Uchunguzi wangu mdogo niliweza kugundua ni haya....
1/Wanawake wengi wa Kiafrika wanapenda sana kuonekana weupe na wenye nywele ndefu (Yaani wanapenda kufanania na wazungu)
2/Wanawake wenye Ngozi nyeupe wanajiamini na Kujivunia zaidi rangi ya ngozi yao kuliko wanawake wenye rangi nyeusi, hiyo ni kwa sababu kiasili wako wachache kwenye jamii za kiafrika lakini pia kwa sababu ya kufanania na wazungu (Sikuwahi kuona popote pale Msichana mweupe akitamani kuwa mweusi)
3/Sehemu kubwa sana ya wanawake wenye rangi ya chocolate(maji ya kunde) kiasili wana rangi nyeusi, lakini kwa ujanja na utundu wa kutumia aina fulani fulani za matunzo ya ngozi kama mazingira, mafuta, lotion, cream na kemikali na kupelekea kuonekana wana rangi ya chocolate.
3/Rangi ya Chocolate asilia kabisa kwa sasa kwenye jamii ni nadra sana kuipata, wengi wao wameishaichakachua na kuwa nyeupe kabisa, na ni vigumu mno kuweza kugundua. (Kifupi kuna wanawake wengi wanaonekana ni weupe kabisa lakini kiasili ni maji ya kunde)
4/Ngozi, nywele na maumbile ya mwanamke wa Kiafrika wa kisasa yamebeba siri nyingi mno, yanatunzwa na kuboreshwa kwa mazaga zaga mengi kupita maelezo. Kiufupi wanawake wengi wa kiafrika wa kisasa kimwonekano ni Fake, Fake, Fake.....
5/Haijarishi mwanamke ni 'mbaya' kiasi gani lakini kama ana rangi nyeupe basi ataonekana 'mzuri' kwenye jamii, na haijarishi mwanamke ni 'mzuri' kiasi gani lakini kama ngozi yake ni nyeusi basi ataonekana wa 'kawaida' kabisa.
MY TAKE.
Binafsi naona mwanamke mwenye rangi nyeusi asili ndio mzuri(Mrembo) zaidi LAKINI tatizo kubwa sana la wanawake wengi wenye rangi nyeusi asili huwa hawajiamini na kujikubali hivyo mwisho wa siku huishia kuja kujichakachua ili wafananie na weupe na hapo ndipo hitimisho langu linaishia kwa kuona ni bora mwanamke mweupe wa Asili kuliko mwanamke mweusi asiyejiamini na kujikubali au anayetamani kujikachua kufanania na mweupe.