Kwa bahati mbaya mke ameshika ujauzito tena

Kwa bahati mbaya mke ameshika ujauzito tena

Tatizo heshima niliyoijenga katika jamii, naheshimika mno, sipo tayari kuikabili aibu hii
Acha mkuu , kwa hiyo kumtia mimba mkeo ni aibu tena, muache mkeo azae , chamsingi Ni kuomba ushauri wa jinsi gani mtamuachisha mtoto kunyonya ili asiathirike , epuka dhambi ya kuua mkuu , usikute huyo un ayetaka kumuua akawa ndio mkombozi wako , maamuzi unayotaka kuchukua sio sahihi , kwani ww sio Wa kwanza mkuu, pia kutoa mimba ni hatari kwa afya ya mkeo pia
 
Uamuzi wa kuitoa bado ni hatari upande wa mama mzee, Tuwaheshimu sana akina mama maana hata kuibeba mimba kwa miezi tisa bado kujifungua nako kunakuwa na changamoto kuna wanaojifungua salama wapo wanaopoteza maisha


Inatolewa katika njia ipi, nani anaitoa na hiyo mimba ina umri gani??!--- hizo ni factors za kuzingatia katika mimba. Ukienda kuitoa kwa madaktari wa vichochoroni mimba ikiwa na miezi zaidi miezi 5 hapo ni hatari, lakini mimba ya mwezi mmoja, miwili hiyo ikitolewa kitaalamu haina hatari unayoifikiria.

Kumbuka kutoa mimba kwa sababu maalum mfano kunusuru MAISHA ya mtu, mimba sio mtu bali ni sawa na kiungo chenye uhai na chenye thamani katika tumbo la mbebaji pia mimba haina independent life kama an individual na hivyo maisha yake hayana thamani kulinganisha na maisha ya mtu.
 
I'm too weary, yaani tuna mtoto wa miezi karibia 9 sasa, ila mke wangu jana kapima ujauzito baada ya kuhisi uchovu, kwa masikitiko makubwa ni mjamzito. Nitaficha wapi sura yangu Mimi? Naheshimika mno inakuwaje wakijua mke wangu mjamzito tena?

Yaani nionekane primitive Mimi? Nafikiria nimuambie tutoe ila navuta muda, mke wangu ndio chanzo cha yote, ananipa show huku mzunguko kausahau, na mimi siku reason!..

Nafikiria nimuambie akaitoe, naombeni mawazo yenu Wanajamvi!! Ndo nadhalilika hivyo
Unavyosema unaheshimika mtaani kweni uliyempa mimba ni Dada yako? Acha Mambo hizo kabisa
 
Ni hatari kwa afya ya mama na mtoto aliyeko tumboni, huyo mama atahitaji lishe ya kumjenga mtoto tumboni na wakati huo huo amnyonyeshe mtoto wa miezi 9!!!, Mwili huo huo mmoja wa mama!!-- kawa punda??!!, si atazaa njiti na mtoto wa miezi 9 si atadhurika kwa utapia mlo??.

Tafakari ndugu.
Si kweli inategemea na afya ya huyo mama, mtoto alienae anaweza kumnyonyesha angali ana mimba hata kwa miezi mitatu ikiwa afya yake sio mbaya na Kisha akamuachisha bila kumstress na miezi sita iliyobaki akajenga afya kwaajili yake na mtoto ajae.
Lakini pia inaonyesha unyonyeshaji wa huyo mama sio wa Mara kwa Mara kwani ukinyonyesha effectively possibility ya kubeba mimba inakuwa chini mnooooo.
 
Inatolewa katika njia ipi, nani anaitoa na hiyo mimba ina umri gani??!--- hizo ni factors za kuzingatia katika mimba. Ukienda kuitoa kwa madaktari wa vichochoroni mimba ikiwa na miezi zaidi miezi 5 hapo ni hatari, lakini mimba ya mwezi mmoja, miwili hiyo ikitolewa kitaalamu haina hatari unayoifikiria.

Kumbuka kutoa mimba kwa sababu maalum mfano kunusuru MAISHA ya mtu, mimba sio mtu bali ni sawa na kiungo chenye uhai na chenye thamani katika tumbo la mbebaji pia mimba haina independent life kama an individual na hivyo maisha yake hayana thamani kulinganisha na maisha ya mtu.
Sababu maaluumu haiondoi hatari inayowezatokea
 
Usiitoe na mpe ushirikiano wa karibu mkeo, ili maneno ya wakulungwa yasimuumize; jibu rahisi ni mmeamua kuzaa haraka haraka ili baadaye mjikite zaidi kwenye majukumu mengine
 
I'm too weary, yaani tuna mtoto wa miezi karibia 9 sasa, ila mke wangu jana kapima ujauzito baada ya kuhisi uchovu, kwa masikitiko makubwa ni mjamzito. Nitaficha wapi sura yangu Mimi? Naheshimika mno inakuwaje wakijua mke wangu mjamzito tena?

Yaani nionekane primitive Mimi? Nafikiria nimuambie tutoe ila navuta muda, mke wangu ndio chanzo cha yote, ananipa show huku mzunguko kausahau, na mimi siku reason!..

Nafikiria nimuambie akaitoe, naombeni mawazo yenu Wanajamvi!! Ndo nadhalilika hivyo
Unafikiria ukaitoe daaah aisee MKUU usijaribu.....
 
I'm too weary, yaani tuna mtoto wa miezi karibia 9 sasa, ila mke wangu jana kapima ujauzito baada ya kuhisi uchovu, kwa masikitiko makubwa ni mjamzito. Nitaficha wapi sura yangu Mimi? Naheshimika mno inakuwaje wakijua mke wangu mjamzito tena?

Yaani nionekane primitive Mimi? Nafikiria nimuambie tutoe ila navuta muda, mke wangu ndio chanzo cha yote, ananipa show huku mzunguko kausahau, na mimi siku reason!..

Nafikiria nimuambie akaitoe, naombeni mawazo yenu Wanajamvi!! Ndo nadhalilika hivyo
Hili jambo nimewahi kutana nalo mimi. Tena kama nilijua leo mtu anakazwa mimba. Kabla hata ya bao kutoka nilimuuliza kama yuko kwenye siku zake ni withdraw. Alihesabu vidole akaruhusu mseleleko. Baada ya mwezi kitu na box.

Nilipoambiwa ndoa imejibu tena mtoto mwingine akiwa na mwaka mmoja niliitika tu sawa na sikuongelea tena kuhusu mimba hiyo kwa wiki moja. Niliwaza mengi sana. Kwanza mke wangu alikuwa amejifungua kwa operation mtoto tunayelea. Kwa ushauri inakuwa baada ya OP mtoto mwingine apatikane angalau baada ya miaka miwili au mitatu, Sasa kwangu aibu inakuja baada ya mwaka , nilijiuliza ntantembeaje nimebemenda mtoto kama watu wanavyosema, halafu kafirst born nakapenda na kukaonea huruma tumekanyima kupata haki zake. Nilikuwa na maumivu hiyo wiki yote. Kuna wakati nilitamani tuitoe ila kwa kuwa sipendi hivyo vitu nilikaa kimya.


Lakini hiyo wiki ilinipa nafasi ya kutafakari thamani ya uhai na zawadi bora ya watoto. Nilijiuliza watu wanatafuta watoto siku wakipata wanabeba mimba mfululizo hata 4 ili kufidia , kwa nini mimi nipaniki? Najuaje baraka atakazo kuja nazo mtoto? Na je sina uwezo wa kulea. Jibu likawa hapana naweza. Niligundua kinachonisumbua ni macho ya watu na mitazamo yao na wala sio kiumbe kijacho.

Baada ya wiki maamuzi binafsi ilikuwa tutalea mimba na tumsubiri kijacho kwa hamu. Watu wanatamani hiyo fursa ya kupata mtoto hawaipati halafu mimi naumia kijinga. Kwanza nilifikiria mtoto mwenyewe ni wa ndani ya ndoa hata waseme vipi mimi naziba masikio nasonga mbele. Sex ndani ya ndoa matunda yake ni watoto haijalishi utavuna mwaka mzima, na sisi tumebarikiwa matunda hayo mazuri ambayo ni zawadi toka kwa Mungu ZABURI 127: 3 nenda kasome.

Jambo nililofanya nikumpigia Daktari wa wife wa mambo ya uzazi ili kujua usalama wa mama kwa ujio mpya wa mtoto na ndani ya tumbo lake ukizingatia alikuwa bado hajapona vizuri kidonda kutoka na kujifungua kwa Operation. Daktari aliamuru apelekwe kwa ajili ya uchunguzi. Baada ya hapo niliambiwa nisiwe na wasiwasi wowote mama na kiumbe cha tumboni watakuwa salama hakuna shida yeyote na alinihakikishia kumfuatilia kwa karibu ukuaji wa mimba yake mpaka atakapojifungua. Pia kuna dawa alipewa wife ili huyu mtoto mwingine ambaye ni binti aendelee kunyonya kwa angalau miezi 5-6 mbele bila kudhurika kutokana na mimba.

Basi nikaziba masikio nikasonga mbele mwishowe wife alijifungua kwa OP tena mtoto wa kiume. Na cha ajabu watoto wangu hawa huwezi fikiri kuwa wametofautiana kama mwaka mmoja na miezi tisa hivi. Dada mtu ana mwili unakimbia balaa utafikiri kamuacha miaka mitatu mdogo wake.

Nipo hapa naenjoy na wanangu ninaowapenda na sijutii kupandanisha mambo kwa kuwa ni matokeo mazuri ya ndoa.

Licha ya andiko refu nafikiri utajifunza kitu hapa na kupata ujasiri wa kusonga mbele. Nakutakia malezi mema ya mimba na mtoto aliyepo. Jambo la msingi Kumbuka kila mtoto anakuja na baraka zake pamoja na ugali wake duniani.

Sent from my SM-A115F using JamiiForums mobile app
 
Sababu maaluumu haiondoi hatari inayowezatokea


Hatari ipi katika mimba changa mfano ya mwezi mmoja??!--- mimba ya umri mdogo inatoka hata kwa kunywa muarobaini, MO energy, Mabendazole, Albendazole au dawa yoyote ya minyoo nk, unapozungumza hatari ni katika mimba pevu miezi 5 and up, na case ya huyo muulizaji ni mimba changa.
 
Si kweli inategemea na afya ya huyo mama, mtoto alienae anaweza kumnyonyesha angali ana mimba hata kwa miezi mitatu ikiwa afya yake sio mbaya na Kisha akamuachisha bila kumstress na miezi sita iliyobaki akajenga afya kwaajili yake na mtoto ajae.
Lakini pia inaonyesha unyonyeshaji wa huyo mama sio wa Mara kwa Mara kwani ukinyonyesha effectively possibility ya kubeba mimba inakuwa chini mnooooo.


Unasema; "si kweli" halafu tena unasema; " inategemea na afya ya huyo mama" !!!??, be specific.

Ili Mtoto awe mwenye afya ya kimwili na kiakili anatakiwa anyonye Maziwa ya mama kwa Atleast 2 YEARS sambamba na supplementary foods , kumuachisha ziwa mtoto chini ya miaka hiyo ni UKATILI KWA MTOTO na ndio maana watoto wetu wengi afya zao za akili na mwili siku hizi ni mgogoro, malaria , vikohozi, mafua nk, kwao ni magonjwa ya kawaida kwani lishe zao wakiwa watoto zilikuwa MGOGORO kwa sababu ya UJINGA wa wazazi wa leo madhara yake yanakwenda hadi kitaifa, unakuta wachezaji wa timu za taifa hawana nguvu ya kucheza, tunafungwa na vinchi vidogo kwasababu wao wakiwa watoto walinyonya bara bara. Huko mashuleni ndio usiseme, mtoto yupo std 7, 5×20 hajui, hajui kusoma wala kuandika, hapo hujaenda secondary na vyuoni, hatujui mchawi kumbe alikuwa ni lishe duni kwa watoto wetu walipokuwa wadogo.

Kama huyo mama alikuwa hanyonyeshi vyema ndipo akapata mimba nyingine katika hali hiyo ya mimba unadhani ataweza kumnyonyesha vyema huyo mtoto wa miezi 9??!!----- fikiria jambo hili vyema, je afya ya huyo mtoto/mtu kama akiwa mtu mzima itakuaje??!!

"You have to think deeper in this case."
 
Hatari ipi katika mimba changa mfano ya mwezi mmoja??!--- mimba ya umri mdogo inatoka hata kwa kunywa muarobaini, MO energy, Mabendazole, Albendazole au dawa yoyote ya minyoo nk, unapozungumza hatari ni katika mimba pevu miezi 5 and up, na case ya huyo muulizaji ni mimba changa.
Unatolea mfano mimba changa alafu unakuwa mvivu wa kufikiria uhai wakiumbe kilichomo tumboni. Haijalishi njia gani uliyotumia kutoa mimba kuna hatari kama kutokwa damu nyingi kuharibu kizazi.
 
Usivune laana ya kutoa utajutia,wewe sio wa kwanza wala wa mwisho hiyo aibu itaisha mtoto akishazaliwa yote mtasahau.
 
Back
Top Bottom