Kuuziwa chakula bei juu kwa Wasafiri ni kero kubwa

Kuuziwa chakula bei juu kwa Wasafiri ni kero kubwa

Zile hoteli mara nyingi zipo Pori , customer ni hao hao wasafiri , na wako limited , operation cost ni kubwa , ili kucover situation inabd bei iwe kubwa mkuu , mana maharage ya kilala, yanachacha wanamwaga , imagine umeyauza Kwa bukubuku
Na kwa nn ziwe pori??
 
Nunua mkate wako wa Buku jero Na soda ya take away buku Anza safari yako Njiani shindia mkate tu utanishukuru baadae
Enzi hizo tukisafiri na mabasi tulikuwa tunabeba chakula kama kawaida. Leo hii kila kitu kimekuwa issue
 
Mimi nawashangaa wanao safiri halafu wanakula njiani mimi siwezi kula kula njiani lazima nitaapike

Hata maji sinywi kuepuka kubanwa na mkojo
 
Hili jambo nadhani ni very challenging kuliko tunavyoliona.

Kuna mdahalo ITV waliitisha kati ya TABOA, Madereva, Abiria, na chama cha watetezi wa abiria kuhusu gharama za vyakula njiani.

Changamoto zilikuwa kama ifuatavyo,

* Abiria wenyewe hawakuwa wanaafikiana,abiria wengine walikuwa wanataka hoteli za hadhi na wako tayari kulipia, na abiria wengine walikuwa wanapendekeza gari lisimame kwenye hoteli za hadhi ya chini. Swali likawa ni Je, basi lisimame mara mbili kukidhi matakwa ya abiria wote? Abiria nwengine hawakuridhia kwa kuona ni upotezaji wa muda.

*Madereva wao wakasema wanatafuta hoteli ambayo kimsingi ipo katikati ya safari, ambapo kiuhalisia ni interior sana na hoteli ni chache. Wakaja na hoja kwamba, huwezi kumtoa abiria katika route ya Dar- Babati alafu ukamshusha akale kibaha mjini kwenye mahoteli mengi kwa sababu ya bei.

*Madereva wakaja na hoja nyingine yenye mgogoro kuhusu CHOO. Wakasema serikali inataka abiria wakashushwe sehemu sahihi za kujisaidia, na mara nyingi hizo sehemu unakuta ni za kulipia na abiria hawataki kabisa gharama, kwa hiyo wanachofanya ni kutumia tu busara kutokana na mazingira ili wananchi wajisaidie majoring bila kuwatesa.
Hoja hizi zote ni mfu.
1. Kwani zamani kabla ya kujenga hizi hoteli za mbugani ilikuwaje? Ni kwamba magari yalikuwa yanasimama stendi za umma. Kwa mfano route ya Arusha to Dar, magari yalisimama Korogwe au Mombo.
2. Vyoo siyo tatizo kwa sababu magari yakisimama stendi za umma, kutakuwa na vyoo vya umma, na vyoo vya hotel. Abiria watakuwa na wigo mpana zaidi wa kuchagua.
3. Kuhusu ''hadhi'' ya hoteli nayo haina mashiko. Stendi za umma zamani zilikuwa na hoteli nzuri tu tena nyingi. Zilikuwa kwa sababu magari hayakuwa yanasimama tena. Wakirudisha utaratibu wa zamani watajitokeza wengi kujenga hoteli nzuri
 
sijawai ona hotel ya hadhi ya juu barabara zote za mkoa ambapo magari husimama kwa ajili ya vyakula ni upigaji tu wa madereva ili wapewe msosi wa bure
Hata mimi nimewaza kama wewe mkuu sijaona hizo hotel zenye hadhi wanazoongelea.
Kwa mfano ukisafiri kutoka Dar kwenda mikoa ya kaskazini kuna sehemu panaitwa Kabuku abiria hushuka na kununua vyakula kwenye vibanda na migahawa ya kienyeji lakini bado bei iko juu,sasa hapo ndio utaona kwamba sababu walizotoa hazina mashiko.
 
Ila acheni masihara kuna watu wanapenda kula safarini daah utafikiri viboko! unakuta ndo kwanza hata hamjatoka mtu kishapanga maandazi, bagia, vitumbua, sambusa. uko mbeleni ataongea sijui yogati, karanga, korosho,,,chaa! mm navyokuaga na stress ya safari vile hata sielewi mtu anapata wapi ujasiri wa kupakia kila anachokiona mbele yake.
 
Tumia akili.

Sio kila safari mtu anatokea nyumbani.

Safari zingine unatokea mkoani kikazi (mfano Musoma/Rukwa), unarudi zako Dar es Salaam.

Unatoka Musoma/Rukwa saa kumi usiku, unafika Dar 11 alfajiri au kesho yake kabisa mchana
Haya tumia akili ndogo tu kwa kununua biskuti na soda ya take awaye au maji

Wengine tunapenda hivyo vyakula vya buku 5
 
Hiyo biashara angefanya hata mwenye basi, wangeokoa muda na angepata faida,
Vyoo vimo kwenye yutong, friji ndani shida iko Wapi
 
Tumia akili.

Sio kila safari mtu anatokea nyumbani.

Safari zingine unatokea mkoani kikazi (mfano Musoma/Rukwa), unarudi zako Dar es Salaam.

Unatoka Musoma/Rukwa saa kumi usiku, unafika Dar 11 alfajiri au kesho yake kabisa
Hata Rukwa Kuna maduka yanauza chupa za chai na hotpot. Kama kweli umelala hotel au lodge ya heshima unaweza kuwaambia wakuwekee chai kwenye chupa yako na pilau au wali kwenye hotpot yako.
I am sorry for you Kama unalala gesti za buku jero ambazo Ni special for short time na hawana jiko.
Think in three dimensions young lady.
 
Shida ya wabongo tunapenda sana kula safarini, safari fupi tu ya Dar -Moshi/Dodoma/Iringa mtu anataka ale nyama choma kuku/mbuzi.! Wakati unaweza kukausha tu ukafika kwako ukapika ugali maharage ukashiba bila gharama
Eti Dar to Tanga gari inasimama njiani kula, tuchimbe dawa tusepe tu
 
Ubebe kutoka wapi..

Tumia akili.

Sio kila safari mtu anatokea nyumbani.

Safari zingine unatokea mkoani kikazi (mfano Musoma/Rukwa), unarudi zako Dar es Salaam.

Unatoka Musoma/Rukwa saa kumi usiku, unafika Dar 11 alfajiri au kesho yake kabisa
Basi fungua mgahawa wako njiani

Ova
 
Mtandikiwe tu pia mikeka hadharani mswali kuwaringishia watu nyinyi ni watu wa dini
Nchi nyingi za africa ukisafiri,vyakula vya njiani huwa ni ghali
Wengine tukisafiri dar to bukoba njiani ni juice na karanga, biskuti, korosho
Sasa unakuta mwingine anataka safiri
Utafikiri anaenda honeymoon

Ova
 
Mtoa mada acha kulalamika do something.
Nunua chupa ya chai na hotpot saizi ndogo. Unaposafiri Safari ndefu say Dar/Mza. Weka chai kwa flaski, tupia wali wa Jana mu hotpot, wengine wakienda kulanguliwa hoteling, wewe kula wali wako na chai.
Nakumbuka enzi za OTC /DMT mama alikua anabeba vyakula Kama kuku wa kukaanga na chai mu flaski
Wabongo sahvi kutwa kulialia tu
Mkuu...
We ukiona bidhaa fulani gharama achana nayo

Ova
 
Hili janga ni kama limerejea tena kwa speed ya kasi mnooo fikiria unapokuwa safarini sahani ya wali maharage unanunu kwa 4000, wali nyama. 5000, kuku robo ni 10,000, Chaji ya rangi 1000.

Kuwa msafiri sio kuwa kosa la kulanguliwa vitu bei juu au ndio kusema na wao wameathiriwa na vita vya Ukraine?
Hakuna mamlaka ya udhibiti hapa.
 
Kufunga siku moja bila kula ufi

Ila mm pia Ni mlaji hvyo jitaid tu utenge 15 kwa safari ya dar Arusha

Otherwise kausha ukifika dar ufakamie za buku 2

Sent from my Infinix X650 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom