Kwa 'body language' tu ya Mama azungumzapo huhitaji Akili Kubwa kujua ya kwamba...

Kwa 'body language' tu ya Mama azungumzapo huhitaji Akili Kubwa kujua ya kwamba...

Kutakuwa na tofauti kubwa ya kiutendaji na Hayati kwa kuwa mama huenda akatumia ushawishi zaidi kuliko usimamizi kwa kuwa hakuna jipya. Kwa jinsi Watanzania walivyo watatumia mwanya huo kufanya "business as usual". Kiasi gani atakuwa mkali kuliko mtangulizi wake, muda utatoa jibu
Business as usual ndio tunalolitarajia mkuu.

Mama kaanza na gia kubwa ila naomba asipoteze muelekeo tu.

Muda ndio kila kitu na kila la kheri kwake mama.
 
Sasa CCM leteni ile agenda yenu ya kuongeza muda wa utawala. Kama ingepita kwa yule sijui ingekuwaje! CCM tumieni akili. Sasa wote mtaanza mapambio ya kumsifia mama yetu, Rais Mpendwa saaaaana aliyekuja kivingine, akiachana na utawala wa kibabe huku mkimtukuza Mwendazake na kumlinganisha na Yesu! Hivi huwa mna ubongo vichwani au mafua tu?!!

Mama Samia Suluhu Ni Faraja baada ya dhiki, ni Heshima penye dharau, ni Pendo penye Chuki, na ni Matumaini penye Kukata tamaa. Yeye hasa ndio MWENGE WA UHURU!!!!!!.
mitano tena kwa mama
 
zege la nyasi
mama ameusoma mchezo,kwamba ili afike mbali anahitaji kuiga mazuri ya mafahali hawa wawili na kuyaacha mabaya yao.

mathalani:
a)jk alikuwa
1)mwanadiplomasia mzuri,
2)mwanademokrasia
3)mjengaji uchumi
4)mzembe katika ufuatiliaji
5)asiye na msimamo

b)jpm alikuwa
1)mfuatiliaji mzuri
2)asiyependa uzembe na uvivu
3)asiyeyumbishwa ovyo
4)mzalendo kwa nchi
5)jaziba isiyojenga
6)dikteta
7)asiyependa demokrasia na diplomasia

mama achagua sifa zimfaazo kati ya hizo hapo juu.
 
Mama anaongea kama kiongozi, wakati huohuo kama mama, kweli ni mapema ila kwa uanzaji wake, sifa tumpe.
Kiongozi kama nchi ya wavivu,watu wenye majungu, maneno mengi kuliko utendaji kama Tanzania haitaji kiongozi awe kama muuza lamba lamba.

Muda ndio mwalimu.
 
1. Baba Mbabe alikuwa hamshirikishi na huenda hata alitamani Kuachana nae

2. Ushauri wake ulikuwa ukipuuzwa na kudharauliwa na Baba

3. Hali ngumu ya Maisha imemkwaza Mama japo Baba aliona anatukomesha

4. Aliwaamini sana Waliodharauliwa na Baba ambao walikuwa Weledi kuliko aliyowateua Yeye Baba

5. Kuna Siri nyingi za Upigaji wa Miradi ya Baba ila alishindwa Kumwambia kwakuwa alishagundua anadharaulika nae

6. Baba Kukitenga sana Kisiwa anakotoka Mama kulimkwaza akiamini hata Kisiwa pia kina Haki ya Keki Tamu na Nono ya Ardhi ya Tanzania

7. Mama ameiva vyema Kidiplomasia na Kiustaraabu japo ana Ukali wa Kiumakini tofauti na Baba aliyekuwa na Ukali, Kukomoa, Chuki na Ujeuri wa Kibabe

Ni mapema mno Kumpongeza Mama ila tusikatae kuwa dalili ya Mvua ni Mawingu na ' Body Language ' ya Mama inaonyesha kuwa Kilio cha Ugumu wa Maisha ya Watanzania ( Vyuma Kukaza ) hata na Yeye ( Mama ) inamuuma.

Hivyo Kipaumbele chake sasa ni Kuturudishia Tabasamu lililopotea katika Sura za Watanzania tokea tarehe 25 Oktoba, 2015 hadi 17 Machi, 2021.
May the Soul of our Hero JPM rest in eternal peace. Let the people talk, but let them keep some words within themselves.. You may praise her at the moment..but mark my words..you are going to regreat..what i saw yesterday, i can say it was a total embarrasment in her regime.
You can not be guided by social media comments when it comes to select or not an individual in a very sensitive possition.
May our beloved country shine in everywhere.
 
Wee ipyana, kila zama na kitabu chake. Pambana na yaliyo mbele yako.
Sema kwa sababu ninyi ni watoto, je kuna raha na uhuru wa kijinga ambao watu waliupata katika kipindi cha kikwete??? lkn walimtukana kila uchao. Hivyo usifikiri huyu mama atakuwa analeta chakula mezani kwako, au kujaza pesa mifukoni mwako, bado wewe binafsi unahitaji kuwa na nidhamu na kujituma kulingana na malengo yako na Mwenyezi Mungu alivyokujalia.
Mosi mimi sio mtoto ,pili ninafanya biashara na ni mhanga wa sera kimeo za Magufuli. Hakuna uhuru wa kijinga as long as sheria zilizopo zimetungwa kwa kulinda haki zetu wote sio kwa watawala tu.
 
Ila wapitisha mizigo na wau flow mita bandarini ili wasilipecvodi ni sawa. Ndio maana ya msemo huu kama hukuzingatia kilichopelekea maamuzi hayo .
Tatizo nyie ni waaribifu kama wew ni mpinzani wa Mama pole yako ila tuliowengi karibia nchi nzima tunayaona matumaini mapya kwa mama Samia na kwa hali hii naomba Mama aongezewe ulinzi
 
Mosi mimi sio mtoto ,pili ninafanya biashara na ni mhanga wa sera kimeo za Magufuli. Hakuna uhuru wa kijinga as long as sheria zilizopo zimetungwa kwa kulinda haki zetu wote sio kwa watawala tu.

Good, pambana na yaliyombele yako. yaliyopita ni historia.
 
Tatizo nyie ni waaribifu kama wew ni mpinzani wa Mama pole yako ila tuliowengi karibia nchi nzima tunayaona matumaini mapya kwa mama Samia na kwa hali hii naomba MAMA AONGEZEWE ULINZI

Wewe si wa kwanza wako wengi wanao niona hivi mwisho wa siku hurudi na kusema jamaa aliliona hili mapema tungalimsikia na kufuata ushauri wake.
 
Huna hoja bora ungenyamaza. Hapo ni chuki binafsi tu kwa jpm kwa kudhibitiwa kwako dhidi ya maslahi ya umma. Kama sio cheti feki kutumbuliwa na kadhalika.
Kubambikiwa kesi, kodi, kuvunjiwa nyumba......utachoka tu kujitoa fahamu kama mafarisayo.
 
Hakuna kitu kitabadilisha maisha kuwa Bora zaid Kama hutojishughulisha na kufanya jambo kwa juhudi na ubunifu vinginevyo utazidi kunyooshea watu vidole na kuamini kuwa unalogwa au unaonewa kumbe the problem is you

Ni kweli kabisa kuwa, msingi wa mafanikio na maisha bora kwa mtu yeyote ni kufanya kazi kwa bidii..

Lakini kwa upande mwingine lazima ujifunze na utambue uwepo na umuhimu wa serikali..

Serikali yoyote ina jukumu kubwa la kipekee sana ku - facilitate au kuhakikisha kuwa watu wana mazingira bora na rafiki kwa ajili kufanya shughuli zao kwa ajili ya kujipatia mkate wao wa kila siku...

Kwa mfano ni wajibu wa serikali;
å Kutoa uongozi bora na siasa safi kwa taiga na watu wake. Kuna sehemu imesemwa, ustawi wa taifa lolote unahitaji uongozi bora na siasa safi.

å kusambaza huduma za kijamii e.g umeme, maji, afya, nk nk nchini kote kwa usawa

å Kuweka mazingira bora na rafiki ya ufanyaji biashara, kilimo, uchimbaji madini nk nk

å Kuweka mifumo rafiki ya kodi kwa watu wote ktk sekta zote

å Kuhakikisha mazingira ya kiusalama na amani kwa watu wote ili wafanye shughuli zao bila bughudha

å Kuhakikisha kuwa mahusiano ya kidiplomasia na mataifa mengine ni mazuri ili kuwezesha watu kuvuka mipaka ya kitaifa kwa urahisi ili wafanye shughuli zao nk nk

KWA HIYO;
¶ Personal efforts ktk kujitafutia riziki zetu za kila siku ni muhimu sana lakini serikali ina nafasi ya 90% kufanya kila mtu ktk taifa lake afurahie maisha kwa kuwa na mahitaji yote muhimu...

¶ Ndiyo maana katika maandiko matakatifu (Neno la Mungu - Biblia) mahali fulani imeandikwa;

"....mtu mwovu atawalapo, watu (wananchi) huugua...."

Kama watu wanaugua tu, maana yake wana njaa na wanaumizwa na uongozi uliopo..

Ndivyo ilivyokuwa Tanzania ya Magufuli...
 
Back
Top Bottom