lao kuu ni lipi??
Uislam umeagiza namna ya kuvaa kwa wanawake, maana yake waarabu hawakuwa wakivaa hivyo kabla ya uislam
Mavazi ni sehemu ya utamaduni ya jamii fulani.

Ndoa za waarabu zilikuwa vipi?? Uislamu ulikuja kuziondoa mitala??
Mitala ilikuwepo kila mahali alipo binaadam, ikiwemo afrika, Quran imeagiza ndoa ziwe vipi kuanzia posa,mahari, maisha ndani ya ndoa na talaka, waarabu hawakuwa wakifuata ndoa kama walivyoagizwa na Quran kabla ya ujio wa mtume
Ndoa ni sehemu ya utamaduni ya jamii fulani.

Dini ni sehemu ya utamduni
Kwa muktadha wa uislam dini ni mfumo wa maisha,hata ubepari ni dini,mfumo wa maisha kea maana ya namna ya maingiliano yote ya kimaisha,
Ili ujue haya ni lazima uruhusu akili yako ifanye kazi vizuri coz usipotumia akili vizuri ndiyo bado utashikilia kuwa Quran imeshuka, imekamilika,sayansi zote zimo ndani yake kumbe zote ni propaganda.
Quran imekamilika ndiyo na ilishushwa,hutumii tu vizuri akili yako kuelewa imeshuka vipi,unadhani imeshuka kama ndege au mvua,usiitegemee sana akili yako,ina ukomo, Quran siyo kitabu cha sayansi bali miongozo kwa binaadam kumjua muumba wake na kuishi kama alivyoagiza
 
Korinto 1:18-31

Kwa sababu neno la msalaba kwao wanaopotea ni upuzi, bali kwetu sisi tunaookolewa ni nguvu ya Mungu. Kwa kuwa imeandikwa, Nitaiharibu hekima yao wenye hekima, Na akili zao wenye akili nitazikataa.
Msalaba anaousema Paulo hapo anamaanisha lile gogo au?????
 
Msalaba ni zana ya kunyongea wahalifu ya utawala wa Warumi (weapon of execution) kama ilivyo kamba ya kunyogea, kiti cha umeme, sindano ya sumu au jambia la kuchinjia. Kama Yesu angechinjwa kwa jambia je tungekuwa tunaweka alama ya ya upanga/jambia juu ya jengo la kanisa au kuivaa kifuani???
Kila mtu ana uhuru wa kutumia anachotaka kama alama ya dini yake.

Wakikubali wenyewe poa tu.

Kama hutaki unaweza kuanzisha dini yako ukatumia alama yako.
 
Kila mtu ana uhuru wa kutumia anachotaka kama alama ya dini yake.

Wakikubali wenyewe poa tu.

Kama hutaki unaweza kuanzisha dini yako ukatumia alama yako.
Sawa mkuu. Nilitaka tu hoja yangu iamshe mawazo ya wakristo. Thanks for your contribution.
 
Mungu anaongea lugha gani?
Mimi sifahamu Mungu anaongea lugha gani.Pia naamini Mungu haongei kiarabu.Wewe unaweza kuniambia Mungu anaongea lugha gani??


Uislam umeagiza namna ya kuvaa kwa wanawake, maana yake waarabu hawakuwa wakivaa hivyo kabla ya uislam
Nimekuambia vazi kuu la waarabu ni vazi gani,waislamu vazi kuu ni vazi gani?? Wewe umeelezea jinsi ya kuvaa hilo vazi.
Mitala ilikuwepo kila mahali alipo binaadam, ikiwemo afrika, Quran imeagiza ndoa ziwe vipi
Ndoa za mitala ilikuwa sehemu ya utamaduni wa kiarabu, uislamu haukulikataza.Wewe umeelezea taratibu za ndoa.

Unaweza kuelezea taratibu za ndoa za utamaduni wa kiarabu??
Kwa muktadha wa uislam dini ni mfumo wa maisha
Dini haiwezi kuwa mfumo wa maisha, dini ni sehemu ya utamaduni.

Wewe kwa kutumia akili yako, kipi ni kikubwa kati ya utamaduni na dini??

Quran imeuweka utamaduni wa kiarabu kwa njia ya maandishi.

Humo ndani kuna mambo mengi.

Nb: Tamaduni huwa zinaingiliana na kumezwa pia.
Quran imekamilika ndiyo na ilishushwa
Acha kumeza propaganda,Quran haijashuswa na haijakamilika.

Maendeleo makubwa ya sayansi na teknolojia yaliyoletwa hapa duniani unahisi yaliletwa kwa kusoma Quran??

Nafikiri umetumia jazba na hisia zaidi kuliko uhalisia.Nimekuambia tumia akili yako vizuri.Toka nje ya boksi.

Huwezi kuutenganisha utamaduni wa kiarabu na uislamu kwa namna moja ama nyingine.
 
Mimi sifahamu Mungu anaongea lugha gani.Pia naamini Mungu haongei kiarabu.Wewe unaweza kuniambia Mungu anaongea lugha gani??
Unasahau hata ulichoandika mwanzo,ulidhihaki waislam kutumia kiarabu,ukauliza huyo Mungu anaongea kiarabu tu,nikakuuliza Mungu anaongea lugha gani,so unapaswa kujibu, kusema hujui Mungu anaongea lugha gani siyo jibu
Nimekuambia vazi kuu la waarabu ni vazi gani,waislamu vazi kuu ni vazi gani?? Wewe umeelezea jinsi ya kuvaa hilo vazi
Waislam hawana vazi kuu, isipokua hijabu kwa wanawake,na hijab ni amri ya Quran, waarabu hawakuvaa hijab kabla ya uislam,kama unadhani kanzu ni vazi kuu la waarabu basi kumbuka yesu na warumi walivaa kabla muhammad hajazaliwa
.

Ndoa za mitala ilikuwa sehemu ya utamaduni wa kiarabu, uislamu haukulikataza.Wewe umeelezea taratibu za ndoa.
Mitala mfalme selemani alikua nayo kule israel,ulaya walikua nayo, africa kwa wingi,mitala siyo utamaduni wa kiarabu
Unaweza kuelezea taratibu za ndoa za utamaduni wa kiarabu??
Hili inabidi ueleze wewe unayezijua taratibu za ndoa za kiarabu kabla ya uislam,maana umedai uislam umeiga huko
Dini haiwezi kuwa mfumo wa maisha, dini ni sehemu ya utamaduni.

Wewe kwa kutumia akili yako, kipi ni kikubwa kati ya utamaduni na dini??
Uelewa wako wa dini ndiyo upo hivyo,lakini uislam unasimamia/elekeza mambo yote ya maisha kuanzia ndoa,mavazi,kula, biashara,mahusiano baina ya jamii,utasemaje siyo mfumo wa maisha,mfumo wa maisha ni nini?
Quran imeuweka utamaduni wa kiarabu kwa njia ya maandishi.

Humo ndani kuna mambo mengi.

Nb: Tamaduni huwa zinaingiliana na kumezwa pia.
Unarudiarudia vitu visivyo na msingi,sisi wenye Quran tunaijua yote na iliyoelekeza,hakuna utamaduni wa kiarabu, maelekezo hayo wakipewa waarabu awali kabla ya walimwengu, waarabu wakiambiwa waache tamaduni zao wafuate Quran
Acha kumeza propaganda,Quran haijashuswa na haijakamilika.

Maendeleo makubwa ya sayansi na teknolojia yaliyoletwa hapa duniani unahisi yaliletwa kwa kusoma Quran?
Quran kushushwa na kukamilika kunahusiana nini na binaadam kuunda roketi,simu na magari!?..hivi unaelewa hata Quran ni kitu gani!?
?

Nafikiri umetumia jazba na hisia zaidi kuliko uhalisia.Nimekuambia tumia akili yako vizuri.Toka nje ya boksi.

Huwezi kuutenganisha utamaduni wa kiarabu na uislamu kwa namna moja ama nyingine.
Nadhani umeamua kukaza fuvu,hutaki kuelewa, waarabu wa makkah walimpiga vita mtume na kumfukuza kwa kuharibu tamaduni zao
 
Msalaba ni zana ya kunyongea wahalifu ya utawala wa Warumi (weapon of execution) kama ilivyo kamba ya kunyogea, kiti cha umeme, sindano ya sumu au jambia la kuchinjia. Kama Yesu angechinjwa kwa jambia je tungekuwa tunaweka alama ya ya upanga/jambia juu ya jengo la kanisa au kuivaa kifuani???
Sio sahihi wewe kama nani? Wenye ukristu wao wameona msalaba unafaa. Anzisha dini yako ambayo hautatumia msalama, and trust me hutakosa wateja
 
Wameamua wenyewe kuchagua msalaba kama share ya ukristo...!!! Ni swala kuchagua na kukubaliana tu...! Sioni kama ni tatizo
 
Sio sahihi wewe kama nani? Wenye ukristu wao wameona msalaba unafaa. Anzisha dini yako ambayo hautatumia msalama, and trust me hutakosa wateja
The earth is full of natural resources sihitaji kuwa tapeli kwa jina la Mungu. Sasa wewe ukimuona ndugu yako anapotea usimuelekeze njia sahihi si biblia na mafundisho hayo hayo yamesema damu yake itadaiwa mikononi mwako? Wewe unasema niachane nae nianzishe dini yangu!!! Ufahamu wako una kasoro.
 
The earth is full of natural resources sihitaji kuwa tapeli kwa jina la Mungu. Sasa wewe ukimuona ndugu yako anapotea usimuelekeze njia sahihi si biblia na mafundisho hayo hayo yamesema damu yake itadaiwa mikononi mwako? Wewe unasema niachane nae nianzishe dini yangu!!! Ufahamu wako una kasoro.
Umejuaje kama anapotea na wewe huko ulipo haupotei? Unaweza niambia kitu gani kinakufanya uamini upo ulipo upo sehemu sahihi?
 
lakini uislam unasimamia/elekeza mambo yote ya maisha kuanzia ndoa,mavazi,kula, biashara,mahusiano baina ya jamii,
utamaduni

mila, asili, jadi na desturi za kundi la jamii fulani


dini

1.
imani inayohusiana na mambo ya kiroho kwamba kuna muumba ambaye aliuumba ulimwengu huu na kwamba ndiye mtawala wa kila kilichomo

2.mfumo fulani wa imani hii na njia ya kuabudu, kusali na kuheshimu/ kutii huyo muumba k.v. Ukristo, Uislamu, Uyahudi, Uhindu au Ubudha


Bado unazidi kukaza fuvu?? Penda kujifunza na kujielimisha coz unaonekana unapenda kubishana (sifa ya mtu mjinga)na siyo kuelekezana (sifa ya mtu mwerevu)
 
The earth is full of natural resources sihitaji kuwa tapeli kwa jina la Mungu. Sasa wewe ukimuona ndugu yako anapotea usimuelekeze njia sahihi si biblia na mafundisho hayo hayo yamesema damu yake itadaiwa mikononi mwako? Wewe unasema niachane nae nianzishe dini yangu!!! Ufahamu wako una kasoro.
Kwamba hili bango lako ndo litafanya wabadilike? Upo serious kweli?
 
Msalaba ni zana ya kunyongea wahalifu ya utawala wa Warumi (weapon of execution) kama ilivyo kamba ya kunyogea, kiti cha umeme, sindano ya sumu au jambia la kuchinjia. Kama Yesu angechinjwa kwa jambia je tungekuwa tunaweka alama ya ya upanga/jambia juu ya jengo la kanisa au kuivaa kifuani???
Kwa uelewa wangu mdogo. Msalaba uko na pembe nne zote zikiwa zimebeba maana ndani yake.

Kuna uelekeo wa kichwa ukiwakilisha uhusiano wa mtu na Muumba wake,
Uelekeo wa miguu ukiwakilisha uhusiano wa mwanadamu na ardhi/unyama wake.
Uhusiano wa pande mbili za mikono ukiwakilisha mema na mabaya ambapo hata kwa mujibu wa biblia pale msalabani Yesu alisurubiwa katikati ya watu wawili na yule wa upande mmoja alimkubali na wa upande mwingine alimkashifu. Lakini yule aliyemkashifu Yesu hakumjibu kitu. Unafikiri ni kwanini hakumjibu ni kwa sababu kati ya mema na mabaya kuna mtu. Na alitambua katika mema kuna mabaya na katika mabaya kuna mema LAKINI hawa wote walichokikosa ni uzima na ndio aliouleta.

Inaweza kuwa ilikuwa ni tamaduni za warumi kutesa wahalifu kwa staili ile lakini haikuwa bahati mbaya kwa Yesu kuwekwa msalabani.
 
utamaduni

mila, asili, jadi na desturi za kundi la jamii fulani


dini

1.
imani inayohusiana na mambo ya kiroho kwamba kuna muumba ambaye aliuumba ulimwengu huu na kwamba ndiye mtawala wa kila kilichomo

2.mfumo fulani wa imani hii na njia ya kuabudu, kusali na kuheshimu/ kutii huyo muumba k.v. Ukristo, Uislamu, Uyahudi, Uhindu au Ubudha


Bado unazidi kukaza fuvu?? Penda kujifunza na kujielimisha coz unaonekana unapenda kubishana (sifa ya mtu mjinga)na siyo kuelekezana (sifa ya mtu mwerevu)
Dini ni neno la kiarabu ambalo limekopwa na kiswahili,hapo wanetafsiri toka kiingereza 'religion',dini kwa muktadha wa uislam ni mfumo wa maisha, ndiyo maana uislam una maelekezo kwa kila nyanja za maisha,kuanzia jinsi ya kuswali mpaka kuongea na watu,kula,kutembea nk
 
Dini ni neno la kiarabu
Nakubaliana na wewe kwa asilimia 100%
dini kwa muktadha wa uislam ni mfumo wa maisha
Hapa unachanganya coz uislamu unajitegemea na dini inajitegemea.

Bado unaamini dini ni mfumo au ni sehemu ya utamaduni??

Bado unaamini dini ni kubwa kuliko utamaduni??
uislam una maelekezo kwa kila nyanja za maisha,kuanzia jinsi ya kuswali mpaka kuongea na watu,kula,kutembea nk
Hapa kwa kutumia akili yako vizuri, huoni utamaduni??

culture

the way of life, especially the general customs and beliefs, of a particular group of people at a particular time:


The five aspects of culture are values and beliefs, language, symbols, rituals, and norms. These aspects shape all other customs.


norm

an accepted
standard or a way of behaving or doing things that most people agree with:

 
Nakubaliana na wewe kwa asilimia 100%

Hapa unachanganya coz uislamu unajitegemea na dini inajitegemea.

Bado unaamini dini ni mfumo au ni sehemu ya utamaduni??

Bado unaamini dini ni kubwa kuliko utamaduni??

Hapa kwa kutumia akili yako vizuri, huoni utamaduni??
Tatizo hutaki kuelewa,ikiwa uislam unaelekeza jinsi ya kuishi na kufanya ibada,huo ni mfumo wa maisha,kama mfumo wa maisha si utamaduni,hilo siyo tatizo langu,kama mfumo wa maisha ni utamaduni basi uislam siyo utamaduni wa kiarabu sababu hayo maelekezo ya kwenye Quran walielekezwa kwanza waarabu ambao walikua na utamaduni wao kabla ya muhammad kuhubiri uislam
culture

the way of life, especially the general customs and beliefs, of a particular group of people at a particular time:


The five aspects of culture are values and beliefs, language, symbols, rituals, and norms. These aspects shape all other customs.


norm

an accepted
standard or a way of behaving or doing things that most people agree with:

Hii elimu yenu mnayofundishwa shule definitions za lugha, kwamba wanyama hawana lugha kisa hawana sijui konsonanti,irabu,nomino sijui vitu gani,inawapotosha
 
Back
Top Bottom