Kwa CV hii ya wakili Mwabukusi na Rais Mteule wa TLS inasadifu hulka na tabia zake

Wakati Mwenyezi Mungu anatupa wengineo UPEO MKUBWA / AKILI NYINGI na MAARIFA haya TUKUKA Wewe uliwa wapi?
Kama wewe mbumbumbu una upepo , Robert Einstein atasemaje? 🀣🀣🀣🀣🀣

Wewe una upeo wa kuona K tuu
 
Umeandika ushuzi mtupu. Wengi wetu tumekulia kwenye hiyo mitaa na kufika mbali kielimu. Ingekuwa kukulia Ngarenaro ni sifa mbaya basi mawakili wasomi wasingemchagua kuwa rais wao.
 
Ndio keshatoboa hivyo wanaosoma wa kuungaunga kutokana na hali zao kiuchumi au wazazi wao huwa wanakuwa wazuri sana kichwani na wenye machungu kwenye uzalendo na kujenga hoja
 
WAtu masikini siku zote wanaona viongozi ndio chanzo cha matatizo yao huishi kwa kulaumu ,kugombanisha watu, fitina na chuki
 
Wewe hujielewi kabisa πŸ’―, wakili Boniface Mwabukusi kaonyesha jamii ya wasomi Tanzania njia na kuwafumbua macho ndondocha kama wewe, ukitoa baadhi ya mawakili ambao ni wazuri kama akina Tundu Lissu, Rugemalila nshala, mabeleka etc majority ya mawakili Tanzania ni wachumia tumbo, mfano issue ya bandari kila mtanzania alijuwa kinachoendelea juu ya hao majambazi yenu, Elimu siyo kwenda vyuo vikuu tu unavyojua wewe, mfano Chuo kikuu cha Dar es salaam hadhi yake imeshuka sana hakipo Tena kwenye ubora kwa vyuo vya Africa na Dunia kwa sababu ya wanasiasa wengi wanachakachua degrees zao hapo chuoni mfano Mwigulu Nchemba anasema ana PhD ya uchumi muda mwingi yuko kwenye siasa muda wa kusoma na kafanya research hakuna anatumia hao maprofessa kumufanyia, yeye ana show up kwenye presentation kudefend hiyo proposal yake wakati huo ameshawajaza mapesa hao watu. Ndo maana anapwaya sana kwenye utendaji kazi wake. Mtu mwingine ni Prof Kitirya Mkumbo huyu naye ni kilaza sana ndo maana JPM aliwaona vilaza na na kuwatoa kwenye baraza lake la mawaziri, Samia aliporudi akawarudisha ndo maana unaona matokeo ya ovyo kwenye uchumi na biashara na uwekezaji.
 

Attachments

  • IMG-20240730-WA0046.jpg
    123.3 KB · Views: 1
Ukilinganisha mapito alie juu sasa hata form 4 hakufaulu....leo ana Phd 5....na ndie Chief Mkuu wa Tanzania
 
Ulikuwa unamtaka huyu kuku wa kizungu anayeuawa na utitiri! Tunalitaka jembe la kupambana na vibaka wa mbogax2 wakiongozwa na guberi kutoka kizmkazi!! Your days are now numbered!.
Tunahitaji jembe la kukamata majambazi yanayoteka raia yakijifichika kwenye kivuli cha kofia za polisi
Muda wenu kweshney!
 
Huyu Mwabukusi kachaguliwa na wanasheria vijana wadogo kiumri, kachaguliwa kishabiki.

Hiyo elimu yake ni ushahidi wa kwanini alishindwa kesi ya TPA suala la DPW. Shule ndogo ya sheria.

Lakini huwezi kuwalaumu wanasheria waliompa kura, wengi wao ni hawa watoto wa instagram, wanasheria vijana wasio na maono mapana juu ya uendeshaji wa nchi.
 
Walimpigia kura ya kumchagua Mwabukusi mmoja wao ni huyu hapa, bwana mdogo kwa kuyasoma maandishi yake tu.
 
Ukilinganisha mapito alie juu sasa hata form 4 hakufaulu....leo ana Phd 5....na ndie Chief Mkuu wa Tanzania
Anairudisha nchi kwenye uchumi wa juu kati kwa kasi kubwa. Samia kwa kasi hii atakuja kuwa rais aliyefanikiwa kuliko wote watano waliomtangulia.

Ni msikivu mwenye utulivu mkubwa wa kufanya maamuzi bila kukurupuka.
 
Unamaana kama jiwe alivyovunja kioo cha dirisha la bweni lake na kutoroka!
 
Hebu wewe mwenye elimu tuonyeshe vizuri alivyoshindwa hiyo kesi ukirejee hukumu iliyotolewa. Kama mahakama ingekuwa inasimama yenyewe hukumu ingekuwa tofauti maana hata hiyo mahakama iliona mapungufu ya mkataba wa bandari? Jiulize kwanini rufaa ya hii kesi inapigwa danadana mpaka leo? Hao TLS wenyewe na uchawa wao waliona mapungufu wa huo mkataba wa bandari.
Unajifanya unajua kumbe ni bumunda tu kama mabumunda mengine
 
Huyu ndiye hasa mpambanaji wa kweli. Kama alipitia njia hii hata kufuzu mafunzo ya sheria na kupata leseni ya uwakili, basi hiki ni kichwa kwelikweli!

Huyu hali vya mezani, vya kuhongwa na kuvizia kama nyie watoto wa mama mnaokula kwa gharama ya kuwabagaza na kuumiza watu wengine ili kufurahisha bwana zenu na kisha wawape chochote ili mweze kuishi.

Huyu anapambana kutafuta kilicho chake. Angalia alivyoiamusha na wananchi kwenye sakata la mkataba wa kiwiziwizi wa Bandari na DP WORLD.

Ni Mkataba unaodaiwa kutengenezwa na hao wanaoitwa wasomi lakini dereva wa daladala tu akawazingua na kuwakosoa vikali kwa kuingiza nchi kwenye shida kwa taka taka ile waliyoiita "Mkataba"

Unawezaje kuwa na akili ya uthubutu wa kumbeza mtu kama huyu badala ya kumpa maua yake?

Poor thinking ChoiceVariable

Kuonewa huwa anaonewa na kunyanyaswa si kwa sababu "yeye hujiona kuwa anaonewa". Bali ni kweli huonewa na kunyanyaswa kinyume cha sheria kwa sababu ya kukosoa hawa wanaojiita wasomi lakini wakiwa ndio wajinga na wapumbavu wasiostahili kupewa dhamana yoyote ya uongozi!
 
Wee popoma kweli tabia za kikei
 
Vivaa!! MWABUKUSI Vivaaa!!!✊️
 
Ila wewe jamaa huwa una roho mbaya kichizi. Mtu kukulia Ngarenaro ndo akose kigezo cha kuwa rais wa TLS? Kuna mwanasayansi wa TZ mkubwa sana duniani kwa sasa naye kakulia Ngarenaro tena ile Ngarenaro ya karibia Matejoo.. ingekuwa wanaangalia background basi jamaa asingepata shavu la makampuni makubwa ya utafiti.
 
Mkataba ungekuwa na mapungufu Adani asingekubaliwa kuwekeza hapo hapo bandarini.

Kwa ufupi ni kwamba mimi na wewe tunaweza kuanzisha kampuni ya masuala ya bandari tukawasilisha vielelezo vyote serikalini na tukapewa tenda ya kuendesha bandari ya Mtwara au ya Tanga, bila ya kujali IGA ya DPW imeandikwa vipii na masharti gani yameandikwa kweenye huo mkataba.

Mahakama ilitupilia mbali hoja zake baada ya kuona hana uelewa mpana wa masuala ya mikataba namna inavyofanya kazi.

Ni aibu kwa Mwabukusi kuonekana nyota, ni ushahidi kwamba tunao mambulula wengi sana hapa Tanzania kwenye sekta mbalimbali na mawizarani.
 
wengi wetu tumetokea maisha kama hayo, tumeishi maisha magumu, lakini Mungu ametusaidia. ninyi wa geti kali hamjui maisha mbona, na wengi wenu mnavaa pampas hadi ukubwani.
πŸ˜‚πŸ˜‚
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…