Kwa alichokiongea Heri Mzozo, Tshabalala ataenda Yanga

Kwa alichokiongea Heri Mzozo, Tshabalala ataenda Yanga

Japokuwa sifurahiswi na hili linaloendelea juu ya mkataba mpya Kati ya Simba na Zimbwe, ila hili swala limevamiwa na watu wengi ambao hawana weledi na mambo ya mikataba, na linapelekwa kinafki Sana

Bongo zozo yeye kama manager wa mchezaji ni jukumu lake kusimamia maslahi ya mchezaji wake, ila analipeleka hili swala kienyeji Sana, analopoka lopoka Sana, yeye kama manager angekuwa anakutana na team tofauti tofauti anafanya bargain then anamjulisha mteja wake na sio kuropoka hovyo

Na huyu mleta mada ni shabiki wa Yanga kaamua Tu kuanzisha Uzi kwa lengo la kufurahisha Wana yanga, pamoja na kuskia maneno mengi ya bongo zozo Ila sijaskia akisema mshahara wa zimbwe kwenye mahojiano, ningeomba mwanzisha Uzi atuletee ushahidi kuwa manager amesema alikuwa anapokea 1.5ml
 
Aseeee sidhani kama zimbwe analipwa 1.5 M.
Na kama analipwa 1.5 M hiyo si ni mkataba wa Nyuma? Ni meneja wake huyo huyo na zimbwe waliona inawatosha asa iweje saiv waone kama walidhulumiwa?
Kama mkataba unaisha team itatoa ofa iliyopo zimbwe atatoa yake wasipokubaliana aende tu, akatafute maslahi pengine.
Ila Simba wakimpa zimbwe hela anayotaka wajiandae kila mchezaji muhimu kutaka mshahara kama wa zimbwe au zaidi.
Na hivyo kuyumbisha team, akikazania sana wamwache aende kwa amani tu, Duniani wachezaji ni wengi.
 
Kama wewe utopolo ujaweka chunvi..Mimi Kama Simba nasema huu Ni ujinga mkubwa Sana kumlipa kidogo Zimbwe wakati akina chama wanalipwa mamilioni..unyonyaji mkubwa!
 
Kama analipwa milioni moja na nusu ni kosa la meneja wake kwanini alishindwa kumsimamia wakati anaongeza mkataba ili alipwe zaidi.
Kwa sababu ya haya mashindano na kuonekana uwezo umeongezeka ameanza kubwata badala ya kukaa na menejimenti ya Simba nq kudai mchezaji wake anastahili kulipwa kiwango bora.
Mbona kina Manura, Kapombe, Bocco wanalipwa vizuri jua hiyo ni kazi ya meneja wao.
Kuna wachezaji wazuri kqma yule wa kmc wanaqeza kuziba pengo lake sasa hivi hawqvumi sababu wanachezea timu ndogo
 
Aseeee sidhani kama zimbwe analipwa 1.5 M.
Na kama analipwa 1.5 M hiyo si ni mkataba wa Nyuma? Ni meneja wake huyo huyo na zimbwe waliona inawatosha asa iweje saiv waone kama walidhulumiwa?
Kama mkataba unaisha team itatoa ofa iliyopo zimbwe atatoa yake wasipokubaliana aende tu, akatafute maslahi pengine.
Ila Simba wakimpa zimbwe hela anayotaka wajiandae kila mchezaji muhimu kutaka mshahara kama wa zimbwe au zaidi.
Na hivyo kuyumbisha team, akikazania sana wamwache aende kwa amani tu, Duniani wachezaji ni wengi.
Zimbwe hawezi kulipwa 1.5 ata iweje, ni mishahara ya kina Rashid juma hiyo, hizo ni propaganda za yanga Tu, lakini pia swala la mshahara ni malidhiano Kati ya club na mchezaji, Simba wataweka ofa wanayoona wanaimudu kulingana na bajeti ya club na sio kumfurahisha mchezaji mmoja

Ila wakisema wampe hela anayotaka manager wake wataondoa hali ya utulivu kwenye kikosi na ata Kwa wachezaji wengine watakuja kutaka hela nyingi, chamsingi ni kupewa unachostahili na club inachoweza kuofa, ikishindikana yupo gadiel unampa mkataba mpya anaanza kusakata kambumbu
 
ile interview kama namkosea sorry ila alikuwa kama kapiga kilajii
ameoneshaa wazi mapenzi yake kwa yanga yawezekana meneja ni shabiki ya timu yetu ya wananchi
hajapresent kama meneja au mimi umeneja ndo nautafsiri vibaya
Jamaa ndio uongeaji wake, ila yote yote hiyo interview tumeiskiliza wengi ila hatujaskia akisema mshahara wa zimbwe, vipi mkuu naww umeskia akisema zimbwe anakula 1.5ml kama mleta mada?
 
  • Thanks
Reactions: Lee
Huyo wakala wa Tshabalala ni mtu mbaya sana kwa mchezaji.Anachofanya ni kuingia katika siasa za soka la bongo jambo lililoanza kumchonganisha mchezaji na washabiki.

Kama ni huko yanga amepewa maslahi mazuri,basi wamgesubiri aende yanga ndipo waseme wanayoyasema sasa.

Huko yanga nako mjue wapo wanaojiona wanaipa timu kuliko wanavyostahili.Kwa hiyo kama wameamua kuwainua wachezaji wetu,wafanye hivyo kwa wote.Nawaunga mkono.

Wakala aache maneno ya shobo.Haya ni maisha huwezi jua kesho yako
 
Jamaa ndio uongeaji wake, ila yote yote hiyo interview tumeiskiliza wengi ila hatujaskia akisema mshahara wa zimbwe, vipi mkuu naww umeskia akisema zimbwe anakula 1.5ml kama mleta mada?
hapana nisiwe muongo sijasikia mkuu
 
Lakini si makubaliano ya mkataba?na yeye akakubali?
Kama ni kweli analipwa milioni moja na nusu hilo ni tusi kubwa sana kwa Vijana wa kitanzania wanaopambana kila siku wakimwangalia shabalala kama role modo wao!

Wanachokiona hapo ni kwamba, hata wakipambana kwa juhudi za kuweza kufika pale alipo zimbwe juhudi zao hazitapewa heshima wanayostahili kwa sababu ya utaifa wao ! Mimi ni shabiki wa Simba lakini hili kama ni kweli si sahihi nalipinga kwa nguvu zote !!!!
 
Wewe sio shabiki bali ni mpenzi wa Yanga, na mimi kama mpenzi wa Simba kwakweli tumesikitshwa kua Tshaba analipwa kamilioni tu kwa mwezi, dah, yani tume betray his love and trust kwa timu anayoipenda na aliyojitolea kuichezea kwa moyo wote, kwakweli aende tu panapomstahili aisee.

Swali fikirishi, ina mana sisi wachezaji watanzania kwenye timu zetu hizi tunadharaulika kiasi hiki, kwamba hatuna hadhi ya kulipwa zaidi ya m15 kwa mwezi sababu tu ni wazawa?

Pia aishi manula naona ameshasoma upepo naye dau lililokuja ni kubwa, na madau yalivyoanza kuja kwa kasi ndio viongozi kuanza kuhaha kuitisha mikutano na wachezaji kujadili mikataba mipya.

Tujifunze hata kwa wenzetu, wachezaji muhimu mikataba unakuta imebakiza mwaka au hata miaka 2, mabosi wameanza kujadili upya mkataba wa mchezaji husika, huku kwetu mchezaji muhimu anabakisha mwezi ndio mnaanza kukimbiakimbia.
Miaka miwili yenyewe ndio mikataba yao mara chache sana itokee mtu ana miaka 3 au 4 mikataba mifupi tu ila hakuna haja ya kwenda kwenye media team kama inakunyima mkataba anza kutafuta sehemu yenye maslahi na wewe basi.
 
Mimi mahojiano nimesikiliza ila sijasikia meneja anataja mshahala anaolipwa Zimbwe Jr labda mleta mada alete maneno ya meneja hapa akitaja mshahala anaolipwa mteja wake na sio kumlisha maneno
Check you tube
 
wadau wa Simba mmeonyesha ukomavu mkubwa sana. Huyu dogo asibembelezwe wala mashabiki wasiwape presha viongozi. Aachwe aende,tuone atafika wapi
Tshabalala hana makuu,na analipwa vizuri tu na si hiyo 1.5 m aliyoandika huyu mtopolo mleta mada,kama mkataba umeisha na Club inamhitaji ni dhahiri ataongezewa mkataba na kuboreshewa masilahi yake. Huyo meneja ana lake jambo na Utopolo na mchezaji mwenyewe ana lake jambo na mabosi wake wa sasa. Muda ndiyo utaongea. Tshabalala hata kama ni darasa la saba lakini anajitambua na hawezi kuingia chaka.
 
Kwa Yanga nayoijua mimi sijui kama hata hiyo 1.5 wataweza kumlipa kama tu Saido aliyekuwa analeta mgomo inasemekana nyuma ya pazia hajafurahia maslahi kiduchu anayolipwa tofauti na alivyoahidiwa wakati wanamsajili,tena ni mchezaji wa nje huyo,wa ndani si mtampa laki saba nyie
 
Eric bailly mkataba ulibaki mwezi mmoja ndio kaongeza jana, messi bado miezi miwili

Ila wachambuzi wanashangaa simba kutomuongezea mkata zimbwe mpaka sasa kana kwamba ni kosa la jinai.

Mkataba ni makubaliano kama hawaafikiani kwa muda tarajiwa acha wavutane mpaka makubaliano
 
Back
Top Bottom