Kuwasili kwa treni ya abiria jijini Arusha kwa mara ya pili baada ya miaka 30

TODAYS

JF-Expert Member
Joined
Apr 30, 2014
Posts
14,747
Reaction score
24,250
Katibu wa itikadi na uenezi wa CCM ndugu Polepole leo anazindua Huduma ya usafiri wa treni kati ya Moshi na Arusha.

Mkoa mzima umetulia kimya na watu wote wameelekea stesheni kushuhudia treni ya kwanza ya TRC iliyobeba makada wa CCM ikianza safari ya kihistoria.


Your browser is not able to display this video.





 
Wanaenda kuona kazi za JPM.
wengine wanakusanya watu kusikiliza mipasho na lawama tu.hata sera awajui kuzieleza.
 
Mbona unachanganya habari mara kuzindua treni mara wamepanda wanaCCM.. so tuelewe nini hapo??
 
Kilimanjaro Soo watu wa kukimbilia kuangalia train. Mkoa wa Mara alikotokea polepole kule sawa.hakunaga njia hata ya train.
 
CCM watu wa ajabu Sana,train kipindi Cha mkapa,mwinyi,JK ilikuwepo hawakuikarabati.Leo wenyewe wanaikarabati kwa Kodi za wananchi wanashangia mbona hamkuikarabati kabla? Mlikuwa wapi?pesa mlikuwa mnapeleka wapi?
 
Ndio maana nimepita maeneo ya ushirika na kwa mr price kinyaa watu hakuna. Jamaa a yangu yupo Uchira anasema wamekodi Coaster kwenda kuishangilia treni. Ccm hoyeeee
 
Leo Jumatatu Shirika la reli linafanya majaribio ya safari za treni ya abiria toka Moshi kwenda Arusha. Mgeni mualikwa ni katibu mwenezi wa ccm Humphrey Polepole.

Nimejiuliza tu kumbe TRC ambalo ni shirika la umma, ni wakala wa CCM siku hizi?

Wakati mwingine Serikali huwafanya wananchi kuchukia mambo yao kwa kuingiza usiasa mwingi. TRC ni mali ya watanzania wote kwa kodi za watanzania wote

Ile kauli ya CCM itatumia dola kuendelea kutawala ndio hii.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…