Kwa hasara ambayo huyu mtoto ameniingizia: Nashauri Sheria itungwe iwe ni shuruti watoto kusaidia Wazazi uzeeni

Angalia asije dondokewa na vitu vizito ikawa ni balaa nyumbani. Tahadhari kabla ya ajali

Sent using Jamii Forums mobile app
asante kwa tahadhari mkuu, tumejaribu kuviweka mbali baada ya kujua shida yake. Leo kafungua fridge, kabeba ile tray, kachukua maziwa ya pact akayamwaga mule ndani ya ile tray, akayachezea kisha kuja kuhamaki anaanza kuyakojolea, ndio kumuwahi.

Yaani mkijifanya bize hammjali dakikka chache tu anaharibu mambo.
 
Usiku mwema, anza sahizi kukaombea hako kwa junior [emoji23]

Sent using Jamii Forums mobile app
poa pouwa kamelala hoi, huwa kanalala hoi utadhani kanabeba zege.
kakiamka asubhi kana ratiba zake za kudumu, kulilia uji, na kisha kukata gogo kwa poti, baada ya hapo kanaogeshwa kanaanza mihangaiko ya siku.

mimi sina shaka nako kabisa mkuu, ninaimani Mungu atakaweka sawa tu, maana nakakubali sana,
 
We jamaa mzembe unamchekea huyo mzazi inabd uwe kauzu dogo akileta wenge. Mie wangu ashiki simu anajua hii simu ya baba hii simu ya mama nachezea makorokoro yake tu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mtoto wangu ana mwaka na miezi sita anahuo utundu anapenda sana simu ukijisahau tu ameshakwapua na kuanza kuchezea by the way Mimi huwa nafrahi kumuona mwanangu anachakalika,but kwa huyo wako endelea kuwa unamkanya kidokidogo ataelewa tu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
mkuu mbona unakuwa nabii wa mabaya tena mkuu kama mwamposa.
Nimepata kesi nyingi ya vitoto vya umri huu hata huyu anaafadhali maana anapenda vitu vya umeme mdogo zaidi (electronics) hivyo vingine vya hatari hata time navyo

Mtoto huwa anakimbilia kuchezea vitu vya wakubwa kama hana vya stage yake, mnunulie vitu vyake vya kuchezea vya kutosha! Uone kama ataharibu hivyo vyako
 
Acha zako wewe

Huyo dogo karithi tabia zako

Badala ya kumshughulikia kwa uwezo unataka kuihusisha serikali kwa simpo Kama hivi very very simpo for gov.size



Sent using Jamii Forums mobile app
 
Yaani mtoto wa miaka miwili tu mnashindwa kumdhibiti, kakiota mapembe si ndo mtatembea na makabati yenu vichwani.
 
Mtoto hahitaji vishindo kumkataza jambo, huyo haelewi ukali wala bakora, anahitaji saikolojia ambayo itamuathiri anapotaka kufanya jambo baya la uharibifu. Soma techniques za kumfanya mtoto akusikilize na atii. Mfano anapolilia kiitu sana hebu jifanye na wewe unalia, atafocus kwako zaidi kuliko kwenye kitu. Zipo njia nyingi.

Zinategemea na aina ya tatizo. Ni challenge sana mtoto wa aina hiyo na ukishindwa kumdhibiti saivi 2 yrs ni tatizo kubwa, ndo mara unasikia baba kapiga kauwa kumbe hakukusudia ni frustration tu zimemzidi na kukosa namna ya kumtrick mtoto vizuri
 
Jamaa yangu mtoto wake ana mwaka na miez mi nne ameshapasua TV na desktop, pia redio amefamya imeungua. Sasa hapa napata picha huyu wangu ndo kwanza miezi sita, labda nitafute mnyororo special wa kumfunga miguuni akikaa sehemu asichomoke tusitiane hasara za kizembe.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kama miaka miwili tu anaweza kufanya uharibifu wote huo,basi huyo mtoto ana akili nyingi kuliko walezi wake.Tafuteni mtu awasaidie malezi.
Na huyo mtu awaoe hao walezi wote wawili.

dodge
 
kuwa mlezi mkuu. mwanangu aliwahi nifanyia huu upuuzi wa soti, nilimdaka kwa sababu angetulia kichwa, nkamwambia hii sitaki nkaenda chukua fimbo, aisee alikula bakora za haja.

now wenzake wanamwambia njoo turuke soti, anasema baba hapendi atanichapa matunduizi,

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Dah! Kama ungekua nchi za mabeberu ungefungwa jela mkuu🤣🤣🤣
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…