Uchaguzi 2020 Kwa hii hotuba ya Tundu Lissu Segerea, amepotosha

najua wewe ni mnufaika wa mfumo kandamizi lakini jaribu kuwa na Utu kidogo maana wanaotaabika kule SGR ni ndugu zako, hakuna pesa imelipwa SGR na Serikali ya CCM tokea mwezi wa nne, kuna njaa Hatari na mda wowote watagoma kufanya kazi ndipo mtapata Aibu ya mwaka endelea kuutetea usumbufu wa malipo tokea Serikali ya CCM mpaka mje kuumbuka.
 
Mkuu Bora umenisaidia anadhani humu jf hakuna mtu anayeishi canada, Hawa cdm waongo sana
Wewe ndiyo muongo unatengeneza propaganda kusaka uteuzi kwa njia haramu
 
Umeandika kishabiki tu. Huna info zozote kuhusu malipo ya sgr wala stiglazi. Endelea kumlamba miguu huyu dikteta wa kihutu.
 
Minyoo
Huyu sio mnufaika wa chochote. Ni shabiki maandazi tu. Namfahamu tangu kitambo.
 
Miradi mingi ya CCM inaenda kusimama kutokana na Serikali ya CCM kuchukua pesa zote kupeleka chato na zingine kwenye kampeni watapata Aibu kubwa mda si mrefu.
 

Ukikopa shilingi 10 ukalipa shilingi 10 kweli unaweza kusema mkopo ule ni hela yako

Lakini ukikopa shilingi 10 ukalipa shilingi 25 sababu ya riba, ile shilingi 15 ya ziada si yako ni cha mkopeshaji hicho

Serikali hii inakopa pesa matrilioni kwa riba kubwa sana ambayo yatazaaa mizigo ya mabilioni mengi ya riba ambayo tutayabeba.

kwa hiyo kwa mikopo hii yenye masharti ya riba za kunyonga uchumi wa Nchi hayatufai hata kidogo. Magufuli aondoke atupishe mikopo yake ni kitanzi kwetu na watoto wetu
 
Nikusaidie kujibu maswali yako,
1.Sio kila uwanja wa ndege ATCL wanatua, kule musoma wanatua? Arusha je? uwanja wa GGM? Sopa Lorge kule ngorongoro? Ras Kutani kule kilwa? mbona atcl wanaenda comoro tumejenga uwanja kule? haimaanishi kila uwanja nchi hii unatumiwa na atcl.

2.kwani kila tender ya manunuzi hutangazwa? ulishasikia tender ya kusupply landcruiser? hivi vitu tunavinunua kwa manufacturer unataka kushindanisha na nani? tunanunua toyota kiwandani tunashindanishaje?

3.hili la deni nimeshajibu au unataka maelezo gani tena?

4.Ulishasikia marekani japan sweden tunisia wanaongeza mishahara? kuwaza nyongeza ya mishahara ni mawazo ya kimasikini watu wanawaza kupata promotion sio nyongeza ya mshahara, tunacho angalia ni purchasing power ya wananchi wetu.

Zimbabwe kima cha chini ni 3m kwahiyo mshahara unatosha? Kenya kima cha chini ni elfu 4 kwahiyo mshahara wao ni mdogo? uingereza wanalipwa pound 40 mbona hawajadai nyongeza ya mshahara,

Lissu hajawahi kuwa mtumishi wa umma wala hajawahi kuwa mjumbe wa TUGHE na hakuwepo nchini miaka mitatu huo muwashowasho wa nyongeza anautoa wapi? si awaache wafanyakazi wadai wenyewe, isitoshe katibu mkuu utumishi ameshalitolea ufafanuzi kasomeni kwanza ndio muje
 
Mwanzo nilikuamini sasa nimekuelewa nakukumbusha elewa humu jf 80% ni waelewa hawalishwi fikra unaoneka ni msomi mzuri sana ila mahaba yamekuzidi kila mtu anauweze wa kusikiliza, kuchambua, kutafakari na kutoa uamuzi ulio sahihi
 
Akikujibu Mkuu ni tag
 
Umeandika kishabiki tu. Huna info zozote kuhusu malipo ya sgr wala stiglazi. Endelea kumlamba miguu huyu dikteta wa kihutu.

Looser bado upo?

Mwenzako ni mhandisi, niko kwenye hiyo miradi.info gani unazo?

Certificate gani zinadaiwa???πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚
 
Lissu ni mbaguzi sana, hatuhitaji Rais wa Tanzania aliye mbaguzi. kawabagua wana Chato na Kanda ya Ziwa waziwazi kana kwamba Kanda ya Ziwa siyo sehemu ya Tanzania, anadhanimkiradi yote mikubwa ikijengwa Dar ndo Uzalendo. Tunahitaji maendelea ya vitu ambayo yanareflect maendeleo ya watu moja kwa moja kama anayofanya Magufuli na siyo kubagua baadhi ya maeneo kwa ajili ya kulifurahisha kundi fulani akidhani atapigiwa kura kumbe Watanzania tulikwishaamua kitambo kwamba NI MAGUFULI TENA 2020-2025
 
... eti fedha zingetumika kuchimba mitaro vingunguti, naona huyu hakuwepo nchini muda mrefu sasa hivi vingunguti ni lami tupu sivyo alivyo acha.
Kwa hiyo barabara zenye lami hazihitaji mitaro?
 
Mnitangaze na mimi!
Nyumbani kulikuwa kukavu watoto wanalia njaa!
Ktk mishe mishe nikapata buku!
Badala ya kununua uka lobo wapoze, nikawanunulia maputo!
Tangazeni!
 

Msimamizi wa maslahi ya wafanyakazi nchi hii ni nani kama sio serikali kupitia vyama vya wafanyakazi? Kwahiyo serikali yako imewalipa Contractors, na Contractors hawataki kuwalipa wafanyakazi wao kisa wanaizungusha hiyo pesa katika mabank yao kutengeneza faida zaidi na serikali yako imekaa kimya! Kama ni kweli huoni serikali imebariki huu unyonyaji unaofanywa na wenye tenda.

Yaani unatuambia kuwa wafanyakazi wanaweza kunyonywa nchi hii halafu serikali isiwe na lakufanya? Team magu akili huwa mnapeleka wapi jamani, kuna hoja sio za kuzitetea hapa JF, JF watu walio wengi wa akili timamu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…