Kwa bahati mbaya mke ameshika ujauzito tena

Kwa bahati mbaya mke ameshika ujauzito tena

Tatizo heshima niliyoijenga katika jamii, naheshimika mno, sipo tayari kuikabili aibu hii

Unajua sikuelewi? Mtu umeoa halafu unawaza utaonekanaje?

Huyo si mkeo? Kwani kwenye ndoa mnaenda kulima bamia?

Hayo ni matunda ya ndoa na mnapaswa muwe grateful. Kuna watu wanahangaika hawapati watoto.

Wengine mtoto wa kwanza anapata vizuri then miaka inapita mtoto wa pili wanatafuta milele daima hawapati. Especially kwa lifestyle diseases za siku hizi kwa wanawake. Karibu kila mwanamke ana fibroid au changamoto ingine ya uzazi.

Be grateful una mtoto mwingine anakuja. Lakini pia ujifunze na mkubaliane na mkeo kupanga uzazi going forward.

Btw: Nimeongea kwasababu imenigusa binafsi pia. Mke wangu alibeba mimba ya mtoto wa pili wakati wa kwanza ana miezi sita na ananyonya bado. Fast forward today, mkubwa ana miaka mitano na mdogo anakaribie minne mwezi wa tatu. Nina raha sana kila nikiwaangalia. Na wametupa nafasi ya kupambana na maswala mengine kwa sasa na kusahau ulezi kwa muda. Wife amerudi pia shule sasa.
 
I'm too weary, yaani tuna mtoto wa miezi karibia 9 sasa, ila mke wangu jana kapima ujauzito baada ya kuhisi uchovu, kwa masikitiko makubwa ni mjamzito. Nitaficha wapi sura yangu Mimi? Naheshimika mno inakuwaje wakijua mke wangu mjamzito tena?

Yaani nionekane primitive Mimi? Nafikiria nimuambie tutoe ila navuta muda, mke wangu ndio chanzo cha yote, ananipa show huku mzunguko kausahau, na mimi siku reason!..

Nafikiria nimuambie akaitoe, naombeni mawazo yenu Wanajamvi!! Ndo nadhalilika hivyo
Kama kweli uña akili timamu USITHUBUTU KUTOA HIYO MIMBA. Pia usipende kujipatia sifa za kipumbavu namna hiyo kwa kutaka kudhuru uhai wa mtoto aliyetumboni. Wewe mwenyewe ni MZEMBE SANA unafanyaje unplanned sex na mkeo then unataka kufanya abortion. Unamparamia mkeo kama nguruwe bila utaratibu, ulitegemea nini???

Kama unaona kwamba MUNGU ni mjinga aliyeruhusu hiyo mimba iingie, NENDA KATOE HIYO MIMBA. Watoto ni ZAWADI KUTOKA KWA MUNGU hakuna anayejileta hapa duniani. Sasa MUNGU amekupa hiyo zawadi unaona kwamba MUNGU ni Mjinga, NENDA KATOE.

Unaeza kutoa hiyo mimba, MUNGU Akaamua kukufanya uwe hanithi yaani usiwe na uwezo tena wa kusex maisha yako yote, (mashine yako iwe haisimami kabisa ) hapo utajisikiaje???

JIRUDIE KWENYE AKILI YAKO TIMAMU, HAYO MAWAZO ULIYOWAZIA NI MAWAZO YA KISHETANI TENA NI IBILISI MWENYEWE NDIYE AMEWAZA NDANI YAKO, BINADAMU MWENYE AKILI TIMAMU HAWEZI KUWAZIA USHENZI HUO.

Wenzako wanalia mchana na usiku wapate watoto lakini hawajapata. Wewe unapata unataka kuua!!? Shame on you
 
Kabla hujaitoa ufikirie yule anayetafuta mtoto usiku na mchana...acha uboya na ufute hayo maneno sijui weary sijui bahati mbaya mtoto ni Baraka haijalishi kapatikana vp.
 
I'm too weary, yaani tuna mtoto wa miezi karibia 9 sasa, ila mke wangu jana kapima ujauzito baada ya kuhisi uchovu, kwa masikitiko makubwa ni mjamzito. Nitaficha wapi sura yangu Mimi? Naheshimika mno inakuwaje wakijua mke wangu mjamzito tena?

Yaani nionekane primitive Mimi? Nafikiria nimuambie tutoe ila navuta muda, mke wangu ndio chanzo cha yote, ananipa show huku mzunguko kausahau, na mimi siku reason!..

Nafikiria nimuambie akaitoe, naombeni mawazo yenu Wanajamvi!! Ndo nadhalilika hivyo
Mwanaume sio vizuri kuomba ushauri mambo madogo kama haya
 
Kaitoe kunusuru afya ya huyo mtoto (mtu kamili) wa miezi 9, hiyo mimba haina thamani kuliko huyo mtu.
Duh! Mwanangu.. humuogopi hata Mwenyezi Mungu. Tena una-insist kabisa, we ndio unaotoa risky.. usiingiize kwenye madhambi ambayo hayakuhusu.
 
Sio kweli


Akili timamu ipo hivi; maisha hafifu yanatakiwa yaangamie kwa ajili ya maisha yenye thamani, na ndio maana sisi binadamu tunaua/chinja kuku, mbuzi, ng'ombe nk, na tunakula nyama zao, ni katika hali ya namna hiyo hiyo hali inapolazimika mimba hutolewa ili kunusuru maisha ya mama mjamzito kwani uhai wa mama unayo thamani kubwa kulinganisha na maisha ya mimba isiyokuwa na maisha ya kujitegemea maisha hafifu, sasa kwanini katika njia hiyo tusinusuru maisha ya mtoto wa 9 months dhidi ya maisha ya mimba isiyotabirika kama itazaliwa au itakufa hapo mbeleleni, mimba yenye maisha hafifu kulinganisha na maisha ya thamani ya mtu kamili/mtoto wa miezi 9.??!.

Tumieni akili kutafakari jambo hilo.
 
Tatizo heshima niliyoijenga katika jamii, naheshimika mno, sipo tayari kuikabili aibu hii
Ebu kwanza mkuu,.
Aibu gani unayoiogopa kwa jamii adi kua tahari kuua kiumbe chako mwenyewe?mbegu yako mwenyewe,uliyoipandikiza kwa raha zote?

Io jamii haijui kua wewe ni mwanaume na ua unafanya tendo la ndoa?

una uhakika kweli wewe ni mwanaume kamili?upo tahari kua muuaji kwasababu ya mitazamo ya watu wengine?
Inashangaza wengine wanahitaji watoto,na wengine wanatoa tu.
 
Duh! mwanangu.. humuogopi hata Mwenyezi Mungu. Tena una-insist kabisa, we ndio unaotoa risky.. usiingiize kwenye madhambi ambayo hayakuhusu.


Wewe sikiliza; kutoa mimba bila sababu za msingi ni uhalifu kama uhalifu mwingine wowote lakini sio sawa na kuua mtu.mwenye independent life na ndio maana madaktari inapothibitika kwamba mama mjamzito anaweza kufa kutokana.na mimba aliyonayo hatua ya KIAKILI ni mimba kutolewa kunusuru maisha ya Mama kwasababu maisha ya mama yanayo thamani kuliko mimba, ni hivyo hivyo yapaswa kupimwa je maisha ya mtoto/mtu yanathamani gani kulinganisha na maisha ya mimba. Kumbuka.mimba sio mtu kamili na haina maisha ya kujitegemea na mtoto ni mtu kamili mwenye maisha ya kujitegemea.
 
Yaani nionekane m-primitive mimi?
Uonekani mprimitive kwa binadamu wenzio?

Kipi Bora uwe msafi machoni pa Mungu au Mbaya machoni mwa binadamu?

Imeshatokea na as a man you should face this challenge, jiamini ww sio wa Kwanza Wala sio wa mwisho kutokewa na hiyo Hali.

Unachotaka kufanya ni kuzidisha matatizo tu badala ya kupunguza.
 
Yaani nionekane m-primitive mimi?
Mwezi wa 8 mwaka juzi 2020 nilipata mtoto wa kiume. Mtoto akiwa na miezi 6 mama yeyoo akabeba ujauzito tena katika mazingira tatanishi ...hata mimi nilikuwa na mawazo kama haya. Ya termination ya mimba...

Mwaka jana mwezi Nov akajifungua mtoto wa kiume tena. Tungemuua mtoto tungepoteza nzagamba hii ilokuja

Muhimu azingatie lishe bora kwake na mtoto, aendelee kunyonyesha mpk miezi 2 kabla ya kujifungua.



Sent from my SM-T555 using JamiiForums mobile app
 
I'm too weary, yaani tuna mtoto wa miezi karibia 9 sasa, ila mke wangu jana kapima ujauzito baada ya kuhisi uchovu, kwa masikitiko makubwa ni mjamzito. Nitaficha wapi sura yangu Mimi? Naheshimika mno inakuwaje wakijua mke wangu mjamzito tena?

Yaani nionekane primitive Mimi? Nafikiria nimuambie tutoe ila navuta muda, mke wangu ndio chanzo cha yote, ananipa show huku mzunguko kausahau, na mimi siku reason!..

Nafikiria nimuambie akaitoe, naombeni mawazo yenu Wanajamvi!! Ndo nadhalilika hivyo
Ishiii maisha yako brother hivii familiar yako unataka mwingine akuongozee unaheshimika na naniii...?? Hebu vuta taswira anatowa Kisha inakuwa Ni sababu ya yeye kutopata Tena mtoto please please nakusihi zaa acha kutowa mimba issue yako Ni Kama ya brother yangu mbona alizaa na maisha yanaendelea
 
Miezi tisa ni mtoto mkubwa tu hivyo kwa dharura kama hiyo anastahiki kuwa na mdogo wake.

Second born wangu na last born wamefuatana kama hivyo. Wife alienda kwao kusalimia alikaa almost a month aliporudi na kichupa so uzalendo ulimshinda hakuweza kuzingatia mzunguko.

Kilichotokea tukakubaliana tulee mimba huyu mwingine aachishwe ziwa maisha yakaendelea.

Hivyo mkuu mambo ya kuogopa kutafsiliwa vibaya na watu ni bora kuliko kuua nafsi isiyo na hatia. Kama mama hana shida kwenye uzazi muache azae tu.
 
Naheshimika mno inakuwaje wakijua mke wangu mjamzito tena? .....Bhagoshaaaa!
 
Back
Top Bottom