Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Naibu spika namuona bado sana hata hivyo hawezi fanya lolote labda kwa muongozo wa watu fulani.aaha wapi? tukimsema Raisi ana nguvu muelewe, kabla hajaitisha wasiojulikana tayari watakuwa wamemchukua, alafu naibu spika anabutua chini ya mtutu
Kweli mkuuNyie ndo mnafanya Jf siku hizi iwe kama facebook. Soma katiba kwanza ndo uandike, tunataka elimu sio hisia na ushabiki.
Mkuu ulivyo andika nikadhani unafahamu kipengele chochote cha katiba kinachosema bunge haliwezi kupiga kura kutokuwa na imani na presida, kumbe nothing!.Hawezi fanya lolote lile jinga la Dodoma, alidekezwa sana, Ebu mwambie ajaribu kutumia kura ya veto? Kwani anayo? Rais anaweza kuvunja bunge wakati wowote, mbili bunge haliwezi kupiga kura ya kutokuwa na imani na rais, bali waziri mkuu. Hivi wewe unajua wabunge wapo upande gani? Ebu kasome katiba acha uvivu.
Hawezi, he is finished!, kwishney finito!.Kwa nafasi aliyonayo dhidi ya ule muhimili anaousimamia japo tayari yupo under control, je anaweza kutumia ile kura ya veto na kusema liwalo na liwe akapindua meza kwenye kikao kijacho cha bunge?.
Na ukapigwa 🎶wimbo hatuna imani naye?.🎵
Kura ya veto ipi? Speaker hana kura ya veto.Hali si shwari kwa wanaofuatilia siasa za nchi hii toka camarada Legendary Pombe alipotoweka dunia.
Pamoja na kuwa katika wakati mgumu kufuatia kushusha siraha nchini na kuonyesha udhaifu kwenye mhimili mwingine.
Kwa nafasi aliyonayo dhidi ya ule muhimili anaousimamia japo tayari yupo under control, je anaweza kutumia ile kura ya veto na kusema liwalo na liwe akapindua meza kwenye kikao kijacho cha bunge?.
Na ukapigwa 🎶wimbo hatuna imani naye?.🎵
Kwanza hana hiyo kura ya turufu (veto). Najua unajua kwamba kwa mujibu wa Ibara ya 46A ya Katiba ya JMT, 1977 Bunge linaweza tu kumshitaki Rais ambapo mlolongo wake ni mreeefu ambao naona kuwezekana kwake ni sawa na ngamia kupita kwenye tundu la sindano! Sijaona Speaker akiwa na kura ya turufu kwenye huo mchakato.Hawezi, he is finished!, kwishney finito!.
PNaogopa sana Ndugai akizungumza ukweli
Ni kweli, anasakamwa lakini sipati picha Ndugai akiamua na yeye kuwa liwalo na liwe! Ki vyovyote vile bado naona Ndugai ana kura ya turufu katika sakata hilo linalovuma. Ndugai anayo mengi ayafahamuyo yenye kingi kishindo yakiwa bayana! Kigezo cha kummaliza Ndugai eti kwa msamiati wa '2025'...www.jamiiforums.com
Nadhani mkuu hufahamu maana ya kura ya veto! Jishughulishe kusoma mkataba wa UN uone jinsi kura ya turufu/veto inavyofanya kazi kwenye Baraza la Usalama na Umoja wa Mataifa.Kura ya kutokuwa na imani na rais, pamoja na kuwa na mlolongo mrefu but ndiyo hiyo tunayosema kura ya veto ambayo inampa spika jeuri endapo tu itafanyika.