Kuuziwa chakula bei juu kwa Wasafiri ni kero kubwa

Kuuziwa chakula bei juu kwa Wasafiri ni kero kubwa

Nunua mkate wako wa Buku jero Na soda ya take away buku Anza safari yako Njiani shindia mkate tu utanishukuru baadae
Mkuu mkate sasa hivi ni elfu 3000 ile superloaf ndogo... Ile kubwa ni elfu 4.. But wazo lako ni mujarabu, mimi majuzi nilikuwa naenda Kigoma na AIFOLA BUS, nyumbani nikawaambia wanikaangie kuku kipande kimoja, viazi mviringo 4, mkate slesi 2, matunda na juice... Nimefika poa kabisa... Na kwenye Bus wakatupa maji na biscuit juuu..
 
sijawai ona hotel ya hadhi ya juu barabara zote za mkoa ambapo magari husimama kwa ajili ya vyakula ni upigaji tu wa madereva ili wapewe msosi wa bure
Unaijua Cate hotel pale Kingoluwira Morogoro?
 
Kabisa.
Unakuta mtu ilimradi tu yupo safarini basi gari likianza tu anaanza kutafuna vyakula, muda ambao angekuwa nyumbani pengine bado amelala au yupo shambani [kazini] bila kula chochote.
Kuna wagonjwa mkuu usi generalize
 
Tumia akili.

Sio kila safari mtu anatokea nyumbani.

Safari zingine unatokea mkoani kikazi (mfano Musoma/Rukwa), unarudi zako Dar es Salaam.

Unatoka Musoma/Rukwa saa kumi usiku, unafika Dar 11 alfajiri au kesho yake kabisa
Kwani huko Musoma au Rukwa hakuna hotels nzuri ambapo unaweza kununua bites, juice and fruits ukabeba?
 
Ubebe kutoka wapi..

Tumia akili.

Sio kila safari mtu anatokea nyumbani.

Safari zingine unatokea mkoani kikazi (mfano Musoma/Rukwa), unarudi zako Dar es Salaam.

Unatoka Musoma/Rukwa saa kumi usiku, unafika Dar 11 alfajiri au kesho yake kabisa
Kwa hiyo wewe unavyo copy na ku paste kila mahala ndiyo umetumia akili gani hapo? C&P nayo ni akili?? [emoji12]
 
Singida wamezidi,chips vipande labda 10,na nyama 7 ndogo.
Nadhani option ya kubeba chakula safarini iwe kipau mbele.
Ishu sio kutumia pesa ni value for money haipo.wanaona hakuna option na ndio maana ukilinganisha na sehem ambapo tuna option bei ni rafiki sana.kuna siku nilikuw natoka mwanza to Dar.Tulikula mgahawa mmoja pale bahi,una paa,la makuti,this ni 2015 soda take away ilikuwa 1500/=
 
Saa kumi usiku?
Sasa kama ulikuwa unajua saa kumi ndio Safari kwa nini hukununua saa kumi na mbili?

Maana saa kumi na moja basi linatoka mjini na kwenda Stand ya Bweri kwa ajili ya safari, na Bweri basi zinaanza kutoka saa kumi na mbili kamili asubuhi. Na hapo Bweri Stand maduka kuanzia saa 11 yapo wazi. Kwa nini Usinunue Cake au Biscuits na Soda za take away?

Na basi likitoka Musoma mnaenda kula Shinyanga na kuchimba dawa
 
Mimi nikijua nna safari tu nakaanga samaki wangu 3 au 4 na viazi vitamu basi nafungasha. Huwa naenjoy sana
 
Shida ya wabongo tunapenda sana kula safarini, safari fupi tu ya Dar -Moshi/Dodoma/Iringa mtu anataka ale nyama choma kuku/mbuzi.! Wakati unaweza kukausha tu ukafika kwako ukapika ugali maharage ukashiba bila gharama
Wewe jamaa haupo serious
Yaani utoke dar saa kumi na mbili ufike Moshi saa Tisa mchana bila kula Wala kunywa?
 
inawezekana hivi vihotel vya barabarani vinamilikiwa na wakuu wa mikoa na wilaya na wakurugenzi wao. haiwezekani unakuta msikaki wa vipande vitatu tu vidogo unauzwa 1000 kwenye kihoteli kichafu, watu wanakula karibu kabisa na vyoo, serikali za mikoa na wilaya zipo zinaangalia tu.
Ajabu na kweli
 
Shida ya wabongo tunapenda sana kula safarini, safari fupi tu ya Dar -Moshi/Dodoma/Iringa mtu anataka ale nyama choma kuku/mbuzi.! Wakati unaweza kukausha tu ukafika kwako ukapika ugali maharage ukashiba bila gharama
Raha ya safari ni pamoja na kula ingawa ni risk.
Huwa natafuna mishkaki tu na chips kavu sio michuzi chuzi
 
Wakuu,mnafahamu kuwa wenye migahawa/hoteli za barabarani wanalipishwa hela nyingi na madereva na wakati mwingine wenye makampuni ya mabasi,ili mabasi hayo yaingie kwenye hoteli zao?Pia kuwa madereva na wafanyakazi wa mabasi hayo wanakula wanachotaka na kunywa ama maji au soda bure?Na kuwa gharama za kulipia kwa basi kwa siku ili basi liingie, zinafika hata elfu sitini,chini kabisa elfu ishirini?
Hili linasababisha gharama za uendeshaji kuwa juu na hivyo gharama za vyakula kupandishwa ili waweze kuendesha biashara hiyo.
Hii sekta ya huduma za chakula kwa wasafiri serikali haijaitupia macho kabisa,ndio maana iko kienyeji hivi!
Wizara husika,hasa inayohusika na Uchukuzi,isaidie hili jambo.
Bonge la hoja hili
 
Haya mambo ya Safari imenikumbusha kuna UZI mmoja jamaa alikuwa analalamika kuhusu Mabasi yenye vyoo ndani...[emoji23] JAMAA ANALALAMIKA KUKATAZWA KUNYA kwenye CHOO ndani ya Bus [emoji23][emoji23][emoji23]
 
sijawai ona hotel ya hadhi ya juu barabara zote za mkoa ambapo magari husimama kwa ajili ya vyakula ni upigaji tu wa madereva ili wapewe msosi wa bure
Hujapita kitungwa (Kama sijakosea spelling) hapo Moro Cate hotel mkuu? Au ule nao ni mamalishe tu?
 
Hili suala juzi kati lililetwa humu ikawa nongwa.
Jana nmepanda basi kuna mwamba alipandia singida, nafkiri ni mkulima. Kwanza kakosa siti, akakaa kwenye korido,. After that akatoa kisu af akafungua mfuko aliokua nao. Ndani kulikua na tikiti.

Jamaa akaanza kuenjoy tunda. Anakata tikiti anakula na anaangalia movue kiulaini sana. Nkajifunza kitu. Next time na mimi ntapanda na mtungi mdogo wa gesi ili kukwepa gharama.
[emoji16][emoji16][emoji16]
 
Back
Top Bottom